Fahamu kuhusu biashara ya kuuza chakula (Mgahawa)

Fahamu kuhusu biashara ya kuuza chakula (Mgahawa)

Ukitaka kuona wabongo tusivyojali mada za maana humu jf hii thread watajitokeza wachache tu kuongelea lakini kama zingekuwa stori za mambo ya ajabu ungekuwa na replies za kufa mtu.
Umesema kweli maana mpaka sasa sina mchango niliopata hahahaa
 
Kabla ya kuwa na hivyo vitu fanya survey ya sehemu unayotaka kuwekeza hakikisha kuna mzunguko wa fedha au eneo lenye mkusanyiko wa watu kama stand ya daladala, vyuo, soko, makanisa makubwa (RC, Luth, etc), mikusanyiko ya taasisi na maeneo yote yenye makutano ya barabara zinazofanya hata bodaboda wajazane (boda boda ni indicator kubwa ya kuonyesha sehemu potential ya biashara hiyo), ukijirizisha andaa vifuatavyo:

1. Viti vya plastic 20
2. Meza 5 za kulia chakula za plastic ni nzuri japo sio lazima hata mabenchi yaeza faa
3. Jiko la gesi zuri la kilo 30
4. Jiko ya mkaa 4 (jiko moja chapati, la maharage, la supu, la maji ya kunawa wateja) chai tumia jiko la gesi
5. Frying pan na vyombo vya kukaangia (ya maandazi, ya chapati, ya kukaangia mayai, etc)
6. Sufuria kubwa tatu(ugali, wali na maharage) na visufuria vidogo hata 7
7. Stand ya kunawia wateja na ndoo yake
8. Blenda ya kutengezea juice na kuponda nyanya
9. Sahani na vijiko vya kulia chakula 50
10 Stirer ya kuchanganyia changanyia bagia, mikate,etc
11. Freezer kubwa (ndogo inafaa kishida shida), ukiwa na oven sio shida
12. Case ya kubebea vyombo (usafi zaidi)
13. Tengeneza sehemu nzuri ya kupikia(mazingira yanayohamasisha usafi)
14. Tumia muda wako kujifunza hii shughuli tafuta wafanyakazi wenye ujuzi wa kupika aina tofauti za chakula na wasafi
15. ulizia mahali wanapika vyakula vitam hasa vya kipemba watu wengi wanapenda sana
16. Kuwa mbunifu usiwe bahili wekeza fedha na walipe vizuri na kwa wakati wafanyakazi wako

KUMBUKA NI HATARI KUPIMA KINA CHA MAJI KWA KUTUMBUKIZA MIGUU YOTE - anza taratibu kwa kuweka vitu vidogo vidogo huku ukiusoma mchezo the more the response the more u invest boresha huduma na waelekeze wafanyakazi wawe na majibu mazuri na kuvutia wateja slowly utakuta demand inakuwa kubwa kulko suply na hapo ndio unaongeza uwekezaji.

Yangu ni hayo tu
 
Biashara ya Mgahawa inataka mambo yafuatayo
- Location- lazima ikar location nzuri na yenye watu wengi

- Aina ya watu unao taka kuhudumia- Je ni wa kipato cha kati au cha chini au mchanganyiko hii nayo itategemeana na location

- Je unataka ulishe watu wa Aina gani? Wafanya biashara au Wafanyakazi? Mfano ukiweka mgahawa mitaa ya Posta jioni au usiku kutakuwa na wateja
wachache kwa sababu pale ni eneo la ofisi hivyo jioni watu huwa wanaenda nyumbanj.

Ukiweka mtaani maana yake utahudumia masaa yote kwa sababu jioni watu wamerudi na watakula hapo.

- Vitendea kazi- Hakikisha ni vya kuvutia kama viti, meza, vikombe, vijiko, sahani na kadhalika, tumia vyombo vyenye kuvutia machoni.

- Wafanyakazi- Hakikisha unawapa semina ya kuhudumia kwanza, wapige shule, zunguka nao migahawa mikubwa na nunueni hata Soda lengo muone huduma zilivyo na muwe na Notebook ya kuandika. tembeleeni migahawa mikubwa na mizuri.
Pia tembeleeni migahawa ya hadhi ua chini kabisa muone huduma zilivyo na waambie waandike mapungufu wanayo yaona pale.

