Fahamu tofauti kati ya Eid ul-Fitr na Eid ul-Adha

Fahamu tofauti kati ya Eid ul-Fitr na Eid ul-Adha

Ahsante ndugu muulizaji na kwa faida ya wengine. Sisi waisilamu tuna miezi yetu ya kiisilamu ambayo ni miezi 12, miezi hii kwa lugha ya kiswahili tunaidadavua kama wa Mfungo.

Eidil-Fitir
(siku kuu ya kula) hii ni siku kuu baada ya kumaliza funga ya swaum katika Mwezi wa Ramadhan ambao kwa kiswahili mwezi wa Ramadhani huitwa mfungo 12. Ramadhan ndio jina la mwezi wa 9 wa kiisilamu, kwa kiswahili ni mfungo 12. Mwezi huo wa Ramadhan, ni lazima waisilamu wafunge mwezi mzima, na wakimaliza kufunga wanasheherekea siku kuu ya kula inaitwa EIDIL - FITR.
Ramadhan = september = mwezi wa 9 = mfungo 12 kwa kiswahili

Eidil- Adh-ha ambayo pia huitwa Eidil-Hajj (Siku kuu ya kuchinja au Siku kuu ya Hija). Hii ni siku kuu ambayo hupatikana kwenye mwezi wa 12 wa kiisilau unaoitwa DHUL-HIJA ambao kwa kiswahili ni mfungo 3. Katika mwezi huu ndio mwezi ambao waisilamu wanatakiwa waende kuhijji Makka (kutufu madhambi), huu ndio mwezi wa 12 yaani mwisho wa mwaka wa kiisilamu, kwa hivyo kwa tukio la wao kwenda kuhijji na kumaliza hijja ndio inatakiwa kusheherekea na ndio maana ikaitwa EIDIL-HAJJ (Siku kuu ya hija). Lakini pia tarehe kama hizo kuna tukio kubwa lilitokea, ambapo Ibrahim alimriwa amchinje Ismail, na kafara yake akachinjwa mnyama. Kwa tukio hilo ndio ikaitwa pia Eidi ya kuchinja yaani (Eidil-Adh-ha).
Dhul-hija = December = mwezi wa 12 = mfungo 3 kwa kiswahili.

Hapa chini nimekuwekea orodha ya miezi ya kiisilamu kama utapenda kuisoma

Mwezi wa 1 unaitwa MUHARAMU = Kwa kiswahili ni Mfungo 4
Mwezi wa 2 unaitwa SWAFAR = Kwa kiswahili ni Mfungo 5
Mwezi wa 3 unaitwa RABIUL-AWAL = Kwa kiswahili ni Mfungo 6

Mwezi wa 4 unaitwa RABIUL-AKHIR = Kwa kiswahili ni Mfungo 7
Mwezi wa 5 unaittwa JAMADIL-AWAL = Kwa kiswahili ni Mfungo 8
Mwezi wa 6 unaitwa JAMADIL-THANI =Kwa kiswahili ni Mfungo 9

Mwezi wa 7 unaitwa RAJABU = Kwa kiswahili ni Mfungo 10
Mwezi wa 8 unaitwa SHAABAN = Kwa kiswahili ni Mfungo 11
Mwezi wa 9 unaitwa RAMADHAN = Kwa kiswahili ni Mfungo 12

Mwezi wa 10 unaitwa SHAUWAL = Kwa kiswahili ni Mfungo Mosi
Mwezi wa 11 unaitwa DHUL-KADA = Kwa kiswahili ni Mfungo pili
Mwezi wa 12 unaitwa DHUL-HIJA = Kwa kiswahili ni Mfungo tatu

Hayo masuala ya mfungo 3 na mfungo 6 ni mambo ya kipuuzi ambayo tunatakiwa tuachane nayo, Tuache kuipeleka dini kimazoea
 
Ahsante ndugu muulizaji na kwa faida ya wengine. Sisi waisilamu tuna miezi yetu ya kiisilamu ambayo ni miezi 12, miezi hii kwa lugha ya kiswahili tunaidadavua kama wa Mfungo.

