Farewell RO....

Status
Not open for further replies.
tujenge hoja zinazojenga sio kwa sababu mtu una komputa chumbani kwako basi unaandika tu kile kinachokujia kichwani. nchi inakabiliwa na mambo mengi makubwa yanayopaswa kujadiliwa kwa kina, leo tunaletewa mjadala wa kujadili maisha ya mtu na familia yake....huku ni kutumia vibaya akili na maarifa uliyopewa bure na mungu
 

Hivi kweli tukianza kutafuta idara zote za serikali mbali na hiyo idara ya usalama wa Taifa hatuwzi kupata watumishi wa serikali waliostaafu na bado wanafanyakazi kwa mkataba? Hivi wanasiasa watakaa wapi wajisafishe kuwa vyama vyao havina udini? iweje kila hoja inayoletwa humu JF lazima iongelee kwa sababu mtu fulani ni dini fulani? siyo udini huu kweli. Nimeona post moja inasema,eti jina lenyewe RASHID, jamani tunakwenda wapi?
 

hata kama wakiamua kustaafu leo, hiki chombo kipo imara na kitazidi kuwa imara, wenye wivu wajinyonge.
 
mkuu acha utani, inamana haya hili hujui?????????? ngoja kigwangalla aje hapa atakwambia anavom attend mgonjwa wake lissu

Maradhi gani yanamsumbua jamaa yetu, inamaana mjengoni safari hii kutakuwa kustaarabu?
 

mkuu nadhani umeenda chaka hapo. mie nasema kuwa suala la ufanisi wa mtu halitokani na rika lake. kama mtu ana uwezo haijalishi ni mzee au kijana. tunachotaka ni kuzuia makosa katika kufanya maamuzi. halafu kumbuka uwepo wa hao watu unaowaita wazee haimaanishi kazi haziendi mkuu. hao unaowaita wazee wanafanya kazi kwa ushauri wa vijana ambao wamewazunguka kila kona. kumbuka penye wazee hapahalibiki neno. hata kule kijijini maamuzi mazito na jukumu la kuangalia jamii wamepewa wazee kwa kuamini kuwa kuishi kwao miaka mingi, wamevumilia mengi na wana busara ya kutosha. cha muhimu ni namna gani ninyi vijana mtatumia busara za wazee kufanya maamuzi sahihi

kuhusu hilo la kuvunjwa kwa sheria hapo dnugu umepotea. pitia sheria namba 2 ya 2002 ya utumishi wa umma pamoja na miongozo yake. utajua kuwa kumbe kuna ajira za kudumu na ajira za mkataba. kama mtumishi amestaafu na mwajiri bado anamhitaji, kinachofanyika ni kuwa anastaafu kwa mujibu wa sheria na mwajiri anampa mkataba kwa kadri inavyofaa. kumbuka anayetoa mkataba ni mwajiri. hivyo huwezi kuanza kulialia eti Othman na Zoka wanazuia nafasi za wengine. hayo ni majembe. hata kule kijijini, mara nyingi jembe zuri halitupwi labda unabadilishwa mpini tu. lakini jembe baya hata kama umelinunua leo unaweza kulitupa darini kwa vile halikusaidii.
 

Mkuu, umesema vyema, lakini humu JF hairuhusiwi kujadili maisha binafsi ya mtu mmoja tu naye ni Mzee wetu WILBROAD PETER SLAA, huyu ukimgusa tu burn.
 
Mwanakijiji hoja yako nimeipenda. Baadh ya wachangiaji wanashindwa kutofautisha mwanasiasa na mtumishi wa umma. Mimi napendekeza sasa ni wakati muhimu mwanakijiji na raia wema kutengeneza dossier inayoonyesha wafanyakazi wote ambao muda wa kustaafu umefika,wamepewa mikataba au wameforge umri ili washugulikiwe na wananchi, human right activist na asasi mbalimbali. Inabid maandamano yafanyike kwenda kila wizara wanayojua hawa watu wameshikilia nafasi nyeti na hawatak kuachia.kuhusu RO, yeye kama kweli muda umeisha apishe. Kipind cha nyerere na mwinyi kila mwananchi,alipenda ajiite mlinzi wa nchi yake.kwa sasa ikionekana umepeleka taarifa muhim kwa tiss,pccb,uamiaji,polisi. Wewe ndiye unakuwa adui. Maadili katika idara hizi hakuna. Mwakyembe anasema madin ya rwanda yalibadilishwa bandalin dar huku polisi,tiss wakiwa wausika wakuu. Idara hizi zote zina kuzi-reassemble na waliotimiza muda wakustaafu wapishe
 

sijamdharau mtu hata mmoja mana hata mimi nina wadogo zangu wamefeli, lakini sababu za msingi zinajulikana, mojawapo ni watoto kutumia mitandao ya kijamii hususan FACEBOOK kutafuta wapenzi na wachumba, kuangalia picha za ngono na lmambo yanayofanana na hayo.......... sheria zinafuatwa ndio mana hao unaotaka wastaafu waliingia kwa sheria na wataondoka kwa sheria....................asante kwa kutambua ignorance yangu kwani ndio sifa ya kibinadam, ila wewe usitumike, ni hatari kwa afya yako na famili na taifa kwa ujumla. be free in ur thinking
 

Unaongea nini wewe?wezi wa EPA,Kagoda,Richmond,Twiga,Pembe za Ndovu,Mwakyembe,Dr nani sijui na uozo mwingine mwingi uko wapi,unakuja kutuletea eti wanakamata majambazi wakati wanakamata vibaka tu.
Think twice mkuu kabla hujatetea hicho chama chako hapa.
 

