ningependa kuona maoni ya
FaizaFoxy .... je hapa Mheshimiwa Zitto yuko sahihi au kachemsha?
Hapo Zitto anaongelea Tax, tena ya Capital gain.
Zitto anaelewa sana kuhusu Tax evasion na Tax avoidance lakini hilo anajifanya kama halijui. Ananshangaza!
Hapo jamaa hawakufanya Tax evasion hapo ni simply Tax avoidance, kisheria.
Hakuna ujanja hapo, kama hawakufanya evasion, walichofanya "avoidance" ni halali kabisa.
Zitto anachoshindwa kueleza ni kuwa IPTL ilikuwa na mgogoro na kampuni ya Kitanzania, kaingia Singasinga kaiona opportunity na kajuwa vipi atatatuwa huo mgogoro, kaongea nao wamekubaliana, kawanunua, kawalipa, kavuta fedha walizokuwa walipwe wao.
Kinachofata hapo ni uhalali wa tax na ndio anauongelea Zitto, kachimbuwa kakuta hakuna tax evasion bali kuna tax avoidance ambayo kisheria ni halali, cha kushangaza hapo hagusii kabisa.
Sijui msichokielewa anachoongelea Zitto zaidi ya hicho ni nini?
Nadhani, Zitto angekuwa kidogo mjanja asingeongelea hilo la kampuni kuuzwa million 6, unless anajuwa anachokifanya ila anataka ku divert msimamo, kuna kila uwezekano na yeye kavuta au anataka kuvuta amma kwa Singa amma kwa IPTL amma kwa huyo Mtanzania mwingine ambae hatajwi sana humu, amma kisha vuta kwa mmoja wao, lakini yeye huyo Mtanzania ndio master-mind wa huu mkorogano na Zitto anajuwa sana hilo.
Hapo sasa hivi kuna kila mtu kutaka kuvuta kwa Singa kwa kupiga makelele, kwa sababu hapo ndio where the buck stopped.
My Take:
Nasema huyo Mtanzania ni mastermind kwa sababu yeye alifikiri akiwabana sana IPTL watakubali yaishe wachukuwe fedha wagawane halafu mitambo yote atabaki nayo yeye aanze kuchuma peke yake kiulaini.
Bahati nzuri au mbaya, Singa kaliona hilo akaingia kati na kuna kila sababu kakubaliana na IPTL kuwa wataumizwa, yeye ana njia mbadala watakuwa ni win win situation, pesa watapata na mitambo haitopotea na wamuamini yeye, na ndicho kilichofanyika.
Hapo aliyeumia ni Mtanzania mwenzetu, tena si kaumia kwa kuwa hajapata faida ya bure, la hasha, faida kapata ya bure tena kubwa sana, kwani yeye hajatia fedha yake katika hili sakata, yeye alikuwa kama godfather tu wa ku-facilitate mambo ndani ya Tanzania. Ndiyo norm kwa biashara zote kubwa duniani.
Alichoumia ni pale alipotaka kubana mpaka mitambo yote ibaki kwake. Kataka kula kiharamu zaidi, ndipo Singa alipoingia na ku rescue.
Sasa, Mbonde kuona hivyo ni lazima apigane, kwani kwa sasa fedha ya kuwalisha wapayukaji hovyo kama akina Tumbili anayo, na afanye nini zaidi? anachofanya ni "kama kukosa tukose wote", lakini amechelewa jamvini karamu imeshaliwa.
Mwisho wa siku, kisheria ataibuka Singa kidedea, labda afanyiwe umafia. Na Singa si mdogo huyo, Tanzania anaijuwa juu chini, kaishi sana pande za Iringa, kama kuna mtu anaikumbuka RCC Iringa, basi ni hao akina Singa, si wageni kabisa Tanzania hii.
Mengine yote ni kubwabwaja, porojo na kuhororoja, kuna mshiko wa watu kunyamazishwa na ndiyo maana unasikia kelele.
Hakuna wizi hapo wa mali ya umma kisheria, kuna "opportunity" na Watanzania kama ujuavyo ni ma "opportunists" kama fisi wanavyongoja mifupa au makopangola wanavyoona mzoga, hawachelewi! ndicho kilichopo.
Usione vinaelea vimeundwa.