Fahamu vitu vinavyotofautisha gharama za ujenzi kwenye majengo yenye kufanana mchoro

Fahamu vitu vinavyotofautisha gharama za ujenzi kwenye majengo yenye kufanana mchoro

Hongera kwa elimu uliyoitoa kuhusiana na baadhi ya mambo ya msingi kuhusu ujenzi.Asilimia kubwa ya watu wanaogopa kuanza ujenzi moja ya sababu ikiwa ni kukosa uelewa kuhusu mchakato mzima wa ujenzi.

Mbali ya elimu ya darasani,elimu itokanayo na uzoefu kazini ni muhimu sana jambo ninaloliona kwako. Japo baadhi wameonekana kukushambulia ila kwa mtazamo wangu uzoefu ulionao ni muhimu sana hasa hasa katika fani ya ujenzi.
Ushauri wangu kwako ni kuendelea kujielimisha kwani kutokana ukuaji wa teknolojia zipo mbinu mpya za ujenzi zenye kupunguza gharama za ujenzi.

Ushauri wangu kwa wanaotarajia kujenga na wataalam wa ujenzi, wasifanye mambo kwa mazoea kwani zipo style nyingi za ujenzi zenye kutumia gharama ndogo kwa mfano matumizi ya interlocking block,semi prefabricated slab(hii ni aina mpya ya ujenzi wa slab(jamvi) yenye kutumia nondo kidogo na zege kidogo bila kuathiri ubora).

Pia ningependa kushauri wengi wetu tujenge tabia ya kuwatumia watalaamu katika hatua za mwanzo kabla ya kuanza ujenzi. Tumia wataalam kupata ushauri na wakuandalie ramani kulingana na mahitaji yako kwani hii inaweza kukusaidia kupunguza gharama zinazoweza kujitokeza baadae.

Mwisho kabisa kwako fundi naomba unieleweshe tiles nzuri zenye ubora ni zipi? Bei yake ikoje? Na katika box moja zinakuwa tiles ngapi na size gani?

Ahsante.


Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu interlocking blocks ndiyo zikoje ?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hongera kwa elimu uliyoitoa kuhusiana na baadhi ya mambo ya msingi kuhusu ujenzi.Asilimia kubwa ya watu wanaogopa kuanza ujenzi moja ya sababu ikiwa ni kukosa uelewa kuhusu mchakato mzima wa ujenzi.

Mbali ya elimu ya darasani,elimu itokanayo na uzoefu kazini ni muhimu sana jambo ninaloliona kwako. Japo baadhi wameonekana kukushambulia ila kwa mtazamo wangu uzoefu ulionao ni muhimu sana hasa hasa katika fani ya ujenzi.
Ushauri wangu kwako ni kuendelea kujielimisha kwani kutokana ukuaji wa teknolojia zipo mbinu mpya za ujenzi zenye kupunguza gharama za ujenzi.

Ushauri wangu kwa wanaotarajia kujenga na wataalam wa ujenzi, wasifanye mambo kwa mazoea kwani zipo style nyingi za ujenzi zenye kutumia gharama ndogo kwa mfano matumizi ya interlocking block,semi prefabricated slab(hii ni aina mpya ya ujenzi wa slab(jamvi) yenye kutumia nondo kidogo na zege kidogo bila kuathiri ubora).

Pia ningependa kushauri wengi wetu tujenge tabia ya kuwatumia watalaamu katika hatua za mwanzo kabla ya kuanza ujenzi. Tumia wataalam kupata ushauri na wakuandalie ramani kulingana na mahitaji yako kwani hii inaweza kukusaidia kupunguza gharama zinazoweza kujitokeza baadae.

Mwisho kabisa kwako fundi naomba unieleweshe tiles nzuri zenye ubora ni zipi? Bei yake ikoje? Na katika box moja zinakuwa tiles ngapi na size gani?

Ahsante.


Sent using Jamii Forums mobile app
Interlocking ata mimi nimezifikiria maana ata cost ya kupaka rangi unaiondoa ila naonaga kama zinapooza sana kimwonekano. Hivi huwezi mtu uka mix baadhi ya kuta zikawa interlocking na nyengine ziwe blocks za kawaida.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu interlocking blocks ndiyo zikoje ?

