Familia ya Hayati Magufuli kusimamisha kijana wao Ubunge wa Chato 2025, Samia kuzunguka naye kimkakati mikoa maalum

Machawa ya mama yalisema Mungu kaamua ugomvi, Sasa wanahitaji ugomvi tena?
 
Hakuna kiongozi anaheshimika nchi hii kama Nyerere Hadi kufikia kupewa hadhi ya Baba wa Taifa. Mbona hatukuwahi kuona Watanzania wakizuzuka na Makongoro Nyerere baada ya Baba yake kufariki? Kwamba Samia akizunguka na Mtoto wa Magufuli kutageuza nyoyo za Wananchi ili wampende kisa tu anaambatana na Mtoto wa Marehemu?
 

Hakuna kitu kinaitwa tume huru dunia hii na hakitokuja kutokea. Aliyeshinda atasema ni huru aliyeshindwa atalalamika
 
Wasijidanganye
Kuna wengi waliumizwa na utawala ule hawajasahau
Utawala uliofuata ni balaa zaidi
Msiwe kama wapumbavu(andiko la Biblia sio mimi)
 

Msemo mtoto wa John sio John
 
Kuna kitu sielewi huwa mnasema jiwe ni dikteta hapendwi sasa kama hapendwi haya yanatoka wapi?

Jiwe ana mapungufu yake lkn ukwei ni kwamba wananchi walikua wanampenda isipokuwa wezi na wale wachache waliondolewa kazini kwa vyeti feki.

Kama ww ni kibaka, muhuni , mvivu, mpenda slop lazima umchukie
 
Hakuna kitu kinaitwa tume huru dunia hii na hakitokuja kutokea. Aliyeshinda atasema ni huru aliyeshindwa atalalamika
Mawazo ya mtu aliyezaliwa Tanzania, akakulia Tanzania na anazeekea Tanzania. Tembea uone!
 
Tatizo wananchi hatujitambui plus msaada kutoka vyombo vya ulinzi na usalama, atashinda tu
 
Tume sio Kila kitu, hata USA uchaguzi unaletaga utata, halafu mfumo hauwezi kuruhusu majitu ya hovyo kwa sababu tu yameshinda uchaguzi.
Cc: MuslimBrotherHood, Misri
Katika miaka 247 ya uwepo wa USA na marais 46 uchaguzi wao umeleta utata mara 2 tu na mara mmoja ikiwa ni mtawala Trump mwenye tabia za madikteta ving'ang'anizi wa Africa akitaka kung'ang'ania madarakani baada ya kushindwa.
 
Binafsi mimi kama mwalimu namulewa sana mama samia,anajari watumishi wa umma,alipoingia tu mafarakani nikapanda daraja,na sasa kuna tetesi kuwa kuna kupanda madaraja tena,nani kama mama,twende na mama 2025
 
Tume sio Kila kitu, hata USA uchaguzi unaletaga utata, halafu mfumo hauwezi kuruhusu majitu ya hovyo kwa sababu tu yameshinda uchaguzi.
Cc: MuslimBrotherHood, Misri
Mbona mfumo hauzuii au kudhibiti majizi ya pesa za umma na mikataba mibovu??
 

Yupi Yule Bongeeee au Mjomba furaha
 
Kuna miradi kadhaa muhimu ingeweza kutumika kujenga taswira chanya kwa Rais wakati wa kampeni 2025 kanda ya ziwa lakini wapambe wanaipotezea mf. kukamilisha ujenzi wa meli kubwa, daraja la JPM,Uwanja wa ndege Mwanza na barabara njia 4 Mwanza ni icon ya miradi Mwanza na kanda yote ya ziwa,imetelekezwa je hii haitaiumiza CCM kisiasa kweli! wana kanda ya ziwa wanaamini angekuwepo hai Magufuli ingeisha lakini nguvu kubwa za miradi zimepelekwa Arusha,Mbeya,Dodoms na Dar.
 
Tume sio Kila kitu, hata USA uchaguzi unaletaga utata, halafu mfumo hauwezi kuruhusu majitu ya hovyo kwa sababu tu yameshinda uchaguzi.
Cc: MuslimBrotherHood, Misri
Mfumo unaofaidika na uwepo wa ccm madarakani huo sio mfumo, Bali ni genge la wapigaji kwa kichaka Cha mfumo. Inshort huo mfumo ni upuuzi kama upuuzi mwingine.
 
hata angegombea urais ningempigia kura
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…