Fikra duni za mbeba maboksi kuhusu mustakabali wa CHADEMA baada ya uchaguzi wao.

Fikra duni za mbeba maboksi kuhusu mustakabali wa CHADEMA baada ya uchaguzi wao.

Mbeba maboksi here I come with my two cents from a distance.

Nianze kwa kuwatakia heri ya Krismasi kwenu waumini wa Kristo.

Kwa wasio waumini, nanyi nawatakieni sikukuu njema na mapumziko mema.

Nimekuwa nikiifuatilia hii mijadala ya uchaguzi wa ndani wa CHADEMA kwa juu juu tu.

Sikuwa kabisa na raghba yoyote ile ya kunifanya niufuatilie kwa kina huo mchakato, hapo awali.

Jana ndo nikapata muda wa kusikiliza kidogo mjadala uliofanyika Clubhouse ambao Tundu Lissu alishiriki.

Nilifurahi zaidi nilipomsikia Bw. Lissu akikubaliana na mtazamo wangu kuhusu yale mazungumzo yao na CCM kuhusu maridhiano.

Kabla ya jana sikuwahi kumsikia Lissu akimkosoa Freeman Mbowe hadharani na kwa uwazi kiasi hicho.

Pamoja na kunifumbua masikio, huo mjadala ulizichochea fikra zangu na kupelekea kuwa na maswali mengi zaidi.

Inavyoelekea huko CHADEMA kuna mpasuko ambao ulikuwa unachemka kwa muda mrefu.

Sidhani kama kwenye miaka ya nyuma tokea Mbowe awe mwenyekiti, aliwahi kupewa changamoto kwenye hizo Chaguzi zao za ndani ya chama. Kama imewahi kutokea, mnaojua mtatujuza na kutukumbusha.

Sasa safari hii sijui ni kitu gani kilichomfanya Lissu naye kugombea hiyo nafasi ya uenyekiti wa chama.

Sijui huo uchaguzi wao utafanyika lini.

Na ukishafanyika na mshindi kujulikana, napata shida kuamini kuwa hali ndani ya chama itakuwa salama.

CHADEMA inaweza kutoka kwenye huo ikiwa ni dhoofu sana.

Atayeshindwa atakubali kuwa kashindwa kihalali na baada ya hapo atabaki kuendelea kukijenga chama?

Wakati mwingine napatwa na fikra za huenda Tundu Lissu katumia mwanya huo wa kumpa changamoto Mbowe ili aje kupata kisingizio cha kujitoa kwenye chama hapo mbeleni…

Kwa sasa tumewasikia hao wawili wakiwa hawako pamoja.

Ningependa sana kuona wanafanya mdahalo ili wapiga kura wao wapate fursa ya kuwaona wawili hao wakijinadi mbele zao.

Ila Mbowe naye…..dah. CHADEMA imesha plateau chini ya uongozi wake.

Kwa nini asijiuzulu tu awaachie na wenzie nao wakiongoze hicho chama?kum
Kujiuzulu siku zote ni hiyari ya mtu sio haki ya mmoja kuidai dhidi ya mwingine unless huyo .mtu hayuko timamu kichwani.

Demokrasia inataka kura ziamue.

Lossu anajua atashindwa na ataondoka CHADEMA kwa hiyari au kufukuzwa maana makosa yake hayavumiliki.

Lissu ameamua aibomoe CHADEMA ili baada ya uchaguzi ife kwa sababu anajua wazi yeye hatakuwepo hivyo anaona kwa nini akiache chama kikiwa imara kwa Mbowe wakati naye alishiriki kukijenga bora wakose wote.

Fikiria Lissu anasema hadharani namna majadiliano ya hoja ndani ya vikao mjumbe gani alisimamia hoja pi. Tangu lini mjumbe ndani ya kikao kuunga mkono hoja tofauti na mwenzake ionekane kosa na huku nje watu wanahukumu: hapa nazungumzia Lissu kudai yeye, Msugwa, Lema; Heahe ndio walipinga maridhiano na wengine waliobakia waliounga mkono maridhiano ni wasaliti na watu huko space wanakubaliana naye! Hii inaonyesha watu wengi hawana akili ya kureason, mitazamo tofauti ya hoja ndani ya vikao halali iwe kosa la usaliti.

