Fahamu zaidi kuhusu Mr Kuku

Fahamu zaidi kuhusu Mr Kuku

Habari wana chamvi, nimesoma uzi kuhusu mada tajwa hapo juu nami nataka kushirikishana uzoefu wangu kuhusu huyo 'mwekezaji".

Huyo bwana anaitwa Tariq, mwaka juzi 2018 nilisoma bandiko lake fb kuhusu mradi wa kilimo cha nyanya cha umwagiliaji, ahadi ilikuwa nzuri kuhusu faidi ambapo kiwango cha chini cha hisa ilikuwa 36 na kila hisa 5000/= hivyo unapata 180,000 /=

Baada ya miezi mitatu unapata 360,000/= nilitamani kuwekeza japo nilikuwa na shaka, niliongea nae akanielewesha kwamba uwekezaji ni kupitia vikundi vya watu 15, hivyo akaniunganisha na wadau tukawa na kikundi cha What App tulikuwa mikoa tofauti ila mm niliiona na advantage kwa kuwa mradi ungefanyika jirani.

Tukaanza taratibu za katiba usajili wa kikundi, kabla ya kusajili kikundi akasema tutume fedha ili mradi uanze kuendana na wakati ili kuwahi soko la nyanya.

Baada ya kutoa fedha tulipitia ubabaishaji mwingi sana, mara mradi wa arusha hauwezekani kuna shamba moro, wadau wakataka kwenda moro baada ya muda akasema kule eneo linapitiwa na reli mradi utakuwa Tanga akatutumia vi picha vya eneo na ka tank. Wadau wakalazimisha wakaenda Tanga kufika hakuna kinachendelea.

Tukaanza harakati za kukamilisha katiba na mkataba ili tujipange kwa hatua zaidi. Baada ya muda sana akasema amepata hasara hivyo fedha iliyobaki atawekeza mradi wa kuku uliopa kigamboni. Tukaendelea kupambana na kufuatilia.

Baada ya mwaka baada ya kuwa na maamuzi ya kwenda vgombo vya sheria ndo akaturudishia mitaji yetu na kuahidi faida baada ya muda. Baada tu ya kurudisha mitaji hakuwa anapokea simu wala kujibu hoja za group la What App ambalo tulianzisha. Baada ya kuanza tena harakati za kutaka kufuatilia faida akatoka katika kundi kwa jazba na kusema tufanye tunavyotaka hayupo tayari kuendelea na sisi.

Kama ambavyo mmeona tangazo lake ndivyo alivyo huwa hajibu wala kutoa ufafanuzi wa kina kuhusu hoja.

Pamoja na kwamba uoga wako ndo umaskini wako ila kwa wawekezaji wa kibongo bora kuwa mwoga. "invest on your own risk"

Nawatakia wakati mwema.
Naona jamaa wamemtia nyavuni tayari
1597072207888.png
 
Muwe mnafuatilia mambo kabla ya kutuhumu watu. Je, mnaamini watu wote walio Segerea kwa Money Laundering ni kweli wametakatisha pesa?

Nendeni Kigamboni Kisarawe 2 karibu na kiwanda cha Maji (Afya) muone mabanda makubwa sana ya kufugia Kuku tena yapo 14 na mlima wa Mbolea ya kuku. Walikua wanafuga Kuku mpaka laki 2 kwa mpigo kutokana na pesa za wawekezaji. Nenda kaulize hata majirani kama hakukua na mradi wa ufugaji uliokua ukiendelea. UPATU unatokea wapi hapo?

Huyo Wankyo Simon ndio kiboko ya kesi za Money laundering. Wanatafuta tu sababu ya kutaifisha hizo Bilioni17 za wananchi.

Kama kweli huu ni Upatu, mbona kuna miradi mingine kama hio mitatu nayoifahamu bado inaendelea na watu wanawekeza huko?

CHEMA - Unawekeza hela kisha baada ya miezi mitano unarudishiwa 60% ya pesa ulowekeza

WEKU - Picha inajieleza

JATU - Hawa wana wanachama zaidi ya 2000 na viongozi wa Serikali hadi Waziri Manyanya kashahudhuria mikutano yao. Unawekeza 1/3, wanakukopesha 2/3 na kukulimia Mahindi, Maharage, Mpunga n.k na baada ya mavuno wanakurudishia 1/3 yako plus faida yote ya mauzo ya mavuno yatokanayo na 3/3 ya mtaji.

Acheni ushamba, kilimo kina faida kikifanywa kitaalamu. Huyo Tariq wa Mr Kuku amesoma SUA na aliajiri maafisa Kilimo waliokua full time pale Shambani. Anachukua pesa yako na kuizungusha kwa faida mara NNE kabla ya kukurudishia 70% ya faida. Broiler anakuzwa kwa mwezi MMOJA tu na kuuzwa, maajabu yako wapi hapo?

Hii ni dhulma tu, hamna maelezo tofauti.

Hio Bilioni 17 imewatoa watu fulani mate.
Screenshot_20200810-205215_Instagram.jpg
Screenshot_20200810-204603_Instagram.jpg
 
Kweli ukiwa mjanja umaskini unaaga mwaka tu ebu fikiria 17B chap tu ya wapenda vitonga
Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
Anasema Kila Siku Tanzania Ni Tajiri

Billions 17 Haraka
 
Umeongea kinyume. Hapa unaniambie niwe mjinga ili unitapeli. Nimekumbia mtawapata hao hao wajinga wapenda vya mtelemko lakini siyo mimi. Mnakotaka kulalia ndiko nilikoamkia. Nina uhakika wa 100% ni suala la muda tu lakini watu mtaliza watu. Nimekuwa karibu na wafugaji kuku wa grade ya juu na wenye mtaji mkubwa kuliko huu mnaotapeli watu na sijaona mfugaji analipata faida kama hii mnayoahidi hapa.
Na imekuwa kama ulivyonena! Heheh ...wanakolalia ndiko ulikoamkia...lo bravo mkuu.
 
Back
Top Bottom