Erick Kabendera kupitia Kitabu chake: Ben Saanane aliuawa na Rais Magufuli na maiti yake ikatupwa Mto Rufiji

Erick Kabendera kupitia Kitabu chake: Ben Saanane aliuawa na Rais Magufuli na maiti yake ikatupwa Mto Rufiji

Nanukuu......
Kitabu cha “In the Name of the President: Memoirs of a Jailed Journalist” kilichoandikwa na Erick Kabendera, @kabsjourno kimeanza kuuzwa leo. Mwandishi anaeleza kuhusu kutekwa na kuuwawa kwa Ben Rabiu Focas Saanane, December 2016 alipigwa risasi na mwili wake kutupwa mto Rufiji.

View attachment 3189981View attachment 3189980
I wish ma ccm yote,yapotee kama hili jambazi la kisukuma,
 
Hiki kitabu nitakipataje? Nakosa uvumilivu wa kukisubiri kinifikie.
Nina wasiwasi kisije kuzuiliwa kuuzika.

Ila Ben Saanane aliniuma sana, pumzika kwa amani rafiki mwema.
Ben nilimfahamu zamani enzi hizo tunasoma Lyamungo boys, mimi nikiwa form 1 yeye alikuwa form 3 kwahiyo namfahamu vizuri enzi hizo. Sikumbuki vizuri kama alishaanza kujihusisha na siasa nachokumbuka alikuwa prefect pale Lyamungo.

Baada ya Lyamungo alienda Galanos I’m not sure.

Fast forward, ninaanza kumuona kwenye siasa za Chadema na hapa JF.

Kwa mtu uyepata kumuona halafu unasikia ametekwa na kuuwawa inahuzunisha hasa kipindi kile mzee wake anaomba mwanaye arudi hata kama ni maiti 🙂
 
Kitabu cha “In the Name of the President: Memoirs of a Jailed Journalist” kilichoandikwa na Erick Kabendera, kimeanza kuuzwa leo. Mwandishi anaeleza kuhusu kutekwa na kuuwawa kwa Ben Rabiu Focas Saanane, December 2016 alipigwa risasi na mwili wake kutupwa mto Rufiji.

View attachment 3190072View attachment 3190073
Hadithi za kufikirika hizi kunogesha mauzo na umaarufu wa kitabu.
 
Angelisema Magufuli alitoa 'maelekezo' ningeweza kumwamini.

hili la kusema eti alikutanishwa na Magufuli Ikulu na kwa vile Magufuli alipenda kubeba bastola, eti akachomoa bastola na kumpiga risasi kwa mkono wake, hainiingii akilini mimi.
Ni ngumu sana jambo hilo kutendeka kama alivyolirahisisha kwa kuliandika.
Nakuunga mkono. Jamaa kaandika kirahisi rahisi kama vile katoka kubugia pombe
 
Ben saanane yuko wapi
Ni hivi kabla ujanunua ugomvi muelewe adui.

Watanzania baadhi hawana mipaka.

Hizi akili sijui watanzania mnazitoa wapi, kuna boundaries in life.

Sawa umechukua risk ya kumtukana ralsi na kuichafua nchi kwenye majarida ya kimataifa tena ukapewa front cover page. Wenyewe wakikujua unategemea nini.

Kuna huu upuuzi kwenye vichwa vyetu watanzania hatujui mipaka, wala kuelewa ukivuka huo mpaka uwe tayari kuishi na consequences zake.

Kwenye kichwa chake Kabendera anaamini alionewa (wakati he took uncalculated risks kwa tamaa zake mwenyewe) worst anapambana na marehemu.

Kabla ujafanya kitu elewa madhara yake.
 
Angelisema Magufuli alitoa 'maelekezo' ningeweza kumwamini.

hili la kusema eti alikutanishwa na Magufuli Ikulu na kwa vile Magufuli alipenda kubeba bastola, eti akachomoa bastola na kumpiga risasi kwa mkono wake, hainiingii akilini mimi.
Ni ngumu sana jambo hilo kutendeka kama alivyolirahisisha kwa kuliandika.
Nakuunga mkono. Ni ujuha kuweza hata kufikiria kuwa simulizi hii inaweza kuwa kweli. Naona kwa makusudi kaamua kuweka hii hadithi ili kuibua utata itaopelekea umaarufu na mauzo ya kitabu hiki.
 
Mwandishi kwa makusudi kabisa ameamua kutumia picha ambayo ilikua ni siku Magufuli anawasilisha silaha zake kufanyiwa ukaguzi kwa maelekezo ya RC wa Dar.

Ambaye alitaka kila mkazi wa Dar apelekw silaha zake kufanyiwa ukaguzi. Ndipo ikapatikana hiyo picha. Watakaoona hicho kitabu na hawajui juu ya hilo wakisoma hicho kipande cha "he always carried a gun" kuna mtazamo wataupata.
What is your point?

Hakubeba bunduki kila mara?

Hiyo picha inawezekana ni sehemu ya kutengeneza plausibility kwamba Magufuli alimuua Saanane kwa mkono wake mwenyewe.

Ukiweka madai kwamba Alhaji Ali Hassan Mwinyi alimuua mtu kwa mkono wake mwenyewe, kwa bastola, wakati hakuna ushahidi wowote kwamba Alhaji Ali Hassan Mwinyi alikuwa na bastola, hatujui hata kama alijua kutumia bastola, madai hayo yanapata ugumu kukubalika.

Ukiweka madai kwamba Magufuli alimuua mtu kwa mkono wake mwenyewe, ingawa madai hayo bado yana ugumu kuyahakiki, lakini ugumu wake si mkubwa kama yale madai ya Alhaji Ali Hassan Mwinyi, kwa sababu angalau Magufuli tunajua alikuwa na bastola, kuna ushahidi wa picha anaionesha, most likely anajua kuitumia.

Hiyo picha ni ya Magufuli, inajulikana, huwezi kusema kapakaziwa picha si yake.

What is your point?
 
Back
Top Bottom