Rufiji dam
JF-Expert Member
- Feb 20, 2020
- 4,107
- 9,671
Ombi la rais ni sheria.Rais Samia amesema "ANAOMBA" wakalimalize swala la Feisal, hapendezwi na ugomvi. Hajasema kama kuwalazimisha au kama amri. Ni "OMBI" ametoa ambalo linaweza likakubaliwa au kukataliwa na hao viongozi wa yanga!!!
Kosa lake ni nini hapo? Mipaka gani achunge?
FIFA haikatai pesa za hamasa wala klabu kusafirishwa kwandege za hisani.Ndiyo muelewe kwa nini FIFA inakataza serikali kuingilia mambo ya mpira wa miguu. Mlikata miuno kupewa ndege,mamilioni ya magoli na kualikwa kwenda kufakamia pilau la ikulu. There is no free dinner.
Inashagaza sana.Mtu anatoa ombi halafu anataka na mrejesho wa mtakapofikia kama una akili timamu lazima ujiongeze.
Huyo mpemba akisaini Simba hii dinner watailaani sana waliokuwa wamedhamiria kumkomoa.
Halafu tuhuma zake alizotoa juzi hazitojibiwa tena hivyo kuaminika ni za kweli.
Ndio hapo sasa wanakuja kulia lia hapa.🫱🏼🫲🏽🫱🏼🫲🏽🫱🏼🫲🏽🫱🏼🫲🏽🫱🏼🫲🏽 kuna mijitu mijinga sana muulize gharama ya ndege kwenda Algeria na kurudivna kwenda Mbeya apige hesabu ya nauli ya watu 250×2 Tz -Algeria
Mhhh kwahyo itakuaje sasa na dogo hamtaki herisi saidiMualiko wa ikulu umekua mchunguu, pilau limegeuka boko boko.
Sahivi ndo mnajua serikali haitakiwi kujihusisha na masuala ya soka? Alipokua anatoa ndege ya serikali buree? Na gharama zote zile? Mbna mlikua hamu muambii hilo??
Tulieni dawa iwaingie vizuriii, na ameshasema hivyoo, kinachotakiwa ni utekelezaji tyuuh.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] patamu hapoooo.
Yanga kiuhalisia hawakua na mpango wa kumuachia dogo walikua wanataka kipaji kipotee na wamchafue dogo. Hayo yote walikua wanaelewa utaratibu mzima na kwann wasikae nae toka sakata limeanza? Yaani bongo bado kwenye mpira tuna kaujing aka kuwekana chini kisa mambo ya ajabu ajabu tuYanga ni waoga Sana Kama FEI Toto hawataki walitakiwa kutangaza Bei ya kumuuza,, lkn wao wamebaki na aje tukae mezani tumalizane au timu inayomtaka iende ikaonanenao??suala Kama Hili halikuhitaji watu wakae mezani wanywe KaHawa.. ilikuwa ni biashara FEI anauzwa ml 500..timu inayomtaka ije ilipe biashara ifanyikeee..ohh turudi mezani.. kuna chakula umeandaa??
Yale mabango ya "Asante mama" yaliyojaa uwanjani siku ya fainali kwa mkapa ni ishara ya kwamba mlikuwa mnaunga mkono siasa kwenye michezo, kwasasa mnajifanya kupinga kwasababu limeng'ata upande wenu sio?Kwani nani alimuomba atupatie ndege?
Kwani nani alimuomba incentives za magoli?
Hawezi kulaghai taasisi kwa dinner ya Milioni 200.
Unahangaika ukiwa wapi?? Kwani hako si maombi tu kunasehem ameforce...ila tupo hpa nyumbani karib mtupe mrejessho...FIFA haikatai pesa za hamasa wala klabu kusafirishwa kwandege za hisani.
FIFA inakataza serikali kuingilia au kuathiri maamuzi ya sokaa
🤣🤣🤣🤣🤣..ohh turudi mezani.. kuna chakula umeandaa??
Habari wanajamvi.
Leo amesikika Rais wa Tanzania Akimdadavulia Rais wa Yanga SC Bw Eng Hersi Said kwa lengo la
kumuhimiza ahakikishe Mchezaji Feisal Salum anapata haki yake.