- Chakula- Hapa sasa wapishi, ikibidi import wapishi hata kutoka mbali unako ona wanafaa, hakikikisha una wapishi bora na sio wapishi wakuokota okota mtaani.

- USIMAMIZI- Nakushauli simamia mwenyewe, ni biashara yako, chagua kuweka watu wengine wasimamie na ufeli au usimamie mwenyewe.
 
kabla ya kuwa na hivyo vitu fanya survey ya sehemu unayotaka kuwekeza hakikisha kuna mzunguko wa fedha au eneo lenye mkusanyiko wa watu kama stand ya daladala, vyuo, soko, makanisa makubwa(RC, Luth, etc), mikusanyiko ya taasisi na maeneo yote yenye makutano ya barabara zinazofanya hata bodaboda wajazane(boda boda ni indicator kubwa ya kuonyesha sehemu potential ya biashara hiyo), ukijirizisha andaa vifuatavyo
1. viti vya plastic 20
2. meza 5 za kulia chakula za plastic ni nzuri japo sio lazima hata mabenchi yaeza faa
3.jiko la gesi zuri la kilo 30
4.jiko ya mkaa 4 (jiko moja chapati, la maharage, la supu, la maji ya kunawa wateja) chai tumia jiko la gesi
5. flam pen na vyombo vya kukaangia (ya maandazi, ya chapati, ya kukaangia mayai, etc)
6. sufuria kubwa tatu(ugali, wali na maharage) na visufuria vidogo hata 7
7. stand ya kunawia wateja na ndoo yake
8. blenda ya kutengezea juice na kuponda nyanya
9. sahani na vijiko vya kulia chakula 50
10.stirer ya kuchanganyia changanyia bagia, mikate,etc
11. frizer kubwa (ndogo inafaa kishida shida), ukiwa na oven sio shida
12.case ya kubebea vyombo(usafi zaidi)
13. tengeneza sehemu nzuri ya kupikia(mazingira yanayohamasisha usafi)
14.tumia muda wako kujifunza hii shughuli tafuta wafanyakazi wenye ujuzi wa kupika aina tofauti za chakula na wasafi
15. ulizia mahali wanapika vyakula vitam hasa vya kipemba watu wengi wanapenda sana
16. kuwa mbunifu usiwe bahili wekeza fedha na walipe vizuri na kwa wakati wafanyakazi wako

KUMBUKA NI HATARI KUPIMA KINA CHA MAJI KWA KUTUMBUKIZA MIGUU YOTE - anza taratibu kwa kuweka vitu vidogo vidogo huku ukiusoma mchezo the more the response the more u invest boresha huduma na waelekez wafanyakazi wawe na majibu mazuri na kuvutia wateja slowly utakuta demand inakuwa kubwa kulko suply na hapo ndio unaongeza uwekezaji.
yangu ni hayo tu
Nimekukubali bure kabisa and i have taken this note.. Thank u na Mungu akubariki sana
 
Wakuu,

Kutokana na changamoto ya ajira nataka nijiajiri kwa kufungua mgahawa mdogo ambao nataka niuze chai chapati wali &ugali nyama/mboga za majani, supu.

Msaada wa kimawazo kwa kilo 2 ya mchele inaweza kutoa sahani ngapi?/ faida kiasi gani? Given price 1,200 na 1,500. Kilo moja ya unga wa ngano inatoa chapati ngapi? Na faida kiasi gani kama market value ya chapati ni 2500.
 
Nenda pale TIC (Tanzania Investment Centre) watakupa maelekezo na biashara yako itaingia kwenye list ya viwanda vipya vya mwijage
 
Wakuu Kutokana na Changamoto ya ajira nataka nijiajiri kwa kufungua mgahawa mdogo
Ambao nataka niuze
Chai
Chapati
Wali &Ugali Nyama/mboga za majani
Supu

Msaada wa kimawazo Kwa Kilo 2 ya Mchele inaweza Kutoa sahani ngapi?/ Faida kiasi gani? Given price 1,200 na 1,500.

