Fahamu kuhusu utando mweupe kwenye mwili mtoto anapozaliwa

Fahamu kuhusu utando mweupe kwenye mwili mtoto anapozaliwa

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Joined
Aug 7, 2018
Posts
685
Reaction score
1,124
1676870466514.png

Ni utando mweupe unaotengenezwa kwenye ngozi ya mtoto kwenye kipindi cha mwisho cha ujauzito, kitaalam huitwa Vernix caseosa.

Huundwa na maji kwa asilimia 80, mafuta kwa asilimia 10 na protini kwa asilimia 10.

Tofauti na jinsi inavyoaminika sana mtaani, utando huu hautokani na kushiriki tendo la ndoa karibu na muda wa kujifungua.

Vernix siyo shahawa, wala haina uhusiano wowote na kitu hicho. Hii inatokana na muundo wa anatomia ya mfumo wa uzazi wa mwanamke ambao huufunga mji wa uzazi kwa kuta imara zisizo ruhusu kuingia kwa shahawa zinazotolewa wakati wa kushiriki tendo la ndoa.

Pia, ifahamike kuwa watoto waliozaliwa wakati sahihi huwa na kiasi kikubwa cha utando huu huku waliozaliwa kwa kupitiliza siku zao huzaliwa na utando kidogo sana.

Kazi zake
• Kuzuia maambukizi ya magonjwa ya ngozi kwa watoto wakati akiwa tumboni na baada ya kuzaliwa.
• Kupunguza msuguano kati ya mama na mtoto wakati wa kujifungua.
• Kutunza joto la wastani linalofaa kwa ajili ya ukuaji wa siku za mwanzo za mtoto.
• Kuipatia ngozi ya mtoto unyevu unaostahili.
• Kuzuia ngozi ya mtoto isiharibike na mabadiliko ya hali ya hewa.

Kwa kuwa mtoto huelea kwenye mfuko wa uzazi uliojaa maji (maji ya uzazi) kwa miezi mingi sana, huwa ni lazima utando huu utengenezwe ili kuilinda ngozi ya mtoto kwanza akiwa bado anaelea tumboni kisha baada ya kuzaliwa.

Baada ya kuzaliwa, utando huu huanza kuisha wenyewe taratibu ukichukua siku hadi wiki kadhaa.

Cc: Mr kenice
 
Swali fikirishi....🤔🤔🤔

Binadamu akiwa kwenye maji hawezi kupumua ama awe na vyombo maalum vya kumpatia hewa. Sababu mapafu yanahitaji oxygen....

Sasa hawa watoto wachanga wanapokuwa tumboni mwa mama zao..... wanapumuaje?
Kama mtoto anakuwa anaelea kwenye majimaji yaliyomo ndani ya mfuko wa uzazi, hawapaliwi na hayo maji yakiingia puani?

Au mfumo wa mapafu unakuwa haujaanza kufanya kazi?

Tafadhali nifafanulie hapo kama hutojali.
 
Swali fikirishi....[emoji848][emoji848][emoji848]

Binadamu akiwa kwenye maji hawezi kupumua ama awe na vyombo maalum vya kumpatia hewa. Sababu mapafu yanahitaji oxygen....
Ngoja nisubirie majibu ili na mimi nijifunze.
 
Swali fikirishi....🤔🤔🤔

Binadamu akiwa kwenye maji hawezi kupumua ama awe na vyombo maalum vya kumpatia hewa. Sababu mapafu yanahitaji oxygen...
Mkuu, habari?

Mtoto anapokuwa tumboni hupata mahitaji yake yote ya hewa, virutubisho pamoja na kutoa takamwili kupitia kitovu ambacho humuunga na mama yake kwenye kondo la uzazi.

Anapozaliwa na kukatwa kitovu ndipo mapafu hufunguka pamoja na mifumo mingine ya mwili huanza kufanya kazi. Kulia kwa mtoto ni ishara ya maumivu anayopata baada ya hewa kuingia kwa kasi kwenye mapafu, ishara ya kwamba sasa anavuta hewa na kujitegema mwenyewe.

