Enyi Manabii wa kizazi kipya ni kweli mmepewa nguvu na Mwenyezi Mungu, au ni ushirikina tu?

Enyi Manabii wa kizazi kipya ni kweli mmepewa nguvu na Mwenyezi Mungu, au ni ushirikina tu?

Kwanini mkuu?

Mbona kuna ambao ni Manabii na wana karama za kuhubiri...

Kuna watu wamepewa karama zaidi ya moja na Mungu.
Swala sio kuhubiri na kuwa nabii sio karama ni huduma. Kuna huduma tano ( Mchungaji,nabii,mtume,mwinjirist, mwalimu)

katika hizo huduma Mchungaji pekee ndio Huwa anauwezo wa kuwa na washirika na kanisa na ndio atakayetoa hesabu juu ya washirika ambao alikuwa nao kanisan kwake kuwachunga.

Kwa lugha nyepes ukiwa nabii unapaswa kuwa chini ya kanisa na chini ya Mchungaji wako,

kukurahisishia kuelewa Kuna mwalimu wa neno la Mungu anaitwa Mwakasege Hana kanisa kwasbu sio Mchungaji yeye ni mwalimu means Yuko chini ya Mchungaji Fulani.

Sasa ukiona Kuna nabii anakanisa binafsi na anawashirika Hali yakuwa kimaandiko hatokuja kutoa hesabu juu ya washirika walipo kwake

lazima ujiongeze kwamba anaweza kuwafanya chochote na hahusiki kutoa hesabu yoyote juu yao siku ya mwisho kwasab hakuitwa kuchunga.

Mwisho wengi wenye huduma za unabii na utume wameamua kujiita wachungaji Kwa Nia njema kabisa Ili wawe na uwezo wa kuwa na washirika na kuwa na makanisa na ni Halali na wakiwa nao hawazuwiwi kuwatabilia chochote na hesabu watatoa.

Eg. Nakupa mifano michache ya wachungaji ambao wanahuduma za kinabii ndani yao Kuna pastor anaitwa Sunbella kyando ni pastor lakini anaprophetic ministry,
Pastor Chris huyu original yake ni Nigeria lakini kwasasa yupo ulaya na Mchungaji maarufu sana lakini ana huduma ya unabii ndani yake.

Over
 
Biblia inasema, hata wawapo wajinga lakini hawata potea. Wewe jitu Lina vaa vikuku, linatoboa pua na kuvaa hereni, make up na ma rasta, matatoo ndio usiseme bado hapo unategemea muujiza c'mon. Hakuna muujiza hapo wala ishara isipokuwa ile ya yona. Hakuna watu ma fuska kama hao mitume na manabii wengi wao huwa na sexual ritual kama sadaka kwa lucifer. Wengi wataangamia kwa kukosa maarifa.
Nakubaliana na wewe mkuu, inashangaza sana watu wanao jiita manabii, kuazia mavazi yao tu, ni ishara tosha kuwa neno la mungu hapo halipo kabisa..
 
Ukisoma vizuri Biblia utaona kuwa nabii ni mtu mwenye jukumu la kupitisha taarifa tu kwa wanadamu na mpeleka taarifa za wanadamu kwa Mungu...

Pia ni mtu aliyewekwa wakfu na Mungu mwenyewe kwa ajli ya kupatanisha watu na Mungu wao...

Hesabu 12
6 Kisha akawaambia,Sikizeni basi maneno yangu;Akiwapo nabii kati yenu,Mimi,Bwana,nitajifunua kwake katika maono,Nitasema naye katika ndoto.

Jaribu kutazama namna ambavyo Musa, Daniel, Eliya, Elisha, Samuel, Yohana Mbatizaji n.k, hawa hawakuwa wakiongoza watu wala kuwa na wafuasi kwa namna ya kusanyiko la kiibada kama kanisa au hekalu au sinagogi...

Nitaandika zaidi nipo mzigoni
Karibu sana mkuu, uje utupe Mwanga zaidi...
 
Roho ni nini?

Vyote hivyo ni nadharia za kufikirika tu.

Roho ni neno linalomaanisha moyo au kitu kinachohusiana na hisia, au nia.