Sent using Jamii Forums mobile app

Hizi ni aina ya tofali zinatengenezwa kwa kuchanganya soil and cement,ziko katika muundo unaozipa uwezo wa kuvaana(interlock) hivyo upangaji wake wakati wa ujenzi utumia mortar(cement and cement) bila kiathiri uimara wa joint zake.

Zimetumika maeneo mengi kwa mfano katika ujenzi wa nyumba za makazi na shule.Pia unaweza zitumia katika ujenzi wa ghorofa inayoshikiliwa na nguzo& beam za zege.

Uzoefu umethibitisha kuwa zinagunguza gharama za ujenzi kwa kiasi kikubwa.Angalia picha hizo kwa muonekano wake katika ujenzi
IMG_7559.JPG
IMG_7560.JPG
IMG_7561.JPG



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapa nitaelezea Sababu za msingi zinazosababisha majengo yanayofanana kujengwa kwa gharama tofauti.

Tuzungumzie mchoro wa nyumba ya vyumba vitatu vya Kulala kimoja kati ya hivyo ni master bedroom, sitting room, dining, kitchen ,public toilet na store.
Mchoro aliununua ndugu anaitwa Juma, baada ya Juma kununua Alitoa copy akawapa majirani zake wawili Hasani na John.

Hawa wote walijengewa na fundi mmoja ambae ni mimi. Lkn Kila mtu kutumia gharama tofauti kusimamisha boma.

SABABU ZA MSINGI ZA KUFANYA GHARAMA ZA UJENZI ZITOFAUTIANE :

1. location
2. Uimara
3.land type. (slop au tambalale)
4.soil type
5.nyakati.

HAPA NITAZUNGUMZIA UIMARA
Msingi wa nyumba imara utajengwa Kama ifuatavyo.
. Utachimbwa kwenda chini urefu WA mita moja au zaidi.
. Utaanza na zege yenye ratio nzuri kabla ya kujenga tofali
.Utajengwa kwa tofali imara
.Utawekewa Beam yenye kusukwa nondo na ratio nzuri
.Utamwagiliwa maji ya kutosha.
ILI HAYA YOTE YAFANYIKE LAZIMA UMPATE FUNDI MZURI.

Juma aliomba nyumba yake nimjengee kwa viwango hivyo, ndio maana nilitumia tofali nyingi,cement nyingi, nondo nyingi, mchanga mwingi, kokoto nyingi, ring za kutosha, maji mengi nk. Ktk kujenga msingi.

John alisema uwezo wake mdogo , yeye alihitaji tuchimbe futi moja kwenda chini baada ya hapo tujenge tofali, hakuishia hapo pia alisema tusiweke Beam.

Kilichotekea ni utofauti wa Tshs zaidi ya million nne kati ya hiyo misingi miwili.

Kiufupi Juma alitumia 6mil
John Tshs 2.8mil
Hasani Tshs 4mil.

Kilichotofautisha ni uimara WA kujenga msingi. Hawa wote ni majirani.

Mpaka tunamaliza boma Juma alitumia 18m
John 7m
Hasani 12m.
Nyumba zote hizi zikipigwa rangi vizuri hutoweza kujua madhaifu ya awali mpaka pale utakapoanza kuona nyufa (expansion joint)

Hoja yangu hapa ni kwamba unapotokea mjadala wa gharama za ujenzi LAZIMA tuzingatie vitu mhimu vinavyosababisha gharama kuwa kubwa au ndogo.

Ushauri.
1.Tusipende kukimbilia kununua nyumba wakati hujui ilijengwa kwa viwango vipi.
2.Jenga nyumba imara ogopa vya Bei cheee
3.Nyumba kuijenga si lelemama, ili kumudu anza mdogomdogo. Ukiwa na 5m anza hata msingi.

Ukihitaji fundi, usisite kunitafuta, Hakina utaenjoy service yangu.
0655173113


UPDATES
tuendelee na mjadala wetu. Hapo awali tulijadili jinsi namna gani uimara wa nyumba unavyoathiri gharama za ujenzi. Leo tujadili namna location inavyoathiri gharama za ujenzi.

