Erick Kabendera: Rais Samia “Thucydides Trap” haitakuacha salama

Baada ya Makonda kupewa nafasi kwenye chama chake, kelele za huruma juu ya CCM na viongozi wake imekuwa kubwa kana kwamba hawajui kwanini Makonda yuko pale.

Amewatoa relini wengi, focus imekuwa kwake kwenye kila tukio lake, na hapo ndio CCM anafanikiwa kwa ulaghai wake kwa wajinga.
 
I can't disagree...focus yote kwa Paulo badala ya kuweka mikakati ya uchaguzi wa local governments in 2024 na general elections in 2025....wakishindwa waje waseme wameibiwa!

Makonda is a decoy and it's working...!
 
Makonda hafai kupewa madaraka yoyote,kwa ili samia Amekosea japo hesabu zake ni kwenye uchaguzi ujao,
 
Huu uzi ni kwa wenye akili tu.

Mtu anapiga simu kwa Mawaziri anatoa maagizo, anasema wazi anatoa maagizo kwa Waziri Mkuu mambo ambayo hata Rais mwenyewe hafanyi alafu kesho akijifanya mtu fulani mnamkana.

Kuna jambo wamelitengeneza wenyewe na kuna siku litawarudia ndo akili zitakaa sawa.

Mwekezaji aliyepitia misukosuko ya kuteswa na makonda kipindi cha Rais Magufuli leo akiona makonda anawa summon mawaziri na wakuu wa Mikoa na Wilaya kamwe hawezi kuwa huru tena kuwekeza hela zake Tanzania.

Hapa ndo dhana ya consistency kwenye sera na matendo ya serikali / wanasiasa inapoingia.

Samia yuleyule anayehubiri 4R anawarudisha na kuwapa nguvu za kuendesha Serikali yake watu walewale waliosababisha alete 4R
 
Wanufaika wa ujanja ujanja nyie kina Kabendera hamuwezi kufurahiha style ya Makonda. Wanyonge ndio wananufaika wa maamuzi papo kwa papo. Nyie kina Kabendera tunawajua huwa mnatumika na watafuna Nchi kupiga kelele kwa kutumia kalamu zenu. Haya na kitabu chenu Cha am the state mmefikia wapi. Mtalipa gharama, muda ni Mwalimu
 
I can't disagree...focus yote kwa Paulo badala ya kuweka mikakati ya uchaguzi wa local governments in 2024 na general elections in 2025....wakishindwa waje waseme wameibiwa!

Makonda is a decoy and it's working...!
Kabisa, kafanikiwa kirahisi sana, wapinzani ndio wamekuwa spika yake ya kila anachofanya.

Siku watakayojua kuwa adui yao mkubwa ni CCM na si wateuliwa ambao leo wapo kesho hawapo watafanikiwa.
 
Acheni unafiki wa kijinga na kitoto sana,

Haya majungu yenu na huu wivu juu ya Makonda mtaongea na kupata sonona bure tu
 
Oyaa, Sisi Watanzania tunamuelewa sana Makonda. Acha apige kazi.

Wewe unajulikana toka mwanzo, una vita na Mwendazake pamoja na wachapakazi wote walioaminiwa naye
 
Makamu Mwenyekiti ni mgonjwa, amechelewa sana kujiuzuru
 
I hope things have already fallen apart as long the emerging Hitler has been given full throttle power of attorney to discombobulate the status quo of nominated oficials with clandestine mission of overtaking the throne
 
Je, kuna ukiukwaji wa katiba kwa Makonda kutoa maagizo kwa mawaziri na watendaji wengine wa serikali? Nijuavyo kazi ya chama ni kuisimamia serikali na hicho ndicho akifanyacho katibu mwenezi wa CCM. Tukumbuke kipindi Cha kikwete Kinana alitembea maeneo mbalimbali ya Tanzania na kuja na hoja ya mawaziri Mizigo.
 
Makonda huyu huyu alieshindwa na Ndugulile Kigamboni tu, tena akiwa mkuu wa mkoa wa Dar na raisi Magufuli.

Ndio anaweza mtisha Samia raisi wa nchi nafasi yake.

Akili zetu zinatutosha wenyewe watanzania.
 
Mkuu weka hapa job description yake tukufafanulie kama amekiukaa au la!
 
Ka flag anawasha kuteuliwa Makonda, alitaka nani ateuliwe?
 
Mi sioni kosa la Makonda,anachofanya ni kukijenga chama,na kukieneza,sasa akikuta sehemu mambo hayaendi inavyotakiwa,kuna shida yeye kuwasiliana na mawaziri au waziri mkuu?
Sioni shida yake.
 
Oyaa, Sisi Watanzania tunamuelewa sana Makonda. Acha apige kazi.

Wewe unajulikana toka mwanzo, una vita na Mwendazake pamoja na wachapakazi wote walioaminiwa naye
Birds of the same feathers fly together! akili za makonda akiwa nazo mtoto wangu namuua mapema
 
Huyu Kabendera yuko kwenye Payroll ya mabeberu hana jipya kwa watu wenye akili
Hii nchi bwana, mnawaita wanaowakosoa wapo kwenye payroll ya wazungu wakati nyie mliopo serikalini kila siku mnatoa mikataba mibovu kwa mabeberu ili mpate commission za pembeni!!
 
Wakati huo visima tunamilili sisi huyo tembo tuone atatoa wapi hayo maji
 
Huyu Kabendera yuko kwenye Payroll ya mabeberu hana jipya kwa watu wenye akili
Inawezekana upo sahihi, lakini la msingi hapa si kuweka focus kwa Kabendera mwenyewe, bali kwenye maudhui au hiyo nadharia ya “Thucydides Trap”. Mimi nitajikita kwenye nadharia.
Nakubaliana na kuwepo kwa hiyo nadharia katika maswala ya uongozi. Ila kuiepuka au kuwa sahihi kufikiri kuwa kwa 100% hutafanya makosa hayo kama kiongozi ni Ngumu sana.

Nitoe mifano kadhaa kwa marais mbali mbali Afrika waliopatikana katika mtego huo:
1) Milton Obote: Alimuamini Idi Amin, baadae kampindua. Obote aliporudi tena madarakani akamuamini kijana mdogo Yoweri Museveni, Naye baadae kamtosa Obote.
2) Mela Zinawe-Ethiopia: Chama chake kimemkuza Abbe Ahmed tokea akiwa chipukizi na kuaminiwa. Chama kilipomchagua Abbe Ahmed kuwa Rais, kawatosa viongozi wenza wote wa Mela Zinawe na hata kuanzisha vita na kundi la Mela zinawe. Hii imepelekea kuiweka Ethiopia yote katika machafuko.

List ni kubwa. Ninachotaka kusema ni kuwa hakuna mwenye uhakika katika hilo ulisemalo na mwenendo wa Makonda. Moja ninalolijua ni kuwa Rais Samia huwa hata hana haya, kuteua na kupangua. Akikuteua usifikiri ndio umefika, jicho lake lipo kwako kwa masaa 24. Hakuna anayejua kuwa Makonda atadumu kwa muda gani, hata yeye mwenyewe hajui. Ndio maana kaamua kucheza ajuavyo, litalotokea na litokee.
Kumbuka, Rais Samia aliwakumbatia viongozi wengi sana toka aingie madarakani, na wengi kati yao kawabwaga baada ya kuonyesha wana uroho wa madaraka. Kwa hili sina wasiwasi na Rais Samia, kwani “Thucydides Trap” imezingatiwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…