Mkuu, elezea ujengaji wa msingi kwa kutumia steps. Maeneo mengi hasa yenye miinuko mafundi wanaweka steps kwenye foundation, hilo hufanya idadi ya matofali ipungue sana, maana kwa eneo kama Kimara hadi Mbezi, Malamba huko maeneo mengi ni ya miinuko.
1. Je, ujenzi wa steps kwenye miinuko una madhara gani katika uimara wa nyumba?
2. Wakati wa kumwaga ground beam, sijawahi kuona fundi akifanya kupima level ya beam, kwa maana ya upande mmoja kuwa sawa na mwingine, hii husababisha beam isiwe level na mwisho nyumba ikatitia kidogo lazima nyufa ndogondogo zitokee. Kwa nini hamfanyi kupima level ili kuwe na ulinganifu kwenye beam?