Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Poleni sana wafiwa. Kweli nyimbo zake ni maarufu sana pengine hata kuliko jina lake hasa huo wimbo wa ' Siku nikilala mauti'. Apumzike kwa amani mtumishi wa Mungu. Amefanya kazi kubwa ya utume.Mwimbaji mkongwe wa nyimbo za injili na Askofu wa Hossana Assemblies of God Ephraim R. Mwansasu amefariki dunia usiku wa kuamkia leo (29/08/2021). Mwasasu alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya moyo kwa muda mrefu, kwa sasa msiba upo Kimara Mwisho.
Mwansasu atakumbukwa kwa nyimbo zake nyingi alizoziimba kwa mvuto wa aina yake na kutoa ujumbe mzuri kwa kila aliyesikiliza na kuona video za nyimbo hizo zilizopendwa na kupata umaarufu Tanzania na nje ya Tanzania.
Baadhi ya nyimbo za Mwasasu ni:
- Siku nikilala mauti.
- Nangojea wakati.
- Kutesa kwa zamu.
- Dunia inapita.
- Tukimaliza kazi.
- Kiama.
- Heri wenye moyo safi.
- Tutatesa milele.
- Wosia wa baba.
- Watoto wachanga.
- Wanawake.
- Maumivu ya Yesu.
Bwana Alitoa na Bwana Ametwaa Jina Lake Lihimidiwe, Pumzika kwa amani nguli wa nyimbo za injili Askofu Ephraim R. Mwansasu.
View attachment 1914996
View attachment 1915817
View attachment 1915016
AmenDaaa apumzike pema "SIKU NIKILALA"
Tuendelee kuutafakari ujumbe maana sisi sote tunapita katika dunia hii.Siku nikilala... toka jana mgoma ipo kwenye playlist yangu tuuu weed on my right hand full meditation
AmenRest in paradise
Amen, tuombe Mwenyezi Mungu atujalie sisi sote mwisho ulio mwema katika hii dunia.Lala salama Mtumishi wa Mungu!
Amen, ni kweli kazi kubwa ya uimbaji ameifanya kwa unyenyekevu wa hali ya juu jambo lililopelekea mafanikio.Poleni sana wafiwa. Kweli nyimbo zake ni maarufu sana pengine hata kuliko jina lake hasa huo wimbo wa ' Siku nikilala mauti'. Apumzike kwa amani mtumishi wa Mungu. Amefanya kazi kubwa ya utume.
Nafikiri umemchanganya na Mwansasu wa MbeyaReal gospel legend from early 1990's. Let him rest
AMEEN!!🙏🙏Amen, tuombe Mwenyezi Mungu atujalie sisi sote mwisho ulio mwema katika hii dunia.
AMINA, Mungu wa mbinguni ampumzishe salamaLala salama Mtumishi wa Mungu!
Kwa nini siku hizi watu hufa kabla ya wakati?
Mkuu aliyefariki ni Ephraim Mwansasu ni mzaliwa wa Mbeya na aliaanza kuimba akiwa Mbeya katika miaka ya 1990.Nafikiri umemchanganya na Mwansasu wa Mbeya
AmenR.I.P
Mwalimu ninamaanisha ukiondoa emergency za kifo kama Ajali...vinginevyo ni kujitakia.Je waweza fafanua zaidi Kufa kabla ya wakati?
Na je wakati sahihi ni upi?
Nashukuru sana kwa ufafanuzi huu wa kina.vinginevyo ni kujitakia.
Vifo vingi chini ya miaka 80 ni vya kujitakia, maana yake ulaji, unywaji wenye makosa na kuishi mazingira yasiyo sahihi hupelekea vifo vya mapema.
Consciousness ni kujitambua na kujua hatari zinazokuzunguka ambazo usipozijua huleta vifo vya mapema.
Amen, mchango wake tutaukumbuka daima.
Mimi nasema wazi kuwa nyimbo za Mwansasu ndizo zilizonibariki sana miaka ya 2004-2010 na ndizo zinazofundisha bila mbwembwe nyingi za kisasa, pamoja na za Mch. Abihudi Misholi na Faustine MunishiTutamkumbuka