FACTS 11: Kama wanasayansi wangesoma BIBLIA, Technology ya sasa ingekuwa Zamani Sana

Nakuelewa hizo ni miongoni mwa maana na zinaweza kurefushwa zaidi ili zikidhi hata akiwa na Mume wake ziingizwe kwenye hiyo Maana ya pornograph kitu ambacho sikubaliani nacho. Kwa maana hizo tatu juu kila kitu ni Pornograph, maana hata hapo ukiandika kitu kikanisisimua nikakujibu kwa mihemko yawezekana hata kukutisha HIYO NAYO NI PORNOGRAPH. Sasa sijajua umetanua wigo wa maana ili kuaccomodate hoja zako, unaweza kuendelea
 

Sasa wewe nipe maana yako ya " pornography" maana niliyoleta mimi kutoka Webster Dictionary huitaki.

Mimi napenda kukuhakikishia sitokuwa punguani kiasi cha kufikiria hayo ya kukuandikia kitu kikakusisimua au una maana kuna vitu unavisoma katika biblia vinakusisimua kwa mihemko?

Tuendelee .

Watazamaji hapa mpaka sasa ni moja bila, mleta mada anaikataa maana ya "pornography" ya Webster Dictionary na tuna ingoja maana yake na nnamuhakikishia maana yoyote ya "pornography" atayoileta yeye mimi ntaikubali mradi iwe ya kweli tu.
 
Kumbuka kuwa hapa nnaiongelea biblia mpaka dakika hii na sijawa attack nyinyi binafsi kama mfanyavyo. Nnawajuza hili ili muielewe "capacity" ya hiki kibibi na yenu, tofauti yake ni kama mbingu na ardhi.
Kuhusu kibibi ulianza kujiita wewe kama sijakosea, hapo naomba uniwie radhi (Kumradhi)maana nilidhani utani haikusumbui kama ulivyowahi kuita wengine watoto Japo wote ni watoto wa adam
namuita mwalimu wako sio kwa kumkejeli maana sio wewe tu bali wengi anawafundisha mambo mengi na anawafuasi wengi. Na usishangae pamoja na ukubwa wa kazi anayoifanya natofautiana nae na sio mimi tu Mahubiri yake yamefungiwa sehemu nyingi tu duniani India, Bangladesh, Canada na United Kingdom.
Na kikubwa kabisa anapingwa na wasomi wengi wa dhehebu lake kuliko hata sisi wa nje. Ila ninamuheshimu kwa sabau pamoja na yote anajibu au anadebate kwa hoja japo zinaweza kuwa tofauti na zisizokubalika. Na anamapungufu mengi pia.
 


Hapana, si kweli hajafungiwa kote huko. Afungiwe India na tasisi yake ipo India? Unashangaza.

Wewe kataa mahubiri yake lakini usizuwe. Hakuna anaemkataa huyo.

Ninachojuwa alinyimwa visa UK na sababu kubwa (ambazo hazisemwi) ni kuwa kila akienda UK anasilimisha kwa maelfu.

Cha ajabu ni kuwa na kumbuka Oxford Union ya Uingereza ikampatia jukwaa la kurusha na sattelite live yeye awe kwao India na audience itakuwa kwenye hall ya Oxford Union, naam, lecture ikampatia watazamaji wengi kuliko angeenda mwenyewe. Kwani dunia nzima wakawa na shauku ya kumsikiliza kwanini huyu anyimwe visa na serikali ya UK lakini wasomi wa nchi hiyo wafanye kila njia kumsikiliza live, jionee:

