Familia nyingine ni za ajabu sana

Familia nyingine ni za ajabu sana

Bi mkubwa miaka 60+ nimchukue nije niishi nae dsm uswaz kwenye nyumba za kupanga mi mwenyewe sijaowa halafu nakaa chumba kimoja
Dah...pagumu sana hapo...ila komaa TU ndugu yangu...wasaidie ndugu zako... Hamna namna nyingine Mungu ndio ameshakupa mtihani huo...amini nakwambia familia zote zipo hivyo...tena familia nyingine zina vichaa Zaidi ya hao ndugu zako. Kikubwa usichoke kupambana,

jitahidi uzidi kunisaidia mama Yako kwani kama wewe TU unatumia kitendo Cha hao ndugu zako kuwa awana maisha ya kueleweka jua. Hata mama pia roho Ina muuma pia sema ndio hivyo kama mzazi Hana jinsi. Wazazi wanajivuniq sana kutuona tumefanikiwa...!​
 
Wewe una uhakika gani kwamba sio walemavu wa akili wewe ndio uliewazaa? Wewe ndie mama yao? Wewe ndie unaewafahamu tangu wanazaliwa walikuaje wakaishi mazingira gani?

Hizo ni assumption zako Ila mimi ninakaa upande wa huyo mama ukitaka kujua uchungu wa mtoto/watoto nenda kamuulize mama Msuya anajisikiaje sasa hivi bora ufuge hata chizi ndani Ila ni mwanao
Sorry madam point yako ni nini haswa kwenye hili ?maana unasema suala la uchungu wa mtoto as if ni la mama tu? Hata huyu mtoa mada anapitia uchungu kwa matendo ya kaka zake. Tusijifiche kwenye uchungu tukaacha kutafuta alternative solutions. Sio kila Mizigo ni ya kasafiri nayo mingine ni ya kuacha stend kama haina faida.
 
Shida huyu ana asili ya uchoyo ukimpa mtu oitu uwezi kumkata asitumie na mtu nisawa kumpa mtu gari afu umkataze asipakie rafiki zake
Pia na wewe unasili ya kulea ujinga hata wahisani wana masharti yao ukiona magumu acha kuomba. Faraja ya msaada ni kumsaidia mtu anayepambana kujikwamua sio sababu ni ndugu yako nikomae kusaidia majitu mazima hayana ulemavu wala magonjwa yanayotatiza uwezo wao wa kufanya kazi kisa sifa za kijinga eti sio mchoyo. BIG NO
 
Ndiomana wanawasumbua pole sana bro
Hapo wa kuokoa jahazi ni mama yako
Na mama ndio umwambii kitu kuhusu hao jamaa yani ukianza tu kuwaongelea bi mkubwa anaishiwa raha na ushirikiano kwenye maongez akupi ila umwambie tu kwamba kuna mtaji unataka kuwapa hao jamaa yani atafurahi kishenz
 
Kijana jitahidi hata kwahicho kidogo ulichonacho kugawana na ndugu zako, kwa life la kijijini hata ukiwa unawatumia just 10K kwa week watakuombea na kukushukuru.
Na sisi hatupo kijijini ni mkoani ndio ila tupo town kabisa tena kwenye wilaya inayobeba hadhi ya mkoa mzima
 
Waafrica uwa wanadhani wazungu hawana uwezo WA kuzaa watoto kibao ,wazungu ufanya ivyo Kwa sababu watoto wachache ni rahisi kuwa manage unavyotaka wawe ,tofauti na watoto wengi,pole sana ,mzee wako alifanya kosa kuzaa watoto wengi pia kunaweza kuwa na mikosi kwenye family pambania maombi,pia usirudie kosa la kuzaa watoto wengi mwisho WA siku utashindwa kuwa manage na wataibukia majambazi ndani ya family,
Shukran mkuu
 
Dah...pagumu sana hapo...ila komaa TU ndugu yangu...wasaidie ndugu zako... Hamna namna nyingine Mungu ndio ameshakupa mtihani huo...amini nakwambia familia zote zipo hivyo...tena familia nyingine zina vichaa Zaidi ya hao ndugu zako. Kikubwa usichoke kupambana,

jitahidi uzidi kunisaidia mama Yako kwani kama wewe TU unatumia kitendo Cha hao ndugu zako kuwa awana maisha ya kueleweka jua. Hata mama pia roho Ina muuma pia sema ndio hivyo kama mzazi Hana jinsi. Wazazi wanajivuniq sana kutuona tumefanikiwa...!​
Sawa mkuu
 
