Eternal Punishment cannot be understandable by any one

Eternal Punishment cannot be understandable by any one

"...Wanakuuliza khabari za Roho, waambie hiyo ni ilmu yake Mwenyezi Mungu, na Ilmu mliopewa nyinyi ni kidogo sana..."
QUR'AN.

"Wanakuuliza je tukishakufa na kusagika mifupa tutarudi tena kwenye uzima?
Waambie je hawakuona mfano wa ardhi iliyokufa kwa ukame na hata mimea iliyopandwa ikanyauka yote? Kisha tukateremsha maji kutoka mawingu, ardhi ikarudi kua hai na mimea ikastawi? Hiyo ni alama tosha kwa wenye akili timamu...."

QUR'AN.

".... Hata kama tungefungua mbingu, wakawa wanapanda na kushuka (kwenda mbinguni na duniani, muda wowote) bado wangesema hakuna lolote, hiki ni kiini macho tu...."

QUR'AN.

"Wanakuuliza Kiyama kitakuja lini, waambie hivi punde tu, hiyo ni ahadi ya Mwenyezi Mungu kwa viumbe wake haina shaka ndani yake...."

QUR'AN.

Kwa hivyo ndugu zangu, mmeona kuna watu kabla yenu walikua wanauliza maswali kama haya mnaojiuliza nyinyi na pengine kuzidi wako wapi sasa hivi? Wamerudi kwa muumba wao na huko wameshapata majibu ya maswali yao,

Hivyo na wewe usiyeamini au unayeamini, ishi hivyo hivyo ukijua kua utakufa na utapata majibu ya maswali yako.
Hakuna shaka juu ya hilo.
 
Mambo mengine nikitafakari,I wish hata nisingexist..am sorry Mungu ila I js don't understand why

Mind your language LadyRed, ni kweli unatamani usinge exist.?Kuna bongofleva mmoja aliwahi kuimba 'aliwazalo mjinga ndilo humtokea'. Hii statement ni ya kweli ktk nyanja zote.
 
Hakuna kitu kama moto wa milele. Hizo story tu vitabu vya dini vinawaambia mambo kimafumbo au lugha ambayo ni ambiguous. Waliandika wana~sodoma na ghomorrah watachomwa moto wa milele, unataka unambie hadi leo bado wanawaka? moto wa milele ni neno ambiguous sana, linaweza kua linamaanisha unachomwa unapotea milele, tofauti na ile kufa then ukafufuliwa. Sijui kama unapata my point? Kwa lugha rahisi kabisa hakuna anayeelewa chochote kile.

Alafu dini ina complications nyingi tu, utamlaumu vipi mtu kazaliwa Pagan? mtu kazaliwa Mkristo, Muislamu? nani mkweli kati yao? Una uhakika gani maana kila moja anaamini anachokiamini ndio sahihi. In other words wote tunajifanya tunajua ila hakuna anayejua ukweli, wote tunaendaenda tu. Presence ya supernatural power yaweza kuwepo au ikawa coincidence tu, no one knows kwa kua hakuna aliyewahi experience.
you are too conclusive..
 
11 kwa maana hakuna upendeleo kwa Mungu.

12 Kwa kuwa wote waliokosa pasipo sheria watapotea pasipo sheria, na wote waliokosa, wenye sheria, watahukumiwa kwa sheria.

13 Kwa sababu sio wale waisikiao sheria walio wenye haki mbele za Mungu, bali ni wale waitendao sheria watakaohesabiwa haki.

14 Kwa maana watu wa Mataifa wasio na sheria wafanyapo kwa tabia zao yaliyo ndani ya torati, hao wasio na sheria wamekuwa sheria kwa nafsi zao wenyewe.

15 Hao waionyesha kazi ya torati iliyoandikwa mioyoni mwao, dhamiri yao ikiwashuhudia, na mawazo yao, yenyewe kwa yenyewe, yakiwashitaki au kuwatetea;

16 katika siku ile Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu, sawasawa na injili yangu, kwa Kristo Yesu.Wayahudi na Sheria
Look!

Let's say unazaliwa katika familia ya wapagani (wasiojua Mungu) then unaishi maisha ya taabu na shida na vipindi vifupifupi vya raha.

Unaishi miaka kadhaa (labda 43) hivi, ukiwa umeelemewa na msongo wa mawazo unaotokana na matatizo mbalimbali, magonjwa na hussles. Then unakufa bila kujua au kusikia kuhusu Mungu.
Nawasilisha!
 
Look!

Let's say unazaliwa katika familia ya wapagani (wasiojua Mungu) then unaishi maisha ya taabu na shida na vipindi vifupifupi vya raha.

Unaishi miaka kadhaa (labda 43) hivi, ukiwa umeelemewa na msongo wa mawazo unaotokana na matatizo mbalimbali, magonjwa na hussles. Then unakufa bila kujua au kusikia kuhusu Mungu (Au hata kama umesikia).

