Phillipo Bukililo
JF-Expert Member
- Dec 29, 2015
- 18,487
- 13,611
Ameandika kupitia ukurasa wa mtandao wake wa Twitter mwanaharakati na mwanasheria maarufu nchini Fatma Karume
"Hao WAARABU msiowapenda wameweza kufanya MAPINDUZI ya Kiuchumu nchii zao kwenye kipindi kifupi sana. Dubai haitegemei mafuta.Badala ya kubaguwa basi ndugu zangu tujifunze.Acheni UBAGUZI Jamani. Ni USHAMBA tu."
Kwa maoni yangu: Hakuna tatizo kufanya biashara na Dubai lakini TERMS za MKATABA lazima ziwe FAIR.Hatuwezi kuwapa “sovereignty” yetu.
Pia Fatma ameandika
"Hakuna aliyeuza BANDARI la Dar.Hoja ni MKATABA wa Kimataifa baina ya Dubai na Tanzania na vipengele vichache vinavyoathiri “sovereignty” yetu.WAPUMBAVU ndie wanaleta ujinga wa*Rais ni KE. WaTZ hawatomuamini rais KE tena.*Rais ni MZNZ anauza mali ya TNG*Uarabu".
View attachment 2653915
Akili za kipuuzi za kibaguzi huwa ni upofu mtupu. Ubaguzi ni dhambi na malipo yake ni hapa hapa juu ya ardhi.
Unambagua Samia au waziri Mbarawa halafu unakwenda Ulaya kutembea unakutana na katoto hakana hata miaka saba duniani kanakurushia ndizi, unabakia kununa na kulaani kwanini umebaguliwa. Kumbe ni malipo ya upuuzi ulioufanya siku za nyuma dhidi ya Rais wako.