 
naona umekimbilia kwanye mashindano hadi unajipa max. Kama umenielewa sijapinga ila nimetanua scope ya maana kwamba inaweza kuwa pana na kumeza kila aspect.
Ukienda kwenye ya hilo neno maana kwenye kiingereza limeanza kutumika mwaka 1857.
Orgin ya hilo neno ni kigiriki PORNOGRAPHOS
Porne(Prostitute/Kahaba) na Graphen(Write) au maandishi kuhusu Makahaba
Mwingine anasema...
Pornography is the portrayal of erotic behavior designed to cause sexual excitement. It is words, acts, or representations that are calculated to stimulate sex feelings independent of the presence of another loved and chosen human being.
Na wengine wengi ingawa mzizi upo kwenye orgin ya neno husika, Sijakupinga ila nimetaua maana Icover range kubwa ili unipe kifungu unachodhani ni porno. Maana hapo lazima tuangalie Intent, Aim, How was it depected or portrayed, Is it figurative, Parable au nini hiyo ni hatua ya pili baada ya kutoa mstari
 
hiyo kazi nakuachia fuatilia. Waziri wa habari Bangradesh alifungia mahubiri ya huyu ndugu baada kuhusishwa kuhamasisha mambo yanayohatarisha usalama kwa mahubiri yake kuhusishwa na matukio ya mauaji huko bangradesh, Kijana Rohan Imtiaz ambaye huyu muhubiri ni influencer wake wa karibu alikuwa ni mmoja wa gunmen kwenye baadhi ya mashambulizi kwa raia kwa mujibu wa vyombo vyua habari nchini hapo. Pitia pitia sources mbalimbali wenda hizi ni update za karibu zaidi ambazo huna
Hii link nakupa ili upitie ila iko nje ya mada na isome kwa hiari yako, sio sehemu ya utetezi wowote juu ya mada kuu Bibilia na Sayansi na Mada iliyoiibua katikati ya kutetea hoja zako.
Who Is Zakir Naik? Bangladesh Bans Controversial Islamic Preacher’s Peace TV Channel
 


Kwa hiyo, hiyo ndiyo maana yako uliyoileta ya "pornography".

Lile moja bila, fanya wewe ndiyo umeshinda kwa kuikataa mana na sasa kurudi kuikubali.

Usiwe muoga kiasi hicho wakati unaamini unatetea maandiko unayodhani kuwa ya Mungu.

Kumbuka upo hapa na FaizaFoxy wa JF na mapenzi yangu ni darsa, nadhani unaelewa maana ya kwenye signature yangu. Usiwe na hofu, Sipo hapa kutaka kukudhalilisha wewe binafsi, la hasha, nipo hapa ku discuss mada yako ya biblia na sayansi ki aina yangu.

Napenda uelewe haya ili labda hofu ikuondoke na uwe muwazi na mkweli na usikubali hata siku moja kusutana na nafsi yako katika mambo ya imani. Ukijadili mambo ya imani unatakiwa uwe muwazi na mkweli kwani ukianza kusutana na nafsi yako utakuwa huna imani ya kweli, itakuwa ni ya kujifanyisha tu.

Pornography ni pornography na sidhani kama Webster Dictionary wamekosea, ingawa ulikataa lakini hiyo uliyoileta ntaikubali kama nilivyoahidi kuikubali maana yoyote ya pornography utayoileta mradi iwe ya ukweli. Na nita i quote hiyo maana uliyoileta ingawa hujaweka source. Mradi usije huko mbele kuikataa tu.

Kwa hiyo ume confirm hiyo uliyoiandika ndiyo maana ya pornography uliyoikubali?
 

= Bangladesh

Anyway, hiyo ya Dr. Zakir Naik kukataliwa siyo issue kwani hata Yesu alayhi salaam watu aliotumwa kwao mpaka leo hii wengi wao hawajamkubali.

Hali kadhalika hata Mtume Muhammad Salla Allahu Alayhi Wasalaam watu wa kwanza kumkataa walikuwa ni wa kwao.

Tuendelee na mada.
 
Naona umeanza kuleta tambo na majigambo yasiyo na maana. Hofu na uoga katika mambo haya sio tu kwamba haipo bali haijawahi kuwepo labda uwe nayo wewe, kuhusu hilo shaka ondoa kabisa. Definition chagua yoyote unayoona wewe itakufaa kuanzia westmister hadi origin.Sijaona darasa lolote ambalo umewahi kulitoa popote.

