Governor of Bettors-GB
JF-Expert Member
- Jul 14, 2013
- 10,568
- 9,710
Hongera kwa ubunifu huo ili uweze kupata ada ya shule.Hata hivyo ni vyema ukajua kuwa sheria ya Tanzania..sheria no 4 ya 2010 (the architects and quantity surveyors registration act no 4 of 2010) inakataza mtu yoyote asiyesajiliwa na board kufanya kazi hizi. Pia inakataza hata wale waliosajiliwa kujitangaza. kwa hali hiyo wewe km ni mwanafunzi bila shaka huna usajili wa kufanya kazi hii..lakini pia hata kama ungekuwa umesajiliwa basi hurusiwi kujitangaza kwa njia hii. maana ramani haziuzwi km tunavyouza magari...au nyumba bali ule ni utaalamu na ukimuhudumia mtu pia utabeba liability ya kazi uliyofanya( kisheria). This is just an information!!!
Aliejenga Ikuli mwenyewe hakukasijiliwa,acha kuzingua watu.
Watu wangapi wametumia wanafunzi wa Chuo pale kwa kujenga majumba yao na hamna kitu.
Nyie ndio mlioenda Darasani kwa kukariri,kama ni masuala ya kisheria mbona miji yenyewe haijapangwa kisheria.
Rais juzi amewapa viwanja na vifaa vya ujenzi mabwepande na watu wameanza kujenga wao wenyewe bila hata huo upuuzi wa kusema sijui mkandarasi.
Acha kukatisha watu tamaa,wewe kama ni mkandarasi tafuta kwa njia yako,maana nyie wakandarasi wenyewe majanga,wizi mtupu,kila siku mnafanya mabalaa,barabara mbovu,maghoofa yanaanguka na wote hao wamesajiliwa.
Mie kuna post niliwahi kumshauri mtu aatafute wanafunzi kama hao ni rahisi sana na wapo makini sana kwenye kazi zao.na mie nilishauri na jamaa mmoja amabe aliejengwa Villa kwa kupitia ushari na design kutoka kwa mwanafunzi.
Kama ni sheria basi karibu mji mzima wa Dar ungekuwa umeishabomolewa.Hilo jengo la nunge Lenyewe lilijengwa na mkandarasi lakini liligundulika na Kreki kibao.
Mleta mada we mjanja na ninakupongeza sana kwa wazo lako,kwanza bei zako nafuu ndio maana wanakuja watu kupoteza mood humu.
Wewe kaza na komaa,nimeku pm kwa plan moja hivi.hakuna Board hapa wala Border.