Sorry madam point yako ni nini haswa kwenye hili ?maana unasema suala la uchungu wa mtoto as if ni la mama tu? Hata huyu mtoa mada anapitia uchungu kwa matendo ya kaka zake. Tusijifiche kwenye uchungu tukaacha kutafuta alternative solutions. Sio kila Mizigo ni ya kasafiri nayo mingine ni ya kuacha stend kama haina faida.
Kabisa mzee huku ni kutiana umaskini tu
 
Mi ningewachinjia NUNGWI kitambo sana.

Ningemchukua bimkubwa hao jamaa watajijua wenyewe.

Siwezi Lea mtu mzima tena mwanaume aheri angekuwa mwanamke au mwenye ulemavu.

Jitu unalipa Hela linakunywa pombe na wanawake tupa kule.

Kuna wakati lazima uwe ROHO MBAYA kweli Ili mambo yaende la sivyo utabaki pale pale hupigu hatua
 
Sanaa mi nimeamuaga tu kukaa kimya niliongea nikachoka,
nikawapa mitaji waliyotaka ili wajitegemee wakatafuna wakarudi palepale.
Mama yao nae ndo kiongozi kuwatetea
Na hao ni over 42

[emoji23][emoji23] ila kuna muda wazazi nao wanakosea ila ukisema uwaambie ukweli unaanza kupewa laana[emoji23][emoji23][emoji119]
 
Mimi siamini kwenye LAANA bwana wazazi wazamani walikuwa wachawi wachawi...ukiwazingua wanakuloga harafu wanajidai wanakulaani...[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]

[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] ila wazazii hapana
 
Haya mambo yapo sana,kuna familia moja bibi wa miaka 80 anawatunza wanae 60yrs mkubwa na 55yrs mdogo. Wote ni wanaume na hamna mwenye mke maana wake zao wote waliondoka wakawaachia watoto ambao ni wajukuu wa bibi sasa. Nao wajukuu wanamtegemea bibi kwa kila kitu. Ulevi ndo alama ya familia hii. Ukichunguza vizuri kuna laana au maagano yamo ndani ya familia hizi na zisipovunjwa huenda zikaendelea kuzitesa familia hizi. Ombea kizazi chako.
 
Mimi siamini kwenye LAANA bwana wazazi wazamani walikuwa wachawi wachawi...ukiwazingua wanakuloga harafu wanajidai wanakulaani...🤣🤣🤣🤣
Mi nilipigwa mkwara wa laana pale airport na maza nikamwambia kiungwana tu.
Umemaliza?
"Umeongea sana utakua na kiu wewe,twende ukapate soda"
Akasmile, nikampa soda yake.
Na mwenzake na visnack snack pale BP.
Nilivyoondoka hatukuonana wala kuongea miaka 10
Mpk alipoomba sana.
Msamaha
 
Kuna familia zingine zinashangaza na zinakatisha tamaa sana.

Sisi kwenye familia yetu tumezaliwa watoto 9 wakiume tupo 6 na wakike wa 3 na uzao wetu umekaa hv kuna kaka zangu wakubwa wa 3 waliozaliwa miaka ya 70 then wanafuata dada 3 waliozaliwa miaka ya 80 halafu ndio sisi tena wakiume wa 3 wa mwisho tuliozaliwa miaka ya 90.

Kiukweli tulilelewa vzr sana na atukuwahi kushinda wala kulala njaa japo mzee alikuwa anafanya kazi ya kawaida sana ila alijitahidi kuhakikisha watoto wake tunalelewa vzr japo kwenye swala la kielimu atukufika mbali sana.

Mzee alijitahidi sana kuwekeza nguvu zake kwa hao kaka zetu wakubwa miaka ya 90 kipindi sisi wengine bado tupo wadogo sana ili wao ndio waje kuwa msaada kwetu.

