Nijuavyo mimi O/D Inatumika kuongeza mkandamizo wa pistoni hivyo kuipa engine nguvu.
Inakua On pale unapominya kitufe cha O/D na kwenye dashboard taa ya O/D itawaka na kuonyesha maandishi ya O/D OFF.
Na kitaalamu inatakiwa uminye O/D gari ikiwa kunzia spee 40 na kuendelea.
Du maelezo humu yanasigana sana. Nilikuwa nimeelewa lkn sasa nazidi kuconfuse kabisa.
mkuu hujaelewa nn?
Nikwamba ukiminya button, taa ya O/D Itawaka,na kwenye dashboard pata onekana maandishi ya taa nyekundu au blue ya O/D OFF= Hii inamana gari inatembea overdrive ikiwa on.
Ukiminya tena,taa ya O/D kwenye dashboard itazima = Hii inamaana gari inatembea overdrive ikiwa off.
Kweli mkuu wengi wanaendesha hizi automatic bila kujua matumizi sahihi ya OD/ON au OFF. Endapo unaendesha kasi na ukiwa hujaweka ON kwa maana ya kwamba hujaminya hako kabatani gari itakuwa inatumia mafuta mengi sana bila sababu na wakati huo huo utakuwa unai-overwork injini hivyo kuichosha haraka. Ile ukiiweka ON ukiwa katika mwendo wa kasi ya kuanzia spid ya km40 au 50 na kuendelea unaifanya gari kuwa nyepesi na hivyo hata mafuta kutumika kidogo. Watu wengi wameyalaumu magari yao kuwa yanatumia mafuta sana kumbe ni wao wanaokosea katika uendeshaji. Wengine huyapeleka kwa mafundi wakidai gari inabugia kiwese sana. Bahati mbaya mafundi wengi wa jua kali nao hawajui maana na matumizi ya Over drive hivyo kuishia kuichokonoa gari bila sababu. Na unapokuwa katika mwendo mdogo halafu umeweka Over drive ON unakuwa pia unaichosha gari kwa maana ya kuwa inakuwa Uncomfortable. Inakuwa ni kama vile umeweka gia namba 4 au 5 kwenye mwendo mdogo ambao ungehitaji gia namba 2 au 3. Ukiwa unaendesha mannual(ya kupanga gia) uatagundua haraka kwani gari inaweza kuzima unapolazimisha kutumia gia ndogo mahali inapohitaji kubwa. Hizi automatic ni zenyewe ni pole sana kwa maana ya kuwa huwa hazizimi unapokosea lakini madhara yake ni kuwa unakuwa unapunguza life span yake. Sasa wasiojua ndio utawsikia wakisema "automatic ni gari mbovu au hazidumu" kumbe wao ndio wabovu wa matumiziMkuu asante sana kwa elimu na ninaomba nichote hii post yako hapa. Nimekuwa nikiendesha na OD/OFF on muda mrefu sana bila kujua na nitakuwa nimechosha sana engine. Matokeo yake OD/OFF imeanza ku blink. Sasa kitaalam over use of it nipe ujuzi. Du nimesikitika sana.
Ukiminya kale kabatani na maandishi OD/OFF kufutika kwenye dsh board, maana yake unakuwa umeweka ON. Unapokwa hujakaminya kale kabatani na taa ya OD/FF ikiwa inawaka kwenye dash board maana yake ni kuwa Over drive iko OFF kama inavyosomeka kwenye dash board. Kwa ufupi ni kuwa inapokuwa ON hakuna maandishi yanayoonekana kwenye dash board yako yaani taa huwa inazima!Asanteni kwa Majibu mazuri; lakini samahani bado naona kuna shida kidogo hapo kwenye wakati gani O/D inakuwa On maana naona majibu yanasigana kidogo na baadhi ya waelimishaji; sasa napata shida hapa nishike lipi?
Lakini vinginevyo nimepata darasa zuri kabisa nashukuru sana.
Sijui gari yako ni aina gani. Lakini ukweli ni kuwa Ukiminya button, taa ya OD/OFF inazima na kwa maana hiyo unakuwa umeweka Over drive ON. Usipominya ile button taa nyekundu au kijani (rangi hutegeana na watengenezaji walivyochagua) inayoonesha maandishi OD/OFF itakuwa inawaka na kwa maana hiyo Over drive iko OFF kama inavyosimeka.mkuu hujaelewa nn?
Nikwamba ukiminya button, taa ya O/D Itawaka,na kwenye dashboard pata onekana maandishi ya taa nyekundu au blue ya O/D OFF= Hii inamana gari inatembea overdrive ikiwa on.
Ukiminya tena,taa ya O/D kwenye dashboard itazima = Hii inamaana gari inatembea overdrive ikiwa off.
mkuu hujaelewa nn?