Hoja ya kupinga maridhiano ilishindwa kwa hoja na hiyo ndiyo nguvu ya vikao hata mwalimu Nyerere aliwahi kuwa mawazo hayapigwi rungs bali yanashindwa kwa hoja.. ina maana Lissu akishinda uenyekiti atawaburuza wajumbe waafiki mawazo yake katika kila jambo?

Hao wanaomshangilia huko space/ club house je ndivyo vkaao ndani ya vyama vinapoaswa viendeshwe yaani huku nje watu waambiwe nani alisema nini katika kikao eti kwa sababu inatakiwa uwazi?

Kwa makosa haya ya Lissu ikiwa CHADEMA watamuacha baada ya uchaguzi nitawahangaa sana ingawa ninajua Lissu ndio bye bye tena.
 
Kama Mbowe atashinda tena, come 2029 anaweza kugombea tena bila chembe ya aibu kwa kisingizio cha "kuombwa na kubembelezwa na viongozi wa dini au wazee wa chama"

Madaraka yanalevya na madaraka makubwa ya muda mrefu yanalevya zaidi, especially pale ambapo hakuna means za kuwadhibiti walafi na waroho wa madaraka
Baada ya kuona lile igizo la wanachama kuvamia nyumbani kwake wakakuta wameandaliwa viti mahema maji na soda nilijua lazima atagombea tu,

Waliopatwa na majanga wakipigani hiki chama wako kwenye maumivu makali sana, Mungu awatie nguvu,

nimeamini hakuna asiyenunulika, ni suala la kufika dau anataka tu,
 
Kwa kifupi Mbowe yupo karibu na CCM zaidi sasa kuliko hapo awali,

Ndio maana anayatetea maridhiano feki, tujiulize kuna maridhiano gani huku wanachama wanauwawa, wengine wanapotezwa, uchaguzi wa Serikali za mitaa umeporwa kinguvu, halafu jitu Zima linashadadia maridhiano,

Kuna watu wamepoteza wapendwa wao, Wana maumivu makali sana halafu Mbowe anawafanyia usanii na Hila,

Hivi familia ya Mzee Kibao na wengine wakijatambua kuwa CDM siyo chama Cha siasa bali ni genge la wafanyabiashara na deal za siasa watajisikiaje?
Kwani wewe hujui kuwa maridhiano yalikwama?

Katika maridhiano yeyote kuna compromise huwezi pata yote.

Mnaompenda Lissu jaribuni kuwa mnafikiri kidogo kila anachosema kabla ya kuamini kama dini.

Ingekuwa sio maridhiano Lissu angefutiwa zile kesi zake? Angelipwa stahiki zake za ubunge? Angepewa paspoti? ,angekuwa anarudi nchini kufanya siasa.

Mtu kama Lema nwenye record ya wizi wa magari kukopa madeni makubwa ambayo hajayalipa yaani kuna watu kabisa wanaamini anatetea maslahi yao..

Mtikila aliwahi kusema zamani tulipata shida kuelimisha wasiosoma lakini siku hizi tunapata shida kuelimisha waliosoma.
 
Katika watu ambao karma imeanza kuwadhibu mapema sana basi ni walibya. Wakifuatiwa na wa Iraq. Jamaa ni wapumbavu sana ndomaana dunia haina tena huruma na wao.

Mtoto akililia wembe mpe tu umkate ili ujinga umtoke.
Kabisa!
 
Lissu na Mbowe na wengineo kama wapo, fanyeni mdahalo muwaeleze wanachama wenu kuhusu sera na itikadi zenu, malengo yenu, na wapi mnakotaka kukipeleka chama katika miaka 5/10 ijayo.
Sidhani kama Mbowe na timu yake wanaweza kukubali.
 
Mbowe na wenzake hawakutegemea challenge yoyote ndio maana pamoja na uchaguzi kuwa January 2025 hukusikia Mbowe au wapambe wake wakiuzungumzia.

Ila baada ya Lissu kutangaza anaitaka nafasi ya Mwenyekiti joto likapanda, wapambe wa Mbowe wakaenda kumshawishi atangaze nia mapema, then mambo tusiyoyajua mengi yanaendelea kufunguka.

Bila Lissu Mwenyekiti angepita kimyakimya kama siku zote.
 