Biblia inazungumzia roho katika muktadha tofauti, lakini mojawapo ya maeneo yanayojadiliwa ni katika Agano la Kale na Agano Jipya.

Katika Agano la Kale, kuna mafundisho juu ya "roho" kama pumzi ya uhai kutoka kwa Mungu. Mfano wa hili unapatikana katika kitabu cha Mwanzo 2:7 ambapo mwanadamu anapuliziwa pumzi ya uhai na kuwa hai.

Katika Agano Jipya, roho inajadiliwa zaidi, na kuna mafundisho juu ya Roho Mtakatifu. Kristo mwenyewe aliongelea kuhusu kuja kwa Roho Mtakatifu kama Msaidizi baada ya kuondoka kwake (Injili ya Yohana 14:16-17).

Biblia inashughulikia mada hii kwa undani zaidi na katika muktadha tofauti, hivyo ni vizuri kusoma maandiko kwa kina ili kuelewa vyema mafundisho yake.
 
Jinga!
Hakuna Mungu sukari kwenye muwa na nanasi aliweka babayenu? Watu hamna fadhila mmbwa nyie!! [emoji32][emoji32]

Barua ya Mtume Paulo kwa Waefeso. Katika Waefeso 4:29 (Tafsiri ya Neno), Paulo anasema:

"Maneno yenu na yawe yenye neema sikuzote, yaliyotiwa chumvi, ili myajue jinsi inavyopasa kila mtu ajibu."


Toa hoja mkuu, usitukane, ✍️✍️✍️
 
Nyinyi manabii mnao vaa visuluali vimebana, manabii mmesuka rasta, manabii mnawapiga mateke wagonjwa, manabii mnawalisha majani waumini, manabii mnawanywesha mafuta ya taa waumini, manabii mnataka sadaka kuazia elfu Tsh 30,000 na kuendelea, je ni kweli hizo nguvu/mamlaka mmepewa na Mwenyezi mungu?? [emoji848][emoji848]

"Kwa maana watatokea makristo wa uongo na manabii wa uongo watafanya miujiza mikubwa na maajabu ili kuwapoteza, kama ingewezekana, hata wateule."

Manabii ni watu wanaoaminiwa kuwa na uwezo wa kupokea ujumbe au mwongozo kutoka kwa nguvu za kimungu, Katika muktadha wa dini mbalimbali, manabii mara nyingi wanachukuliwa kama watu wanaotekeleza mapenzi ya mungu au nguvu za juu. Wanaweza kutabiri mambo ya baadaye, kutoa mafundisho ya kiroho.

Muktadha wa manabii unaweza kutofautiana kulingana na dini na imani. Kwa mfano, katika Ukristo, manabii wanaweza kutazamwa kama wale waliotumiwa na Mungu kutoa ujumbe wa kimungu. Yesu Kristo mwenyewe anachukuliwa na Wakristo wengi kama Mwana wa Mungu na Mtume wa mwisho.

Hata hivyo, mifumo mingine ya imani inaweza kuwa na maoni tofauti kuhusu manabii na uhusiano wao na nguvu za kimungu.

Katika imani ya Kikristo, manabii wanachukuliwa kuwa watu ambao Mungu aliwatumia kutoa ujumbe wake kwa binadamu. Manabii wa Agano la Kale, kama vile :- Isaya, Yeremia, Adamu, Nuhu, Abrahamu, Musa, Miriamu (dada ya Musa), Haruni, Debora, Samweli, Nathani, Eliya, Elisha
, Yona, Amosi, Hosea, Isaya, Mika, Nahumu, Habakuki, Zefania, Haggai, Zakaria na Malaki , wanachukuliwa kuwa wawakilishi wa Mungu waliotabiri mambo ya baadaye na kutoa maonyo na mafundisho. Hapa ni baadhi ya manabii na kazi zao walizo zifanya:-

• Musa: Alipelekwa na Mungu kuwaongoza Waisraeli kutoka utumwani.

• Eliya: Mmoja wa manabii wakubwa wa Kiyahudi, aliyefanya miujiza mingi.

• Isaya: Alikuwa nabii wa wakati wa Ufalme wa Yuda na aliandika kitabu cha Isaya.

