FBI walivyomdaka Thomas Lyimo 1998. Hata kama huwapendi wamarekani, basi tuwaheshimu tu

FBI walivyomdaka Thomas Lyimo 1998. Hata kama huwapendi wamarekani, basi tuwaheshimu tu

Kumsaidia gaidi wa kiislamu , kwa mchaga ni ndoto
Tuache unafiki wale jamaa ni wapinga Kristo
Na mchaga anahamu na fursa , na sio hela -
Kama wangekuwa wanapenda hela sana , Basi ungekuta ni machangudoa
But ninapitaga sana Moshi , Ni hakuna machangudoa
Nenda Moshi, Dar es Salaam street ukajionee machangudoa. Wachaga kwenye hela hawajui Yesu. Kinachowasaidia huwa wako smart sana
 
Yeye alifuatwa na wateja na kumpa design ya Tank(lilowekwa chemicals za bomu na kilipuzi (bom detonetor ) wakamlipa na kuchukuwa tank lao. akuusika kama muunda bomu
Kibongo bongo nae angeonja joto ya jiwe.

Wenzetu wanafanya kazi kwa weledi na haki mtu usiyehusika hupewi case kizembe bongo ukihisiwa tu kwa lolote hata kama ulikatiza eneo la tukio muda linatokea unaweza ukaoga mvua.
 
Tuwaheshimu kwakuwadharau polisi wetu!? Kwani ugaidi na Tanzania wapi na wapi!?
Kila nchi ina uzoefu wa kukabiliana na uhalifu uliokithiri kwenye nchi zao

Kwa Polisi hawa wa Wambura, unawezakuta 50% ya wanaodaiwa ni wahalifu, sio wahalifu kwa sababu inatumika akili ndogo sanaaaa kuwatambua wahalifu
 
Pale walikuwa wanamwinda tu Sadam. Ile propaganda ya nuclear ilikuwa gear ya kumdaka Sadam kama walivyomfanyia Gadafi. Mwisho wa picha wakamdaka jamaa shimoni. Na Gadaf wakamdaka chooni sijui. Wako kumlia timing Putin. Ni saa zinahesabika hapo,watamuokota jalalani. Namuona M7 nae anajipendekeza. Ashukuru tu umri umeenda. USA wameadvance sana. Taget zao hazikukosi. Mchina tu ndio kashtukia picha. Amegoma kukivamia moja kwa moja kisiwa cha Taiwan

Ulianza vizuri ukamalizia na pumba. Marekani hawazi kumnasa Putin na ikitokea wakafanya hivyo either marekani au Urusi inaweza futika kwenye ramani ya duniani
 
Ilikuaje,hebu tupe faida na sisi

Kilikua ni kipindi kigumu cha vurugu za kidini katika miaka ya 90's mwanzoni nchini India.
Dutt baba yake ni mhindu mama yake alikua ni muislamu, kwahiyo hilo halikumuacha salama akawa anapokea barua za vitusho nyingi kutoka watu wasiojulikana akishutumiwa kama kuwa ana damu ya kiislamu na wao wahindu hawamtaki kuwa pamoja nao na wanaweza kumfanyia baya lolote. Jamaa alivyooona vitisho ni vizito sana, akaona isiwe tabu akatafuta connection ya kupata silaha ya kujihami.
Kwahiyo akapata connection kwa arm dealers wakamuahidi watamuekea mambo sawa.
Bomb Blast ya Bombay ilifanywa na Gangsters' amabao ndio walikua waki rule ma gang ya kihuni Mumbai ambao majority yao walikua ni waislamu. SO ulipofanyika ule mchongo wa miripuko mzigo ulipitia Bahari ya Gujrati ukasafairishwa kwa malori mpaka mumbai. Wengi walioshiriki hili jambo hawakuwa waki juwa lolote kama ilivyo matukio mengi ya Kigaidi. Wanaokua wanafahamu ni wachache sana.
Mzigo uliingia Gujrat ukionekanwo kama mizo wa Pombe ukisimamiwa na Wavuvi na maofisa Neavy. Kipindi hicho Gujrat Pombe ilipigwa marufuku kwahiyo Pombe ilikua ndio dili kubwa ya kimagendo ukanda ule. Na baada ya hapo ukasafirishwa kwa malori mpaka Mumbai. Ulipofika Mumbai mzigo ukaelekea moja kwa moja kwenye Nyumba ya Dutt. akapewa Bunduki yake. Na jamaa wakamuomba awahifadhie gari ilikua na mzigo kwa muda wa siku mbili tatu watakuja kuuchukua waende nao sehemu zao husika. Yeye akaona isiwe noma akawahifadhia gari lao ndani ya kompound yake huku yeye akijua kua lile gari limebaba silaha na risasi za biashara ambazo walikua wakiuuza kwa magendo. Kumbe ndani yake hamkua na silaha tu bali mulikua na Mabomu yaliyotumika kuripulia.
Baada siku mbili tatu wakachukua mzigo wao maisha yakaendelea.
Mara tu baada mabomu kuripuka katika msako wa ufuatiliaji ndio ikagundulikana kuwa mzigo uliwahi lala kwenye nyumba ya Dutt kwa siku mbili tatu, nayeye akaingizwa kundini ya watuhumiwa. ALikaa ndani kwa muda wa miaka miwili, na alipotoka kesi iliendelea kwa zaidi ya miaka 10. Na mwisho alshinda kesi kuwa hakuhusika na ugaidi, Ila alihukumiwa kufungwa miaka 6 kwa kosa la umilikaji wa sialha kinyume na Sheria.