Eidil-Fitir
(siku kuu ya kula) hii ni siku kuu baada ya kumaliza funga ya swaum katika Mwezi wa Ramadhan ambao kwa kiswahili mwezi wa Ramadhani huitwa mfungo 12. Ramadhan ndio jina la mwezi wa 9 wa kiisilamu, kwa kiswahili ni mfungo 12. Mwezi huo wa Ramadhan, ni lazima waisilamu wafunge mwezi mzima, na wakimaliza kufunga wanasheherekea siku kuu ya kula inaitwa EIDIL - FITR.
Ramadhan = september = mwezi wa 9 = mfungo 12 kwa kiswahili

Eidil- Adh-ha ambayo pia huitwa Eidil-Hajj (Siku kuu ya kuchinja au Siku kuu ya Hija). Hii ni siku kuu ambayo hupatikana kwenye mwezi wa 12 wa kiisilau unaoitwa DHUL-HIJA ambao kwa kiswahili ni mfungo 3. Katika mwezi huu ndio mwezi ambao waisilamu wanatakiwa waende kuhijji Makka (kutufu madhambi), huu ndio mwezi wa 12 yaani mwisho wa mwaka wa kiisilamu, kwa hivyo kwa tukio la wao kwenda kuhijji na kumaliza hijja ndio inatakiwa kusheherekea na ndio maana ikaitwa EIDIL-HAJJ (Siku kuu ya hija). Lakini pia tarehe kama hizo kuna tukio kubwa lilitokea, ambapo Ibrahim alimriwa amchinje Ismail, na kafara yake akachinjwa mnyama. Kwa tukio hilo ndio ikaitwa pia Eidi ya kuchinja yaani (Eidil-Adh-ha).
Dhul-hija = December = mwezi wa 12 = mfungo 3 kwa kiswahili.

Hapa chini nimekuwekea orodha ya miezi ya kiisilamu kama utapenda kuisoma

Mwezi wa 1 unaitwa MUHARAMU = Kwa kiswahili ni Mfungo 4
Mwezi wa 2 unaitwa SWAFAR = Kwa kiswahili ni Mfungo 5
Mwezi wa 3 unaitwa RABIUL-AWAL = Kwa kiswahili ni Mfungo 6

Mwezi wa 4 unaitwa RABIUL-AKHIR = Kwa kiswahili ni Mfungo 7
Mwezi wa 5 unaittwa JAMADIL-AWAL = Kwa kiswahili ni Mfungo 8
Mwezi wa 6 unaitwa JAMADIL-THANI =Kwa kiswahili ni Mfungo 9

Mwezi wa 7 unaitwa RAJABU = Kwa kiswahili ni Mfungo 10
Mwezi wa 8 unaitwa SHAABAN = Kwa kiswahili ni Mfungo 11
Mwezi wa 9 unaitwa RAMADHAN = Kwa kiswahili ni Mfungo 12

Mwezi wa 10 unaitwa SHAUWAL = Kwa kiswahili ni Mfungo Mosi
Mwezi wa 11 unaitwa DHUL-KADA = Kwa kiswahili ni Mfungo pili
Mwezi wa 12 unaitwa DHUL-HIJA = Kwa kiswahili ni Mfungo tatu
Asante, nimesoma nakuelewa, nikuongeze swali dogo, nimeona mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa 9 na ndio pekee huwa mnafunga, sasa kwanini na hii miezi mingine nayo mmeipa majina ya "mfungo" wakati huwa hamfungi?
 
Kwenye Biblia Isaka ndo alitakiwa kutolewa kafara alf kwenye Quran Ishmael ndo alitakiwa kutolewa sadaka

Kila mtu anavutia upande wake
 
Asante, nimesoma nakuelewa, nikuongeze swali dogo, nimeona mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa 9 na ndio pekee huwa mnafunga, sasa kwanini na hii miezi mingine nayo mmeipa majina ya "mfungo" wakati huwa hamfungi?
Kabla ya yote itambulike kuwa mwezi mtukufu wa Ramadhani na ambao ndio mwezi maarufu zaidi kwa walio wengi ni mwezi wa tisa(9) katika mpangilio wa miezi 12 ya kiislam.
Lakini kutokana na taratibu za kimila na kitamaduni kwa kuwa mwezi wa Ramadhani ni mwezi wa mfungo basi ilizoeleka kuiita miezi mingine ya kiislam kwa kuipa namba ya kuwa ni mwezi wa ngapi kufungua baada ya mwezi wa mfungo ambao ni Ramadhani, hivyo mwezi wa kwanza kufungua baada ya Ramadhani ambao ni Shawwal uliitwa mfunguo mosi au "Mfungo mosi" , mwezi wa pili kufungua tokea kuisha kwa Ramadhani ambao ni Dhulqaa'dah nao uliitwa mfunguo pili au "Mfungo pili" nakuendelea kama inavyooneshwa hapa chini

