Faidika na darasa la FaizaFoxy; Uliza chochote utajibiwa

Vipi Aya zako ukizoahidi kuleta za adhabu za kaburi kwenye Qur'an yamekushinda? Huwezi na hutoweza kuleta porojo ya adhabu ya kaburi ndani ya Qur'an.
Hizo naziweka pindi ukishajibu maswali yangu. Ondoa shaka juu ya hilo. Wewe jibu maswali nikuwekee aya nyingine. Tuna hazina bibie.
 
Bibie ibada zako unazifanya vipi ? Hili mbona hujibu ?

Allah ameihifadhi Qur'aan na amezihifadhi Hadithi za mtume pia, ndio maana leo hii tunazijua zipi hadithi sahihi, zipi hadithi hassan, zipi hadithi dhaifu na zipi hadithi maudhui. Hili kwetu halina shida.

Swali, unasali vipi wewe ? Rakaa nne katika sala ya adhuhuri ipo kwenye Qur'aan ?
 
Nimeanza kuwa nawasiwasi na wewe faiza foxy au labda sijakuelewa unachokusudia nini? Kwamba unasema hakuna adhabu za kaburi kwamujibu wa qur'an au? Na pia hakuna aya inayoelezea ktk swala la ndoa muoaji ni wanaume? Au unakusudia nini?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa nani amekubali hapo kama al Bar'wan anayo tafsiri, hana Tafsiri ya Qur'aan. Maarufu alifanya tarjama ya kitabu cha Tafsiri kiitwacho "al Muntakhab al Akhbar". Tuliza akili acha mawenge.
Kwi kwi kwi teh teh teh

Kumbe hata Kiswahili kinakupiga chenga? Kile nilichokuwekea usome juu kule cha Barwan ni nini kile kama si tafsiri ya Qur'an? Huwa sikisii kijana. Soma...


Fata link: Qurani Karimu – Tafsiri ya Qurani – Swahili
 
Acha porojo wewe. Jibu hili kwanza kabla hujaanzisha lingine...

Vipi Aya zako ukizoahidi kuleta za adhabu za kaburi kwenye Qur'an yamekushinda? Huwezi na hutoweza kuleta porojo ya adhabu ya kaburi ndani ya Qur'an.
 
Acha porojo wewe. Jibu hili kwanza kabla hujaanzisha lingine...

Vipi Aya zako ukizoahidi kuleta za adhabu za kaburi kwenye Qur'an yamekushinda? Huwezi na hutoweza kuleta porojo ya adhabu ya kaburi ndani ya Qur'an.

Silei ujinga bi mkubwa, ukijibu maswali yangu, nitakuwekea aya nyingine. Hiki lisikupe shida, ila itifaki inazingatiwa, huchelewi kuhamisha goli.
 
Nnakushauri kwanza soma Qur'an Surat ANNAS ya mwisho kabisa kwenye Qur'an (114) umuombe Allah akuepushe na wasiwasi. Soma mara tatu.

Kisha rudi uulize swali moja moja ndiyo itakuwa raha zaidi. Usichanganye mada.
 
Nakwambia kila siku, bi mkubwa huna unalo lijua.

Kuna Tarjama za Qur'aan kwa Kiswahili, na hakuna Tafsiri ya Qur'aan kwa Kiswahili. Hili ni kosa wanalo lifanya waswahili wengi, mahala pa Tarjama wanatumia tamko Tafsir.

Nakudai maswali yangu
 
Silei ujinga bi mkubwa, ukijibu maswali yangu, nitakuwekea aya nyingine. Hiki lisikupe shida, ila itifaki inazingatiwa, huchelewi kuhamisha goli.
Huna ndiyo ujinga wenyewe huo uliolelewa nao.

Kinakushinda nini?
 
Nakwambia kila siku, bi mkubwa huna unalo lijua.

Kuna Tarjama za Qur'aan kwa Kiswahili, na hakuna Tafsiri ya Qur'aan kwa Kiswahili. Hili ni kosa wanalo lifanya waswahili wengi, mahala pa Tarjama wanatumia tamko Tafsir.

Nakudai maswali yangu
Wewe punguani maana ya tarjama kwa Kiswahili ni tafsiri.

Mpaka nimekupigia picha hapo bado huelewi.

Wewe mama'ko basi yupo mashakani sana na alipata taabu sana kukukuza wewe.
 
Rakaa nne unazo sali katika adhuhuri na Alasiri umezipata wapi ?

Silei ujinga.
Vipi Aya zako ulizoahidi kuleta za adhabu za kaburi kwenye Qur'an yamekushinda? Huwezi na hutoweza kuleta porojo ya adhabu ya kaburi ndani ya Qur'an.
 