• Yeremia: Alionywa kuhusu uharibifu wa Yerusalemu na utumwa wa Waisraeli.

• Ezekieli: Nabii wa kipindi cha utumwa Babeli, aliyeandika kitabu cha Ezekieli.

• Danieli: Alikuwa nabii katika utawala wa Babeli, na aliwekwa katika mazingira ya kifalme.

• Hosea: Alikuwa nabii wa Israeli na alionya juu ya unafiki wa kidini.

• Yoeli: Alitoa unabii kuhusu siku ya Bwana na mwisho wa nyakati.

• Amosi: Alikuwa mkulima na mchungaji, nabii wa haki na hukumu.

• Obadia: Alikuwa nabii mfupi, akitabiri juu ya hukumu ya Edomu.

• Mika: Alikuwa nabii wa haki na alihoji dhuluma na udanganyifu.

• Nahumu: Alikuwa nabii wa hukumu dhidi ya Ninawi.

• Habakuki: Alisimulia mazungumzo yake na Mungu na kuuliza maswali.

• Sefania: Alikuwa nabii wa hukumu na toba kwa watu wa Yuda.

• Yohana Mbatizaji: Alijitokeza kama mtangulizi wa Yesu Kristo na alibatiza watu kwa kutumia ubatizo wa toba. Kuhusiana na Yesu Kristo, yeye mwenyewe anachukuliwa kama Mwana wa Mungu na kama mwisho wa unabii.

Biblia inaonya kuhusu uwepo wa manabii wa uongo. Katika Agano Jipya, hasa katika kitabu cha Mathayo, sura ya 24, Yesu anatoa unabii wake wa mwisho, na miongoni mwa mambo aliyotabiri ni kuja kwa manabii wa uongo. Mathayo 24:24 (NIV) inasema:

"Kwa maana watatokea makristo wa uongo na manabii wa uongo watafanya miujiza mikubwa na maajabu ili kuwapoteza, kama ingewezekana, hata wateule."

Hapa, Yesu anawaonya wafuasi wake kuhusu hatari ya kupotoshwa na manabii wa uongo watakaofanya miujiza ili kuwapotosha watu.

Mimi kama Nyafwili Nasema ni muhimu kuwa macho na kuwa na busara katika kufuatilia ujumbe wa kiroho.... [emoji3578][emoji3578][emoji3578]
Kasome biblia imeandikwa kuwa shetani ujiinua kwa kila kiitwacho mungu kisicho mungu....maneno hayo maana yake ni pana sana...kwa kifupi shetani hutia nguvu kila kitu potovu kinacho usishwa na mungu mfano mafundisho potovu ....ibada potovu ...mitume feki ...manabii feki ...watakatifu feki wote hao upokea nguvu kutoka kwa shetani iwe ni kwa kujua au kutokujua ...ndiyo maana ikaandikwa kuwa siku ya mwisho watasema je hatukutoa pepo kwa jina lako na kuponya kwa jina lako na yeye atawaambia wazi ondokeni kwangu nyinyi watenda maovu.
 
Mungu hayupo.

Dini ni utapeli.
Ndg zangu wakati mwingine napata contradiction kuhusu nguvu na mamlaka ya Mungu hapa duniani ila tu niwaambie kweli Mungu mkuu mtakatifu na mwenye uwezo wa kila kitu yupo, pia ana kusudi kufanya yote haijalishi ya kheri au shari, yeye ndiye mwenye Siri kuu ya Dunia na ulimwengu.[emoji2969][emoji120][emoji1666]


Yeye ndiye Alfa na Omega
Yeye ndiye mwenye huruma
Yeye ndiye mwenye umiliki na mamlaka yote
Yeye ndiye hukiriwa na falme zote za kuzimu kwa uwezo wake wa ajabu


Mungu hachunguziki
Mungu nayemzungumzia hapa haeleweki
Mungu nayemsema hapa ndiye mwenye kusema iwe na ikawa, ndiye mwenye kukubali nakukataa kata kata

Mungu huyu ndiye mwenye kusudi kuu la kila jambo litokealo hapa Duniani


Pamoja na makosa yake shetani na falme zake zote za giza bado wanamkiri kwenye vinywa na nafsi zao kuye Yeye ndiye Bwana wa majeshi, yanayoendelea Duniani ni Ishara kuwa ndiye muweza wa yote, ndiye huwezi ukamtafakari ukammaliza, hachunguziki, haeleweki na haelezeki.