Shida ni kuwa kaka zangu wawili walikuwa ni watu wa starehe na pombe mwisho wa wakafukuzwa kazi. Mmoja aliiba pesa kiac cha sh milioni 2 kazini kwake akakimbilia nchi jirani ya kenya hiyo ni milioni 2 miaka ya 90 haikuwa pesa ndogo, huko alikokwenda pia aliendekeza starehe kama kawaida mwisho pesa zote zilikwisha na mbaya zaidi aliugua sana ikabidi tena mzee aende kumfata huko alipokuwa,

na kaka yangu mwingine alienda mbali zaidi kufikia hatua ya kuingia chumbani kwa mzee na kuiba kiac kikubwa cha pesa na kukimbilia uganda,
Japo nilikuwa mtoto ila sikushindwa kujua maumivu aliokuwa nayo mzee, kwa mara ya kwanza nikamuona mzee akitokwa na machozi mbele yangu aisee niliumia sana.

Mwamba huko uganda akawa mtu wa starehe sana ni mwendo wa pombe na wanawake mwisho pesa zilikwisha akarudi tanzania akawa anakuja nyumbani kwa siri, Siku moja usiku muda wa saa 8 baba aliskia kama mchakacho akachukua panga akakutana na mtu anatoka koridoni mzee akataka kumkata panga akijua kuwa ni mwizi kwa bahati nzuri bro akawahi kutoa sauti ndio mshua akashusha panga.

Kama mjuavyo wazazi ni watu wenye huruma akamsamehe mambo yakaisha japo mshua akuwa na upendo nae tena.

Imepita miaka kadhaa wakaja na project kwa mzee hiyo ilikuwa 2008 mzee akaona sio mbaya akawapa tena mtaji wakiwa wawili rejea nyuma hao wote walishaiba pesa katika vipindi tofauti.

Ila cha kusikitisha hakuna cha maana walichofanya kumbuka hapo nguvu ya mzee katika kufanya kazi imeshaanza kupungua halafu akikumbuka watoto wake wakubwa ambao aliwekeza kwao amna cha maana walichofanya zaidi ya kumtia tu hasara ilifikia stage mpaka sisi wadogo mshua akawa anatuchukia kwa makosa ya kaka zetu wale wakubwa japo sisi bado ni watoto wadogo na tunasoma ila mara nyingi alikuwa anamwambia mama unaona watoto wako hawa wadogo pia wakikua watakuwa kama kaka zao aisee hilo jambo lilikuwa linaniumiza sana.

Ila nachoshukuru kati ya wale kaka zangu wakubwa watatu kuna mmoja yeye alipomaliza shule alienda dar miaka ya 2000 alihustle ila kiac alifanikiwa na ndio huyo akawa anampa mshua back up pale hali inapokuwa mbaya.

Kuna kipindi huyo bro aliyumba kiuchumi na mshua alikuwa mgonjwa na kama mjuavyo familia nyingi za kimaskini ni mpaka mzee atoke ndio familia ipate kula bac mshua baada ya kuwa katika mazingira yale alianza kupata stress akikumbuka nguvu aliyowekeza kwa vijana wake wakubwa ilivyopotea bure mpaka sasa familia aina chakula na yeye ambae ndio mtafutaji yupo chini bac mzee alianza kudhoofu sana hiyo ilikuwa 2011 kipindi hiko mi nipo form2 bac kuyumba kwa mzee vile ilipelekea tukakosa ada bac nikakaa home.

○Mzee maradhi na stress vilimuandama sana mwisho akalazwa hospitali kwa bahati mbaya akafariki. Bac tukaanza namna ya kutafuta mawasiliano ya wale kaka zangu wawili watukutu maana walikuwa wilaya nyingine kipindi hiko tuliwapata aisee jamaa wamekuja msibani hawana hata mia yani wamechakaa kinoma. Bac yule bro ambae yupo dar alijitahidi kwa nguvu zake mwenyewe akamiliza msiba fresh.

○Na ndio anaetoa msaada mkubwa kumlisha mama toka mzee amefariki yeye ndio tegemeo la familia maana dada zangu pia maisha yao ni tabu tu na wote hawajaolewa mpaka sasa.
○Wanaishi kwa kuunga unga tu aisee kuna baadhi ya familia ukizaliwa ni shida sana.

Cha kusikitisha kingine ni kwamba wale kaka zangu wawili mpaka leo hii mmoja ana miaka 50 mwingine ana miaka 45 bado wapo wapo tu wakipata pesa ni pombe na wanawake awana wake wala watoto na mbaya zaidi wao wote wamerudi home wanaishi na mama lakini awajishughulishi na chochote wamekaa tu wanakula kwa mgongo wa bi mkubwa kiukweli kuna familia nyingine zinakera sana.