Hivyo, kwa maana rahisi kabisa, akiwa bado tumboni hutegemea kila kitu kutoka kwa mama yake.
 
Swali fikirishi....[emoji848][emoji848][emoji848]

Binadamu akiwa kwenye maji hawezi kupumua ama awe na vyombo maalum vya kumpatia hewa. Sababu mapafu yanahitaji oxygen..
Placenta ya mama husaidia mtoto "kupumua" wakati anapokua tumboni. Oksijeni na kaboni dioksidi hupita kupitia damu kwenye placenta. Zaidi ya hayo huenda kwenye moyo na inapita kupitia mwili wa mtoto. Wakati wa kuzaliwa, mapafu ya mtoto hujazwa na maji.
 
Swali fikirishi....🤔🤔🤔

Binadamu akiwa kwenye maji hawezi kupumua ama awe na vyombo maalum vya kumpatia hewa. Sababu mapafu yanahitaji oxygen...
Kuna Ile wanaita placenta ambapo inaunganisha mtoto na mama Kwa Ile mrija wanaita umbilical cord.

Na hio ndo inasafirisha kila kitu kuanzia oxygen, virutubisgo, na mazagmazaga mengine.
 
hii ndio huku uswahilini wanasema mam alikua anatumika na baba had mtoto akatoka na manii binadam hawaishi vituko
Me pia nlijua hvoo kumbe sivyo.
Huku kwetu Wana husianisha na Imani tofauti sana.
 
"Epuka Imani Potofu, Epuka Imani Potofu"

Usimkatae mwanao pindi atakapo zaliwa na white stuff, Wengi wanafikiria kwamba hutokana na kamwagiwa ndani katika kipindi cha Ujauzito,

Nikutoe hofu, Kitaalamu hujulikana kama "Vernix Caseosa" Ni hali ya kawaida na hutokea kwa wanawake wachache sana,

NB: Hakuna uhusiano katika ya white stuff kwa mtoto na tendo, Kumbuka kushiriki tendo kipindi cha uzazi hakuna madhara yeyote...✍
 
Mkuu, habari?

Mtoto anapokuwa tumboni hupata mahitaji yake yote ya hewa, virutubisho pamoja na kutoa takamwili kupitia kitovu ambacho humuunga na mama yake kwenye kondo la uzazi.

Anapozaliwa na kukatwa kitovu ndipo mapafu hufunguka pamoja na mifumo mingine ya mwili huanza kufanya kazi. Kulia kwa mtoto ni ishara ya maumivu anayopata baada ya hewa kuingia kwa kasi kwenye mapafu, ishara ya kwamba sasa anavuta hewa na kujitegema mwenyewe.

Hivyo, kwa maana rahisi kabisa, akiwa bado tumboni hutegemea kila kitu kutoka kwa mama yake.

Safi sana kiongozi
 
Swali fikirishi....🤔🤔🤔

Binadamu akiwa kwenye maji hawezi kupumua ama awe na vyombo maalum vya kumpatia hewa. Sababu mapafu yanahitaji oxygen....

Sasa hawa watoto wachanga wanapokuwa tumboni mwa mama zao..... wanapumuaje?
Kama mtoto anakuwa anaelea kwenye majimaji yaliyomo ndani ya mfuko wa uzazi, hawapaliwi na hayo maji yakiingia puani?

Au mfumo wa mapafu unakuwa haujaanza kufanya kazi?

Tafadhali nifafanulie hapo kama hutojali.
Mtoto hapumulii mapafu yake akiwa tumboni hupata oksijen kupitia plasenta ya muunganiko wa mama na MTOTO yaani hewa au gaseous exchange hufanyika kupitia plasenta humonkuna mishipa inayopeleka damu ya oksijen kwa mtoto na ile inayotoa damu chafu TOKA KWA MTOTO kwenda KWA mama!!!
 
Back
Top Bottom