Sidhani kama Mbowe na timu yake wanaweza kukubali.
Itabdi wakubali, wakikataa ni point tatu za muhimu kwa timu Lissu, itawaziba mdomo kutaka mijadala ya wazi na vyama vingine kama CCM nk.
 
Mbowe ninasset ya serikali na chama tawala kina nufaika na uwepo wake chadema, how and why? Yeye ndie anae keep chadema from going aggressive kwenye siasa , yeye ndie anaelimit, na katika kulimit huko chama tawala ndio kimefaidika kuliko chadema

Look at them the kwa siasa za mbowe? Wamefaidika nini?

Lissu anakuja na sera nyoofu, hi is opposite of mbowe. And chama tawala na state dont want that
Wako willing ku offer pesa yoyote mbowe akae pale

Lakini pia probably that is lissu exit strategy, probably anajua he wont make it, but atleast atapate kisingizio
Sahihi kabisa, Mbowe amekuwa akitumika kuzima hari ya mabadiliko kwa Chadema, wakati wa kesi yake ya ugaidi, joto la siasa lilikuwa juu sana, ilitegemewa kama angetoka moto ungekuwa mkubwa ila ikawa kinyume chake, mojakwamoja Ikulu na the rest is history.
 
Itabdi wakubali, wakikataa ni point tatu za muhimu kwa timu Lissu, itawaziba mdomo kutaka mijadala ya wazi na vyama vingine kama CCM nk.
Kuupangua ukweli ni ngumu sana ndugu yangu, hususani ukutane na mtu aina ya Lissu.

Lissu anajua kuongea, Lissu ana fikiri, Lissu ana uwezo wa kujenga hoja! Mbaya kabisa ni mbobezi kwenye fani ya sheria, na mbaya zaidi ana vithibitisho vyote vya madai anatoyatoa dhidi ya Chadema chini ya uongozi wa Mbowe.

Kwa mtu aina ya Lissu akiwa Mbowe akienda naye kwenye mdahalo ata aibika vibaya sana. Ndiyo mwisho wa Mbowe.

Mbowe na watu wake wanalijua hili! Bora apate aibu ya kukimbia mdahalo kuliko kupata aibu ya kujimaliza kabisa wazi wazi kwenye ulimwengu wa sisa. Na ndicho Mbowe na kamati yake watakachofanya.
 
Kwani wewe hujui kuwa maridhiano yalikwama?

Katika maridhiano yeyote kuna compromise huwezi pata yote.

Mnaompenda Lissu jaribuni kuwa mnafikiri kidogo kila anachosema kabla ya kuamini kama dini.

Ingekuwa sio maridhiano Lissu angefutiwa zile kesi zake? Angelipwa stahiki zake za ubunge? Angepewa paspoti? ,angekuwa anarudi nchini kufanya siasa.

Mtu kama Lema nwenye record ya wizi wa magari kukopa madeni makubwa ambayo hajayalipa yaani kuna watu kabisa wanaamini anatetea maslahi yao..

Mtikila aliwahi kusema zamani tulipata shida kuelimisha wasiosoma lakini soku hizi tunapata shida kuelimisha waliosoma.
 
Ni mara chache mimi na wewe tunakubaliana and here is my two cents from the neighbouhood!

Na mimi natoa tahadhari kwa mwenyekiti wa Chadema FAM kwamba wapambe maslahi ni wa kuogopwa kama ukimwi.

Baba wa taifa alitaka kuachia uongozi mapema sana lakini wapambe maslahi hawakuwa tayari, walimlilia wakitaka aendelee kwa kudai hakuwepo mtu wa kuvaa viatu vyake.

Mwaka 1975 wapambe maslahi walimsihi aendelee wakidai haukuwa wakati muafaka wa kuachia madaraka kati kati ya chochoko za Idi Amin Dada wa Uganda zikiwa zimepamba moto.

Mwaka 1980, wapambe hao hao nuksi walimuomba aendelee tena wakidai ndiyo tumetoka vitani (vita vya Kagera) na hivyo uongozi wake bado ulihitajika kuliko wakati wowote ule!

Mwalimu alikubali lakini kwa sharti moja ingekuwa awamu yake ya mwisho na kweli mwaka 1985 aling'atuka baada ya kutembea nchi nzima akimnadi mrithi wake Hasan Mwinyi wa Zanzibar.

