Fikra duni za mbeba maboksi kuhusu mustakabali wa CHADEMA baada ya uchaguzi wao.

Fikra duni za mbeba maboksi kuhusu mustakabali wa CHADEMA baada ya uchaguzi wao.

Mbeba maboksi here I come with my two cents from a distance.

Nianze kwa kuwatakia heri ya Krismasi kwenu waumini wa Kristo.

Kwa wasio waumini, nanyi nawatakieni sikukuu njema na mapumziko mema.

Nimekuwa nikiifuatilia hii mijadala ya uchaguzi wa ndani wa CHADEMA kwa juu juu tu.

Sikuwa kabisa na raghba yoyote ile ya kunifanya niufuatilie kwa kina huo mchakato, hapo awali.

Jana ndo nikapata muda wa kusikiliza kidogo mjadala uliofanyika Clubhouse ambao Tundu Lissu alishiriki.

Nilifurahi zaidi nilipomsikia Bw. Lissu akikubaliana na mtazamo wangu kuhusu yale mazungumzo yao na CCM kuhusu maridhiano.

Kabla ya jana sikuwahi kumsikia Lissu akimkosoa Freeman Mbowe hadharani na kwa uwazi kiasi hicho.

Pamoja na kunifumbua masikio, huo mjadala ulizichochea fikra zangu na kupelekea kuwa na maswali mengi zaidi.

Inavyoelekea huko CHADEMA kuna mpasuko ambao ulikuwa unachemka kwa muda mrefu.

Sidhani kama kwenye miaka ya nyuma tokea Mbowe awe mwenyekiti, aliwahi kupewa changamoto kwenye hizo Chaguzi zao za ndani ya chama. Kama imewahi kutokea, mnaojua mtatujuza na kutukumbusha.

Sasa safari hii sijui ni kitu gani kilichomfanya Lissu naye kugombea hiyo nafasi ya uenyekiti wa chama.

Sijui huo uchaguzi wao utafanyika lini.

Na ukishafanyika na mshindi kujulikana, napata shida kuamini kuwa hali ndani ya chama itakuwa salama.

CHADEMA inaweza kutoka kwenye huo ikiwa ni dhoofu sana.

Atayeshindwa atakubali kuwa kashindwa kihalali na baada ya hapo atabaki kuendelea kukijenga chama?

Wakati mwingine napatwa na fikra za huenda Tundu Lissu katumia mwanya huo wa kumpa changamoto Mbowe ili aje kupata kisingizio cha kujitoa kwenye chama hapo mbeleni…

Kwa sasa tumewasikia hao wawili wakiwa hawako pamoja.

Ningependa sana kuona wanafanya mdahalo ili wapiga kura wao wapate fursa ya kuwaona wawili hao wakijinadi mbele zao.

Ila Mbowe naye…..dah. CHADEMA imesha plateau chini ya uongozi wake.

Kwa nini asijiuzulu tu awaachie na wenzie nao wakiongoze hicho chama?
Mbowe ninasset ya serikali na chama tawala kina nufaika na uwepo wake chadema, how and why? Yeye ndie anae keep chadema from going aggressive kwenye siasa , yeye ndie anaelimit, na katika kulimit huko chama tawala ndio kimefaidika kuliko chadema

Look at them the kwa siasa za mbowe? Wamefaidika nini?

Lissu anakuja na sera nyoofu, hi is opposite of mbowe. And chama tawala na state dont want that
Wako willing ku offer pesa yoyote mbowe akae pale

Lakini pia probably that is lissu exit strategy, probably anajua he wont make it, but atleast atapate kisingizio
 
Lissu na Mbowe na wengineo kama wapo, fanyeni mdahalo muwaeleze wanachama wenu kuhusu sera na itikadi zenu, malengo yenu, na wapi mnakotaka kukipeleka chama katika miaka 5/10 ijayo.
Mbowe hana mental capacity ya kufanya mdahalo unataka yamkute ya Joe Biden ?🐼

1000017725.jpg
 
Whether Mbowe anatetea kiti cha uenyekiti au anashindwa, tayari 👉"ameingia" kwenye kapu moja na akina Lipumba, Momose Cheyo, Dovutwa, Mzee wa Ubwaba na marehemu Augustino Mrema

Wote hawa wana kitu kimoja in common: ULAFI wa pesa.
Ameingia au alikuwepo kitambo sema nyinyi waona karibu hamkujua.

Wajanja tulijua kitambo kama jamaa ni aina ya kina Lipumba, ila tulipotaka kuwajulisha na nyinyi ili mshtuke mapema mliishia kutukejeli na kutuona wababaishaji. Bora sasa hivi mmejionea wenyewe baada ya kuonesha wazi kile mlichokuwa hamkijui kuhusu mwenyekiti wenu.

