Habari ndungu zangu wote wana Barcelona. Barca Up!!
Ndugu zangu Napenda tutumie nafasi hii kueleweshana kujuzana Mambo mbali mbali ambayo yamekua yakitupa shida na kuleta maswali mengi Vichwani Mwetu sisi au mimi kama Mshabiki wa Ukweli Barca.
Yah! Nikuhusu Mwendo watimu kwa miaka ya hivi karibuni sote tutakubaliana sio wakuridhisha sana.. ukilinganisha na miaka mitatu au minne iliyopita kipindi timu yetu ikinolewa na kocha Pep Guardiola. Ktk misimu mitatu au miwili ilyopita tume pata makocha wawili ambao ni Tito Villanova(R.I.P) "Tata" Geraldo Martino na huyu wa sasa luis Enrique ni wa tatu. Misimu yote kuanzia wata Villanova na Wa Martino imekuwa ni misimu isiyoridhisha japo tuna shinda sawa lkn si kiuhakika ni kibahati bahati tuu na tuna timu nzuri pamoja na Academy bora kuliko zote za football Duniani.
Hii hali ya kubahatisha ilinipa shida sana b'coz tunakikosi na academy bora kwanini tunasuasua.na matokeo ya kusuasua huku tuliona kwenye mechi ya Barcelona Vs Bayern Munchen na mechi nyngne kama Barca Vs Chelsea na derbies kadhaa dhidi ya madrid na Atletico madrid. Yani tulikua tukikutana na timu kubwa tunapata shida.
Tukisema ni kocha yawezekana na gatwa waliomfuatia walkua wababaishaji. bt sitakikuamini sana wapo wanaosema Guardiola ndio anaijulia barca.. yah! Nahuo nao ni mtazamo. Yah! as we knw kwamba ndie kocha aliyepata mafanikio zaid kuliko yeyote kwa kipndi kifupi. Ni sawa kabisa na tunamshukuru kwa hilo.. lakini mimi pengine ninaweza nikawa na mtazamo tofauti.. kuna Makocha aliopita Barcelona ambao sitakaa ni wasahau kwakuiunda timu na kuifanya iwebora kama luis Van Gal, Yohan Cryff, Frank Rijkaard. japo hawakutisha kama Guardiola ila na wanastahili pongez kubwa sana za dhati pia naweza nikasema kama sio wao pengine Guardiola angekuwa kama Martino au Villanova kwani wao ndio waliunda timu ikianziwa kwa Van Gali aliyeibua vipaji mbali mbali kama Xavi Hernandez, Iniesta na wengine kibao.. Yohan Cryff (barca legend) akiiunda timu na kuendelezwa na Frank Rijkaard na kumaliziwa na Pep Guardiola huyu kafaidi mwisho matunda yawenzake waliomtangulia walioyatolea jasho. Sifa kwao wote.
Tatizo ni kwamba huwezi kuifananisha Barcelona ya vipindi hivi na ya sasa.. iliyopita ilikua bora zaidi sasa badala ya kuendelza ubora tunazidi kushuka ktk viwango vya ubora. Hii imenipa changamoto kidogo na nikatafari sana tatizo liko wapi? Baada ya kufikiria kwa makini Sana nikagundua tatizo linaweza kuwa katika sehemu kuu tatu.. nazo ni :a) Uongozi wa timu b) kocha c) wachezaji
Uongozi wa timu unaweza kuwa umekaa kibiashara sana badala ya kiushindani au kisoka zaidi b) kocha: kufeli kimbinu, kutopewa ushirikiano na Uongozi wa timu pamoja na kutopewa muda wa kutosha, kocha kutopewa ushirikiano na Wachezaji. C) wachezaji; kuwa na migogoro na uongozi wa timu juu ya maslahi yao wa matatizo yao binafsi, kuto kushirikiana na kocha au kutokuwa na maelewano nae.
Barcelona kwakumleta Enrique au kwa kuabadili Makocha itakuwa imetibu tatizo???? La hasha!! Hivyo sasa nini kifanyike? maana me sioni kama Barcelona imesha settle. Bado hajijakaa kama ile ya Guardiaola bado tunashinda kibahati bahati tu.. previews Barcelona vs villareal, Barcelona vs A. Bilbao. Barca vs Apl N.k sisemi kuwa kocha Enrique ni m'mbaya NO! Ameshinda michezo yake yote mi 4 ya ligi na 1 wa Uefa ni takwimu nzuri bt bado kuna ushindi finyu ambao huwezi ukalinganisha na ubora wa wachezaji wetu.
Wadau Mnaona TATIZO NININI? NA NINI Kifanyike turudishe Hadhi yetu. Coz Mimi sina uhakika sana na timu yangu tukikutaba na timu kubwa. labda mtakuwa mnajua zaidi naombeni mnieleweshe tatizo likowap? Na nini Kifanyike? Tuendeleze ule Ufalme Wetu???