Tetesi: EU waanza kujitoa rasmi? KfW wajitoa kusaidia huduma za mama na mtoto

Waondoke tu, kodi inatosha. Mtu aje kwako halafu akupe masharti ya kubweka kama jogoo ndo akusaidie, hapana kwa kweli
Kataa misada yote ya wazungu tuone kama hiyo Kodi inatosha
 
Sababu kubwa za wazungu kuinyima Tanzania misaada na kufikiria kuiwekea vikwazo ni udikteta pamoja na kuminya demokrasia kurudia chaguzi kwa gharama kubwa pasipo sababu ya msingi, kuwapiga Risasi Wapinzani kuwabambikia kesi Wapinzani na unyanyasaji wao wote
 
Waondoke tu, kodi inatosha. Mtu aje kwako halafu akupe masharti ya kubweka kama jogoo ndo akusaidie, hapana kwa kweli
labda kama hujui bajeti yetu 65 tunategemea wahisani.
 
Nafikiri hii ndio sustainability inayohitajika kwa Taifa tuweze kupiga hatua hata kama ni kidogo kidogo kwa step.
Kuna watu walitaka wanyonye mpaka wanaingia kaburini au afe au mama afe ndio iwe mwisho kunyonya. Program zingine ni pilot tu, kisha tunaachiwa wenyewe. Sasa tutajifunzaje au lini tukisaidiwa maisha yote?!
Ni sawa wameondoka, watakuja kutuangalia nu vipi tumeuendeleza, tumekwama wapi na kwanini.
 

Wewe ndiyo unaefikiri kusaidiwa wewe familia yako ndiyo utapata maendeleo.unasadiwa na ka nchi km ebelgiji kanakolingana au kuzidiwa na hifadhi ya selou. Hajui km misaada ndiyo umasikini wetu. Waarabu ushoga ni kunyongwa nchi nyingine ni kifungo cha maisha. Misaada gani inayotaka tuache utamaduni na ustaarabu wetu? misri wapinzani na waandishi wa habari wamefungwa mbona hawapewi masharti? Paul Kagame anafunga wapinzani hovyo mbona hakuwekewa vikwazo?
 
Hahahahahaha

Biashara haramu ipi? Nimekuuliza swali nijibu ili nishawishike na mawazo yako maana ninachokiona kutoka kwako ni kwamba umekaririshwa ushoga ushoga kutoka kwa hao wanasiasa uchwara
We nae walewale tu nnaona umeanza kutangaza biashara haramu
 
Lile fuko la wajerumani lililokuwa linasaidia huduma za mama na mtoto kwenye idara ya afya hapa nchini hasa mawilayani wametangaza kusitisha huduma hiyo 31.12.2018.

Hilo ni pigo kwa nchi yetu.

Wenye kuwadharau EU sasa ndiyo mjiandae.
wewe huwezi kuchangia huduma hiyo.acha umasikini Wa akili
 
Wameona hawapati faida time hii, wazungu wana mahesabu makali sana, sijui kwa nn wanawaitaga wahisani wakati ni hizo vitu ni biashara
Hivi nchi kama Dernmark, Norway, Sweden, Japan, Germany wanafaidika nini toka Tanzania.

Tusiwe wendawazimu wa kuamini kuwa kila anayekupa kitu ni lazima apate kitu toka kwako. Kwa mfano wewe unapompa ombaomba wa barabarani 1,000, huwa unatarajia upate nini toka kwa huyo ombaomba?
 
Hawa watu wamedemand vitu vingi sana kutoka serikali yetu..lakini sisi tumesimamia hoja moja tu ya ushoga..mengine tuko kimya..Mbona utawala wa JK ulikuwa hauruhusu ushoga lakini mbona waliendelea kutoka misaada..
 
hivi dozi ya ARV huwa ni sh ngapi?
Sijui ni kiasi gani lakini naambiwa dawa zinazoongoza kwa uaghali ni za:
1) ARV
2) Chanjo
3) Kifua Kikuu
4) Saratani

Na zote hizo huwa tunapewa ndiyo maana zinatolewa bure.

Wake wendawazimu wa kushangilia kila kauli ya Rais hata kama ni ya kipuuzi hawana uwezo wa kusaidia kutoa japo panadol za bure kwa kijiji kimoja.
 
Hapo sasa wanapoambiwa kuwa ni bure wanadhani ni bure kweli kumbe yanakuwa yamelipiwa na wafadhili
 
Hapo ndiyo ujue kuwa hayo mengine 14 yaliyobakia ni mwiba mkali kwao ndiyo maana hawayagusii
Hawa watu wamedemand vitu vingi sana kutoka serikali yetu..lakini sisi tumesimamia hoja moja tu ya ushoga..mengine tuko kimya..Mbona utawala wa JK ulikuwa hauruhusu ushoga lakini mbona waliendelea kutoka misaada..
 
nyie mnaosema waende tu Tanzania inajiweza itafanya mambo peke yake...mie hii thread naisubscribe ,hapa tulipo tu tumebanwa na Magufuli,misaada ikikatwa mjue tutakatwa kodi hata kwenda chooni...think,people think...
 
Wewe mwenyewe kula kulala na unamtegemea shemeji ili uishi utayaonaje magumu ya nchi hii?
Nonsense,were huwezi kuchangia huduma hiyo.acha umasikini Wa akili
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…