Kilo moja ya Unga wa Ngano inatoa Chapati ngapi? Na faida Kiasi gani kama market value ya Chapati ni 2500

NAJUA HILI JUKWAA NI LA SIASA NIMEPOST HUKU ILI NISAIDIWE MODERATORS NAOMBENI UKAE KWA MUDA. Kwani Majukwaa mengine nikipost kitu kinakaa hadi kinapotea mtu haja jibu.

Kilo moja ya mchele inatoa sahani 5 hadi sita. Na kilo ya ngano inatoa chapati hadi 16..sasa hapo angalia na soko la sehemu ya biashara yako kama ni uswahilini watu wanataka kushiba so unaweza toa sahani 4 tu za wali. Hiyo biashara ni nzuri ukiwa na eneo zuri ila inahitaji usimamizi wako wa karibu
 
Kilo moja ya mchele inatoa sahani 5 hadi sita...na kilo ya ngano inatoa chapati hadi 16..sasa hapo angalia na soko la sehemu ya biashara yako kama ni uswahilini watu wanataka kushiba so unaweza toa sahani 4 tu za wali...hiyo biashara ni nzuri ukiwa na eneo zuri ila inahitaji usimamizi wako wa karibu
Daah Asante kwa kunitoa gizani
 
Habari wakuu, Nina wazo LA kufungua mgahawa Dodoma kwa mtaji wa milioni tano. Naombeni mawazo yenu ktk maeneo yafuatayo:

1. Eneo zuri kwa kufungua biashara tajwa kwa Dodoma
2. Bei za fremu kwa wenyeji wa Dodoma
3. Kama mtaji huo ni reasonable ukilinganisha na ushindani wa mji
4. Mambo machache ya kuzingatia kwa biashara ya mgahawa mjini Dodoma.

Asanteni.
 
Kwa Dodoma ni mtihani mno!! Kwani centre zote nzuri wameshawahi na ukitaka kuanzisha inabidi uwe mbunifu wa hali juuu
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Dodoma sehemu sahihi ni katikati ya mji ambapo kweli sehemu jamaa wengi wamechukua hivyo utakutana na kizingiti cha kupata sehemu bora ya kufanyia biashara yako but pia nikupe wazo unaweza kuweka mgahawa wako pembezoni mwa mji ukawa una supply lunch maofisini direct means unapaswa uwe na chakula bora then uende kwenye maofisi mbalimbali kuwaconvice uwe unawapelekea chakula packaging direct katika maofisi yao ili mchana wasiangaike kwenda kwenye migahawa hii njia unaweza kutusua but inahitaji uwe na vitendea kazi kama bodaboda au bajaji ili kuzunguka katika maofisi mbalimbali
 
Dodoma sehemu sahihi ni katikati ya mji ambapo kweli sehemu jamaa wengi wamechukua hivyo utakutana na kizingiti cha kupata sehemu bora ya kufanyia biashara yako but pia nikupe wazo unaweza kuweka mgahawa wako pembezoni mwa mji ukawa una supply lunch maofisini direct means unapaswa uwe na chakula bora then uende kwenye maofisi mbalimbali kuwaconvice uwe unawapelekea chakula packaging direct katika maofisi yao ili mchana wasiangaike kwenda kwenye migahawa hii njia unaweza kutusua but inahitaji uwe na vitendea kazi kama bodaboda au bajaji ili kuzunguka katika maofisi mbalimbali
Asante kwa ushauri ndugu, appreciated!!
 
Habarini wanajamvi,

Nimekaa na kufikiria biashara ya kuwekeza japo milioni 1 kwa kipindi hiki cha uchumi mdororo na kutokana na ufinyu wa muda wangu nimepata wazo la kuwatafta mama Ntilie wa mtaani kama wawil watatu nikaboresha mazingra yao na kuwaongezea mtaji alafu tukaelewana pesa ya kunilipa kwa sku kwa mfano 20000 kwa kila mmoja wao.

Mwenye uelewa au ambae ashawahi kufanya hii naomba muongozo.

Nipo Dar, makazi yangu ya kudumu ni Ubungo.
 
Mama Ntilie wengi wanauza tu chakula lakini hawajitambui kabisa na wala hawajui chochote kuhusu biashara. In short niseme tu they are not serious - may be they just do it for fun
 
Sidhani kama umefanyya utafiti wa kutosha, hiyo hela ni nyingi mno na ili chakula kitoke kizuri ni gharama haswa.
 
Back
Top Bottom