Erick Kabendera kupitia Kitabu chake: Ben Saanane aliuawa na Rais Magufuli na maiti yake ikatupwa Mto Rufiji

Erick Kabendera kupitia Kitabu chake: Ben Saanane aliuawa na Rais Magufuli na maiti yake ikatupwa Mto Rufiji

Kabendera ana bahati ingekuwa nchi za waislamu kama syria watu wangemtafuta wakajitoa muhanga kwa ujinga wake. Yaani sasa tunawaza namna ya kuongoza east africa kwa uchumi halafu kuna mjinga mjinga anaanza kuleta ujinga wa kudhihaki mamlaka ya rais ambao ndiyo ngao yetu kama taifa. Yaani tubanane kwenye hoja ila siyo kudharau mamlaka ya rais. Mamlaka ya rais tukiruhusu idharauriwe matokeo yake ni kama Burundi na Congo na yaliyotokea Rwanda au Uganda. Mamlaka ya rais inapaswa kulindwa kwa gharama yeyote na iheshimike. Amani yetu ni kwa sababu ya uimara wa taasisi ya urais na rais mwenyewe. Leo hii anatokea mjinga tu kisa anajua kuandika anaaza kudhihaki mamlaka ya rais, inakera sana. Kabendera n mjinga sana na hana akili kabisa, hana tofauti na ayatola zito aliyesema wanaompenda Dkt Magufuli eti waende kwenye kabuli chato, very idiot ayatola zito
Wasukuma acheni kupaniki bwana
 
Never say Never Katika hii dunia.

Usimuamini mtu hawezi kufanya kitu, siku ukipata ushahidi kua kafanya utaweka wapi sura yako?
Kwa hiyo leo hii tukiskia wewe umebaka mbuzi au ng'ombe tuziamini tuhuma hizo Moja Kwa Moja na kukuchukulia hatua za kisheria/kinidhamu mpaka pale utakapotoka ushaidi kwamba wewe hujafanya tukio Hilo sio?????

Hizi reasoning za kipuuzi sijui Huwa mnazitoa wapi
 
Wasukuma acheni kupaniki bwana
Kwanini unaona kila mwenye mawazo kinzani kwenye hili jitabu la kibendera ni msukuma????

Kwani Magufuli waliokuwa wanampenda na kumkubali ni wasukuma pekee tu???

Kichwa chako kimejaa stereotypes za kipumbavu sana, halafu unajiita tajiri WA kusini badilisha hiyo username jiite hata "mjinga WA kusini" itakufaa
 
Sio swala la chuki hapo tatizo mtu akikosoa mamlaka hii nchi basi uwa anapachikwa jina la kibaraka..

Hapo huyo mwandishi amemtuhumu aliyekuwa rais wa nchi yetu na mimi sioni tatizo maana alikuwa binadamu na inawezekana alikuwa na mapungufu pia ambayo baadhi ya watu waliyaona maan walipata madhira mbalimbali.

Sasa kama serikali inataka kumtetea mwenda zake basi utaratibu ufuatwe sio kuanza kumwita mtu msaliti sijui katumwa na maadui wa nchi..

Maadui gani hao ilhali nchi yenyewe nusu ya budget ni misaada kutoka nje huo uadui ni upi hasa sisi km tuta battle basi kaa ukijua ni ku battle na nchi jirani tu hapo kenya , uganda rwanda hao ndio saizi zetu tofauti na hapo ni kujidharirisha.

Nchi yetu ni changa mno na tunajitafuta karibu kwenye kila nyanja.
Alafu muda mwingine tutue common sense.
Swali lako, kwanini amekitoa hiki kitabu kipindi hiki ambacho muhusika hayupo?

Lengo kuu la yeye kutoa kitabu hiki ni Nini hasa Kwa kipindi hiki?

Na kwanini ametumia lugha ya kingereza ambayo tunajua zaidi ya 80% ya watanzania hawaijui Kwa ufasaha?

Je, targeted audience yake ni akina nani hasa?

Yaani unaona tukimuita huyu jamaa ni kibaraka na msaliti tunakosea?
 
Lengo sio Magufuli bali ni Tanzania.


Kwa ujumla wake Tanzania inakuwa sana kiuchumi.

Sasa hilo ni tishio kwa nchi mahasimu.

Moja ya njia wanayotumia ni kuharibu sifa ya nchi.

Na Magufuli ni kama sababu tu.

Ila maadui wa nchi wako busy kuhakikisha hatuwapiti kiuchumi kuja kuwa super power.
Kuna wapumbavu hapa wanadhani hiki alichokifanya Kibendera impacts yake itaishia kwenye kudunisha legacy ya Magufuli tu, hawajui kwamba muathirika mkuu Kwa Sasa ni serikali iliyopo madarakani na taifa zima Kwa ujumla.

Serikali ya Sasa ni muendelezo wa serikali ya Magufuli, asilimia kubwa WA wafanyakazi kwanzia raisi mwenyewe mpaka vyombo vya usalama ndio vile vile vilivyofanya kazi na Magufuli.....!

Kwa hiyo tuhuma hizi Moja Kwa Moja zinaihusu na serikali hii ya Samia, hivyo basi kama Kuna athari zozote zitakazotokana na kitabu hiki basi zitaikumba serikali hii ya Sasa na sio Magufuli.

Kuna vitu ukiwa na akili timamu ambazo ni fikirivu huwezi kuvishabikia ikiwemo hili alilofanya Kibendera hapa....

Hawa haters wa Marehemu wakati wanafurahia na kumpongeza kibendera, wasisahau kuwa wanampongeza Kwa kuichafua serikali iliyopo madarakani, japo akilini mwao wanaamini anayechafuliwa ni Magufuli.
 