Nadhani watu kama ninyi mnahitajika ili muwe mnatufafanulia masuala ya msingi kama haya hasa pale ambapo tunataka kupotoshwa kwa sababu tu hatujui na hivyo tunabakia kuona serikali yetu haifai kumbe sivyo. Ila pamoja na kutojua bado mleta mada alini-bore pale alipo tajamajina ya watu wanaotakiwa kustaafu na kuongeza kuwa na wengine wengi, sasa nikajiuliza huyu jamaa interest yake katika hili ni nini? nikaanza kujiuliza naye anafanyakazi huko idara ya usalama wa taifa na anaona amezibiwa riziki au basi tu.
 

taratibu mkuu, hasira haijengi, hata ruzuku ya chama pia imeliwa na inazidi kuliwa, wakihoji wanatimuliwa
 
UDINI udini utatumaliza sana tu watanzania, kumbe tatizo hapa ni jina na siyo umri tena? kazi ipo! Basi RASHID aondoke aingie PETER SLAA au vipi. Nimesha kuwa bored, hivi tutafika wapi na udini udini huu.

Mbona CAG alionezewa mda lakini watu hawasemi.
 

hiki chombo hakitabomoka kirahisi kama mnavodhani mkuu mwanakjj.........na wala hakitayumba, due to its proffessionalism........ajenda zenu za kisiasa hazitafanikiwa...........jaribu tena baadae.
 

Umewahi kusikia msemo wa kiswahili kuwa WINGI SI HOJA? Mnaweza kuwa wengi kwenye taasisi; if you do not have the power, you are castrated!! It is he who has the power that will influence the direction to be followed na ndio maana Kikwete cannot hide from his involvement in tearing this nation asunder on religious lines; kwenye huo mfano wako Kikwete ndio Kocha na wote wanacheza kufuatana na formation yake kwani yeye ndiye anayepanga timu kufuatana na itikadi ya vipedo.
 

Jicho langu la tatu linaona mbali sana. Sasa tuendako siko, Sidhani kuna sababu yoyote ya kujibu post kama hii ya KAJUNGU. Mikataba hiyo inayosemwa kwenye ajira ipo kisheria na imepitishwa bungeni, lakini kwa sababu Wabunge wetu hao hao ndiyo wanaotunga sheria na ndo hao hao wanaokuja kunadamana kuwa sheria zimevunjwa wanaweza kufanya hivyo.
 

Kwanza to put the records straight sina ndugu aliyefanya mtihani wa form 4 mwaka ulopita, na je mkuu wa Green Acres aliyelalamikia wanafunzi wa shule yake walowekewa maksi kwenye masomo ambayo hawakufanya na walofaulu bila kufanya mtihani unawaongeleaje? kinachoniuma ni number of failures tunaongeza mtaani kila uchao, niliposema mfumo ndo umewafelisha watoto hao nilikuwa na maana yangu, km una kumbukumbu nzuri serikali kupitia kwa aliyekuwa Waziri Mkuu Mh. Lowassa ndo walioanzisha shule za kata na walikuwa na kusudi zuri, lakini shule hizi zilisahaulika baada ya kuingia Mh. Pinda aliyekuja na sera ya kilimo kwanza, so to say shule za kata zingekuwa well furnished kwenye walimu ambao wapo well paid, maabara, maktaba, vitabu vya kiada na ziada hzo zero zingepungua na watoto hao waloelimika wangeendesha kilimo cha kisomi zaidi, vilevile imefika kipindi shule zetu zote wafundishe vocational skills ambazo zingewasaidia hata hao walopata zero kupata kitu cha kujikimu, kuliko sasa ambapo hawajielewi maana hawana mbinu mbadala wa kujikimu, hence kwa hali hii tutazalisha vibaka na machangudoa wengi coz hata wakiingia umachinga na mama ntilie mgambo hawatawaacha salama.
 
kuna baadhi ya waandishi, wachangiaji hapa JF wenye majina makubwa wanazidi kuporomoka umaarufu wao kutokana na kuleta mada za chuki, fitna, majungu na zinaoonyesha hasira ama kukosa kitu flani hivi kama madaraka au mali... hii haitatufikisha mbali kama taifa.
 

Mbona unaonekana sana kuguswa na hii hoja ya MM,Please whats so apecial abt this thread kamanda
 


Mbatia hapo alipo amefika kwa sababu ya huruma ya magamba, vinginevyo angekua anagmbania ruzuku na viongozi wenzake.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…