Fahamu kuhusu biashara ya kuuza chakula (Mgahawa)

Fahamu kuhusu biashara ya kuuza chakula (Mgahawa)

Sidhani kama umefanyya utafiti wa kutosha, hiyo hela ni nyingi mno na ili chakula kitoke kizuri ni gharama haswa
Well said mkuu, yaani kwa mazingira na hali ya sasa ya maisha kuipata iyo pesa ni kasheshe na yeye pia awe amepata faida yake kando.
 
Wadau naombeni mnisaidie mawazo Nataka nianzishe biashara ya Mgahawa hapa dar sema natafta sehem Nzur ambapo naweza kuanzisha mgahawa wangu...naombeni mawazo yenu tafadhali
 
Jaribu kufanya utafiti mwenyewe ni sehem ipi nzuri kwako, cha kufanya angalia sehem ambayo inamkusanyiko mkubwa wa watu kwa mfano kwenye vituo vikubwa vya dala dala nk
 
Pia unaweza jaribu Maeneo ya jirani na vyuoni kama kule kikuyu(st. Johns) au Ngh'ongh'ona (UDOM) wateja ni uhakika cha msingi ujipange kuingia ktk bei za ushindani za ki uanafunzi(1000 to 1500 per meal). Jaribu kutembelea sehemu hizo uone wanafanyaje biashara, vitu wanavyo pendelea wanafunzi nk.
 
Katikati ya mji maeneo ya chakula yapo sehemu chache.
 
Habari wakuu, Nina wazo LA kufungua mgahawa Dodoma kwa mtaji wa milioni tano. Naombeni mawazo yenu ktk maeneo yafuatayo:

1. Eneo zuri kwa kufungua biashara tajwa kwa Dodoma
2. Bei za fremu kwa wenyeji wa Dodoma
3. Kama mtaji huo ni reasonable ukilinganisha na ushindani wa mji
4. Mambo machache ya kuzingatia kwa biashara ya mgahawa mjini Dodoma.
Asanteni...
Karibu Dodoma,njoo Uni PM sehem zipo kibao kuanzia Barbara yà 6,7,8,9,10 na 11.pia hiZo PESA zinatosha biashara Moja ambayo sitaitaja hapa.
 
Karibu Dodoma,njoo Uni PM sehem zipo kibao kuanzia Barbara yà 6,7,8,9,10 na 11.pia hiZo PESA zinatosha biashara Moja ambayo sitaitaja hapa.
Nitakutafuta nikirudi bongo kuanzia wiki ijayo kaka.
 
chamsingi uwe na chakula kizuri maana wengi pale hawajui kupika, halafu uwasambazie maofisini hapo utatusua maana wale hawana huduma nzuri wala kauli kwa wateja.
 
Usijaribu vyuoni, yan wakifunga chuo na ww biashara unafunga
 
Kuwa na makundi tofauti ya wateja na kupanga bei za vyakula kulingana na uwezo wa makundi hayo ya wateja ni kitu muhimu sana, wateja kwa mfano wale wa kipato cha kati na kipato cha chini ni wengi sana lakini unaweza usiwapate kwa sababu tu umeamua wewe mgahawa wako kuuza chakula kwa bei moja tu ya juu ukilenga upate faida kubwa.

Sikatai unaweza ukaweka chakula cha bei ya kuu kwa wateja wale wenye uwezo mkubwa lakini weka hata ugali na maharage, wali/ugali kwa mbogamboga za majani, mihogo ya kuchemsha, hivi ni kwa ajili tu ya wale wateja wadogowadogo ambao hawamudu vyakula vya bei kubwa. Kwa mtindo huo unaweza kukuta unapata wateja wengi sana na hivyo faida kuwa kubwa pia.
 
Good evening my guys!!

Helo mwana JF
Nataka kuanzisha mgahawa tafadhari mwenye uzoefu msaada kwa pm hata kwa malipo anisaidie jinsi navoweza kuanza Na Jinsi navoweza kupata faida
 
Jamani mmm natamani kuanzisha biashara ya kutengeneza milango ya aluminium! Nipo Dar naombeni usahauri
 
Good evening my guys!!

Helo mwana JF
Nataka kuanzisha mgahawa tafadhari mwenye uzoefu msaada kwa pm hata kwa malipo anisaidie jinsi navoweza kuanza Na Jinsi navoweza kupata faida
Hongera. Nenda kwenye mgahawa mkubwa jifunze kwa vitendo. Ila uhakika wa usafi, wafanyakazi ladha, muonekano na ubora wa chakula na lugha kwa wateja ndo uchawi wako mkuu
 
Ni biashara ya faida but ina risks nyingi

usafi

quality...ya chakula

location nzuri
 
Ushauri wa maneno ni mzuri ila wa vitendo ni mzuri zaidi. Hivyo basi tenga muda katika mizunguko yako nenda kwenye mgahawa unaoona wako vizuri na u aokisa unachokifikiria, pata huduma kisha ulizia unayotaka kujua. Utashangaa hata muhudumu tu anajua mengi sana yatakayo kufungua.macho pakuanzia. Kwa matomezo zaidi nenda muda usiobize. Ni namna fulani ya tafiti isio rasmi.
 
Back
Top Bottom