Wengi waliohusika kwenye lile tukio hawakuelewa kabisa kinachoendelea. Wengine walielewa ni Ishu za Pombe haramu, wengine walijua ni Madawa ya kulevya, wengine walijua silahi za biashara. So walishirikishwa bila kufahamu nini wanafanya. Wengi waliteswa, wengine walijiua kwa fadhaa, wengine walifia majela. Wako waliokuja kutoka siku za mbele ila mpaka leo wanashindwa kuishi kwa amani.

Magaidi wa kimataifa ni watu wanaofanya mambo yao kwa kutumia akili kubwa mno.
 
Huyu Bwana yuko zake Kimara Bucha kwenye kasri au tuite hekalu lake mithili ya ikulu ndogo ya Singida, anakula bata huku akilea wajukuu,ameshazeeka sasa.

Yeye na kizazi chake walipigwa ban wasikanyage USA wala kusogelea ubalazi wao.

Wakati ubalozi wa Marekani unalipuliwa nchini pamoja na Nairobi Kenya, polisi na wapelelezi wetu wakaanza kukamatakamta watu ovyo eti ni washukiwa,watu wasiopungua 200 walikuwa shimoni kule Central Police, DSM.

FBI wakapata taharifa kuwa kuna suspects wamekamatwa wako central, wakaomba kuwaona. Kufika kule wakawaambia polisi wa bongo kuwa waachieni wote hakuna suspect hapa, hakuna gaidi anavaa yeboyebo amepauka kwa njaa.hawa ni vibaka tu,IGP akaambiwa u know anything about terrorism?

Jamaa wakaingia chimbo wakaomba akaunti za wafanyabiashara na vionhozi wote wa kisiasa na wanaharakati ambao wameingiziwa mpunga mrefu ndani ya miezi kadhaa (sikumbuki) Thomas Lyimo mfanyabiashara aliyekuwa na garage yake Kimara bucha na vibanda vya maziwa Dar nzima enzi hizo akajikuta matatani, ni baada ya kuonekana akaunti yake iliingiziwa pesa hazina maelezo, kipindi hicho sheria ya money laundering haijatungwa.

Kufustilia kwa kina ni kweli bomu lililolipua ubalozi liliunganishiwa kimara kwenye garage yake.

Hayo yakifanyika mastermind alikuwa kijana mdogo toka Zanzibar Ahmed Khalfan Ghailan,mshirika wa Alqaeda ambaye baadae anakuja kuwa mtu wa karibu kabisa na Osama Bin Laden
ndie alimuingizia huo mpunga kabla ya kukimbilia Nairobi na uarabuni.alikuwa kijana mfogo tu wa miaka 24 au 25, kwa sasa bwana Ghailan ni mtu mzima sasa anakaribia miaka 50 yuko Guantanamo Bay Camp chini ya ilinzi mkali.

Huwapendi USA ila una vingi vya kujifunza kwao

OKW BOBAN SUNZU
Kenya siku mbili baada ya kushambuliwa alitumwa Fbi mmoja ambaye kwa maelezo yake alikuwa hajawahi kukanyaga ardhi ya Afrika , let alone Kenya ,
Jamaa ndani ya saa 24 toka kuingia kenya alifanikiwa kumkamata mtuhumiwa akiwa anauguzwa hospitalini kwa kutumia jina bandia ..
 
