Fedha zilizokuwa katika akaunti maalumu ya IPTL (Tegeta Escrow account), ni mali ya umma

Utakuwa unafaidi "matunda" ya nchi wewe kama Prince Rizmoko

Mkuu hakuna haja ya sisi kugombana ktk mitandao bila sababu, wanasiasa mama yao ni mmoja, hawa wanaoitwa wakombozi wa nchi, hawajachukua madaraka, fuso used 600M, wanajikopesha 160M, na mengineyo, je wakichukua madaraka si itakuwa balaa?
 
Hao jamaa ni wajinga sana, wana lialia wakati wanajua kuwa tanesco ilikuwa inalipa deni la huduma ya umeme kwenye escrow account ili wale shareholders waliokuwa na kesi mahakamani waelewane kwanza ili hizo pesa zilipwe kwao,.....
 

ningependa kuona maoni ya FaizaFoxy .... je hapa Mheshimiwa Zitto yuko sahihi au kachemsha?
 
Last edited by a moderator:
Liko Tatizo....leo jioni niliwasikiliza sana Kafulira na Zitto kuhusu ac ya tegeta escrow. Wanamaelezo mazuri lakini hawathubutu kutaja kama ni serikali ya ccm na wanaccm wenyeewe ndo changizo kubwa la ufisadi kiasi hiki!
 

Hivi hizi hela zilienda huko kwa sababu ya Ugomvi wa share Holders ? au Ugomvi wa IPTL na Tanesco kuhusu gharama za Umeme?
 
Ningeshauri tuingie msituni kuikomboa hii nchi kutoka mikononi mwa mkoloni mweusi kwani kwa ujinga wa waTz (sio upole/upendo) na akili ya CCM (eg. bi Asha Bakari) wamejipanga kuhakikisha nchi haichukuliwi kwa kipande cha karatasi

Ndugu yangu wewe ulitegemea Mwigulu apelekwe pale kimchezo?Hiyo ndio Kazi iliyompeleka pale.
 
Hoja nzuri na makini kutoka kwa Zitto.Pia ni vibaya kutanguliza lawama kwa upinzani kuwa umemuachia hili suala Kafulila pekee!

John Mnyika ameliongelea hili ndani na nje ya Bunge mara nyingi.Lilikuwepo pia kwenye hotuba yake kwa niaba ya kambi ya upinzani.Yeye na Kafulila wamewasilisha ushahidi kwa spika kuhusiana na jambo hilohilo.

Muda mwingine ni vizuri kuachana na haya mawazo ya kibinafsi na umimi au "usisi wa Kigoma".Zitto asijitenge na kambi ya upinzani pale maslahi ya taifa yanapolindwa hata na watu asiowapenda.
 
ningependa kuona maoni ya FaizaFoxy .... je hapa Mheshimiwa Zitto yuko sahihi au kachemsha?

Hapo Zitto anaongelea Tax, tena ya Capital gain.

Zitto anaelewa sana kuhusu Tax evasion na Tax avoidance lakini hilo anajifanya kama halijui. Ananshangaza!

Hapo jamaa hawakufanya Tax evasion hapo ni simply Tax avoidance, kisheria.

Hakuna ujanja hapo, kama hawakufanya evasion, walichofanya "avoidance" ni halali kabisa.

Zitto anachoshindwa kueleza ni kuwa IPTL ilikuwa na mgogoro na kampuni ya Kitanzania, kaingia Singasinga kaiona opportunity na kajuwa vipi atatatuwa huo mgogoro, kaongea nao wamekubaliana, kawanunua, kawalipa, kavuta fedha walizokuwa walipwe wao.

Kinachofata hapo ni uhalali wa tax na ndio anauongelea Zitto, kachimbuwa kakuta hakuna tax evasion bali kuna tax avoidance ambayo kisheria ni halali, cha kushangaza hapo hagusii kabisa.

Sijui msichokielewa anachoongelea Zitto zaidi ya hicho ni nini?

