Enyi Manabii wa kizazi kipya ni kweli mmepewa nguvu na Mwenyezi Mungu, au ni ushirikina tu?

Enyi Manabii wa kizazi kipya ni kweli mmepewa nguvu na Mwenyezi Mungu, au ni ushirikina tu?

Nyinyi manabii mnao vaa visuluali vimebana, manabii mmesuka rasta, manabii mnawapiga mateke wagonjwa, manabii mnawalisha majani waumini, manabii mnawanywesha mafuta ya taa waumini, manabii mnataka sadaka kuazia elfu Tsh 30,000 na kuendelea, je ni kweli hizo nguvu/mamlaka mmepewa na Mwenyezi mungu?? 🤔🤔

"Kwa maana watatokea makristo wa uongo na manabii wa uongo watafanya miujiza mikubwa na maajabu ili kuwapoteza, kama ingewezekana, hata wateule."

Manabii ni watu wanaoaminiwa kuwa na uwezo wa kupokea ujumbe au mwongozo kutoka kwa nguvu za kimungu, Katika muktadha wa dini mbalimbali, manabii mara nyingi wanachukuliwa kama watu wanaotekeleza mapenzi ya mungu au nguvu za juu. Wanaweza kutabiri mambo ya baadaye, kutoa mafundisho ya kiroho.

Muktadha wa manabii unaweza kutofautiana kulingana na dini na imani. Kwa mfano, katika Ukristo, manabii wanaweza kutazamwa kama wale waliotumiwa na Mungu kutoa ujumbe wa kimungu. Yesu Kristo mwenyewe anachukuliwa na Wakristo wengi kama Mwana wa Mungu na Mtume wa mwisho.

Hata hivyo, mifumo mingine ya imani inaweza kuwa na maoni tofauti kuhusu manabii na uhusiano wao na nguvu za kimungu.

Katika imani ya Kikristo, manabii wanachukuliwa kuwa watu ambao Mungu aliwatumia kutoa ujumbe wake kwa binadamu. Manabii wa Agano la Kale, kama vile :- Isaya, Yeremia, Adamu, Nuhu, Abrahamu, Musa, Miriamu (dada ya Musa), Haruni, Debora, Samweli, Nathani, Eliya, Elisha
, Yona, Amosi, Hosea, Isaya, Mika, Nahumu, Habakuki, Zefania, Haggai, Zakaria na Malaki , wanachukuliwa kuwa wawakilishi wa Mungu waliotabiri mambo ya baadaye na kutoa maonyo na mafundisho. Hapa ni baadhi ya manabii na kazi zao walizo zifanya:-

• Musa: Alipelekwa na Mungu kuwaongoza Waisraeli kutoka utumwani.

• Eliya: Mmoja wa manabii wakubwa wa Kiyahudi, aliyefanya miujiza mingi.

• Isaya: Alikuwa nabii wa wakati wa Ufalme wa Yuda na aliandika kitabu cha Isaya.

• Yeremia: Alionywa kuhusu uharibifu wa Yerusalemu na utumwa wa Waisraeli.

• Ezekieli: Nabii wa kipindi cha utumwa Babeli, aliyeandika kitabu cha Ezekieli.

• Danieli: Alikuwa nabii katika utawala wa Babeli, na aliwekwa katika mazingira ya kifalme.

• Hosea: Alikuwa nabii wa Israeli na alionya juu ya unafiki wa kidini.

• Yoeli: Alitoa unabii kuhusu siku ya Bwana na mwisho wa nyakati.

• Amosi: Alikuwa mkulima na mchungaji, nabii wa haki na hukumu.

• Obadia: Alikuwa nabii mfupi, akitabiri juu ya hukumu ya Edomu.

• Mika: Alikuwa nabii wa haki na alihoji dhuluma na udanganyifu.

• Nahumu: Alikuwa nabii wa hukumu dhidi ya Ninawi.

• Habakuki: Alisimulia mazungumzo yake na Mungu na kuuliza maswali.

• Sefania: Alikuwa nabii wa hukumu na toba kwa watu wa Yuda.

• Yohana Mbatizaji: Alijitokeza kama mtangulizi wa Yesu Kristo na alibatiza watu kwa kutumia ubatizo wa toba. Kuhusiana na Yesu Kristo, yeye mwenyewe anachukuliwa kama Mwana wa Mungu na kama mwisho wa unabii.

Biblia inaonya kuhusu uwepo wa manabii wa uongo. Katika Agano Jipya, hasa katika kitabu cha Mathayo, sura ya 24, Yesu anatoa unabii wake wa mwisho, na miongoni mwa mambo aliyotabiri ni kuja kwa manabii wa uongo. Mathayo 24:24 (NIV) inasema:

"Kwa maana watatokea makristo wa uongo na manabii wa uongo watafanya miujiza mikubwa na maajabu ili kuwapoteza, kama ingewezekana, hata wateule."

Hapa, Yesu anawaonya wafuasi wake kuhusu hatari ya kupotoshwa na manabii wa uongo watakaofanya miujiza ili kuwapotosha watu.

