EWURA: Nchi ina hifadhi ya Mafuta inayojitosheleza, Petrol inatosha kwa siku 19 na Diesel siku 18

EWURA: Nchi ina hifadhi ya Mafuta inayojitosheleza, Petrol inatosha kwa siku 19 na Diesel siku 18

Mkurugenzi mkuu wa EWURA Dr James Andilile amewataka hofu Wananchi kwa kusema Nchi ina hifadhi ya kutosha ya Nishati ya Mafuta

Dr Andilile amesema kuna Hifadhi ya Petrol ya kutosha siku 19 na Diesel ya kutosha siku 18.
---

View attachment 2738849
Mkurugenzi wa EWURA Dkt. James Andilile
Mamlaka ya udhibiti wa Nishati nchini Tanzania (EWURA) imekifungia kituo vya MATEMBA kilichoko Tuliani na CAMEL OIL kilichopo Msamvu Mkoani Morogoro kwa kipindi cha miezi sita kujihusisha na Biashara ya uuzaji mafuta kwa kile ambacho EWURA imedai ni kwenda kinyume na taratibu zinazoendesha Biashara ya mafuta.

Mkurugenzi wa EWURA Dkt. James Andilile amesema Nchi ina hifadhi inayojitosheleza kwa Nishati ya mafuta ambapo amesema kwa upande wa Petrol nchi ina akiba ya Nishati hiyo ya kutumika kwa siku 19 na upande wa Diesel Nchi ina akiba ya kutumika kwa siku 18 hivyo wananchi wasiwe na wasiwasi kuhusu upatikanaji wa Nishati hiyo.

Source: Jambo TV
Ni hatua nzr, ningeomba mzungeke Hadi sheli za ndani zaid kama huko geita, kilombero, katavi Kuna ujinga mwingi sna muwajibishe hata kufutia leseni maana wanakwamisha nchi
 

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati (EWURA) Dkt. James Andilile amesema hayo na kufafanua kuwa Petrol iliyopo inatosheleza matumizi ya siku 19 na Dizeli ipo ya kutumika kwa siku 18.

Aidha, EWURA imevifungia kwa miezi 6 Vituo 2 vya Mafuta ambavyo ni Camel Oil na Mtemba vilivyopo Msamvu na Turiani Morogoro huku Kituo GBP cha Ipuli Tabora kikifungiwa kwa muda usiojulikana baada ya kutuhumiwa kuficha Mafuta.

Takwimu za Mahitaji ya Mafuta Nchini zinaonesha Tanzania inatumia Lita Milioni 4.5 za Petroli kwa siku na Dizeli Lita Milioni 6.6 kwa siku.
 
View attachment 2739153
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati (EWURA) Dkt. James Andilile amesema hayo na kufafanua kuwa Petrol iliyopo inatosheleza matumizi ya siku 19 na Dizeli ipo ya kutumika kwa siku 18.

Aidha, EWURA imevifungia kwa miezi 6 Vituo 2 vya Mafuta ambavyo ni Camel Oil na Mtemba vilivyopo Msamvu na Turiani Morogoro huku Kituo GBP cha Ipuli Tabora kikifungiwa kwa muda usiojulikana baada ya kutuhumiwa kuficha Mafuta.

Takwimu za Mahitaji ya Mafuta Nchini zinaonesha Tanzania inatumia Lita Milioni 4.5 za Petroli kwa siku na Dizeli Lita Milioni 6.6 kwa siku.
 
Mafuta yenyewe wananunua kwa ‘bulk procurement’ wote wanatoa order kwa siku moja.

Lead time ya kuleta mafuta ni siku 26, halafu wewe unaweka inventory ya siku 16.

Hela yenyewe ya kuagizia mafuta wafanya biashara hawana, kwa hivyo volumes za kuagiza pia zinapungua.

Soon tunaenda tengeneza matatizo ya Bangladesh kukosa hadi hela ya kuagiza mafuta kabisa.

Amtoe na huyo Majaliwa, hilo jumba bovu lianguke haraka. Si anataka vijana yeye, hawa-hawa waliotengeneza shida ya umeme TANESCO halafu wanamuongopea wananchi wameilewa sana TANESCO mpya huku wakimuonyesha upuuzi wao kwenye TV na kupeana tuzo za upuuzi eti shirika lililofanya turnaround.

Hakuna raisi wa nchi hapo, hilo ndio tatizo halisi; mengine matokeo tu ya uongozi wake.
Kazi ipo huku Tz.
Kazi tunayo.
 
Ni aibu na fedheha msomi wa PhD mwenye nyadhifa aliyotunukiwa kuongoza taasisi kubwa ya namna hiyo alafu anakuja kuzungumzia swala la siku dhidi ya uhifadhi wa mafuta mbele ya hadhira na dunia kwa ujumla ikiwa inakutazama, kukusoma na kukusikiliza.... teh! teh! Eti siku
Dahh! Sisi bado sana! Alafu kuna mjinga anasema jeshi letu ni la sita (6) duniani... vitu nyeti kama hivyo ambavyo nchi inatakiwa iwe navyo sisi vimetushinda.

Amini Nawaambieni... kama mna watoto wenu bora muwapeleke Majuu tu huku ni kwa hovyo sana!
 
Back
Top Bottom