Sasa shuhudia lawama alizopewa Mwalimu baada ya kung'atuka madarakani alipopinga Mwinyi huyo huyo kuongezewa miaka mingine mitano baada ya kumaliza muda wake mwaka 1995!

Wapambe maslahi wa Mwinyi walimtaka Mwalimu akae kimya wakidai inakuwaje apinge wakati yeye mwenyewe aling'ang'ania madaraka kwa miaka zaidi ya ishirini bila kumpisha mtu!

Chama kile kile, wapambe wale wale...na sasa tunawashuhudia wapambe wa mwenyekiti wa chama mbadala Chadema wakiwa kazini wakifuata nyayo za wapambe wa CCM, hakuna cha ajabu!

Birds of a feather fly together...ndege wafananao huruka pamoja! Ni Lissu tu ndio mpaka sasa ameaonesha nia na ari ya kulikwamua taifa letu kutoka mikononi mwa walafi, wanafiki na wafuata nyayo!
IMG_7184.jpeg
 
Kujiuzulu siku zote ni hiyari ya mtu sio haki ya mmoja kuidai dhidi ya mwingine unless huyo .mtu hayuko timamu kichwani.

Demokrasia inataka kura ziamue.

Lossu anajua atashindwa na ataondoka CHADEMA kwa hiyari au kufukuzwa maana makosa yake hayavumiliki.

Lissu ameamua aibomoe CHADEMA ili baada ya uchaguzi ife kwa sababu anajua wazi yeye hatakuwepo hivyo anaona kwa nini akiache chama kikiwa imara kwa Mbowe wakati naye alishiriki kukijenga bora wakose wote.

Fikiria Lissu anasema hadharani namna majadiliano ya hoja ndani ya vikao mjumbe gani alisimamia hoja pi. Tangu lini mjumbe ndani ya kikao kuunga mkono hoja tofauti na mwenzake ionekane kosa na huku nje watu wanahukumu: hapa nazungumzia Lissu kudai yeye, Msugwa, Lema; Heahe ndio walipinga maridhiano na wengine waliobakia waliounga mkono maridhiano ni wasaliti na watu huko space wanakubaliana naye! Hii inaonyesha watu wengi hawana akili ya kureason, mitazamo tofauti ya hoja ndani ya vikao halali iwe kosa la usaliti.

Hoja ya kupinga maridhiano ilishindwa kwa hoja na hiyo ndiyo nguvu ya vikao hata mwalimu Nyerere aliwahi kuwa mawazo hayapigwi rungs bali yanashindwa kwa hoja.. ina maana Lissu akishinda uenyekiti atawaburuza wajumbe waafiki mawazo yake katika kila jambo?

Hao wanaomshangilia huko space/ club house je ndivyo vkaao ndani ya vyama vinapoaswa viendeshwe yaani huju nje watu waambiwe nani alisema nini katika kikao eti kwa sababu inatakiwa uwazi?

Kwa makosa haya ya Lissu ikiwa CHADEMA watamuacha baada ya uchaguzi nitawahangaa sana ingawa ninajua Lissu ndio bye bye tena.
Umesema ukweli kabisa.

Wengi ya wafuasi wa Lisu wanaaamini kila asemacho, yani kwao Lisu ni zaidi ya msaafu. Ukikutana nao wanaanza Lisu kasema... Lisu kasema..., halafu ukiwauliza alichokisema unaushahidi nacho? au umeamini vipi kwamba ni kweli? Ohoo Lisu anajenga hoja, unaushahidi wa alichokiongea hakuna, Huyo Lisu alikuonyesheni ushahidi wa alichokiongea, Hapana...kwasababu Lisu kasema, unajua Lisu ni mwanasheria..??

Lisu akisikiliza stori za vijiweni anaita press, anasema nimeambiwa na mtu mzito na wafuasi watakubali.
Juzi hapa alikuja press akaisema Tigo, Makonda na kila anaye muhisi, kwa sababu alisoma habari kwenye gazeti la Mbinguni huko linaitwa "The Gardian" hata ushahidi hana akaita press. Mpaka sasa kimyaaa.

Kachukua Fomu kaita press, karudisha fomu, kajikinga na Bullet Proof na Press.

Lisu alisema kwenye moja ya Press zake " Mkutano wake na Abdul na hao waliokuwepo ulikuwa recorded, tupe nasi tujionee na tusikilize tupate ukweli. wafuasi wake wanasema Wenje ni Muongo, kwa vipi? Lisu Kasema??!