Mwanasiasa wa kweli na mwenye moyo wa kizalendo kama mchungaji Mtikila amekufa hana chawa, wala mtu wa kumsikiliza hoja zake za kupigania Tanganyika, haki nk.

Lakini muhuni fulan na mfanya biashara wa siasa ndo akawa anaonekana mkombozi hadi kupelekea kumiliki mamilioni ya chawa wakiwemo wasomi mbali mbali.
 
Kwa nini asijiuzulu tu awaachie na wenzie nao wakiongoze hicho chama?
Wazo Kuntu Sana hili ndugu yangu Nyani Ngabu, sijui, labda atalifanyia kazi hili wazo lako. Iko hivi, Kampuni inapoyumba, solution huwa ni kutoa kiongozi wake, iko vivyo hivyo kwenye timu za mipira duniani kote, hata kwenye vyama vya siasa pia humu duniani.

Ni Tanzania pekee ambapo viongozi hawana tabia ya kuachia mawazo mapya wanaposhindwa kuwapa wananchi wao kitu walicho waahidi.

Mpaka sasa sijaona mawazo yeyote tofauti kutoka kwa Mbowe ni jinsi gani ataileta katiba mpya au tume huru.. yeye kaongelea tu kwamba anataka kuwepo hapo hadi afikie miaka 68- yaani miaka 2 kabla ya ule uliotajwa kwenye biblia. Tufike mahali tuwalazimishe kikatiba hawa viongozi waachie ngazi mara baada ya miaka 10 ili waendane na katiba ya nchi. Hawawezi kujitunguia tunguia tu mambo kinyume na katiba hata kama hiki ni chama chao. Mambo yote yanatakiwa kuakisi kitu kilichomo kwenye katiba- ndio maoni yangu hayo.

Hii ingeondia kabisa hili tatizo la Mbowe na akina Cheyo na Lipumba kungangania kuendelea kuwa viongozi, na sijui ni kwa nini watu wanapenda sana kuongoza wengine au labda hawataki kuongozwa- ni control freaks?
 
Walibya walisema hivyo dhidi ya Gaddaf, Libya ipo wapi sasa!!!
Si mtetei kwa sababu hoja aliyotoa ya umri kuhalalisha kupewa tena uwenyekiti sikubaliani nayo.
Yani Mbowe unamfananisha na Gaddafi ambae asilimia kubwa ya raia wake walineemeka chini ya utawala wake japo nchi ilikuwa ndani ya vikwazo vya muda mrefu.

Legacy ya Mbowe ni ipi kwa nchi yake, chama chake au jimbo lake?

Ebu msome muona mbali mwl Nyerere mara moja, utajifunza kitu.
 

Attachments

  • Screenshot_20241216-104004.jpg
    Screenshot_20241216-104004.jpg
    445.8 KB · Views: 1
Sasa pata picha kama Mbowe ndo angekuwa Rais wa Tanzania…..Angefia madarakani.
Sahihi. Yaani ukimsikiliza jinsi anavyojaribu kujenga hoja ya ukomo wa uongozi, unapata shida sana kuelewa logic yake. Moral Authority ya kuwafokea CCM waachie ngazi inakosekana kabisa

Na hii sasa ndio modus operandi ya viongozi wote wa vyama vya upinzani.
 
Gaddafi ambae asilimia kubwa ya raia wake walineemeka chini ya na utawala wake japo nchi ilikuwa ndani ya vikwazo vya muda mrefu
Unanitonesha kidonda cha namna walivyokuwa wapuuzi kiasi cha kusaliti kiongozi wao!
===
Aikael ana changamoto na Lissu anachangamoto; wote hawafai kuongoza chadema!
 
Unanitonesha kidonda cha namna walivyokuwa wapuuzi kiasi cha kusaliti kiongozi wao!
===
Aikael ana changamoto na Lissu anachangamoto; wote hawafai kuongoza chadema!
Katika watu ambao karma imeanza kuwadhibu mapema sana basi ni walibya. Wakifuatiwa na wa Iraq. Jamaa ni wapumbavu sana ndomaana dunia haina tena huruma na wao.

Mtoto akililia wembe mpe tu umkate ili ujinga umtoke.
 
Mbowe akibaki madarakani CHADEMA kutawahakikishia CCM kuendelea kubaki madarakani kwa miaka mingine 50. Hii ni kwa sababu Mbowe anakwenda sasa kufanya controlled demolition ya CHADEMA ambayo ndiyo threat kuu kwa CCM.
 