Then gafla kiti cha enzi kinatokea, juu yake yupo Mungu mwenye upendo wote, mwenye uwezo wote. Anakuhukumu moto wa milele na milele kwa makosa uliyofanya ukiishi hapa duniani (ambapo napo ulikuwa na baadhi ya wema). Moto usiozimika, unounguza mara dufu ya moto wa kawaida (kwa mujibu wa vitabu vya dini). Hivi hii kitu nyie mnaelewa logic yake?

Hata binadamu tu hatujawahi kuwa na kifungo cha gerezani cha milele, iweje Mungu awe na adhabu kali namna hiyo? Can anyone tell me? I just can't understand!

Nawasilisha!

Hakuna mungu huyo. Idea yake inajipinga yenyewe na hivyo haiwezi kuwepo.
 
"...Wanakuuliza khabari za Roho, waambie hiyo ni ilmu yake Mwenyezi Mungu, na Ilmu mliopewa nyinyi ni kidogo sana..."
QUR'AN.

"Wanakuuliza je tukishakufa na kusagika mifupa tutarudi tena kwenye uzima?
Waambie je hawakuona mfano wa ardhi iliyokufa kwa ukame na hata mimea iliyopandwa ikanyauka yote? Kisha tukateremsha maji kutoka mawingu, ardhi ikarudi kua hai na mimea ikastawi? Hiyo ni alama tosha kwa wenye akili timamu...."

QUR'AN.

".... Hata kama tungefungua mbingu, wakawa wanapanda na kushuka (kwenda mbinguni na duniani, muda wowote) bado wangesema hakuna lolote, hiki ni kiini macho tu...."

QUR'AN.

"Wanakuuliza Kiyama kitakuja lini, waambie hivi punde tu, hiyo ni ahadi ya Mwenyezi Mungu kwa viumbe wake haina shaka ndani yake...."

QUR'AN.

Kwa hivyo ndugu zangu, mmeona kuna watu kabla yenu walikua wanauliza maswali kama haya mnaojiuliza nyinyi na pengine kuzidi wako wapi sasa hivi? Wamerudi kwa muumba wao na huko wameshapata majibu ya maswali yao,

Hivyo na wewe usiyeamini au unayeamini, ishi hivyo hivyo ukijua kua utakufa na utapata majibu ya maswali yako.
Hakuna shaka juu ya hilo.
sasa hayo majibu huko yatatusaidia nini, kwanini hakuweka kila kitu waziwazi
 
Look!

Let's say unazaliwa katika familia ya wapagani (wasiojua Mungu) then unaishi maisha ya taabu na shida na vipindi vifupifupi vya raha.

Unaishi miaka kadhaa (labda 43) hivi, ukiwa umeelemewa na msongo wa mawazo unaotokana na matatizo mbalimbali, magonjwa na hussles. Then unakufa bila kujua au kusikia kuhusu Mungu (Au hata kama umesikia).

Then gafla kiti cha enzi kinatokea, juu yake yupo Mungu mwenye upendo wote, mwenye uwezo wote. Anakuhukumu moto wa milele na milele kwa makosa uliyofanya ukiishi hapa duniani (ambapo napo ulikuwa na baadhi ya wema). Moto usiozimika, unounguza mara dufu ya moto wa kawaida (kwa mujibu wa vitabu vya dini). Hivi hii kitu nyie mnaelewa logic yake?

Hata binadamu tu hatujawahi kuwa na kifungo cha gerezani cha milele, iweje Mungu awe na adhabu kali namna hiyo? Can anyone tell me? I just can't understand!

Nawasilisha!

Mungu ni mwingi wa huruma. Na ni hakimu wa haki. Hukumu yake hakuna awezaye kuijua ingawa viongoz wetu wa dini hasa wale 'vibrant' huwa kwa namna moja wanashndwa elewa hiyo hukumu ya Mungu. Ndo maana ktk kuelewa kdogo huko kuna wale ndugu zetu wakatolik wao wanaamn kuwepo kwa adhabu kali kwa wale ambao walikua wema lakin walikua pia na uovu wanasema watu kama hao c sahh kuhukumiwa milele kwenye huo moto ila watapitia utakaso ambapo kuna mateso kadhaa ili hiyo nafsi ipate kutakasika kuingia paradiso. Lakn pamoja na hekma hz bado Mungu anabak kuwa mwenye upendo,huruma na haki.
 
nipo ili niishi.
Ukiwa umetoka wapi mpk uje hapa Duniani kuishi?
Unaishi kwa sababu gani?
Na kama upo hapa kwa ajili ya kuishi tu, kwanini unakufa?
Ukifa waenda wapi?
Huko kuna nini?

Je waujua mwanzo wako?
Je waujua mwisho wako?

Jibu kwanza hayo hlf tutaendelea.
 
Mind your language LadyRed, ni kweli unatamani usinge exist.?Kuna bongofleva mmoja aliwahi kuimba 'aliwazalo mjinga ndilo humtokea'. Hii statement ni ya kweli ktk nyanja zote.
Nkielezea maybe hautanielewa,life can be difficult sometimes
 
Mpagani ni mtu au watu wasioamini uwepo wake Mungu au ni mtu au watu wasioamini Dini yoyote ila wanaamini uwepo wa Mungu? Naomba kujua.
 