TABAKIA KUWA MUNGU TU. SIO MUNGU WAKUFIKIRIKA NI MUNGU ALIYE DHAHIRI NA KUNA SIKU WOTE TUTAPATA KUONA UKUU WAKE BILA KIFICHO. [emoji5]


Haelezeki naomba niishie hapa... [emoji2758]


Ombi langu rudi kwake fanya toba, ni msikivu atakusikia atakusamehe atakupa bega lake uegemee, atakufuta machozi haijalishi ulimkosea kiasi gani, usione shida zinaendelea hapa dunia, mf vita, umasikini magonjwa ukasema sio Mungu wa huruma, hapana


Huyu ndiye mwingi wa huruma. [emoji846]
 
Swala sio kuhubiri na kuwa nabii sio karama ni huduma. Kuna huduma tano ( Mchungaji,nabii,mtume,mwinjirist, mwalimu)

katika hizo huduma Mchungaji pekee ndio Huwa anauwezo wa kuwa na washirika na kanisa na ndio atakayetoa hesabu juu ya washirika ambao alikuwa nao kanisan kwake kuwachunga.

Kwa lugha nyepes ukiwa nabii unapaswa kuwa chini ya kanisa na chini ya Mchungaji wako,

kukurahisishia kuelewa Kuna mwalimu wa neno la Mungu anaitwa Mwakasege Hana kanisa kwasbu sio Mchungaji yeye ni mwalimu means Yuko chini ya Mchungaji Fulani.

Sasa ukiona Kuna nabii anakanisa binafsi na anawashirika Hali yakuwa kimaandiko hatokuja kutoa hesabu juu ya washirika walipo kwake

lazima ujiongeze kwamba anaweza kuwafanya chochote na hahusiki kutoa hesabu yoyote juu yao siku ya mwisho kwasab hakuitwa kuchunga.

Mwisho wengi wenye huduma za unabii na utume wameamua kujiita wachungaji Kwa Nia njema kabisa Ili wawe na uwezo wa kuwa na washirika na kuwa na makanisa na ni Halali na wakiwa nao hawazuwiwi kuwatabilia chochote na hesabu watatoa.

Eg. Nakupa mifano michache ya wachungaji ambao wanahuduma za kinabii ndani yao Kuna pastor anaitwa Sunbella kyando ni pastor lakini anaprophetic ministry,
Pastor Chris huyu original yake ni Nigeria lakini kwasasa yupo ulaya na Mchungaji maarufu sana lakini ana huduma ya unabii ndani yake.

Over
Katika Agano la Kale la Biblia, makanisa kama tunavyoyaelewa leo hayakuwepo kama taasisi ya kidini. Makanisa, kama vile yanavyoonekana katika muktadha wa Kikristo, yalianza baada ya Yesu Kristo, hasa katika Agano Jipya.

Hata hivyo, katika Agano la Kale, kulikuwa na manabii walioitwa na Mungu kutoa ujumbe wake kwa watu wa Israeli. Hawa manabii hawakuanzisha makanisa, bali walikuwa wanahubiri na kutangaza ujumbe wa Mungu kwa jamii ya watu wa Israeli. Walitumwa kurekebisha, kuonya, na kuelekeza watu kwa njia ya haki...

Kwa maandiko haya, hao manabii wa sasa ni matapeli...
 
Mkuu, Kitabu cha Biblia kinasema, nabii wa mwisho kwa upande wa kikatoliki ni yesu, na Mungu bado hajatuma nabii yeyote yule, je hao manabii wengine wamekuja kwa njia ipi??
Mtume wala nabii siyo matokeo ya kutumwa na mungu ....maana mungu anaweza hakatuma hata mbuzi kufanya jambo fulani ...mtume na nabii ni madaraja ya watakatifu na uchamungu na thawabu yoyote mwenye kiwango cha uchamungu na utakatifu na thawabu ya juu huyo ni mtume au nabii hata kama hafanyi utume au unabii
 
Back
Top Bottom