Labda nilete kidogo kile unachoshindwa kukiweka ili kufupisha mjadala maana Sayansi haipo kwenye hija zako ulizoziibua

NOTE:Bibilia sio kama kitabu kile ambacho kiko moja kwa moja.
Ndani ya bibilia kuna Nyimbo,Unabii,Mafumbo, Story,Methali,Mafumbo,Maelezo ya moja kwa moja, Masimulizi, Ndoto, Njozi, Record ya Maovu ya watu, Mazuri ya watu, kila kitu. Na mambo yote yameandikwa kwa Uongozi wa roho mtakatifu na kwa malengo maalumu.
Hapo ndipo wengi ukiwemo na wewe unapigwa chenga, na ndio maana kuna wapinzani wengi sana kila siku.Ili Uelewe inabidi BIBILIA ikuongoze kwenda kwenye Wazo lililo nje yake na Sio wazo ulitafutie hoja hapo lazima uishie huko ulikokwama sasa.

Nimepitia hoja na critics nyingi za Islam juu ya point yako hiyo ya Pornograph, Mafungu haya ndio yanawachanganya.

Ukisoma bibilia yote ndio utaenjoy na kumuelewa Mungu sio kwa kudokoa kishabiki.
Matendo17:29-Basi, zamani zile za ujinga Mungu alijifanya kama hazioni; bali sasa anawaagiza watu wote wa kila mahali watubu.

1:Mwanzo 19:30-38, Pale Lutu alipoleweshwa watoto wake wazini nae. Bibilia inaendelea kuaminika kama kitabu cha kutumainiwa maana inaonyesha udhaifu wa wanadamu wa Enzi hizo na sio intent za kupromote hicho wanachosema hao jamaa.

2:Ezekiel 23
Huyu ni nabii, lazima uelewe unabii na nabii anakazi gani na pia Uelewa kwa unabii Bibilia inaposema kuzini inamaanisha nini. na lugha iliyotumika kuwasiliana na waisraeli waliokuwa katika dimbwi la dhambi lililopitiliza.

3:Wimbo uliobora
Ni kitabu amacho kimeandikwa kwa tafsiri sisisi utapotea sana. Humo pamoja na Solomoni kumsifia mke wake Lamueli pia ni kielelezo cha upendo wa Mungu kwa kanisa lake kwa maana ya ndani. Kwa kujua hivyo ndio maana wananzuoni Muslim wengine wanadai Mtume alitabiriwa Katika Wimbo uliobora 5:16 japo hapo alikuwa anazungumziwa David au mtu mwingine kulingana na Orgin Hebrew translation.

4:Hosea 2:
Soma kitabu chote cha hosea, Hadi kuna mahala anaambiwa akamuoe mke wake walioachana ambaye anajiuza barabarani. Kisha Mungu atatoa tafsiri ya unabii wa kitabu.
Uzinzi kwa ufupi unaozungumziwa ni Kumuacha Mungu na Kufuata Miungu Mingine kama Mawe, au Kuwa upande wa shetani kwa Mungu ni kama mwanamke kuzini. Object lesson hizo, sasa ukiingia na kutafsiri unavyotaka bila kujua unachotaka lazima utaishia kwenye conclution hizo.

Nimepitia arguments za wanaoleta hizo story nimegundua huwa mnadanganyana mengi sana. Na kwa definition zote za Pornograph zinazungumzia Intent, na hapo pia kuna shida naiona kwa wafasiri wa Mojakwamoja bila kujua intent. Ndio maana sijawahi kusikia Mkristo kajishughulisha na mambo ya kipornographic popote duniani akiwa powered na haya mafungu. Ila kuna uwezkano kwa maandiko yale ya upande wa pili kuna uwezekano mzee wa miaka 55 kuoa motto wa miaka 6 which is beyond porn

Nimejaribu kupitia hiyo document uliyoiattack hakuna la maana. Nilichogundua Wanatunga Kitu then wanaenda kudokoa mafungu yanayosupport bila kujali kama nini kinazungumziwa pale ila lengo kuu ni kukidhi haja ya uzushi ule. Pia nikagundua katika pitapita upande ule uliopo ndio
 


Hakika nimefurahi sana kuwa jinsi nnavyojadili na wewe unahisi kuwa nimeanza "kuleta tambo na majigambo yasiyo na maana."