Ebu fikiria vijana wakubwa wawili miaka 40+ wanashindwa kumlisha mama yao nao wamekaa wanalishwa, just imagine mpaka umeme wa elfu 2 unapigiwa simu dar wakati home kuna vijana wawili wakubwa wao wakipata pesa zao wanaenda kuishi guest mpaka wahakikshe hizo pesa zimeisha ndio wanarudi home halafu wanasubili sisi ndio tuwalishe kifupi tu ni kwamba hao ma bro washakula pesa za watu nyingi na hawajawahi kurudisha.
na kipindi nipo mkoa nilikuwa najaribu kuwashauri ila nilikuwa naishia kukabwa na kutaka kupigwa

Wengine ndio tumepata ajira jana tu hata kujipanga bado lakini simu za mzazi zimekuwa nyingi wakati pale home kuna vijana wakubwa hawataki kujishughulisha na mbaya zaidi mama hata kuwashauri wanae hawezi sometime wanakuja kukaa hapo na wanawake zao halafu bado pesa ya kula sisi ndio tunatafuta ukimtumia mama nae anakaa anakula na wanae, yani wanaenda kuzurura huko wakirudi wanakuta mama kawaachia msosi wanakula wanaondoka tena wanaenda kuzurura wakirudi usiku tena unakuta bi mkubwa kawaachia msosi wanakula wanaenda kulala kesho tena hivohivo jamani halafu fikirieni watu wanaofanya hivo ni watu wenye miaka 40+

Na pesa ya matumizi ikiisha bi mkubwa anawatafuta tena mnaangaika mkipata mnatuma bi mkubwa anaendelea kula na wanae halafu mbaya zaidi nayeye hata awashauri wanae ukimueleza awashauri watoto wake pia wajishughulishe anakwambia sasa kama hawa kaka zako hawana pesa wafanyeje utadhani sisi ndio tunahela wakati tunaangaika ili mama apate kula wengine hata mambo ya wanawake tulishasahau kutokana na majukumu ya kifamilia jinsi yanavyotubana.
Lakini unakuta hapo kuna baadhi ya ndugu zako tena wengine wangeweza hata kukuzaa wao wamekaa wanasubili wewe uhangaike uwatumie pesa wao wale.

Hapa toka jana mama ameshaanza kusumbua anahitaji pesa ya matumizi na sio muda mrefu nilimtumia laki moja na bro school bus yake pia iliangukiwa na mti ipo right off namimi na saiz bado mambo yangu ayajakaa sawa.
Halafu fikiria hapo home kuna wazee wazima ambao hata sio walemavu wamekaa wanasubili uhangaike utume pesa wale.

Aisee kuna familia nyingine zinakatisha tamaa sana kama ni laaana bac hii ya familia yangu imezidi mpaka najuta ni kwanini nilizaliwa na ndugu kama hawa, jamani nimechoka just imagine mpaka umeme wa elfu mbili mama anakupigia simu dar.
Pole sana mkuu. Namna rahisi ya kumuua kupe ni kumnyima damu. Kwa kuwa mama yupo peke yake kijijini (pamoja na hawo walevi). Nakushauri kama itawezekana kaka yako wa mjini amchukue bi mkubwa au umlete aishi kwako halafu tuone hawo walevi na malaya zao watakula nini. Simple like that!
 
Kuna familia zingine zinashangaza na zinakatisha tamaa sana.

Sisi kwenye familia yetu tumezaliwa watoto 9 wakiume tupo 6 na wakike wa 3 na uzao wetu umekaa hv kuna kaka zangu wakubwa wa 3 waliozaliwa miaka ya 70 then wanafuata dada 3 waliozaliwa miaka ya 80 halafu ndio sisi tena wakiume wa 3 wa mwisho tuliozaliwa miaka ya 90.

Kiukweli tulilelewa vzr sana na atukuwahi kushinda wala kulala njaa japo mzee alikuwa anafanya kazi ya kawaida sana ila alijitahidi kuhakikisha watoto wake tunalelewa vzr japo kwenye swala la kielimu atukufika mbali sana.

Mzee alijitahidi sana kuwekeza nguvu zake kwa hao kaka zetu wakubwa miaka ya 90 kipindi sisi wengine bado tupo wadogo sana ili wao ndio waje kuwa msaada kwetu.