NAMNA LOCATION INAVYOSABABISHA GHARAMA ZA UJENZI KUWA TOFAUTI.

Mungu aliumba ardhi ktk mionekano tofauti. Kuna tambalale, milima na mabonde.
Ujenzi ktk Eneo tambalale unagharama nafuu kulinganisha na Eneo lenye slope . Lakini pia ujenzi wa Eneo tambalale lililoko Chanika mkoni DSM Unaweza kuwa na gharama tofauti na ujenzi wa Eneo tambalale lililoko msasani mkoani DSM. Hivyo hivyo ujenzi wa DSM unagharama kubwa kuliko ujenzi wa Mbeya.

SABABU ZA KUTOFAUTISHA GHARAMA KATI YA ENEO TAMBALALE NA LENYE SLOP.

sanasana hapa kimbembe huwa ktk kujenga msingi wa nyumba.

Msingi uliotumia tofali 1500 katika eneo tambalale, msingi huohuo ukitaka kuujenga ktk eneo lenye slope unaweza kutumia tofali 2300 au zaidi kulingana na ukali wa slope.
Tukumbuke kwamba Kwa kadri tofali zinavyoongezeka ndivyo na material mengine yanavyozidi kuongezeka kitu ambacho hupelekea kuongezeka kwa gharama za fundi. Si ajabu kumalizia 10mil ktk msingi wa nyumba ya Vyumba vitatu ktk Eneo LA slope.

Hivyo basi kama hutaki kutumia gharama kubwa kwenye ujenzi epuka kununua viwanja vilivyo na slope.

Jambo lingine linaloathiri ktk location ni upatikanaji wa material.
Mfano mtu anaejenga mbezi beach atanunua tani 18 Za mchanga zaidi ya 450.000 Tshs wakati mtu wa Chanika atanunua Kwa 220,000tshs.

Pia boma utakalojenga kwa 8mil Mbeya, DSM utalijenga Kwa zaidi ya 15mil. Sababu Mbeya tofali ni cheap, labour ni cheap nk.

Kwa ujenzi imara na wakisasa tutafutane 0655173113
Naomba kuuliza uwiano wa rangi na maji ktk uchanganyaji wa gympsum kwa ajili ya skimming ya ukuta

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni Kipindi gani kinafaa kuchimba msingi wa nyumba, Msimu wa Mvua au Kiangazi?
 
Kipindi chochote kinafaa, cha msingi nikufahamu tabia za udongo
Sawa sawa. Kuna ile dhana kwamba msimu wa mvua hasa masika sio kipindi kizuri cha kuchimba msingi wa Nyumba. Nadhani ni mafundi tuu wanakuwa wanakwepa kuchota maji kwenye msingi endapo utajaa maji. Ile kimtazamo ni muda mzuri maana hutahitaji kumwaga maji na pia cement itakauka taratibu na kuwa imara zaidi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
We muongo mafundi wote mnajenga na kutindua, kuhusu chimney inahitajika kwenye majiko yote popote sio lazima kuwe na baridi, sema hamjui lakini sio kusingizia baridi.
Architecture anachora nyumba haweki chimney, ok unawrza kusema ni kazi ya structure engineer lakini naye haweki.
Masaki zile nyumba zilijengwa na wazungu zina chimney, wao hawana joto pale?!
Naomba kutofautiana na wewe kidogo ktk suala la kusema kwamba mafundi wote ni wazembe kwa upande wa kuset vyoo&wiring,mimi fundi wangu alimwaga zege vyooni na bafuni ila akabakiza nafasi za kuweka vyoo na kitolea maji machafu bafuni alipokuja mtaalam wa choo baada ya kuviweka akamalizia yeye kuziba pengo la zege lililobaki.

Wiring na mfumo wa maji machafu ya jikoni hakuna namna utafanya ili usitindue kuta shida itakuja pale unapookota mafundi uchwara mtaani wanakuja wanatindua kuta wanalaza mabomba na wire kisha wasizizibe na mchanga ili kumrahisishia fundi plaster kufanya kazi yake kwa ufanisi hapa lazima utaona wote wanafanana akili ila siyo hivyo.

Sent from my Redmi Note 5 using Tapatalk
 
Back
Top Bottom