Fikra duni za mbeba maboksi kuhusu mustakabali wa CHADEMA baada ya uchaguzi wao.

Fikra duni za mbeba maboksi kuhusu mustakabali wa CHADEMA baada ya uchaguzi wao.

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
94,296
Reaction score
122,540
Mbeba maboksi here I come with my two cents from a distance.

Nianze kwa kuwatakia heri ya Krismasi kwenu waumini wa Kristo.

Kwa wasio waumini, nanyi nawatakieni sikukuu njema na mapumziko mema.

Nimekuwa nikiifuatilia hii mijadala ya uchaguzi wa ndani wa CHADEMA kwa juu juu tu.

Sikuwa kabisa na raghba yoyote ile ya kunifanya niufuatilie kwa kina huo mchakato, hapo awali.

Jana ndo nikapata muda wa kusikiliza kidogo mjadala uliofanyika Clubhouse ambao Tundu Lissu alishiriki.

Nilifurahi zaidi nilipomsikia Bw. Lissu akikubaliana na mtazamo wangu kuhusu yale mazungumzo yao na CCM kuhusu maridhiano.

Kabla ya jana sikuwahi kumsikia Lissu akimkosoa Freeman Mbowe hadharani na kwa uwazi kiasi hicho.

Pamoja na kunifumbua masikio, huo mjadala ulizichochea fikra zangu na kupelekea kuwa na maswali mengi zaidi.

Inavyoelekea huko CHADEMA kuna mpasuko ambao ulikuwa unachemka kwa muda mrefu.

Sidhani kama kwenye miaka ya nyuma tokea Mbowe awe mwenyekiti, aliwahi kupewa changamoto kwenye hizo chaguzi zao za ndani ya chama. Kama imewahi kutokea, mnaojua mtatujuza na kutukumbusha.

Sasa safari hii sijui ni kitu gani kilichomfanya Lissu naye kugombea hiyo nafasi ya uenyekiti wa chama.

Sijui huo uchaguzi wao utafanyika lini.

Na ukishafanyika na mshindi kujulikana, napata shida kuamini kuwa hali ndani ya chama itakuwa salama.

CHADEMA inaweza kutoka kwenye huo uchaguzi ikiwa ni dhoofu sana.

Atayeshindwa atakubali kuwa kashindwa kihalali na baada ya hapo atabaki kuendelea kukijenga chama?

Wakati mwingine napatwa na fikra za huenda Tundu Lissu katumia mwanya huo wa kumpa changamoto Mbowe ili aje kupata kisingizio cha kujitoa kwenye chama hapo mbeleni…

Kwa sasa tumewasikia hao wawili wakiwa hawako pamoja.

Ningependa sana kuona wanafanya mdahalo ili wapiga kura wao wapate fursa ya kuwaona wawili hao wakijinadi mbele zao.

Ila Mbowe naye…..dah. CHADEMA imesha plateau chini ya uongozi wake.

Kwa nini asijiuzulu tu awaachie na wenzie nao wakiongoze hicho chama?
 
Ningependa sana kuona wanafanya mdahalo ili wapiga kura wao wapate fursa ya kuwaona wawili hao wakijinadi mbele zao.
Yeah!...hili wazo zuri sana...


Ila Mbowe naye…..dah. CHADEMA imesha plateau chini ya uongozi wake.

Kwa nini asijiuzulu tu awaachie na wenzie nao wakiongoze hicho chama?
Mbowe anajiona 'Angela Merkel' wa Chadema.
 
Mbowe akijitoa, na akakubali kumuunga mkono Lissu na wakaweka tofauti zao Pembeni Chadema itakuwa ya moto kuliko siku zote,

Mbowe akikomaa na akashinda basi Chadema itadhoofika kuliko siku zote za uwepo wake na mama atapata 90+ % uchaguzi ujao.

Natamani kusikia na maoni ya
Mzee Mwanakijiji
 
Lissu na Mbowe na wengineo kama wapo, fanyeni mdahalo muwaeleze wanachama wenu kuhusu sera na itikadi zenu, malengo yenu, na wapi mnakotaka kukipeleka chama katika miaka 5/10 ijayo.
 
Mkuu Nyani Ngabu chaguzi zote ndani ya CDM Mwenyekiti Mbowe hakuwahi kupingwa kama uchaguzi wa sasa, this time mambo mengi yameibua hisia ya Wanachama yakiwemo
1. Upotevu na utekaji wa vijana wetu wakiwa katika majukumu ya Chama.
2. Ubakaji wa Demokrasia katika uchaguzi.
3. Kuna jambo la kulamba asali.

