Kibri ya kujificha wewe umeijuaje?
halafu swala la kutotoa mkono hili mimi nalihesabu kama slogani mahususi kulinda heshima ya mziki wake.
Mziki wa hapa bongo bila bifu ni ngumu kutusua, ukifatilia wasanii waliopata mafanikio hapa bifu lilihusika kwa namna fulani, mfano mr nice na dudu baya bila bifu hapa mr nice asingeweza kutusua. Hii nimeiona hata kwenye bongo movies kuna kipindi fulani kulikua na battle kati ya kanumba na ray yaani ni battle ambayo inawagawa mashabiki kuweka upinzani kama wa simba na yanga
Binafsi naamini alikiba na diamond hawana bifu ila bifu liko kwa mashabiki wa hizi timu mbili. Bifu lao ni kama battle yaani lime base kimuziki sio katika maisha ya halisia, mfano bifu ya tory lanez na joyner lucas hua inaishia kwenye mziki tu lakini hainamaana kama wanachukiana
Pengine alikiba angetoa mkono kumpa diamond angepunguza upinzani na kuonekana kama hawana bifu ni acting tu kwa ajili ya manufaa yao kimuziki.
Kuhusu fid q
Kiukweli nilikua namkubali sana fid q wa "ielewe mitaa", "propaganda" na latest "sumu" fid Q wa sasa kalegeza mno yaani nilishangaa naye ameanza mipasho kama ya afande sele kuchambana na wasafi