Kuna haja gani yeye kuongea saaana ya wenzake, na mengine yalikuwa ni maamuzi ya vikao na yeye alikuwemo?
Ninamuona kama Msigwa, alianza na Press akasema Mbowe hanitishi na maneno meengi, baada ya hapo Tena Press ya kuahama Chadema na kutangaza vita na Mbowe, mpaka sasa.

Hata Lisu akishinda Chadema haitakuwa ile kama wafuasi wake wnavyotaka tuamini. Kesha fanya damage ya kutosha, watamuachia chama akijenge, na mwakani baada ya uchaguzi wafuasi wake utawaona humu wakisema Mbowe kamuhujumu, kwasababu Mbowe ni agent wa CCM.

Lisu alipiga kelele kabla hajashinda TLS, aliposhinda tulitegemea mengi, lakini bahati mbaya alipata matatizo labda angefanya makubwa sijui.

Leo hii anataka kuwa mwenyekiti kwa mapinduzi, wafuasi wake ndio kabisaaa hawataki uchaguzi, wanataka Mbowe ajitoe, Lisu apite bila kupingwa, wao kila siku hawataki wagombea wa chadema waenguliwe na ccm, lakini wao wanataka Mbowe ajiondoe, eti ni dhaifu, hana jipya. sasa kwanini msifurahie Lisu kushinda na mgombea dhaifu asiye na jipya ili amshinde vizuri?

Halafu wanasema Lisu hana tamaa ya madaraka, Mbowe anatamaa sana ya madaraka, Lisu yeye anachokitafuta sijui ni nini kama siyo madaraka?

Mimi nataka sana Mtakatifu Lisu ashinde ili waone hiyo chadema ya Lisu, na amshinde SSH mwakani tutangaze uhuru wa Tanganyika.
 
Lissu na Mbowe na wengineo kama wapo, fanyeni mdahalo muwaeleze wanachama wenu kuhusu sera na itikadi zenu, malengo yenu, na wapi mnakotaka kukipeleka chama katika miaka 5/10 ijayo.
Sidhani kama Mbowe atakubali kitu inaitwa mdahalo dhidi ya lissu.
Mtu kakaa madarakani miaka 21 atakuwa na jipya gani kwsnye huo mdahalo.
 
Kwani wewe hujui kuwa maridhiano yalikwama?

Katika maridhiano yeyote kuna compromise huwezi pata yote.

Mnaompenda Lissu jaribuni kuwa mnafikiri kidogo kila anachosema kabla ya kuamini kama dini.

Ingekuwa sio maridhiano Lissu angefutiwa zile kesi zake? Angelipwa stahiki zake za ubunge? Angepewa paspoti? ,angekuwa anarudi nchini kufanya siasa.

Mtu kama Lema nwenye record ya wizi wa magari kukopa madeni makubwa ambayo hajayalipa yaani kuna watu kabisa wanaamini anatetea maslahi yao..

Mtikila aliwahi kusema zamani tulipata shida kuelimisha wasiosoma lakini soku hizi tunapata shida kuelimisha waliosoma.
Mkuu, kwa mtazamo wangu, mambo uliyoyaorodhesha kama manufaa ya maridhiano kiuhalisia sio manufaa ya maridhiano. Hizo gestures zilikuwa hatua za awali za kuandaa meza ya mazungumzo.

Mtu akikupora gari lako, huna ulazima wa kumshukuru na kumpongeza kwa uamuzi wake wa kukurudishia gari lako. Hatua yake ya kukurudishia hilo gari ilikuwa inatengeneza tu mazingira mazuri ya ninyi wawili kukaa kwenye meza ya usuluhishi! Mkishindwa kwenda beyond this maana yake hakuna reconciliation iliyofanyika.
 
Mbowe akijitoa, na akakubali kumuunga mkono Lissu na wakaweka tofauti zao Pembeni Chadema itakuwa ya moto kuliko siku zote,

Mbowe akikomaa na akashinda basi Chadema itadhoofika kuliko siku zote za uwepo wake na mama atapata 90+ % uchaguzi ujao.

Natamani kusikia na maoni ya
Mzee Mwanakijiji
Ngumu mbowe kuachia

Zikipita kaguzi za fedha pale Aibu yake itakua kubwa sana
 
Back
Top Bottom