Ethiopia inaenda kuvunjika kama Yugoslavia

Mkuu hebu fanya maarifa umwage tena huo uzi, najua wenye roho mbaya hawapo tena.
 
Kabla utumwa haujapigwa marufuku ethiopia. Hao wa kaskazini (watigray na Amhara) walikuwa wakifanya hawa wa kusini , weusiweusi, waoromo kama watumwa. Na Ethiopia wamechelewa sana kukomesha utumwa, mwaka 1931.
 
Kabla utumwa haujapigwa marufuku ethiopia. Hao wa kaskazini (watigray na Amhara) walikuwa wakifanya hawa wa kusini , weusiweusi, waoromo kama watumwa. Na Ethiopia wamechelewa sana kukomesha utumwa, mwaka 1931.
Japo Oromo ni wasomi wengi maprofesa ila wanadharaulika sana na makabila ya Tigray na Amhara. Yani ni barbaric yako hovyo hovyo tu. Utakuta muoromi akijenfa nyumba juu chini anapaka rangi ya kijani.

Tigray ni smart hasa wanaume ni watanashati na maplayers. Tangu udogoni wanafundishwa hao ni masterace kama ndugu zetu akina PK.

Kwa uchache wao waliwamobilize wa Ethiopia wakangia msituni na kumngia Mengistu Haile Mariam.

Inasadikika sanduku la agano lile la Musa liko Tigray (Aksum). Mji wao mkuu huko Makele
 
Ndicho chadema walitaka kuigawa nchi na kutaka ili baadae tusambaratike kimakabila. Unapotengeneza umajimbo unaandaa nchi kusambaratika.
Siyo kweli mkuu, majimbo huwa yanashika nchi, ni serikali tu ziheshimu mipaka yake. Pengine leo bila majimbo nchi kama Ethiopia na Nigeria zingekuwa zimeshasambaratika au zipo kwenye vita. Kuna nchi kama Burma zinataka kuingia kwenye mfumo wa majimbo kuepuka kusambaratika. Mtu akiona anadhurumia au anatengwa ndiyo hushawishika kujitenga.
 
Afu eti chadema wanataka watugawe kwa majimbo, ndo maana tuliwapiga spana mbaya!
 
Ndicho chadema walitaka kuigawa nchi na kutaka ili baadae tusambaratike kimakabila. Unapotengeneza umajimbo unaandaa nchi kusambaratika.
Wakati CHADEMA wakitaka utawala wa kimajimbo wenye lengo la kuwaunganisha wananchi wote katika majimbo machache ili kuwapa wananchi uhuru wao wa kufanya maendeleo, CCM kwa karibu miaka sitini wameendelea kuigawa nchi kwa mikoa zaidi ya 27 na wilaya zaidi ya 120 mpaka kufikia sasa wakiweka mipaka iliyozingatia kabila, asili na tamaduni zao.

Sasa tafakari ndani ya box na nje ya box kabla ya kutoa Comment yoyote hapa JF.
 
Mkuu ukipata muda fanya Mpango utushushie Uzi kuhusu nchi ya Ethiopia (Uso ulioungua) na uhasama wao wa kikabila na hata kisiasa.
 
Tanzania hakuna kabila lenye watu million 30 Kama lilivyo kwa oromo, au watu million 18 Kama ilivyo kwa amhara acha uongo
Suala sio kabila acha ujinga, suala ni majimbo yenye mamlaka na jeshi. Hayo majimbo Ethiopia yana majeshi yake na watawala wanaochaguliwa na wananchi na wanamamlaka ya kukatalia hata serikali kuu.

Ndio upumbavuu waliotaka kuanzisha Chadema
 
Tofautisha mikoa na majimbo yenye mamlaka. Hata kama mikoa imegawiwa kwa makabila lakini bado viongozi wake wanasimamia serkali kuu tofauti na autonomy wanayoitaka Chadema ambayo italeta mvurugano na kugawa nchi. Mkuu wa mkoa ni mteule wa serikali kuu anayetekeleza mikakati ya serikali kuu akiwa TAMISEMI
 
mi nadhani shida kubwa ni hao wa Tigray waliozoea kukalia madaraka na kujipatia mali, sasa wanaona wanaonewa.
Zenawi aliwabeba Sana hawa Tigray, ila huyu Abiy amekuwa akijaribu sana kuliweka hili kabila chini ya ushawishi wake bila mafanikio.

Ila kwa hii njia aliyoichagua Abyi huenda ikaleta maafa zaidi na kuzidisha uhasama.
 
Suala sio kabila acha ujinga, suala ni majimbo yenye mamlaka na jeshi. Hayo majimbo Ethiopia yana majeshi yake na watawala wanaochaguliwa na wananchi na wanamamlaka ya kukatalia hata serikali kuu.

Ndio upumbavuu waliotaka kuanzisha Chadema
Mkuu ndio Ethiopia ni fideral state. Lakini swala ukabila ndio chanzo halisi ya uhasama. Na hii ilitokana baada ya Mengistu Haile Mariam kupinduliwa na TPLF (Tigray) ikiongozwa na, akina Melez Zinawi.

WAtigray kwa asili wanajpenda na kujikuza japo niwachache. Walipichukua mamlaka wakaconsoldate power na kuhodhi Mali nyingi na pesa. Na kuwadharau na kuwauwa wa Oromo wengi na kuwasweka ndani.

Jeshi lote la Ethiopia lilikuwa chini ya Tigray hadi Abiy alipoingia.

Melez Zenawi alipokufa Tigreans walishikwa na hofu sana wakijua genocide itatokea.

Kosa ambalo Melez Zenawi alifanya na kuacha ni vitambulisho vya taifa national IDs Ethiopia vinaonyesha ama kuandikwa kabila lako.

Kama Dayaspora tu ya waEthiopia wanachukiana na hawawezi kukukutana kujadiliana mambo ya nchi yao kwa pamoja mikutano yao ipo kimakabila tu. Hata Ethiopian new year hawasherekei pamoja. Pia Ethiopian Christmas (Orthodox Christmash) awasherekeipamoja.

Ethiopia is a divided nation long time ago since the death of Melez sasa hivi kila Jimbo lina bendera yake. Wa Oromo wanata bendera yao ba Addis ni yao Nazareth/ adanma na awasa ni ya kwao kuna sehemu addis ukiongeleshwa kioromo usijibu na waone kitambulisho ni tigrai wanakucuchinja.

Gondar na Bahir Dar ni ya amhara

Tigray yote na Aksum ni ya Watigrai.
 
Kuna 'wapare wa Ethiopia ama wakinga wa Ethiopia' kabila la Gurage lugha yao ni cushitic. Yani ni mabahiri balaa mpare ni cha mtoto. Karibia wote ni Waislamu. Na ni wafanyabiashara wazuri sana hasa za maduka magenge na migahawa na gesti.

Gurage hata kama ana hela utakuta anakula mlo mmoja kubana Matumizi. Ila ni wakarimu na liberals.

Kuna hawa Hafar kutoka arar wanaume wao wana mila za kuweka mitindo ya nywele za ajabu ajabu
 
Swadakta KABISA...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…