Nimefurahi kwa kuwa ukweli wangu ndiyo unaokufanya uone hivyo na ukweli ukidhihiri uongo hujitenga.

Nimefurahi sana tena sana kukusoma kuwa hujaona darsa langu mpaka sasa. Hiyo ni furaha kubwa sana na ndiyo moja katika mbinu za kusomeshwa nilizofundishwa na wewe umeniyakinishia kuwa nnafanya vyema bila wewe kujijuwa. Ahsante sana kwa hilo.

Tukirudi katika mengi uliyoyabandika hapo juu, kwanza nnaona unaweka namba ya aya lakini unashindwa ku i quote hiyo aya na badala yake unajaza maneno yako.

Hivi ni sahihi kuweka namba ya aya ya biblia halafu badala ya kuweka hiyo aya unajaza maneno yako?

Nnahisi si sahihi, unaweza kuweka namba ya aya na ukaiweka hiyo aya kisha ukaitolea maelezo, hapo ndipo mjadala utanoga.

Nimefurahi pia kuwa umelirudia tena suala la maana ya "pornography", hilo sasa hivi si muhimu sana kwani nimeshakubali maana yako uliyoileta na nnakuahidi ntaitumia hiyohiyo.

Kumbuka tu, mpaka sasa bado nipo katika kujadiliana na wewe namna tutavyoendesha huu mjadala.

Nashauri, inapokuja katika ku quote biblia au Qur'an tutumie namba za aya kisha tuweke hiyo aya kisha tuweke maelezo yetu na ikiwezekana aya tuzi bold.

Nasubiri jibu lako kwa hili.
 
Mijadala ya namna hii huwa sihitaji inipotezee muda kabisa....

Sitakujibu tena kama hutafanya kipaswacho....

Kila la kheri bibie..

Ninauthamini sana muda wangu....
 
Mkuu unapoteza muda wako tu na ninakuhakikishia hutafanya chochote hapo.Mtu anamuona huyu daktari kuwa wa maana utaweza kujadiliana naye nini mkuu?


 
Unapotofautiana na mwenzako jua hapo unafikiri mwenyewe na siyo kufikiri kwa niaba ya mtu mwingine...

Ninamfahamu sana Gavana na wengine wengi sana maana nilishafanya nao majadiliano sana tu,ninachoweza kusema ni kwamba ninaokoa muda wangu kwa kutokujadiliana nao chochote maana hakuna kipya ni kupoteza muda tu....

Nakubaliana na wewe kwamba wapo ambao wanajielewa kabisa lakini unapoona mtu anamuona Dr Zakiri Naik kuwa ni mtu wa maana sana kumfanyia rejea huyo hata sita argue naye maana ni tatizo tayari hilo....

Kuanza kusema fulani amesema hivi na kutaka tuanze kujadili alichokisema huyo bila kusema alichokisema kinakubaliana namna ipi na Biblia ni kupoteza muda tu.Kwanini nione fulani anasema kweli wakati hata hujasema ni kwa namna ipi yupo sawa na maandiko matakatifu ya Biblia?

Mtu anasema ndani kwako kuna sahani ina miguu,ukimwambia nioneshe anaanza kukuambia kubali au kataa kwanza,hiki si kituko? Yaani kuna uhusiano upi kati ya kauli yangu na uwepo wa sahani hiyo ambayo yeye anajua ipo? Kwanini asinioneshe tu?

Ukiona mtu anaacha madai yake na kuanza kutaka wewe uyathibitishe huyo ana matatizo makubwa sana....

Sijadili tena kuhusu suala la Dr Zakir Naik maana ni kama unajadili ni kwanini mtoto anajisaidia kwenye nguo...

Labda kukiwa na kingine cha maana nitajadili.....
 