Shida ni kuwa kaka zangu wawili walikuwa ni watu wa starehe na pombe mwisho wa wakafukuzwa kazi. Mmoja aliiba pesa kiac cha sh milioni 2 kazini kwake akakimbilia nchi jirani ya kenya hiyo ni milioni 2 miaka ya 90 haikuwa pesa ndogo, huko alikokwenda pia aliendekeza starehe kama kawaida mwisho pesa zote zilikwisha na mbaya zaidi aliugua sana ikabidi tena mzee aende kumfata huko alipokuwa,

na kaka yangu mwingine alienda mbali zaidi kufikia hatua ya kuingia chumbani kwa mzee na kuiba kiac kikubwa cha pesa na kukimbilia uganda,
Japo nilikuwa mtoto ila sikushindwa kujua maumivu aliokuwa nayo mzee, kwa mara ya kwanza nikamuona mzee akitokwa na machozi mbele yangu aisee niliumia sana.

Mwamba huko uganda akawa mtu wa starehe sana ni mwendo wa pombe na wanawake mwisho pesa zilikwisha akarudi tanzania akawa anakuja nyumbani kwa siri, Siku moja usiku muda wa saa 8 baba aliskia kama mchakacho akachukua panga akakutana na mtu anatoka koridoni mzee akataka kumkata panga akijua kuwa ni mwizi kwa bahati nzuri bro akawahi kutoa sauti ndio mshua akashusha panga.

Kama mjuavyo wazazi ni watu wenye huruma akamsamehe mambo yakaisha japo mshua akuwa na upendo nae tena.

Imepita miaka kadhaa wakaja na project kwa mzee hiyo ilikuwa 2008 mzee akaona sio mbaya akawapa tena mtaji wakiwa wawili rejea nyuma hao wote walishaiba pesa katika vipindi tofauti.

Ila cha kusikitisha hakuna cha maana walichofanya kumbuka hapo nguvu ya mzee katika kufanya kazi imeshaanza kupungua halafu akikumbuka watoto wake wakubwa ambao aliwekeza kwao amna cha maana walichofanya zaidi ya kumtia tu hasara ilifikia stage mpaka sisi wadogo mshua akawa anatuchukia kwa makosa ya kaka zetu wale wakubwa japo sisi bado ni watoto wadogo na tunasoma ila mara nyingi alikuwa anamwambia mama unaona watoto wako hawa wadogo pia wakikua watakuwa kama kaka zao aisee hilo jambo lilikuwa linaniumiza sana.

Ila nachoshukuru kati ya wale kaka zangu wakubwa watatu kuna mmoja yeye alipomaliza shule alienda dar miaka ya 2000 alihustle ila kiac alifanikiwa na ndio huyo akawa anampa mshua back up pale hali inapokuwa mbaya.

Kuna kipindi huyo bro aliyumba kiuchumi na mshua alikuwa mgonjwa na kama mjuavyo familia nyingi za kimaskini ni mpaka mzee atoke ndio familia ipate kula bac mshua baada ya kuwa katika mazingira yale alianza kupata stress akikumbuka nguvu aliyowekeza kwa vijana wake wakubwa ilivyopotea bure mpaka sasa familia aina chakula na yeye ambae ndio mtafutaji yupo chini bac mzee alianza kudhoofu sana hiyo ilikuwa 2011 kipindi hiko mi nipo form2 bac kuyumba kwa mzee vile ilipelekea tukakosa ada bac nikakaa home.

○Mzee maradhi na stress vilimuandama sana mwisho akalazwa hospitali kwa bahati mbaya akafariki. Bac tukaanza namna ya kutafuta mawasiliano ya wale kaka zangu wawili watukutu maana walikuwa wilaya nyingine kipindi hiko tuliwapata aisee jamaa wamekuja msibani hawana hata mia yani wamechakaa kinoma. Bac yule bro ambae yupo dar alijitahidi kwa nguvu zake mwenyewe akamiliza msiba fresh.

○Na ndio anaetoa msaada mkubwa kumlisha mama toka mzee amefariki yeye ndio tegemeo la familia maana dada zangu pia maisha yao ni tabu tu na wote hawajaolewa mpaka sasa.
○Wanaishi kwa kuunga unga tu aisee kuna baadhi ya familia ukizaliwa ni shida sana.