Angelisema Magufuli alitoa 'maelekezo' ningeweza kumwamini.

hili la kusema eti alikutanishwa na Magufuli Ikulu na kwa vile Magufuli alipenda kubeba bastola, eti akachomoa bastola na kumpiga risasi kwa mkono wake, hainiingii akilini mimi.
Ni ngumu sana jambo hilo kutendeka kama alivyolirahisisha kwa kuliandika.
Hilo mbona kusemwa halikuanzia kwa Kabendera! Habari hiyo imesemwa sana na watu wa ndani kabisa wa jengo kuu hata kabla mwendazake hajaenda safari yake ya mwisho.
Ni jambo linafahamika ila tu Kabendera kaliweka wazi tuu kitabuni.
Hakuna siri chini ya jua nasi wengine tunaamini Kabendera kafanya wajibu wake kuweka wazi badala ya minong'ono
 
Tapeli kwenye Moja na mbili hahahahah Tanzania ukitaka kuwanasa wajinga Tunga uongo tu hapo wajinga wanaenda kupigwa atawanasa wajinga ila sisi wenye akili tunaona kabisa huo ni uongo
"Sisi wenye akili" unajihisi nawe ni mmoja wao? Mbona unafikiri kinyume na hao wenye akili?
We huamini hilo kwa mtu alikuwa ana mpa adhabu ya push up na kichura chura mkewe kwa sababu ya kuhamisha matofali bila ruhusa yake?
Jiwe alikuwa anaweza kufanya chochote isipokuwa kulamba sumu tuu.
Kaulize pale Ujenzi au kwao Chato.
 
Sina uhakika ni kiasi gani. Lkn jua ya kuwa miamala yote ya pesa kutoka/kwenda nje, inamulikwa. Kabendera alikutwa kwenye akaunti yake pesa iliyotoka nje kama US$ 200,000. Ambayo haikuonesha alilipwa baada ya biashara gani.
Mbona Hela ndogo sana hii mkuu
Yaani nchi ihangaike na 500m kweli?
 
Mbona Hela ndogo sana hii mkuu
Yaani nchi ihangaike na 500m kweli?

Duniani kote, mapato yasiyoeleweka chanzo chake, lazima wahangaike na wewe.
Isitoshe, kiasi hicho cha pesa kwa Afrika siyo kidogo.
 
Siku zote usiamini usichokiona. ukisikia bila kuona ni kuokosa ushaidi mahakama haimini habari za kusadikika.
Take Note
 
Kwanini unaona kila mwenye mawazo kinzani kwenye hili jitabu la kibendera ni msukuma????

Kwani Magufuli waliokuwa wanampenda na kumkubali ni wasukuma pekee tu???

Kichwa chako kimejaa stereotypes za kipumbavu sana, halafu unajiita tajiri WA kusini badilisha hiyo username jiite hata "mjinga WA kusini" itakufaa
Nitajiitaje mjinga wakati mimi ni tajiri?
 
Duniani kote, mapato yasiyoeleweka chanzo chake, lazima wahangaike na wewe.
Isitoshe, kiasi hicho cha pesa kwa Afrika siyo kidogo.
Hizo pesa ndogo sana, tunatuma na kupokea hizo pesa kila siku na hatujawahi kusumbuliwa.

Ni ngumu Kwa nchi kuanza kusumbuka na muamala ya 500m labda una kesi za wizi.

But sio rahisi serikali ikuhoji kisa 500m itakuwa serikali ya kipuuzi. Huo muamala sio wa kutisha
 
Nanukuu......
Kitabu cha “In the Name of the President: Memoirs of a Jailed Journalist” kilichoandikwa na Erick Kabendera, @kabsjourno kimeanza kuuzwa leo. Mwandishi anaeleza kuhusu kutekwa na kuuwawa kwa Ben Rabiu Focas Saanane, December 2016 alipigwa risasi na mwili wake kutupwa mto Rufiji.

View attachment 3189981View attachment 3189980
Tatizo lengo la kitabu ni kumchafua magufuli, Erick alikuwa na makosa hadi akafungwa, kitabu hiki kingeandikwa na mwandishi ambaye hana interest na magufuli kingefaa lakini kitabaki kama kitabu cha udaku na kinaweza mrudisha rumande kwa mara ya pili
 
Uongo.yaani magufuli ampige risasi yeye mwenyewe?haiwezekani na ni uongo kabisa.Bora angesema alikuawa na wasiojulikana angalau tungeamini na siyo kwamba magufuli mwenyewe eti alimpiga risasi Kwa mikono yake yenyewe.Kabendera acha uongo.Chuki zako za magufuli usimtungie uongo mzalendo wetu magufuli
😡
 
Sina uhakika ni kiasi gani. Lkn jua ya kuwa miamala yote ya pesa kutoka/kwenda nje, inamulikwa. Kabendera alikutwa kwenye akaunti yake pesa iliyotoka nje kama US$ 200,000. Ambayo haikuonesha alilipwa baada ya biashara gani.
Kwahiyo kalipwa tena?
 
Tuhuma nzito sana hii dhidi ya aliyewahi kuwa kiongozi mkubwa wa nchi. Anyway acha tuone mamlaka zitasemaje

Ila ninachokiona watu wamepata upenyo zaidi wa kuongea watakacho kutokana na udhaifu mkubwa wa aliyepo madarakani kwa sasa kwani wanajua kabisa hana uwezo wa kuwafanya chochote and the system is loose
 
Back
Top Bottom