Mambo haya yameibua Wanachadema kutaka mabadiliko ya Uongozi wao wa juu.
 
Kwa Mujibu wa Tundu, wana ugomvi mkubwa sana personal na Chairman..

Tundu, Lema, Heche, Msigwa

Na anasema mahusiano yao yamebaki civil na sio kama zamani.

Na malalamish yao ni kuwa Chairman amekuwa akiwatenga...

Now they play smart kama vile ni issue ya demokrasia na ubadhirifu ndani ya CDM na Dira mpya ya CDM

FAM has been betrayed by people he trusted, na TL anasema kwenye huo ugomvi ana fair share yake.

TL anasema issue ni maridhiano, lakini wengi wanaona FAM kala hela za "mama Abdul' kama anavyosema.. madai ambayo ni questionable..

Lakini zaid ni baada ya Kutoka Moshi kwenye mjengo wa FAM..
Kwamba FAM amelipwaje pesa zake na sisi hamna chochote... Jealousy?

TL kamfanyia FAM ambush kipindi hiki, nadhani hii imepelekea FAM aoneshe na yeye msuli.

Hate na retribution style ya TL ni alarming, ana collabo na SyW wanaotaka kujibu mapigo kwa kunyimwa platform na CDM kwenye mambo yao ya harakati za DP world.

Hii ni personal fights ndani ya CDM zaidi ya hiz blabla tunazosikia.

Wakwenda waende, atakaeshidna ashinde, atakaeshonwa ashonwe..

TL anasema ha hami mtu... Ila FAM baada ya kushinda atam monitor TL alafu atamtimua..

Time.
 
Ila Mbowe naye…..dah. CHADEMA imesha plateau chini ya uongozi wake.

Kwa nini asijiuzulu tu awaachie na wenzie nao wakiongoze hicho chama?
Whether Mbowe anatetea kiti cha uenyekiti au anashindwa, tayari ameingia kwenye kapu moja na akina Lipumba, Momose Cheyo, Dovutwa, Mzee wa Ubwaba na marehemu Augustino Mrema

Wote hawa wana kitu kimoja in common: ULAFI wa pesa.
 
Mkuu Nyani Ngabu chaguzi zote ndani ya CDM Mwenyekiti Mbowe hakuwahi kupingwa kama uchaguzi wa sasa, this time mambo mengi yameibua hisia ya Wanachama yakiwemo
1. Upotevu na utekaji wa vijana wetu wakiwa katika majukumu ya Chama.
2. Ubakaji wa Demokrasia katika uchaguzi.
3. Kuna jambo la kulamba asali.

Mambo haya yameibua Wanachadema kutaka mabadiliko ya Uongozi wao wa juu.
Deus Soka
 
Kilichonifurahisha kwenye mazungumzo ya Lissu na watanzania jana ni kuwa anaonekana ana vision kubwa ya reforms anazotaka zifanyike ndani ya CHADEMA na kwa Taifa kiujumla. Sijasikia Mbowe yeye anataka CHADEMA ya aina gani baada ya kuwa ameshaongoza chama kwa miaka takriban 20
 
Mbowe akijitoa, na akakubali kumuunga mkono Lissu na wakaweka tofauti zao Pembeni Chadema itakuwa ya moto kuliko siku zote,

Mbowe akikomaa na akashinda basi Chadema itadhoofika kuliko siku zote za uwepo wake na mama atapata 90+ % uchaguzi ujao.

Natamani kusikia na maoni ya
Mzee Mwanakijiji
Maoni yangu siifahamu SIASA lakini nadhani Mbowe na Lissu wote kuna asali wamekwisha lambishwa kwa hiyo wanaitendea haki ili asali nyingine iliyo baki wakabidhiwe baadae....
 
Whether Mbowe anatetea kiti cha uenyekiti au anashindwa, tayari ameingia kwenye kapu moja na akina Lipumba, Momose Cheyo, Dovutwa, Mzee wa Ubwaba na marehemu Augustino Mrema

Wote hawa wana kitu kimoja in common: ULAFI wa pesa.
Sasa pata picha kama Mbowe ndo angekuwa Rais wa Tanzania…..

Angefia madarakani.
 
Kilichonifurahisha kwenye mazungumzo ya Lissu na watanzania jana ni kuwa anaonekana ana vision kubwa ya reforms anazotaka zifanyike ndani ya CHADEMA na kwa Taifa kiujumla. Sijasikia Mbowe yeye anataka CHADEMA ya aina gani baada ya kuwa ameshaonoza chama kwa miaka takriban 20
Mbowe kwa sasa hana jipya.
 