Mkuu wa anga ameshika ufahamu wake ukumbuke Kristo alipokuwa akimjibu mmoja wa wanafunzi wake ya kwamba kwa nini alisema nao wengine kwa mafumbo, inawezekana kabisa hajajaliwa kuzijuwa siri za mbinguni! Ndio kisa amekuwa mbishi sio kosa lake,
Huyo dada nimeshamshauri sana lakini hanielewi kabisa...

Siyo kosa lake lakini....
 
Mijadala ya namna hii huwa sihitaji inipotezee muda kabisa....

Sitakujibu tena kama hutafanya kipaswacho....

Kila la kheri bibie..

Ninauthamini sana muda wangu....


Mbona unakuwa na kiherehere na papara? Mwenzako kisha jaza namba za aya kibao kwa kujishuku tu, lakini kashindwa ku quote hata aya moja.

Ukipitia mjadala utaona kuwa tumeshakubaliana ni nini maana ya "pornography" ingawa kwanza mwenzako aliikataa halafu kaikubali halafu kalalamika, nnaomba umsaidie kuchangia ingawa tumekubaliana nae lakini nnahisi mchango wako kuhusu ni nini maana ya "pornography" utakuwa na msisitizo, mimi nime i quote maana ya "pornography" kutoka Webster Dictionary na link nimeweka.

Na nimetowa ushauri namna ya kujadiliana hii mada kuhusu namna ya kuweka aya na namba zzake ili iwe faida kwa sote, ukipitia mjadala utaliona hilo na sitopenda uondoke na kutuwacha kwenye huu mjadala, nataka wewe ushiriki na wenzako wengine mjumuike. Ni mada yenye maana sana hii kwa sote.

Usiondoke tafadhali, bado tunakupenda.
 

NAOMBA NIKUPE KIDOGO MAELEZO HAYA KABLA SIJAFUNGA KUHUSU HUYU MWALIMU
Usichukulie kirahisi hivyo ndio maana umesema anaangaliwa na watu 100M kwa far east na india hiyo ni idadi ndogo sana ya watu ukilinganisha na population ya huko.
Huyu unayemuona kama Role model wako wa imani anapingwa na kukwepwa na waislamu wasomi wa kitabu wengi tofauti na unavyomsifia.

Mfano hii Fatwa kutoka kwa kiongozi wa kuheshimika
“He seems Ghair Muqallid and his knowledge is not deep. Therefore, he is not reliable and Muslims should avoid listening to him…. We know that he is an agent of Ghair Muqallideen, away from knowledge and wisdom, spreading mischievous things and misguiding simple Muslims to wrong path” (Mufti of Deoband).

Kwa Ufupi usidhani wakristo hawajishughulishi kujua mkoje huko historia yenu inasemaje na mapungufu makubwa yaliyopo ila ni uvumilivu wa kidini na asili ya bibilia inashambulika na inaalika changamoto kuliko upande wa pili ambapo kwa maana ya kutetea imani wanaenda mbali zaidi ya majadiliano ya kihoja. Huku tunaamini maadam FF anaweza kuokolewa na kristo kwa hata maneno mawili tu na ukawa muinjiristi mzuri huku ukiweka pembeni yote uliyodhani ni sahihi.

Dunia inaaminishwa ni wamoja Mungu mmoja na Mtume mmoja lakni kiukweli japo kitabu ni kimoja (Ambacho chanzo chake ni controversial kuliko kawaida) lakini kiila kikundi kina tafsiri zake tofauti kabisa na kingine.

Japo Tunaaminishwa Kuwa ni Dini moja isiyojipinga lakni Ukweli ni kwamba Kuna Madhahebu zaidi 72 duniani yanayopingana katika tafsiri ya kitabu kwa utofauti wa mbingu na nchi. Na Huu sio Muujiza bali Ulianza pale baada ya mwanzilishi kufariki, na Abu Bakar kuchaguliwa bila kumshirikisha Ali ambaye alidhani ndiye alifaa kuchukua nafasi hiyo kuu ktik imani(Caliph), Na kosa kubwa kabisa hata pale Ali alipodhani ni zamu yake Akachaguliwa tena Umar, akaja Uthman aliyecompose hicho kitabu bila maridhiano ya kutosha na Ali ambaye alikuwa mtu wa karibu kuliko wote kwa mwanzilishi na alijua mengi.Kuanzia hapo hakujawahi kuwa na imani moja ya hicho unachoamini.

