Faidika na darasa la FaizaFoxy; Uliza chochote utajibiwa

Faidika na darasa la FaizaFoxy; Uliza chochote utajibiwa

Nioneshe wapi biblia imesema hivyo.

Halafu unaonesha link niliyokuweka hujaisoma. Jisomee:


Qur'an 4:
3. “Na ikiwa mnaogopa kuwa hamtowafanyia mayatima uadilifu, basi oeni mnaowapenda katika wanawake, wawili au watatu au wane. na mkiogopa kuwa hamwezi kufanya uadilifu, basi mmoja tu...” An-Nisaa: 3
1478863554429.png


Hiyo hapo...
 
Nioneshe wapi biblia imesema hivyo.

Halafu unaonesha link niliyokuweka hujaisoma. Jisomee:


Qur'an 4:
3. “Na ikiwa mnaogopa kuwa hamtowafanyia mayatima uadilifu, basi oeni mnaowapenda katika wanawake, wawili au watatu au wane. na mkiogopa kuwa hamwezi kufanya uadilifu, basi mmoja tu...” An-Nisaa: 3
Soma Timotheo 1-1:2
 


Sasa kijana hapo ndiyo kuoa mmoja tu? Hicho ni kisa cha Adam na hapo ni mambo ya kimwili, hebu kisome vizuri.

Biblia kuhusu kuoa zaidi ya mmoja inasema hivi:

Kutoka 21:
10 Kwamba ajitwalia mke mwingine, chakula chake huyo, na nguo zake, na ngono yake, hatampunguzia.

2 Samweli 5
13 Naye Daudi akazidi kujitwalia masuria na wake huko Yerusalemu baada ya kutoka Hebroni; wakazaliwa zaidi kwa Daudi wana na binti.

1 Wafalme 11
3 Akawa na wake mia saba binti za kifalme, na masuria mia tatu; nao wakeze wakamgeuza moyo.
 
Ught Faiza hivi ulishawahi kusoma kitabu cha "Secret terrorist"? Unaweza kuyaelezeaje yaliyomo ndani
 
Hivi unaamini nini katika suala la kusema fulani ana "nyota kali".

Je,mafanikio ya mtu ni bidii zake mwenyewe au kudra tu za Mungu?

Na kama muumba anajua yote si inamaanisha kuwa fate ya mtu tayari iko pre-destined

Siamini hayo mambo ya "Nyota Kali" ni katika mambo ya ramli ambayo Uislam unakataza.

Mafanikio ya mtu ni kutoka kwa Mwenyeezi Mungu na bidii ya mtu. Mtihani.

Kuhusu "predestined" ni ilm ndeeefu na ina maelezo mengi sana. Naam, kwa maana hiyohiyo, Allah ni mjuzi wa yote na si sisi.

Nnakushauri pitia mjadala huu, kuhusu hayo: Is everything predestined in a muslim's life?
 
Sina chuki na Joyce Ndalichako bali nnauhakika si kiongozi mzuri, alivurunda kama mkuu wa NECTA mpaka baadhi ya Waislam wa Tanzania wakaandamana kumkataa. Jikumbushe:

DSC08684.jpg
Tatizo dada yangu unajua nini hapo??,Ukweli ni kwamba ninyi wenzetu huwa mnaweka nguvu nyingi kwenye kujifunza Quaran kuliko masomo mengine ya darasani halafu kwenu ninyi nasikia ni heri mtoto afeli masomo mengine kuliko kufeli Elimu ya Kiislamu.Kwa hiyo huna sababu ya kumchukia Prof.Ndalichako,maana kwa mtindo huo lazima madogo wafeli tu.
 
Tatizo dada yangu unajua nini hapo??,Ukweli ni kwamba ninyi wenzetu huwa mnaweka nguvu nyingi kwenye kujifunza Quaran kuliko masomo mengine ya darasani halafu kwenu ninyi nasikia ni heri mtoto afeli masomo mengine kuliko kufeli Elimu ya Kiislamu.Kwa hiyo huna sababu ya kumchukia Prof.Ndalichako,maana kwa mtindo huo lazima madogo wafeli tu.


Nnakuomba pitia hapa, kuna mjadala kuhusu hilo: Waislam wa Tanzania na tatizo la udini katika Wizara ya Elimu
 
Usije kumuamini kiumbe kinachoitwa Jinni hata siku moja. Waongo balaa, atakuja kwa sura ya Fatma wakati yeye ni Zwangedaba. Alafu makata ni jina la asili ujue !!.

Joke aside, Majinni au mapepo au kwa kiingereza Genie (Refer: if you want to be with me, there's some price to pay, am a genie in a bottle...) ni viumbe vilivyopo, wameumbwa kwa moto na wana advantage ya kutuona wakati sie bin Adam hatuwaoni.

Wamekuwepo duniani kabla ya bin adamu, kwa kuwa binadamu ndie kiumbe cha mwisho kuumbwa.

Kisheria, majinni wanapaswa kuishi kama wao katika communities zao, na ni makosa kwao kuwaingia binadamu na kuwasababishia madhara mbali mbali.

Na hapo ndipo tunapoambiwa kuwa Jinni anapokuwa mwema basi si Shetani na binadamu anapokuwa muovu naye huitwa Shetani kwa kuchukua yale matendo ya kishetwani.

Binadamu Mcha Mungu ana fadhila zaidi kuliko Kiumbe kingine chochote, na kwa ucha Mungu huo Nabii Suleiman kwa mfano alipewa uwezo wa kutawala jeshi kubwa la majinni waliokuwa watiifu kwake na waliomtumikia kwa kila jambo.

Back to your question, Uislamu ni dini iliyoshushwa kwa binadamu na majinni. Kama isemavyo aya kuwa 'Mwenyezi Mungu amewaumba binadamu na majinni ili wamuabudu.' Wale wanaomuabudu watakuwa ni waislamu kwa kuwa wamejisalimisha na kunyenyekea kwa Mola wao na wale wasioabudu si Waislamu. Hivyo hautamuona Jinni mwenye kuabudu akimuingia binadamu ili amdhuru, lakini utawaona wale wasioabudu wakifanya hivyo na kujiita majina wayatakayo wao ili ku create confusion.
Yaani kama kweli we ni muislam ,,, nimekukubali kwa majibu yako hata kama umenidanganya lakini maelezo yako yamenyooka. Wengine ukiwauliza wanakuwa na jazba ila wewe umekubali kwamba waislam wana undugu na majini - rejea usemi huu ... "MUISLAM NDUGUYE MUISLAM"
 
Back
Top Bottom