Mpagani ni mtu au watu wasioamini uwepo wake Mungu au ni mtu au watu wasioamini Dini yoyote ila wanaamini uwepo wa Mungu? Naomba kujua.
Wapagani ni watu wasioamini dini hizi zilizopo ila wanaamini uwepo wa Mungu
 
Eternal punishment!! Hata kama ningekuwa muamini wa dini, hii doctrine ninsingeamini kwasababu nyingi tu. Naona imetegenezwa kufanya watu waogope.
 
Zaburi ya 145
1Ee Mungu wangu, Mfalme, nitakutukuza, Nitalihimidi jina lako milele na milele.
2 Kila siku nitakuhimidi, Nitalisifu jina lako milele na milele.
3 Bwana ndiye mkuu mwenye kusifiwa sana, Wala ukuu wake hautambulikani.
4 Kizazi kwa kizazi kitayasifu matendo yako, Kitayatangaza matendo yako makuu.
5 Nitaifikiri fahari ya utukufu wa adhama yako, Na matendo yako yote ya ajabu.
6 Watu watayataja matendo yako ya kutisha, Nami nitausimulia ukuu wako.
7 Watalihubiri kumbukumbu la wema wako mkuu. Wataiimba haki yako.
8 Bwana ana fadhili, ni mwingi wa huruma, Si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema,
9 Bwana ni mwema kwa watu wote, Na rehema zake zi juu ya kazi zake zote.
10 Ee Bwana, kazi zako zote zitakushukuru, Na wacha Mungu wako watakuhimidi.
11 Wataunena utukufu wa ufalme wako, Na kuuhadithia uweza wako.
12 Ili kuwajulisha watu matendo yake makuu, Na utukufu wa fahari ya ufalme wake.
13 Ufalme wako ni ufalme wa zamani zote, Na mamlaka yako ni ya vizazi vyote.
14 Bwana huwategemeza wote waangukao, Huwainua wote walioinama chini.
15 Macho ya watu wote yakuelekea Wewe, Nawe huwapa chakula chao wakati wake.
16 Waufumbua mkono wako, Wakishibisha kila kilicho hai matakwa yake.
17 Bwana ni mwenye haki katika njia zake zote, Na mwenye fadhili juu ya kazi zake zote.
18 Bwana yu karibu na wote wamwitao, Wote wamwitao kwa uaminifu.
19 Atawafanyia wamchao matakwa yao, Naye atakisikia kilio chao na kuwaokoa.
20 Bwana huwahifadhi wote wampendao, Na wote wasio haki atawaangamiza.
21 Kinywa changu kitazinena sifa za Bwana; Wote wenye mwili na walihimidi jina lake takatifu milele na milele.
 
Kama ambavyo unajituma kutafuta pesa na maisha, juhudi kama hiyo ungeifanya kumtafuta Mungu utampata, utamtambua tu.
If god does not like the way I live .let him tell me not you

Nitumie nguvu za nn kumtafuta,
 
If god does not like the way I live .let him tell me not you

Nitumie nguvu za nn kumtafuta,
Kwa kila umma, Mungu ametuma mjumbe ili awafikishie ujumbe viumbe vyake.
Hili pia hulifahamu?
Kama hulifahamu soma vitabu hivi.
1. faith and progress link http://www.al-dawah.dk/boger/engelske/pdf/Faith_and_Progress.pdf
2. The true religion of God link http://www.islamreligion.com/ebooks/True-Religion-of-God.pdf
3. Quran link Al-Qur'an al-Kareem - القرآن الكريم hii ya kiswahili link Sikiliza Qurani Tukufu, Maana yake na Maelezo
Ingine ya kiswahili. Qur'ani Tukufu

Baada ya kuvisoma vitabu hivyo jipime kama unapenda kweli unavyoishi.

 
Kwa kila umma, Mungu ametuma mjumbe ili awafikishie ujumbe viumbe vyake.
Hili pia hulifahamu?
Kama hulifahamu soma vitabu hivi.
1. faith and progress link http://www.al-dawah.dk/boger/engelske/pdf/Faith_and_Progress.pdf
2. The true religion of God link http://www.islamreligion.com/ebooks/True-Religion-of-God.pdf
3. Quran link Al-Qur'an al-Kareem - القرآن الكريم hii ya kiswahili link Sikiliza Qurani Tukufu, Maana yake na Maelezo
Ingine ya kiswahili. Qur'ani Tukufu

Baada ya kuvisoma vitabu hivyo jipime kama unapenda kweli unavyoishi.


Msicho elewa kuwa hata hivyo vitabu viliandikiwa na watu
Inshort n vitabu.vya kusadika tuu..

Napo amua kuvisoma.navisoma sawa navyo soma vitabu vingine..hakuna.cha zaid

Nacho ambulia n yale mazur na nayatumia ktk maisha ila sina huo muda na sion sababu ya kuabudu huyu mtu mmwetae mungu/allah
 
Back
Top Bottom