Mimi kama Nyafwili Nasema ni muhimu kuwa macho na kuwa na busara katika kufuatilia ujumbe wa kiroho.... ✍️✍️✍️
sijui nikujibu vipi papaa!!!...ila kuna habari ilishai chapishwa kwa kuna waganga wawili wenye nguvu sana,,mmoja yupo senegal na mwingine yupo nigeria,,,nasikia wanauwezo wa kukupa hiyo power{sina hakika]....lakini kisingi tu ni kwamba,,kwa ufhamu wangu mdogo,,,wa wa kweli wa MUNGU huwa ni wa2 simple sana,,yaani ata uvvaji wo mwingi ni simple mno kwani muda mwingi wpo bize kujiandaa na kesho{ kifo} na tayari wamshaidharau dunia kwani weshajua "dunia ni mapito",,,,sasa hawa manabii wanaoulamba kama koffi olomide!!!!,,sijui nisemeje!!!.....shetani yupo kazini man,,,,,at YESU alipata kujaribiwa na mzee shetani,,alipandishwa kwenye kilele ch a mlima afu mzee shetani akamwambia"hakika ukinisujudi kivo uvionvo vyote ni mali yako bahati nzuri YESU ALISHINDA,angefeli sijui ingekuaje???,,,manake ADAM na HAWA walivodanganywa wakakubali,,,ndo tukapewa adhabu ya kifo,,,so YESU alikuja kutukomboa kwamba ingawa tutakufa,lakini tutafufuliwa!!!!!........ujue nikue kasamari kadogo,,,nabii wa kweli anahubiri kuhusu maisha baada ya hapa duniani{mbinguni na jehanam},,nabii wa uongo atatangaza ufahari na mali za dunia....kuhusu sadaka,,YESU alipata kumbariki bibi mmoja mzee aliyetoa kiasi kidogo sana cha pesa badala ya kubariki matajiri waliotoa mipesa kibao!!!!!!,hawa manabii hawakemei pesa haramu hata kidogo,,,,,wao wanachojua ni pesa tu,,
 
Mkuu, Kitabu cha Biblia kinasema, nabii wa mwisho kwa upande wa kikatoliki ni yesu, na Mungu bado hajatuma nabii yeyote yule, je hao manabii wengine wamekuja kwa njia ipi??
YESU hakuwa nabii,YESU alikuwa MASIH!!!"masihi yuko viwango vya juu kuliko nabii"''''kuna masih mmoja tu aliyewahi kutokea hapa dunia,na atakuja tena kama alama ya kiama na tutamwona akishuka toka mawinguni na masih huyo ni YESU peke yake,,ndugu ze2 waislam pia wanamtambua kama MASIH ISSA BIN MARIAM!!
 
sijui nikujibu vipi papaa!!!...ila kuna habari ilishai chapishwa kwa kuna waganga wawili wenye nguvu sana,,mmoja yupo senegal na mwingine yupo nigeria,,,nasikia wanauwezo wa kukupa hiyo power{sina hakika]....lakini kisingi tu ni kwamba,,kwa ufhamu wangu mdogo,,,wa wa kweli wa MUNGU huwa ni wa2 simple sana,,yaani ata uvvaji wo mwingi ni simple mno kwani muda mwingi wpo bize kujiandaa na kesho{ kifo} na tayari wamshaidharau dunia kwani weshajua "dunia ni mapito",,,,sasa hawa manabii wanaoulamba kama koffi olomide!!!!,,sijui nisemeje!!!.....shetani yupo kazini man,,,,,at YESU alipata kujaribiwa na mzee shetani,,alipandishwa kwenye kilele ch a mlima afu mzee shetani akamwambia"hakika ukinisujudi kivo uvionvo vyote ni mali yako bahati nzuri YESU ALISHINDA,angefeli sijui ingekuaje???,,,manake ADAM na HAWA walivodanganywa wakakubali,,,ndo tukapewa adhabu ya kifo,,,so YESU alikuja kutukomboa kwamba ingawa tutakufa,lakini tutafufuliwa!!!!!........ujue nikue kasamari kadogo,,,nabii wa kweli anahubiri kuhusu maisha baada ya hapa duniani{mbinguni na jehanam},,nabii wa uongo atatangaza ufahari na mali za dunia....kuhusu sadaka,,YESU alipata kumbariki bibi mmoja mzee aliyetoa kiasi kidogo sana cha pesa badala ya kubariki matajiri waliotoa mipesa kibao!!!!!!,hawa manabii hawakemei pesa haramu hata kidogo,,,,,wao wanachojua ni pesa tu,,
• Asante sana mkuu, Kwa mchango wako mzuri ✍️✍️.
 
YESU hakuwa nabii,YESU alikuwa MASIH!!!"masihi yuko viwango vya juu kuliko nabii"''''kuna masih mmoja tu aliyewahi kutokea hapa dunia,na atakuja tena kama alama ya kiama na tutamwona akishuka toka mawinguni na masih huyo ni YESU peke yake,,ndugu ze2 waislam pia wanamtambua kama MASIH ISSA BIN MARIAM!!
• Upo sahihi mkuu, katika sura kama vile Sura ya 16, ambapo Petro anamtambulisha Yesu kuwa Masihi.