Mfano ni hili dhebehu la Wahhabi ambalo huyu mwalimu anabasezaidi japo anachanganya.Hawa wanamisimamo hatari isiyokumbatia amani sana na inaamini ni maelezo yao ndio yako sahihi kabisa kuhusu kwenda peponi.Maana yake wengine wote kunauwezekano ikawa ni motoni. Ili kuwavuta wengine Zakir anachanganya na Mafundisho ya wengine kama waismail,Qadiyanis, Wahabis,shia, etc na kuwa na version yake mwenyewe ya mafundisho ambayo wenzake wapenda amani wanapingana nae kwa mengi.

Sijui wewe unafanya kazi wapi, lakini miongoni Dogma za huyu mwalimu Zakir mwanamke hapaswi kufanya kazi za ofisini, Maana kuna uwezekano ilatokea akabaki peke yake na mwanaume humo ndani, Anatakiwa kuwa peke yake na mume wake tu au ndugu wa karibu kabisa na zaidi ya hapo haruhusiwi kabisa kushiriki kwenye michezo. Anaenda zaidi kwa kucheza na maneno na statistics kutetea ndoa za wake wengi kinyume na misingi hadi kuna baadhi ya mafunsiho yake anasema uwezo wa mwanamke uko chini kiasi cha wanawake wawili ni ndio wanakamilisha akili moja kamilifu.

Kuna wengine wameenda mbali zaidi wakamuita shetwain kutokana na mafundisho yake. Wote hao sio wakristo. Na pia wengine wanamemchoka na kusema hajui hata kiarabu ila mambo mengi anacopypaste kutoka kwa mwalimu mwingine wa aina yake Ahmed Deedat ambaye ndiye yuko mstari mbele kwenye hizo story la swali lako.
Zakir Naik Hatred for Prophet Muhammad (Salallaho aliayhay wasullam)-1/2 - YouTube
Haya ni baadhi ya maoni kuhusu huyu mwalimu.

Kuhusu hii hoja ambayo inakuwa propagated na baadhi ya wahubiri mafano huyu Dr zakir na Ahmed Deedat sitapenda kuendelea mbele. Kwa maana itatulazimu tushindanishe vitabu hivi viwili pamoja na Hadhi zote tuziweke mezani zinazoaminika na zilizoachwa wenda kwa sababu maneno yake yangeaibisha imani. Na naona nikizama ndani zaidi nagundua kule upande wa pili uliko hii mada au swali ulilouliza Linaushahidi kutoka kitabuni humo na adithi zake usio na kifani. Na kwa uzoefu mdogo kila mjadala ulipohitaji kuhusisha Kufunua kitabu na Hadhithi zake kuwa unachochea mihemko ya Hasira (Definition ya tatu Westminster post 297) upande wa pili. Maana ntahitajika Kukuonyesha Jinsi ambavyo sio tu hilo tukio ovu kuhamasishwa bali hadi Peponi kunategemewa kuwa kama mji wa ngono na sio mahala patakatifu kama tunavyofundishwa na bibilia. Nitalazimika Kuzungumzia vitu kama "HOURIES", Wanawake walioandaliwa yaani Vifua vimesimama, umri mchanga, Hawaingii MP, Hawana wala hawazai watoto wala hawana majukumu zaidi ya tendo la ndoa 24hrs huko peponi, Itanibidi nizungumzie hadithi zinazoonyesha Paradiso ambazo zinazungumzia mambo ya ajabu yasiyostahili kuwekwa hapa jamvini.