Nadhani, Zitto angekuwa kidogo mjanja asingeongelea hilo la kampuni kuuzwa million 6, unless anajuwa anachokifanya ila anataka ku divert msimamo, kuna kila uwezekano na yeye kavuta au anataka kuvuta amma kwa Singa amma kwa IPTL amma kwa huyo Mtanzania mwingine ambae hatajwi sana humu, amma kisha vuta kwa mmoja wao, lakini yeye huyo Mtanzania ndio master-mind wa huu mkorogano na Zitto anajuwa sana hilo.

Hapo sasa hivi kuna kila mtu kutaka kuvuta kwa Singa kwa kupiga makelele, kwa sababu hapo ndio where the buck stopped.

My Take:
Nasema huyo Mtanzania ni mastermind kwa sababu yeye alifikiri akiwabana sana IPTL watakubali yaishe wachukuwe fedha wagawane halafu mitambo yote atabaki nayo yeye aanze kuchuma peke yake kiulaini.

Bahati nzuri au mbaya, Singa kaliona hilo akaingia kati na kuna kila sababu kakubaliana na IPTL kuwa wataumizwa, yeye ana njia mbadala watakuwa ni win win situation, pesa watapata na mitambo haitopotea na wamuamini yeye, na ndicho kilichofanyika.

Hapo aliyeumia ni Mtanzania mwenzetu, tena si kaumia kwa kuwa hajapata faida ya bure, la hasha, faida kapata ya bure tena kubwa sana, kwani yeye hajatia fedha yake katika hili sakata, yeye alikuwa kama godfather tu wa ku-facilitate mambo ndani ya Tanzania. Ndiyo norm kwa biashara zote kubwa duniani.

Alichoumia ni pale alipotaka kubana mpaka mitambo yote ibaki kwake. Kataka kula kiharamu zaidi, ndipo Singa alipoingia na ku rescue.

Sasa, Mbonde kuona hivyo ni lazima apigane, kwani kwa sasa fedha ya kuwalisha wapayukaji hovyo kama akina Tumbili anayo, na afanye nini zaidi? anachofanya ni "kama kukosa tukose wote", lakini amechelewa jamvini karamu imeshaliwa.

Mwisho wa siku, kisheria ataibuka Singa kidedea, labda afanyiwe umafia. Na Singa si mdogo huyo, Tanzania anaijuwa juu chini, kaishi sana pande za Iringa, kama kuna mtu anaikumbuka RCC Iringa, basi ni hao akina Singa, si wageni kabisa Tanzania hii.

Mengine yote ni kubwabwaja, porojo na kuhororoja, kuna mshiko wa watu kunyamazishwa na ndiyo maana unasikia kelele.

Hakuna wizi hapo wa mali ya umma kisheria, kuna "opportunity" na Watanzania kama ujuavyo ni ma "opportunists" kama fisi wanavyongoja mifupa au makopangola wanavyoona mzoga, hawachelewi! ndicho kilichopo.

Usione vinaelea vimeundwa.
 
Hivi hizi hela zilienda huko kwa sababu ya Ugomvi wa share Holders ? au Ugomvi wa IPTL na Tanesco kuhusu gharama za Umeme?

It doesn't matter ni ugomvi upi, kama ni wa Tanesco na IPTL basi umeisha, kama ni ma shareholders pia umeisha.

Post ya juu hapo #50 nimeelezea hili sakata likoje.

Wajinga ndio waliwao.
 
Hapa naona Zitto analazimishwa kuungwa mkono na upinzani wakati yeye huwa hapendi kuungana wapinzanj wenzake kwani atawauzi ccm au ccm hawatamsifia. Ukipenda kujitenga na kujiona msomi na mbinafsi endelea mwenyewe na hao watakaokuunga mkono. Zitto akumbuke yeye ndio sehemu ya kuuvunja upinzani nguvu kwa kujifanya msomi, kuleta mawazo ya ukabila sijui ukanda huku akipata sifa toka ccm na kuvimba kichwa, leo inakuwaje tena kutaka msaada toka upinzani hata kama ni hoja yenye manufaa kwa wananchi?
 