Wewe punguani maana ya tarjama kwa Kiswahili ni tafsiri.

Mpaka nimekupigia picha hapo bado huelewi.

Wewe mama'ko basi yupo mashakani sana na alipata taabu sana kukukuza wewe.
Kwa heshima na taadhima naomba nifunge mjadala na wewe. Maana hujui mambo mengi.

Nenda kaulize kote Tarjama kwa Kiswahili ni Tafsiri ?
 
Kwanini hujibu maswali yangu ?
Kwa heshima na taadhima naomba nifunge mjadala na wewe. Maana hujui mambo mengi.

Nenda kaulize kote Tarjama kwa Kiswahili ni Tafsiri ?

Huna cha heshima wala taadhima.

Unakimbia huna jibu, umekosa ayat za Qur'an zenye adhabu ya kaburi, "unatoka nduki".

Kiri tu huna nianze kukupa darsa la salat na udhu na rakaa na kingine chochote utachouliza kutoka ndani ya Quran, labda utaelewa kuwa Qur'an inafundishwa na Allah na si hadithi.

Soma...

Qur'an 55:

1. Arrah'man, Mwingi wa Rehema 1


2. Amefundisha Qur'ani.
2
 
Vipi Aya zako ukizoahidi kuleta za adhabu za kaburi kwenye Qur'an yamekushinda? Huwezi na hutoweza kuleta porojo ya adhabu ya kaburi ndani ya Qur'an.
kwakuwa hukuanzisha uzi huu ili uwe ni mdahalo, bali umeanzisha kwa ajili ya "kuulizwa maswali" na siyo wewe kujibiwa maswali,.

kwa muktadha huo basi jibu maswali hayo uliyoulizwa ili uende sawa na "kichwa ha habari"

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Langu kwake "technically" siyo swali bali yeye aliahidi kunifundisha ayat za Qur'an zenye adhabu ya kaburi tena kasema zipo nyingi tu na mwenzake mmoja ajiitae safuher ni hilo hilo.

Sasa wanashindwa hawaleti na mimi nawafanyia istihzai, makusudi kabisa. Waelewe kuwa hicho kitu hakuna kwenye Qur'an.

Sasa wewe In Shaa Allah tumia fursa hii uulize hayo maswali ntakujibu.

Uliza upendalo, moja moja lakini ili tusichanganye mada.
 
Nilikujibu mwaka 2016 leo tupo 2020.

Umepata majibu mapya?
 

Poa
 
Vipi Aya zako ulizoahidi kuleta za adhabu za kaburi kutoka kwenye Qur'an?Yamekushinda?

Huwezi na hutoweza kuleta porojo ya adhabu ya kaburi ndani ya Qur'an. Open challenge kwa yeyote yule, si wewe tu. Kumbuka hilo.

Mkome kuizulia Qur'an.

Qur'an ni uongofu aliopewa Mtume Muhammad na kwa kuihama kwenu na kufanya maneno ya kujitungia, mnajiingiza kwenye matatizo tu kwa kumfata shetani.

Soma unafundishwa nini na Qur'an...

Qur'an 25:

27. Na siku ambayo mwenye kudhulumu atajiuma mikono yake, na huku anasema: Laiti ningeli shika njia pamoja na Mtume! 27


28. Ee Ole wangu! Laiti nisingeli mfanya fulani kuwa rafiki! 28


29. Amenipoteza, nikaacha Ukumbusho, baada ya kwisha nijia, na kweli Shet'ani ni khaini kwa mwanaadamu. 29


30. Na Mtume alikuwa akisema: Ee Mola wangu Mlezi! Hakika watu wangu wameifanya hii Qur'ani ni kihame. 30


31. Na vivi hivi tumemfanyia kila Nabii adui miongoni mwa wakosefu, na Mola wako Mlezi anatosha kuwa Mwenye kuongoa na Mwenye kunusuru. 31


32. Na wakasema walio kufuru: Kwa nini hakuteremshiwa Qur'ani kwa jumla moja? Hayo ni hivyo ili tuuthibitishe moyo wako, na ndio tumeisoma kwa mafungu. 32


33. Wala hawatakuletea mfano wowote, ila na Sisi tutakuletea (jawabu) kwa haki, na tafsiri iliyo bora. 33


34. Wale ambao watakao kusanywa na kubururwa kifudifudi mpaka kwenye Jahannamu, hao watakuwa na mahali pabaya, ndio wenye kuipotea sana njia. 34

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…