Fahamu mambo mbalimbali kuhusu Kilimo cha Korosho

Timtim

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2008
Posts
608
Reaction score
124


Naomba niwasilishe kutaka kuelezwa zaidi juu ya kilimo cha Korosho kwa Mkoa wa Pwani. Naomba mwenye kuelewa atufahamishe mimi na wengine gharama toka awali za kupanda mikorosho katika shamba la ekari 20. Gharama na takwimu hadi kuvuna na kiasi cha mavuno kwa mwaka.

Natanguliza shukrani zangu.

WADAU WENGINE WANAOHITAJI UELEWA WA KILIMO HIKI

MICHANGO YA WADAU




 
Hii kitu hii!

Wameacha kukopa, kulipwa hela nusu, nyingine mpaka wakauze mzigo india? Mikorosho mizuri mbegu za india, inakua mifupi kama miembe ya kisasa, inazaa baada ya miaka 3, mazao yanaongezeka kadri ya matunzo na muda.
 
Heshima kwenu wakuu

Kutokana na bei ya korosho kukaa vizur nimepata wazo la kupanda mikorosho maeneo ya Rufiji.

Kwa anayejua idadi ya niche ya mikorosho kwa heka moja anisaidie na distance kati ya mche na mche ni mita ngapi?

Na pia nitumie mbegu gani nzuri ambayo hutoa mazao mengi mazuri.

Asante
 
Habari wajasiriamali.

Ni kijana mwenzenu ambaye ni mkulima wa korosho mkoani Mtwara wilaya ya Tandahimba. Kesho naenda kutembelea na kufanya farmer works na kurudi home.

Nitawajulisha nikifika. Inshaaalah

great thinker
 
Ukifika usiache kunitag kutupa update
 
Hiki tunaita kilimo cha SIMU!! Yaani unalima kwa simu, unapalilia kwa simu, unaweka mbolea kwa simu na unavuna kwa simu!! Kuwa makini mkuu kilimo ni uti uti wa mgongo wa taifa, hakiitaji ulelemama!!
Kulima sio lazima uwepo kila siku eneo la field.Huu ni mwaka wangu wa pili kulima hili zao. Last year nilipata mafinikio mazuri tu.

great thinker
 
Kulima sio lazima uwepo kila siku eneo la field. Huu ni mwaka wangu wa pili kulima hili zao. Last year nilipata mafinikio mazuri tu.

great thinker
Kwani linalimwa Mara 2 Mkuu? Ukilima mara moja si basi.
 
Hiki tunaita kilimo cha SIMU!! Yaani unalima kwa simu, unapalilia kwa simu, unaweka mbolea kwa simu na unavuna kwa simu!! Kuwa makini mkuu kilimo ni uti uti wa mgongo wa taifa, hakiitaji ulelemama!!
Mkuu umenikumbusha kipindi flani niliwahi lima kwa simu basi jamaa yangu ananambia twende tufike tushuhudie mie namwambia namwamini jamaa.

Nikampa mkwanja wa debe 4 animwagie mpunga heka 4 si akachukua mbegu zake (za hovyo ndo kamwagia) kuja kwenda umeota mbali na alilima hovyo majani yamejaa.

Basi namwomba ushauri jamaa yangu tufanyaje ananijibu twende town tumrushie jamaa mkwanja atamaliza kila kitu. Nilikuwa nakasirika sana. Tangu hapo lazima nifike sehemu nijionee.
 

Pole sana mkuu vipi uliacha au still unaendelea na kilimo.

great thinker
 
Ilishanitokea hata mimi mkuu sina hamu na kilimo cha simu!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…