Cha kusikitisha kingine ni kwamba wale kaka zangu wawili mpaka leo hii mmoja ana miaka 50 mwingine ana miaka 45 bado wapo wapo tu wakipata pesa ni pombe na wanawake awana wake wala watoto na mbaya zaidi wao wote wamerudi home wanaishi na mama lakini awajishughulishi na chochote wamekaa tu wanakula kwa mgongo wa bi mkubwa kiukweli kuna familia nyingine zinakera sana.

Ebu fikiria vijana wakubwa wawili miaka 40+ wanashindwa kumlisha mama yao nao wamekaa wanalishwa, just imagine mpaka umeme wa elfu 2 unapigiwa simu dar wakati home kuna vijana wawili wakubwa wao wakipata pesa zao wanaenda kuishi guest mpaka wahakikshe hizo pesa zimeisha ndio wanarudi home halafu wanasubili sisi ndio tuwalishe kifupi tu ni kwamba hao ma bro washakula pesa za watu nyingi na hawajawahi kurudisha.
na kipindi nipo mkoa nilikuwa najaribu kuwashauri ila nilikuwa naishia kukabwa na kutaka kupigwa

Wengine ndio tumepata ajira jana tu hata kujipanga bado lakini simu za mzazi zimekuwa nyingi wakati pale home kuna vijana wakubwa hawataki kujishughulisha na mbaya zaidi mama hata kuwashauri wanae hawezi sometime wanakuja kukaa hapo na wanawake zao halafu bado pesa ya kula sisi ndio tunatafuta ukimtumia mama nae anakaa anakula na wanae, yani wanaenda kuzurura huko wakirudi wanakuta mama kawaachia msosi wanakula wanaondoka tena wanaenda kuzurura wakirudi usiku tena unakuta bi mkubwa kawaachia msosi wanakula wanaenda kulala kesho tena hivohivo jamani halafu fikirieni watu wanaofanya hivo ni watu wenye miaka 40+

Na pesa ya matumizi ikiisha bi mkubwa anawatafuta tena mnaangaika mkipata mnatuma bi mkubwa anaendelea kula na wanae halafu mbaya zaidi nayeye hata awashauri wanae ukimueleza awashauri watoto wake pia wajishughulishe anakwambia sasa kama hawa kaka zako hawana pesa wafanyeje utadhani sisi ndio tunahela wakati tunaangaika ili mama apate kula wengine hata mambo ya wanawake tulishasahau kutokana na majukumu ya kifamilia jinsi yanavyotubana.
Lakini unakuta hapo kuna baadhi ya ndugu zako tena wengine wangeweza hata kukuzaa wao wamekaa wanasubili wewe uhangaike uwatumie pesa wao wale.

Hapa toka jana mama ameshaanza kusumbua anahitaji pesa ya matumizi na sio muda mrefu nilimtumia laki moja na bro school bus yake pia iliangukiwa na mti ipo right off namimi na saiz bado mambo yangu ayajakaa sawa.
Halafu fikiria hapo home kuna wazee wazima ambao hata sio walemavu wamekaa wanasubili uhangaike utume pesa wale.

Aisee kuna familia nyingine zinakatisha tamaa sana kama ni laaana bac hii ya familia yangu imezidi mpaka najuta ni kwanini nilizaliwa na ndugu kama hawa, jamani nimechoka just imagine mpaka umeme wa elfu mbili mama anakupigia simu dar.
Hao ndio ndugu sahihi wa kuwatoa kafara unateseka wakati mali zipo jiongeze
 
Kama kuna uwezekano, mchukueni bi Mkubwa muishi nae alaf nyumba pangisheni. Haya majamaa yaachieni chumba kimoja.

Hakikisheni hati na documents muhimu za nyumba mnazitoa hapo home. Baada ya hapo, hakuna tena sababu ya kuwatumia hela ya matumizi
Mkuu umemaliza kila kitu. Hakuna haja ya kuendelea kuwalea hawo jamaa kwa sababu ya uzembe wao wa ulevi. Wangekuwa walemavu hata mimi ningewaonea huruma na kuwatunza. Lakini kwa kuwa wana uwezo wa kufanya kazi na wakipata pesa wanaenda kunywea na kut0mbEa, siwezi ku entertain ujinga huo. Ningekuwa mimi ningewatia adabu wasingekuja kunisahau.
 
Back
Top Bottom