Mkuu Nyani Ngabu chaguzi zote ndani ya CDM Mwenyekiti Mbowe hakuwahi kupingwa kama uchaguzi wa sasa, this time mambo mengi yameibua hisia ya Wanachama yakiwemo
1. Upotevu na utekaji wa vijana wetu wakiwa katika majukumu ya Chama.
2. Ubakaji wa Demokrasia katika uchaguzi.
3. Kuna jambo la kulamba asali.

Mambo haya yameibua Wanachadema kutaka mabadiliko ya Uongozi wao wa juu.
Kwa kifupi Mbowe yupo karibu na CCM zaidi sasa kuliko hapo awali,

Ndio maana anayatetea maridhiano feki, tujiulize kuna maridhiano gani huku wanachama wanauwawa, wengine wanapotezwa, uchaguzi wa Serikali za mitaa umeporwa kinguvu, halafu jitu Zima linashadadia maridhiano,

Kuna watu wamepoteza wapendwa wao, Wana maumivu makali sana halafu Mbowe anawafanyia usanii na Hila,

Hivi familia ya Mzee Kibao na wengine wakijatambua kuwa CDM siyo chama Cha siasa bali ni genge la wafanyabiashara na deal za siasa watajisikiaje?
 
Lissu na Mbowe na wengineo kama wapo, fanyeni mdahalo muwaeleze wanachama wenu kuhusu sera na itikadi zenu, malengo yenu, na wapi mnakotaka kukipeleka chama katika miaka 5/10 ijayo.
Mbowe hawezi kukubali

Odemba tu alijaribu kumualika kwenye mdahalo wa peke yake baada ya zile kashfa za Msigwa lakini Mbowe hakuwa tayari.

Kwenye huu mdahalo Mbowe hawezi kabisa kuruhusu hilo lifanyike.
 
Kwenye kupambana na CCM, CDM haaitaji Mbowe wala Lissu kutoboa.

CDM inahitaji tume huru ambayo katiba mpya ilikuwa na maoni haya yote.

Lissu kama makamu mwenyekiti alikuwa nafasi ya juu kiuongozi kuweza kufanya chochote katika chama kiasi kuwa siamini akiwa mwenyekiti kamili anaweza kubadili jambo lolote ndani ya chama.
 
Kwa nini asijiuzulu tu awaachie na wenzie nao wakiongoze hicho chama?
Ni mara chache mimi na wewe tunakubaliana and here is my two cents from the neighbouhood!

Na mimi natoa tahadhari kwa mwenyekiti wa Chadema FAM kwamba wapambe maslahi ni wa kuogopwa kama ukimwi.

Baba wa taifa alitaka kuachia uongozi mapema sana lakini wapambe maslahi hawakuwa tayari, walimlilia wakitaka aendelee kwa kudai hakuwepo mtu wa kuvaa viatu vyake.

Mwaka 1975 wapambe maslahi walimsihi aendelee wakidai haukuwa wakati muafaka wa kuachia madaraka kati kati ya chochoko za Idi Amin Dada wa Uganda zikiwa zimepamba moto.

Mwaka 1980, wapambe hao hao nuksi walimuomba aendelee tena wakidai ndiyo tumetoka vitani (vita vya Kagera) na hivyo uongozi wake bado ulihitajika kuliko wakati wowote ule!

Mwalimu alikubali lakini kwa sharti moja ingekuwa awamu yake ya mwisho na kweli mwaka 1985 aling'atuka baada ya kutembea nchi nzima akimnadi mrithi wake Hasan Mwinyi wa Zanzibar.

Sasa shuhudia lawama alizopewa Mwalimu baada ya kung'atuka madarakani alipopinga Mwinyi huyo huyo kuongezewa miaka mingine mitano baada ya kumaliza muda wake mwaka 1995!

Wapambe maslahi wa Mwinyi walimtaka Mwalimu akae kimya wakidai inakuwaje apinge wakati yeye mwenyewe aling'ang'ania madaraka kwa miaka zaidi ya ishirini bila kumpisha mtu!

Chama kile kile, wapambe wale wale...na sasa tunawashuhudia wapambe wa mwenyekiti wa chama mbadala Chadema wakiwa kazini wakifuata nyayo za wapambe wa CCM, hakuna cha ajabu!

