Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Alichofanya harmonize ni ushamba.
Mi sio shabiki kabisa wa ally kiba lakini hata wewe utaonaje ukiwa umeenda msibani na muislamu mwenzako (harmonize) amekuja kavaa mahereni mabodyguard kibao n.k kama anaenda kupiga show kinyume kabisa na maadili yetu ...
[\b]
Ni kheri walivyoondoka maana inaonyesha wazi kabisa bwana mdogo alikuja kuvimba na sio kuzika
hapo kwenye mr nice umedanganya..Tengua kauliKibri ya kujificha wewe umeijuaje?
halafu swala la kutotoa mkono hili mimi nalihesabu kama slogani mahususi kulinda heshima ya mziki wake.
Mziki wa hapa bongo bila bifu ni ngumu kutusua, ukifatilia wasanii waliopata mafanikio hapa bifu lilihusika kwa namna fulani, mfano mr nice na dudu baya bila bifu hapa mr nice asingeweza kutusua. Hii nimeiona hata kwenye bongo movies kuna kipindi fulani kulikua na battle kati ya kanumba na ray yaani ni battle ambayo inawagawa mashabiki kuweka upinzani kama wa simba na yanga
Binafsi naamini alikiba na diamond hawana bifu ila bifu liko kwa mashabiki wa hizi timu mbili. Bifu lao ni kama battle yaani lime base kimuziki sio katika maisha ya halisia, mfano bifu ya tory lanez na joyner lucas hua inaishia kwenye mziki tu lakini hainamaana kama wanachukiana
Pengine alikiba angetoa mkono kumpa diamond angepunguza upinzani na kuonekana kama hawana bifu ni acting tu kwa ajili ya manufaa yao kimuziki.
Kuhusu fid q
Kiukweli nilikua namkubali sana fid q wa "ielewe mitaa", "propaganda" na latest "sumu" fid Q wa sasa kalegeza mno yaani nilishangaa naye ameanza mipasho kama ya afande sele kuchambana na wasafi
Acha uongo bana Harmo alikwenda na walinzi wake hakwenda na waandishi bali waandishi ndio walikuwa kwenye msiba.Mnao support huyo konde boy ni wapumbavu kiwango cha Lami kama una chuki na kiba Sema mengine lakin sio kuhalalisha aliyoyafanya Konde boya huwez kwenda msiban ghafla na ma body guard na waandishi halafu watu waanza kuambiwa wawapishe shughuli yenyewe ipi uswahili misiba hii ya kiislam hainaga hata pa kukaa VIP umeenda kuleta vurugu...mtoto wa kiislam marangi kichwan....kama unamkubali mtu mkubali kwa kazi zake na kama unamchukia mtu mchukie kwa kaz zake, Kina kiba alionesha uungwana kumuachia uwanja jamaa afanya yaliyomleta sababu walikuwepo pale muda wote na palikuwa pametulia tu..!..usihalalishe hata upumbavu sababu tu mtu unampenda Konde boya namkubali ila alichofanya sio ubinadamu ile sio shighuli ya lwenda kufanya show off hana u star wa mtu kumvizia had misiban
Sema hawa dabiliusibii nao wanapenda sana 'attention', kaja na hao mabodigadi utafikiri labda kuna tishio fulani dhidi ya uhai wake, mbwembwe nyiiingi, watu wapo msibani unakuja na show-off za kishamba, who is Harmonize by the way? Haoni wenzake akina Shetta wapo bize kuhudumia waombolezaje, kawapita moguls Kiba na Fid hapo kama hawaoni, kesho hawahawa ndo unasikia anaumwa sana anahitaji watu wamchangie! Tujifunze kuishi maisha ya kawaida na kuachana na kiki misibani! Shwain!
Jibu wewe,ni kosa kuondoka msibani mda wowote ukijiskia???Kwa hiyo sasa ni kosa kuwa na walinzi?
Mbona na mimi niliondoka hapo au hamjaniona wadau!?
Unavaa hereni msibanihebu twambie msibani wana vaa vipi?
Tena mtoto wa Kiislam kwenye msiba wa Muislam mwenzako!Unavaa hereni msibani
Mwanaume ?
Stupid rubbish and empty mindset
Jamaa kanikera sanaTena mtoto wa Kiislam kwenye msiba wa Muislam mwenzako!
Tena kiwango cha PHDUmeandika Ujinga.
Hisia zake tu, huyu mtu Ali Kiba anamuumaga roho sijui anatamani yeye ndio angekuwa Kiba[emoji134][emoji134][emoji134]Sio kwamba ni hisia zako tu!