Mtannzania unayemzungumzia ni Ishomire Rugemalila? Yeye si ameshalipwa akaamua kunyamaza?

uhusiano wa hii issue na kina Muhongo na Maswi ukoje? ... ukiangalia kwa mbali unapata picha kuwa kina Muhongo na Maswi hawataki kujihusisha na hizi kelele wanataka ziishe haraka au kama zinaendelea wasiingizwe huko ndani! .... pia sielewi roles za wabunge wa upinzani & wa CCM (wanaopigia kelele hii issue), Spika (anayejaribu kunyamazisha kelele), TANESCO, Werema kama AG
 

Huyo Ishomire or whatever he is, ndiyo master-mind wa mgogoro, kashtuka ngoma iko wavuni.

Mhongo na Maswi, wanaonewa tu, hawana chochoe katika hili, wao wameingia Wizarani IPTL tayari wana mgogoro na Tanesco na wamepelekwa mahakamani.

Kuwaingiza hao ni ujinga tu watu fulani fulani ambao siasa zimewashinda na kilichobaki wanatafuta kila aina ya harufu ya uvundo waifanye ndio pakutokea.

Wanasiasa wa Tanzania wamekosa ubunifu, wao wako kwenye kutafuta media support kwa njia ya mkato, na waandishi wetu si unajuwa? kibahasha kikiingia mfukoni wataandika chochote utakacho. Kama unabisha muuliza Pasco, mzee wa vibahasha.

Uozo mtupu, waandishi uozo, wanasiasa uchwara. Matokeo ndio huu upuuzi, hakuna chochote cha maana. Mwenye kufikiri japo kiduchu anajuwa kua hapa hakuna wizi kuna "opportunity".
 
Mwenye akili za kauzimwa tu ndio hatamuelewa Zitto anasubiri bwana zake wahafidhina waseme ndio aingie kibla,anayesema Zitto mla rushwa si ndio inatakiwa aweke ushahidi mezani?acheni ukilaza mnakubali ingizwa mkenge na fisadi Maswi?achen unafiki wa kimburula mkitegemea Zitto kudharirika hiyo ni ndoto usiitegemee kabisa
 
waandishi wetu si unajuwa? kibahasha kikiingia mfukoni wataandika chochote utakacho. Kama unabisha muuliza Pasco, mzee wa vibahasha.

Uozo mtupu, waandishi uozo, Matokeo ndio huu upuuzi, hakuna chochote cha maana.
FF, kuniita "mzee wa vibahasha" so kunitendea haki!, watu humu watadhani mimi ndio mzee wa kupokea hivyo vibahasha!. Kwenye vibahasha mimi ni msambaza sio mpokea!.

Hili la waandishi uozo nalikubali na ndio reflection ya jamii yetu sisi Watanzania, tukianzia serikali uozo mtupu, inayoongozwa na chama uozo mtupu kilichoozoa kwa rushwa, kinatoa harufu nzito ya uvundo wa rushwa, huku kikiwa na wafuasi uozo mtupu kama kina FF, ambao kila wakipumua ni harufu ile ile ya uozo mtupu!, wanaounda jamii ya uozo mtupu, na waandishi kama sehemu ya hii jamii ya uozo mtupu, ndio wanaowandikia uozo mtupu, na jamii inapokea uozo mtupu, na kuusoma huo uozo mtupu, na kuuamini huo uozo mtupu hivyo Tanzania kuwa ni taifa la uozo mtu katika ujumla wake na ndio maana hakuna chochote cha maana!.

Kama serikali ni uozo mtupu!, bunge nalo ni uozo mtupu!, mahakama nayo ni uozo mtupu!, what do you expect kwa taifa let alone sisi waandishi uozo mtupu?!.

Mungu Saidia!.

Pasco.
 

Wacha kucheza na maneno, mwenyewe ulikiri umeshavipokea sana tu, au tukuwekee ulivyoandika?

Halafu utasambaza nini bila wewe kuvipokea vibahasha unavyosambaza? wacha kucheza na maneno.
 

umeeleweka..thanx
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…