Nikwamba ukiminya button, taa ya O/D Itawaka,na kwenye dashboard pata onekana maandishi ya taa nyekundu au blue ya O/D OFF= Hii inamana gari inatembea overdrive ikiwa on.
Ukiminya tena,taa ya O/D kwenye dashboard itazima = Hii inamaana gari inatembea overdrive ikiwa off.
Hii ON na OFF inachanganya...Mbalamwezi;561997]Keizer, Ndege ya Uchumi salaam!
Kwa lugha rahisi, OD ni gia namba 5 ambayo inakupa mwendo uliotulia, wa kasi lakini kwa mzunguko mdogo wa injini (RPM). Hii hukuwezesha kuwa na matumizi madogo ya mafuta pengine kwa kasi zaidi.
Unaweza kuitumia pia ikiwa unataka kuipita motakaa nyingine, mathalan, kwenye kilima ambapo nawe motakaa yako inakuwa umepungua nguvu, hivyo unaweza kuiweka off (hapa unakuwa kama umerudisha namba 4), na injini itabadili kasi ya mzunguko, utaiweka uklisha maliza tena matumizi yake.
Eneo lingine, ni mara gurudumu la motaklaa yako linapopasuka. Ikitokea hivyo, unaweza kuondoa OD, huku ukiwa umeacha kukanyaga pedeli ya mafuta, kwa maana ndiyo utakuwa unaomba mwendo upungue pasi na kukanyaga breki. Katika hali kama hii, utakuwa umesaidia kupunguza mwendo wa gari wakati ukithibiti muelekeo wa motokaa pia.
Watu wengine katika hali kama hii huwa wanakanyaga breki. Kufanya hivi ni hatari, maana unasimamisha kabisa mwendo wa gurudumu lililopasuka, na matokeo yake mwendo wa motokaa, badala ya kwenda mbele, itajaribu kutii amri ya gurudumu linalogomea motokaa kwenda mbele na kuamua kwenda upande wa gurudumu lilipasuka, nikiwa na maana kwamba hapo motokaa itakuwa inaacha njia na au kupinduka.
Kwa giaboksi zenye kujibadili zenyewe, ni vema basi tukaziacha OD zijiendeshe zenyewe, maana kuziondoa hatari yake ni kuwa unaweza kusahau kuiweka tena unapokwenda zaidi ya km 70 kwa saa, mfano barabara ya Nyerere, na kusababisha matumizi makubwa ya nishati ya kuendeshea mtambo.
By Mbalamwezi
Keizer, Ndege ya Uchumi salaam!
Kwa lugha rahisi, OD ni gia namba 5 ambayo inakupa mwendo uliotulia, wa kasi lakini kwa mzunguko mdogo wa injini (RPM). Hii hukuwezesha kuwa na matumizi madogo ya mafuta pengine kwa kasi zaidi.
Unaweza kuitumia pia ikiwa unataka kuipita motakaa nyingine, mathalan, kwenye kilima ambapo nawe motakaa yako inakuwa umepungua nguvu, hivyo unaweza kuiweka off (hapa unakuwa kama umerudisha namba 4), na injini itabadili kasi ya mzunguko, utaiweka uklisha maliza tena matumizi yake.
Eneo lingine, ni mara gurudumu la motaklaa yako linapopasuka. Ikitokea hivyo, unaweza kuondoa OD, huku ukiwa umeacha kukanyaga pedeli ya mafuta, kwa maana ndiyo utakuwa unaomba mwendo upungue pasi na kukanyaga breki. Katika hali kama hii, utakuwa umesaidia kupunguza mwendo wa gari wakati ukithibiti muelekeo wa motokaa pia.
Watu wengine katika hali kama hii huwa wanakanyaga breki. Kufanya hivi ni hatari, maana unasimamisha kabisa mwendo wa gurudumu lililopasuka, na matokeo yake mwendo wa motokaa, badala ya kwenda mbele, itajaribu kutii amri ya gurudumu linalogomea motokaa kwenda mbele na kuamua kwenda upande wa gurudumu lilipasuka, nikiwa na maana kwamba hapo motokaa itakuwa inaacha njia na au kupinduka.
Kwa giaboksi zenye kujibadili zenyewe, ni vema basi tukaziacha OD zijiendeshe zenyewe, maana kuziondoa hatari yake ni kuwa unaweza kusahau kuiweka tena unapokwenda zaidi ya km 70 kwa saa, mfano barabara ya Nyerere, na kusababisha matumizi makubwa ya nishati ya kuendeshea mtambo.
Karibu mkuu,hii ndio tofauti ya JF na mitandao mingine ya kijamii.Ahante kwa elimu hii, sikuwa hata najua maana yake hii, nimetembea O/D ikiwa off kwa maana ya taa kuwa kwenye dash board kwa muda kidogo, leo ndio nimejua nini ni nini
JF na idumu
[/QUOTE]Hii ON na OFF inachanganya...