Birds of a feather fly together...ndege wafananao huruka pamoja! Ni Lissu tu ndio mpaka sasa ameaonesha nia na ari ya kulikwamua taifa letu kutoka mikononi mwa walafi, wanafiki na wafuata nyayo!
 
inaelekea kabla ya mapinduzi waliahidiana mengi na makubwa, sasa wameshindwa kutimiziana na hapo ndipo tifu lilipo, tundu lisu ana ugomvi mkubwa personal na the power that be, kwa upande wa power that be walishamalizana na tundu lisu na hana deni naye, hela ndefu alishapewa, alishatembelewa mpaka ughaibuni tena rasmi kabisa hivyo walishamalizana lkn tundu lisu anadai bado ukiangalia alitangulizwa mbele, binafsi naamini kabisa tundu lisu ni team makamba, nape, rostamu & co. muda utaongea huko mbele …
 
Kwa kifupi Mbowe yupo karibu na CCM zaidi sasa kuliko hapo awali,

Ndio maana anayatetea maridhiano feki, tujiulize kuna maridhiano gani huku wanachama wanauwawa, wengine wanapotezwa, uchaguzi wa Serikali za mitaa umeporwa kinguvu, halafu jitu Zima linashadadia maridhiano,

Kuna watu wamepoteza wapendwa wao, Wana maumivu makali sana halafu Mbowe anawafanyia usanii na Hila,

Hivi familia ya Mzee Kibao na wengine wakijatambua kuwa CDM siyo chama Cha siasa bali ni genge la wafanyabiashara na deal za siasa watajisikiaje?
CHADEMA wakimchagua watakuwa wapumbavu kama wale wafuasi wa Kibwetele na Mkenya. Mbowe anawachukulia wanaCHADEMA kama wehu. Kama ulivyo sema, ni maridhiano gani Mbowe anayalinda wakati bado wagombea wa vijiji na mitaa bado hawajasahau kuonewa mchana kweupe! Nafikiri kuna mambo mawili, eidha Mbowe amepatwa na Kichaa au amelipwa " mafao" na serikali.
 
U
Mbeba maboksi here I come with my two cents from a distance.

Nianze kwa kuwatakia heri ya Krismasi kwenu waumini wa Kristo.

Kwa wasio waumini, nanyi nawatakieni sikukuu njema na mapumziko mema.

Nimekuwa nikiifuatilia hii mijadala ya uchaguzi wa ndani wa CHADEMA kwa juu juu tu.

Sikuwa kabisa na raghba yoyote ile ya kunifanya niufuatilie kwa kina huo mchakato, hapo awali.

Jana ndo nikapata muda wa kusikiliza kidogo mjadala uliofanyika Clubhouse ambao Tundu Lissu alishiriki.

Nilifurahi zaidi nilipomsikia Bw. Lissu akikubaliana na mtazamo wangu kuhusu yale mazungumzo yao na CCM kuhusu maridhiano.

Kabla ya jana sikuwahi kumsikia Lissu akimkosoa Freeman Mbowe hadharani na kwa uwazi kiasi hicho.

Pamoja na kunifumbua masikio, huo mjadala ulizichochea fikra zangu na kupelekea kuwa na maswali mengi zaidi.

Inavyoelekea huko CHADEMA kuna mpasuko ambao ulikuwa unachemka kwa muda mrefu.

Sidhani kama kwenye miaka ya nyuma tokea Mbowe awe mwenyekiti, aliwahi kupewa changamoto kwenye hizo Chaguzi zao za ndani ya chama. Kama imewahi kutokea, mnaojua mtatujuza na kutukumbusha.

Sasa safari hii sijui ni kitu gani kilichomfanya Lissu naye kugombea hiyo nafasi ya uenyekiti wa chama.

Sijui huo uchaguzi wao utafanyika lini.

Na ukishafanyika na mshindi kujulikana, napata shida kuamini kuwa hali ndani ya chama itakuwa salama.

CHADEMA inaweza kutoka kwenye huo ikiwa ni dhoofu sana.

Atayeshindwa atakubali kuwa kashindwa kihalali na baada ya hapo atabaki kuendelea kukijenga chama?

Wakati mwingine napatwa na fikra za huenda Tundu Lissu katumia mwanya huo wa kumpa changamoto Mbowe ili aje kupata kisingizio cha kujitoa kwenye chama hapo mbeleni…

Kwa sasa tumewasikia hao wawili wakiwa hawako pamoja.

Ningependa sana kuona wanafanya mdahalo ili wapiga kura wao wapate fursa ya kuwaona wawili hao wakijinadi mbele zao.

Ila Mbowe naye…..dah. CHADEMA imesha plateau chini ya uongozi wake.

Kwa nini asijiuzulu tu awaachie na wenzie nao wakiongoze hicho chama?
chaguzi ni 23/01/2025
 
Back
Top Bottom