USHAURI WANGU:
Ninashauri tuendelee ma Mada Tajwa juu pale kwenye thread, kama unashida na content yoyote pale au mada nzima ueleze itajadiliwa. Ila kwa akili yangu hii ndogo baada ya assessment ya progression ya Hiyo mada uliyoiibua maana itabidi tuweke Bibilia,Quran, Hadithi unazozipenda na Usizozipenda (wengi huzikimbia na kusema hizo tulizikataa), Rejea za wanananzuoni na hivyo kuharibu mwelekeo wote wa hii mada juu pale. Kama kauli hizi kwako utahesabu kuwa nimekimbia au nimeshindwa pia sitashtuka wala kutia neno.

UKWELI UDUMUO NA USIOPINGIKA.
Bibilia ni Neno la Mungu lililokamilika lenye uwezo wa Kumuokoa mwanadamu yoyote ikiwemo wewe.
Ule unaotafsiriwa kuwa ni mapungufu na mikanganyiko ni Kwa sababu Dunia inashindwa kujua Bibilia ni kitabu ambacho ndani yake kinazungumzia wanadamu na mahusiano yao na Mungu pamoja na Shetani anavyowaangusha. Kuna record za wanadamu Mitume,Manabii,Watumishi,Wafalme katika Vilele vya ubaya wao na Vilele vya Uzuri wao. Kurecord mfano mabaya ya Mtu mwanadamu Mdhambi au Mwovu kabisa haukifanyi kitabu bibilia kuwa Na Makosa au haifai bali ni Ushahidi tosha wa kukifanya kiaminike kabisa maana kinaonyesha uhalisioa kuwa Watu sio Maroboti. Ila kama kuna kitabu kinachozungumzia wanadamu walionyooka kama rula na kufuta au kwa siri kuondoa haya za udhaifu wao kama Uongo, Mauaji,Uzinzi, Uasi ni lazima kiache maswali mengi ni aina gani ya watu waliishi enzi hizo. Ni yesu(Mungu pamoja na wanadamu) tu ndie aliyeishi bila kutenda dhambi. Pia kuna mifano,mafumbo,historia,mithali,unabii,lugha za picha etc zinazoweza kukwachanganya wanaoipinga. Kuisoma biblia bila Roho mtakatifu ni sawa na Kunyoosha nguo kwa kutumia pasi ya umeme ambayo haijachomekwa kwenye socket. Maneno ya bibilia yameandikwa na Watu waliobgozwa na Mungu kwa Uvuvio wa Roho mtakatifu nayo yamevuviwa.


Maneno ya bibilia ni ya kina kifupi sana ambacho mtoto mchanga Anaweza kuogelea bila Kuzama, Pia bibilia hiyohiyo maneno yake ni ya KINA sana kiasi kwamba WASOMI,WAPINZANI WAKE,WAZUSHI,WANATHEOLOJIA, WANAHISTORIA,
WACHAMBUZI NA WABOBEZI WA MAMBO wanawezakuzama kutafuta maarifa bila kufikia kina chake.

KARIBU
 
Mkuu MSEZA-MKULU, Kwanza pole sana kwa juhudi kubwa unayoifanya ya kuelimisha na kutangaza kwa nguvu zote jinsi ya biblia inavoshabiana na Science kwa ujumla wake.
Katika watu waliojitahidi kitendea haki thread zao nawewe unaongoza. . Na kwa kweli umeiva kwenye mada uliyoiweka.

Mimi naomba nianze kwa kusema inaonekana unaijua sana historia ya mambo ya kale ki-Biblia na ki-Sayansi kwa uzuri kabisa hapa ninakisifu na kwa kweli umeiva. Ila kujua hizo historia kwa sana haikufanyi ukawa na ushawishi au nguvu ya hoja wa kuwateka the so called MATERIALIST , shida uliyonayo ni kuwa unaeleza historia nyingi ambazo at the end unajichanganya na kumpoteza mbwa kwa miluzi mingi-----na ndio maana pamoja na kujenga hoja nyingi sana hujaweza washawishi wengi humu kufuata unachokizungumza/kukiamini maana hoja zako hazina mashiko.
Kwanin nasema hazina mashiko:

Mosi; Unachanganya mambo sana, mfano wadau wengi wanakuasa kuwa biblia inazungumzia (imani) wakati sayansi inazungumzia (facts) hii ni sawa na maji na mafuta. Huu ni ukweli wa wazi kabisa unaotakiwa kuukubali.