9.Ramadhani (mwezi wa mfungo)
10.Shawwal (Mfungo mosi)
11.Dhulqaa'dah (Mfungo pili)
12.Dhul-Hijjah (Mfungo tatu)
1.Muharram (Mfungo nne)
2.Swafar (Mfungo tano)
3.Rabiiu'l awwal (Mfungo sita)

Hivyo kwa maana hiyo hata Rabiiu' thaani ungeweza kuitwa "mfungo saba" na Rajab ungeweza kuitwa mfungo au "mfunguo 10" kwa kuwa ni mwezi wa 10 tokea kufungua Ramadhani iliyopita na Shaaban kuitwa kama mfungo au "mfunguo 11" kwa kuwa ni mwezi wa 11 tokea kufungua Ramadhani iliyopita.
 
Ila Dah jamaa ni bingwa wa kucopy kupaste na kuformat. Kahamisha Mengi kutoka kwenye biblia alivyokuwa anaanzisha dini yake. Ja ajabu kapotezea kabisa story ya Samson alivyokuwa anagawa dozi za uhakika kwa wapalestina. Sijui kwa nini hii alikwepa kucopy na kupaste
Vipi Mtume wetu Muhammad (s.a.w) atacopy na kupaste ilihali alikuwa hajui kusoma wala kuandika, hiyo nayo ni miujiza iliyo tukuka
 
Kwanini mwezi wa Ramadhan mnauita mwezi wa haki,miezi mingine siyo ya kutenda haki?

Kwanini wakati wa mwezi wa Ramadhan misikiti inajaa lakini sasa hivi ni mitupu?
Je,ni sahihi kuacha dhambi mwezi wa Ramadhan na kuendelea kutenda dhambi miezi mingine?
 
Ndo hapo sasa alivyoandika mwenyewe akiwa pangoni akianzisha dini yake malaika Gabriel yeye kamtungia Jina Jibril akawa anamuambia andika mafungu ya kurani akawa anamuangalia tu Gabriel akampazia sauti andika Mudi akawa anamuangalia tu. Gabriel akamaindi akaanza kumshushia kibano kikali cha haja. Jamaaa alilia kwa uchungu sana na kumuambia Gabriel unanionea tu sasa nitaandikaje wakati sijui kusoma na kuandika.

Gabriel akasema tu FAK.

Siyo mimi ni mudi mwenyewe kaandika.

[/USER] EINSTEIN112
Ungelikuwa haupo kwa ajili ya chuki ningelikujuza zaidi, lakini kwakuwa umejawa chuki, fitina na hasadi haufai hata kuwa mkristo, kwasababu wakristo hawako namna hiyo. Angalia wenzako wanavyojadiliana kwenye comment
 
Kwanini mwezi wa Ramadhan mnauita mwezi wa haki,miezi mingine siyo ya kutenda haki?

Kwanini wakati wa mwezi wa Ramadhan misikiti inajaa lakini sasa hivi ni mitupu?
Je,ni sahihi kuacha dhambi mwezi wa Ramadhan na kuendelea kutenda dhambi miezi mingine?
Ahsante, uisilamu unahimiza kutenda haki na kusimamia haki, hivyo swala la kutenda haki halifungamani na mwezi bali ni muongozo wa dini kwa aujumla. Kwa hivyo ambaye hatendi haki katika miezi mingine huyo bado hajaufahamu uisilamu na bado imani yake ina ukakasi. Swala la kutenda haki halifungamani na mwezi bali ni mfumo mzima wa maisha ya mwanaadamu anatakiwa kuishi kwenye haki.

Misikiti inajaa mwezi huu mtukufu wa ramadhan kwasababu ni mwezi wenye fadhila nyingi, ni mwezi wenye rehema nyingi na pia ni mwezi ambao Mwenyezi MUNGU huacha wazi milango ya toba kwa ajili ya watu kuomba msamaha kutokana na madhambi yao, ndio maana watu wengi hujaa misikitini. Lakini kwa ujumla mwenye kuendelea kutenda dhambi baada ya Ramadhan huyo anachukuliwa kama mtu mwenye kumfanyia mzaha Mwenyezi MUNGU. Hata katika miezi mingine haipaswi muisilamu kutenda madhambi.
 
Asante, nimesoma nakuelewa, nikuongeze swali dogo, nimeona mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa 9 na ndio pekee huwa mnafunga, sasa kwanini na hii miezi mingine nayo mmeipa majina ya "mfungo" wakati huwa hamfungi?

hilo neon mfungo halina mahusiano ya dini, ni mazoea ya waswahili tu
 
Back
Top Bottom