Ninacho fahamu kuwa Mama Samia hana ufahamu sahihi wa kinacho endelea baina ya mgogoro uliopo kati ya Yanga SC na Mchezaji husika. Hisia zake kama Mzanzibar ndizo zimempelekea kusukumwa kutoa mapendekezo yake pasi na kuhitaji kulifahamu zaidi swala hilo.
Ndugu Hersi Said, unapaswa kucheza karata zako makini mno kwenye hilo. Kumbuka Mama Samia ametumia gharama kiduchu sana kwenye kampeni ya zawadi za kila goli, Dinner la Ikulu pampja na usafiri wa ndege. Kumbuka hajafanya haya si kwa mapenzi ya dhati na masuala ya michezo, bali alilenga zaidi kuilaghai taasisi ya michezo ili iache kusimamia misingi ya kisheria na kikanuni ya michezo.
Kwa kawaida, ni muhimu kwa Rais wa nchi kuzingatia majukumu yake kikatiba na kutofautisha majukumu ya mamlaka nyingine za kiserikali na taasisi mbalimbali. Mgogoro kati ya klabu na mchezaji ni suala la kisheria ambalo linapaswa kusuluhishwa na mamlaka husika za sheria na kanuni za michezo.
Rais Samia Anahitaji Elimu zaidi.
Kwa hiyo Rais wa nchi kuingilia kati ktk mgogoro kama huo unaweza kusababisha mchanganyiko wa majukumu na kuingilia uhuru wa mamlaka nyingine. Ni muhimu kwamba kila mamlaka ifanye kazi yake. Kitendo cha Rais kuwapa Incentives mbalimbali basi isiwe sababu ya kuhalalisha kuingiliana ki mamlaka katika mihimili inayo jitegemea kiutendaji.
Rais Samia anahitaji mrejesho, Basi ni wasaa sahihi kuhakikisha anaandikiwa mrejesho wa kumuelimisha kuwa masuala ya migogoro ya kisoka/kimpira yana namna yake ya kutatuliwa. Muelewesheni kuwa zipo sababu za msingi kwanini hili suala linakawia kufikiwa tamati.
Ni vyema akafahamu kuwa uvunjwaji wa taratibu na mchezaji yeyote wa klabu ni lazima kuadhibiwe pasi na kujali kama huyu ni mchezaji wa kizanzibar, wa bara au wa kimataifa. Na hukumu kwa mchezaji wa namna hiyo hautotokwa kwa upendelea wa kibusara eti kwa kisingizio kuwa mchezaji ni mzawa au la.
Mshaurini Rais kuwa licha ya kuyafurahia mafanikio haya madogo ya klabu, kuna watu nyuma ya pazia ambao wanawekeza pesa zao na wasingependa kuona wanapata hasara ktk biashara ya mauzo ya wachezaji. Tukiruhusu kuingilia maamuzi ya taasisi huru ambazo zina sheria zake za usuluhishi basi tunajiweka katika nafasi ya kuwafukuza wawekezaji aina ya wakina GSM na Mo Dewji katika mpira wa Tanzania.
Kuna madhara makubwa sana endapo klabu kama klabu itashindwa kusimamia misingi ya taratibu zake na kusuluhisha migogoro na kesi za kimpira kwa kutumia tu mapendekezo ya wana siasa. Je Mama Samia anatoa ushauri kama nani? Je ni kama mtu mwenye ufahamu wa kanuni na taratibu za uendeshaji wa mpira? au Kama
Hili liwe fundisho kwa mawakala wa wachezaji.
Lazima kuwa na kipengele katika mkataba kinachoonesha.
1. Timu ikitaka kuvunja mkataba wa mchezaji muda wowote ifate kanuni gani.
Kuna wakati mchezaji anabadilikia kutabia au anaisaliti timu na anatakiwa kuachwa lazima kuwa na kipengele cha namna ya kumwacha.
.
Achana nao mkuu GSM akiambiwa achague kati ya biashara zake na Fei toto unafikiri atachagua nini?Sasa endelea kubishana na Mamlaka ya nchi. Maana wabongo huwa mnaubishi wa ujuaji mwingi.
Sio kila misingi ni lazima isimamiwe, ndio maana umepewa brain......thinking na busara ni muhimu.
Rais ametoa MAELEKEZO, hupaswi kujadili maagizo ya Rais, Bali anatakiwa kutafuta njia bora ya kuyatekeleza in mutual understanding.
Otherwise, aendele kupuuza na kubaki kwenye misingi yake.
Ombi la rais ni sheria.