• Lakini Watu wanamwita Yesu nabii kwa sababu ya mafundisho yake, unabii uliotimia kupitia maisha yake, na jukumu lake la kuleta ujumbe wa Mungu. Ingawa kwa upande mwingine anachukuliwa kama Masihi, jina "nabii" linaweza kutumika kumaanisha mtu aliyetumwa na Mungu kutoa ujumbe na mwongozo kwa watu wake.

Yesu alitoa mafundisho ya kiroho, alitoa unabii kuhusu mambo yanayokuja, na aliwakilisha utume wa Mungu duniani. Kwa hiyo, kumwita nabii ni njia ya kuelezea jukumu lake kama mwakilishi wa kimungu na mtoa ujumbe wa Mungu kwa wanadamu.
 
WEWE KAMA NI MFUASI WA MITUME NA MANABII
1.JUA YA KWAMBA WEWE SIO MFUASI WA KRISTO(SIO MKRISTO) WEWE NI WA NABII/MTUME, NA KWMBA WEWE
2.ZOMBII,
3.UNATATIZO LA AFYA YA KILI

NA KWAMBA U MASKINI WA AKILI, UCHUMI, NA IMANI.
MITUME NA MANABII HAWANA SHIDA, SHIDA NI WAUMINI WAO
 
Kama hawamo kwenye kitabu kitakatifu basi hao sio manabii watokanao na kitabu kile yawezekana wanavyo vitabu vyao.
Nabii unasema eeeti 1988 ulionana na Yesu Mara sijui una namba zake za WhatsApp.
Wizi mtupu
 
• Upo sahihi mkuu, katika sura kama vile Sura ya 16, ambapo Petro anamtambulisha Yesu kuwa Masihi.

• Lakini Watu wanamwita Yesu nabii kwa sababu ya mafundisho yake, unabii uliotimia kupitia maisha yake, na jukumu lake la kuleta ujumbe wa Mungu. Ingawa kwa upande mwingine anachukuliwa kama Masihi, jina "nabii" linaweza kutumika kumaanisha mtu aliyetumwa na Mungu kutoa ujumbe na mwongozo kwa watu wake.

Yesu alitoa mafundisho ya kiroho, alitoa unabii kuhusu mambo yanayokuja, na aliwakilisha utume wa Mungu duniani. Kwa hiyo, kumwita nabii ni njia ya kuelezea jukumu lake kama mwakilishi wa kimungu na mtoa ujumbe wa Mungu kwa wanadamu.
Nabii,neno la kiarabu ambalo kiswahili kimekopa,maana yake ni mtu aliyechaguliwa na mungu akiwasiliana nae kumpa maagizo ayafikishe kea watu,wanafunzi wa yesu hawakuwa nabii,hao mbuzi wanajiita manabii
 
Nabii,neno la kiarabu ambalo kiswahili kimekopa,maana yake ni mtu aliyechaguliwa na mungu akiwasiliana nae kumpa maagizo ayafikishe kea watu,wanafunzi wa yesu hawakuwa nabii,hao mbuzi wanajiita manabii
ok,,walimwita nabii,but maandish yanamtambulisha kama masih kwenye vitabu vyote,QU'RAN TUKUFU na BIBLI TAKTIFU!!
 
WEWE KAMA NI MFUASI WA MITUME NA MANABII
1.JUA YA KWAMBA WEWE SIO MFUASI WA KRISTO(SIO MKRISTO) WEWE NI WA NABII/MTUME, NA KWMBA WEWE
2.ZOMBII,
3.UNATATIZO LA AFYA YA KILI

NA KWAMBA U MASKINI WA AKILI, UCHUMI, NA IMANI.
MITUME NA MANABII HAWANA SHIDA, SHIDA NI WAUMINI WAO
• kitabu cha Waraka kwa Warumi na Waraka wa kwanza wa Mtume Paulo kwa Wakorintho. Kinatafsiri tofauti kulingana na madhehebu na mafundisho ya Kikristo.

• Mkuu Tunawasaidiaje watu walio tumbukia kwenye manabii fake, Au tuwaache waendelee na safari yao. 🤒🤒
 
Kama hawamo kwenye kitabu kitakatifu basi hao sio manabii watokanao na kitabu kile yawezekana wanavyo vitabu vyao.
Nabii unasema eeeti 1988 ulionana na Yesu Mara sijui una namba zake za WhatsApp.
Wizi mtupu
Inafikirisha sana, nabii amekomaa kuishi DSM. Kupiga hela za maskini.
 
Wakristo wanajiona wamesoma sanaaa kuliko waislamu ila ila ila hakuna watu wanotapeliwa kiurahisi kama wakristo poleni sanaa
 
ok,,walimwita nabii,but maandish yanamtambulisha kama masih kwenye vitabu vyote,QU'RAN TUKUFU na BIBLI TAKTIFU!!
Masihi ni kiranja wa zamu,yaani bado ni kiranja ila wiki hii ni zamu yake,kuwa masihi hakumfanyi yesu asiwe nabii...japo umenielewa vibaya
 
Back
Top Bottom