Erick Kabendera: Mwendazake aliendesha genge la wahuni na alikusudia kumkamata Rais Mstaafu Kikwete

Erick Kabendera: Mwendazake aliendesha genge la wahuni na alikusudia kumkamata Rais Mstaafu Kikwete

Ilikuwa safi sana kwa Jpm Kuwakomesha wahuni wote walioifikisha hii nchi hapa ilipo
Mimi ni mmoja ya watu wanaoamini ni kweli utawala wa Kikwete ulikuwa mbovu na Magufuli alipoingia alikutana na mengi. Tatizo liko kwenye njia ambazo alikuwa anachukuwa kujaribu kufanya marekebisho. Njia za kihuni, za kisiri na zisizofuata sheria. Na mbaya zaidi akadhani kila anayemkosoa ni adui na anafaa kuawa.
 
Duh!

Ndio maana alisema kuna wastaafu wanawashwawashwa.

Huyu Bwana alikuwa ni mtu hatari sana!

Ukiangalia ile picha aliyokuwa amepiga magoti akiomba kura kwenye kampeni za 2020, unaweza hata kumuonea huruma na ukapata picha kuwa ni mtu mpole na humble, kumbe ni kinyume chake kabisa!

Niliwahi sema humu na leo narudia: Mwendazake alikuwa na kipaji kikubwa sana cha uigizaji, sema tu hakuingia kwenye hiyo sanaa ange-fit zaidi huko.
Ni wengi hawajui undani wa kutekwa kwa MO, na mashambulizi aliyokuwa anarusha yule mhuni mwanaharakati huru. Hata haya maandishi ya Kabendera ni sehemu ya ''undani'' wenyewe. Na kama ukijua undani, na kama wewe kweli ni mzalendo, mtanzania mwenye kutaka haki sana sana utaishia kusema: ''kumbe haya mafisi yalifikia hatua ya kuparurana kiasi hik! Basi tunahitaji katiba mpya haraka sana''
 
View attachment 2386088
Legacy inazidi kuzamishwa chini zaidi. Mwendazake alikuwa wa hovyo sana

====
Aliyoandika Kabendera

Wale mliouza mali zenu kupata pesa za kuhonga kusaidia plea bargain zenu zikubaliwe mjitokeze kutoa ushahidi. Wafanyabiashara mliopelekwa ofisi maarufu ya serikali, mkatishwa kwa mitutu ya bunduki wakati Mwendazake akiangalia kupitia CCTV, mkalazimishwa kutoa pesa mjitokeze.

Kuna mfanyabiashara maarufu alipitia mateso makali kwa kipindi cha miaka minne, ikiwemo kubinywa korodani, akilazimishwa aseme uongo kuwa alitoa dola milioni 100 kwa Rais Kikwete. Mwendazake alitaka kutumia ushahidi huo kumkamata Kikwete. Ni lazima atendewe haki.

Tuhuma dhidi ya Mwendazake kuanzisha na kuendesha genge la kihalifu nje ya mfumo wa serikali na kutoa maelekezo kwa genge hili kuwaua viongozi wa vyama vya upinzani, CCM na viongozi wakuu wastaafu ambao wangekuwa kikwazo kwake kutawala milele zichunguzwe pia.

Si mara ya kwanza zoezi kama hili kufanyika; Rais Mwinyi aliunda tume ya kupitia upya kesi zote ya uhujumu uchumi alizoziendesha Sokoine baada ya kuingia madarakani na kuna watu walirudishiwa mali zao.

Binafsi nimeombwa kuwasilisha maelezo ya maandishi kwa mamlaka husika kuhusu vitisho alivyovitoa Ndugu Biswalo dhidi yangu mara kwa mara baada kuachiwa huru na nimefanya hivyo.
Duu yaani yule jamaa aliona baada ya kumtoa Mkapa ilibidi ammalize na JK Ili abakie huru,aisee Dunia ina Siri hii..

Anyway Mungu ni fundi amejua kumkomesha aliyepanga mambo ya Hila za kudhuru gizani.
 
Sasa hayupo na hawezi chunguzwa, Saa 100 mwenyewe lazima alishiriki mambo yanayosemwa mfano ununuzi wa ndege nk

Haina maana kwa sasa,na viongozi wa sasa ni kama mwendazake tu ndio maana waliimba ccm ni ile ile
Pengine alijua ila sio kushiriki..Lisu mwenyewe anakiri kwamba hajawahi pata kashfa yeyote kumhusu Rais Samia.
 
Magufuli nikiongozi bora kuwahi kutokea kwenye Taifa hili.yaani hata mumchafue vipi amewakuna kunako takiwa kwani kumkamata kiongozi wa mafisadi nizambi

Nani aliyemchafua? Kuibuka kwa magenge ya wahuni(sabaya,DAB,Mwanaharakati huru etc) ,watekaji na kupora mali za wafanyabiashara ndio sisi tuliofanya? Fedha za maduka ya kubadilishia fedha walizopora ziko wapi? Nani aliyempiga tundu lissu risasi? Nani aliyempoteza Bensaa8?

Waliomteka Roma/MO? Ni watu wasiojulikana.
Waliompiga risasi Lissu? Ni watu wasiojulikana
 
NI kweli marehemu alikuwa na michezo ya kihuni.
Ila kwa Sasa haya unayofanya bwana kabendera hayana maana.
Yupo zake chato anajigeuza geuza.
Na kule alipo Hana smartphone
Wapo waliotekeleza huu ufala ndio anawalenga Kabendera.. Mwenda zake alikua anatoa maagiizo tuu.
 
Aibu hii sio Magufuli ni ya state nimetoa onyo. Mkitaka msifieni lakini kunajisi state hapana
Wapo viongozi wengi wa nchi waliofanya uhalifu wakiwa madarakani. Mambo hayo yakiwekwa wazi siyo aibu bali ndiyo uthibitisho wa uimara wa state yenyewe.
Hata hivyo, sina maana ya kwamba hili linalojadiliwa lina ushahidi wa kutosha kuthibitisha.
 
Mwendazake alipata urais kwa bahati tu , sio kwa kupangiliwa na kundi la ndani. Sasa hivi nafasi hutokea naturally, na ikitokea akaja mwingine asiye na genge kama hilo utawajibika tena.
Ndio maana uovu wa viongozi waliopita tangu wakiouza mashirika ya Umma kwa bei za kutupa na wale wa Richmond na EPA waliachwa ili kutoendeleza mlolongo wa kulipizana.
Bahati mbaya zaidi Mwendazake hayupo , wala huwezi kumlipiza na ikiwezekana basi Katiba ijayo iangalie makosa yaliyofanywa na viongozi kwa kutumua ofisi zao vibaya washtakiwe na kufilisiwa.
Hapa walio hai na familia zao wawajibike.
 
Hata huyo mkwere naye alivuruga na anajua hilo. Haya mambo ukiyaelewa kwa undani sana sana utasema: ''du mafisi kumbe yalifika hatua ya kusalitiana kiasi hiki?''
Politics 🙌, ishu ni kwamba Mwendazake bado hakuwa na mbinu za kijasusi za kumuondoa Mkwere, jamaa alikuwa na pupa + mihemuko na huu mchezo hautaki haraka wala hasira, mpaka hii ishu imevuja kwa kina Kabendera ni wazi jamaa hakuwa na watu wa uhakika mpaka siri zikavuja.
 
Back
Top Bottom