Pili; Ni kweli kama unavosema kuwa biblia imejaa ilmu mbalimbali ila wewe umeamua ku-site areas zinazohusu masuala ya kisayansi, hatukatai upo sawa tu maana kiukweli Bible ni kapu lenye kila aina ya maarifa kinachotakiwa ni jinsi mtu anavyoitumia anachukua kipi na kipi anakiacha. Ila unapokosea ni pale unapotulazimisha tuamini kuwa bible in its general inasupport sayansi, kitu ambacho si kweli---maana yapo maeneo kibao bible ina criticise sayansi kabisa na kuna sehemu inaenda beyond sayansi hasa kwenye masuala ya miujiza. Sasa kitabu kama hichi huwezi ukatoa a general statement kuwa eti kinasupport sayansi 100% na kitumike ktk maswala ya kisayansi as a reference maana kitachanganya watu hasa pale watakapokutana na mistari inayopinga sayansi humohumo. WEWE ULITAKIWA USIONESHE MAPENZI MAKUBWA NA YA KU-GENERALIZE KUWA BIBLE NA SAYANSI VINAOANA KWA UJUMLA WAKE. Kwa maana ukisema hivo unaleta contradiction kama nilivoeleza hapo.

Tatu; Unatakiwa utambue kuwa si kwa sababu wewe unaamini jambo fulani bac ukaona we ndio mueleeewa kuliko wengine , nimefurahi ulivyonanwa na mdau mmoja hapo juu ukakiri kuwa wachina, wajapani na hata mataifa & makabila mengine yameweza kufanikiwa sana tena sana kwa maarifa na skills nje ya biblia unayoiamini wewe, hapa ndio unatakiwa ufahamu kuwa knowledge is beyond very far beyond what you believe as MSAZE MKULU . Ni hivi yapo maarifa mengi sana yanaelea hewani na yapo pande zote kinachotakiwa ni mtu kuwa na vision kali na kutuliza mind yako ili uya-capture . Hili linathibitishwa kupitia wanasayansi wengi ambao kama tulivoona hapo kabla kuwa walikuwa christian ila baada ya kuzidi ku-crack vichwa waliamua kuachana na ukristo na either kuwa wapagan au kuhamia pande nyingine ya imani, ila hiyo haikuwafanya kushindwa kifanikiwa , matokeo yake walifanikiwa sana tena sana. Hivyo maarifa yapo everywhere the matter is how to capture them. Hivyo unvyong'ang'ania biblia ndio kila kitu unakosea maana si kweli , bali biblia wengi wanaichukua kama reference ktk kakipengele flan tu na anaendelea na theory zake nyingine, sasa wewe ukiona amesite kamfano kamoja unawehuka kisema biblia yote ni kisima cha sayansi hapo unakosea, hamna kitu kama hicho. (hapa unadhihirisha unavoweka mapenzi mbele badala ya logic) usihubiri we weka fact zitajitetea zenyewe.

NOTE:
Biblia ni kweli unaweza itumia kama unavosema ikakupanua kiakili katika areas flan flan ila pia biblia hiyohyo unaweza itumia ikakupumbaza jumla ktk mambo flanflan.
(AKILI KUMKICHWA)
 
Na ile safina ya Nuhu bibilia inasema vilikufa viumbe vyote isipo kuwa vilivyo ingia kwenye safina. Swali Nuhu na baadhi ya watu wake ndio waliingia na wakaokoka na garika sisi tumetoka wapi? Au wazungu wametoka wapi? Au wahindi wametoka wapi na wengineo. JIBU TAFADHARI STAKI POVU.
 
kumbuka tayari watu kama akina Eliya walipaa angani.
 
Huyu mama ameifanya Google kuwa mungu wake.

kila kitu lazima akatafute kwa Google.
Hasomi vitabu akaelewa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…