Kenya siku mbili baada ya kushambuliwa alitumwa Fbi mmoja ambaye kwa maelezo yake alikuwa hajawahi kukanyaga ardhi ya Afrika , let alone Kenya ,
Jamaa ndani ya saa 24 toka kuingia kenya alifanikiwa kumkamata mtuhumiwa akiwa anauguzwa hospitalini kwa kutumia jina bandia ..
Dah wwnzetu wako mbali kwenye mambo ya intelligence
 
Dah wwnzetu wako mbali kwenye mambo ya intelligence
Ni hadi upate nafasi ya kujua wanayoyafanya , otherwise utaona marekani na intelligence yao ni ya kawaida .
Shambulio la Nairobi lilikuwa na changamoto ya taarifa ,mashuhuda walikuwa wanasema gari lililokuwa limebeba bomu lilikuwa canter, uhalisia ninkuwa gari lililobema bomu lilikuwa ni Isuzu, ambayo kwa wakati huo nalo lilikuwa maarufu kwa jina la canter , pamoja na misleading info , Fbi walikamata wahusika
 
Ni hadi upate nafasi ya kujua wanayoyafanya , otherwise utaona marekani na intelligence yao ni ya kawaida .
Shambulio la Nairobi lilikuwa na changamoto ya taarifa ,mashuhuda walikuwa wanasema gari lililokuwa limebeba bomu lilikuwa canter, uhalisia ninkuwa gari lililobema bomu lilikuwa ni Isuzu, ambayo kwa wakati huo nalo lilikuwa maarufu kwa jina la canter , pamoja na misleading info , Fbi walikamata wahusika
Hatari
 
Kilikua ni kipindi kigumu cha vurugu za kidini katika miaka ya 90's mwanzoni nchini India.
Dutt baba yake ni mhindu mama yake alikua ni muislamu, kwahiyo hilo halikumuacha salama akawa anapokea barua za vitusho nyingi kutoka watu wasiojulikana akishutumiwa kama kuwa ana damu ya kiislamu na wao wahindu hawamtaki kuwa pamoja nao na wanaweza kumfanyia baya lolote. Jamaa alivyooona vitisho ni vizito sana, akaona isiwe tabu akatafuta connection ya kupata silaha ya kujihami.
Kwahiyo akapata connection kwa arm dealers wakamuahidi watamuekea mambo sawa.
Bomb Blast ya Bombay ilifanywa na Gangsters' amabao ndio walikua waki rule ma gang ya kihuni Mumbai ambao majority yao walikua ni waislamu. SO ulipofanyika ule mchongo wa miripuko mzigo ulipitia Bahari ya Gujrati ukasafairishwa kwa malori mpaka mumbai. Wengi walioshiriki hili jambo hawakuwa waki juwa lolote kama ilivyo matukio mengi ya Kigaidi. Wanaokua wanafahamu ni wachache sana.
Mzigo uliingia Gujrat ukionekanwo kama mizo wa Pombe ukisimamiwa na Wavuvi na maofisa Neavy. Kipindi hicho Gujrat Pombe ilipigwa marufuku kwahiyo Pombe ilikua ndio dili kubwa ya kimagendo ukanda ule. Na baada ya hapo ukasafirishwa kwa malori mpaka Mumbai. Ulipofika Mumbai mzigo ukaelekea moja kwa moja kwenye Nyumba ya Dutt. akapewa Bunduki yake. Na jamaa wakamuomba awahifadhie gari ilikua na mzigo kwa muda wa siku mbili tatu watakuja kuuchukua waende nao sehemu zao husika. Yeye akaona isiwe noma akawahifadhia gari lao ndani ya kompound yake huku yeye akijua kua lile gari limebaba silaha na risasi za biashara ambazo walikua wakiuuza kwa magendo. Kumbe ndani yake hamkua na silaha tu bali mulikua na Mabomu yaliyotumika kuripulia.
Baada siku mbili tatu wakachukua mzigo wao maisha yakaendelea.
Mara tu baada mabomu kuripuka katika msako wa ufuatiliaji ndio ikagundulikana kuwa mzigo uliwahi lala kwenye nyumba ya Dutt kwa siku mbili tatu, nayeye akaingizwa kundini ya watuhumiwa. ALikaa ndani kwa muda wa miaka miwili, na alipotoka kesi iliendelea kwa zaidi ya miaka 10. Na mwisho alshinda kesi kuwa hakuhusika na ugaidi, Ila alihukumiwa kufungwa miaka 6 kwa kosa la umilikaji wa sialha kinyume na Sheria.

Wengi waliohusika kwenye lile tukio hawakuelewa kabisa kinachoendelea. Wengine walielewa ni Ishu za Pombe haramu, wengine walijua ni Madawa ya kulevya, wengine walijua silahi za biashara. So walishirikishwa bila kufahamu nini wanafanya. Wengi waliteswa, wengine walijiua kwa fadhaa, wengine walifia majela. Wako waliokuja kutoka siku za mbele ila mpaka leo wanashindwa kuishi kwa amani.

Magaidi wa kimataifa ni watu wanaofanya mambo yao kwa kutumia akili kubwa mno.
Asnt mkuu kwa simulizi nzr
 
Back
Top Bottom