CHADEMA wakimchagua watakuwa wapumbavu kama wale wafuasi wa Kibwetele na Mkenya. Mbowe anawachukulia wanaCHADEMA kama wehu. Kama ulivyo sema, ni maridhiano gani Mbowe anayalinda wakati bado wagombea wa vijiji na mitaa bado hawajasahau kuonewa mchana kweupe! Nafikiri kuna mambo mawili, eidha Mbowe amepatwa na Kichaa au amelipwa " mafao" na serikali.
Mbowe amekuwa mtu wa hovyo sana, pia CDM wajifunze kutokana na makosa ya kuchezea katiba Yao, hasa kubadilisha ukomo wa vipindi viwili tu,

Sasa matokeo yake Mbowe amekuwa kinganganizi, hataki kutoka madarakani pamoja na kwamba alishaahidi hatogombea Tena,

Chadema imekuwa mali binafsi ya familia ya Mbowe, Mungu apishie mbali tusipata Rais mwenye tabia za kilaghai kama huyu, hatokuwa na tofauti na Mugabe,
 
Lissu na Mbowe na wengineo kama wapo, fanyeni mdahalo muwaeleze wanachama wenu kuhusu sera na itikadi zenu, malengo yenu, na wapi mnakotaka kukipeleka chama katika miaka 5/10 ijayo.
Mbowe atakubali? Pengine. FYI huyu jamaa kaalikwa Clubhouse mara chungu nzima lakini anakwepa
 
Mkuu Nyani Ngabu chaguzi zote ndani ya CDM Mwenyekiti Mbowe hakuwahi kupingwa kama uchaguzi wa sasa, this time mambo mengi yameibua hisia ya Wanachama yakiwemo
1. Upotevu na utekaji wa vijana wetu wakiwa katika majukumu ya Chama.
2. Ubakaji wa Demokrasia katika uchaguzi.
3. Kuna jambo la kulamba asali.

Mambo haya yameibua Wanachadema kutaka mabadiliko ya Uongozi wao wa juu.
Ningependa kujua zaidi kuhusu namna Mbowe anavyohusika katika utekaji wa vijana wa CDM.

Amandla...
 
Either way, chadema itapoteana. Kitakachoiokoa Chadema ni Mbowe kushindwa na aendelee kumuunga mkono aliyeshinda. Tofauti na hapo chadema itakufa kama kina TLP na .wenzake NCCR.
 
inaelekea kabla ya mapinduzi waliahidiana mengi na makubwa, sasa wameshindwa kutimiziana na hapo ndipo tifu lilipo, tundu lisu ana ugomvi mkubwa personal na the power that be, kwa upande wa power that be walishamalizana na tundu lisu na hana deni naye, hela ndefu alishapewa, alishatembelewa mpaka ughaibuni tena rasmi kabisa hivyo walishamalizana lkn tundu lisu anadai bado ukiangalia alitangulizwa mbele, binafsi naamini kabisa tundu lisu ni team makamba, nape, rostamu & co. muda utaongea huko mbele …
Mapinduzi gani?
 
Sasa matokeo yake Mbowe amekuwa kinganganizi, hataki kutoka madarakani pamoja na kwamba alishaahidi hatogombea Tena,
Kama Mbowe atashinda tena, come 2029 anaweza kugombea tena bila chembe ya aibu kwa kisingizio cha "kuombwa na kubembelezwa na viongozi wa dini au wazee wa chama"

Madaraka yanalevya na madaraka makubwa ya muda mrefu yanalevya zaidi, especially pale ambapo hakuna means za kuwadhibiti walafi na waroho wa madaraka
 
Ni mara chache mimi na wewe tunakubaliana and here is my two cents from the neighbouhood!

Na mimi natoa tahadhari kwa mwenyekiti wa Chadema FAM kwamba wapambe maslahi ni wa kuogopwa kama ukimwi.

Baba wa taifa alitaka kuachia uongozi mapema sana lakini wapambe maslahi hawakuwa tayari, walimlilia wakitaka aendelee kwa kudai hakuwepo mtu wa kuvaa viatu vyake.

Mwaka 1975 wapambe maslahi walimsihi aendelee wakidai haukuwa wakati muafaka wa kuachia madaraka kati kati ya chochoko za Idi Amin Dada wa Uganda zikiwa zimepamba moto.

Mwaka 1980, wapambe hao hao nuksi walimuomba aendelee tena wakidai ndiyo tumetoka vitani (vita vya Kagera) na hivyo uongozi wake bado ulihitajika kuliko wakati wowote ule!

Mwalimu alikubali lakini kwa sharti moja ingekuwa awamu yake ya mwisho na kweli mwaka 1985 aling'atuka baada ya kutembea nchi nzima akimnadi mrithi wake Hasan Mwinyi wa Zanzibar.

Sasa shuhudia lawama alizopewa Mwalimu baada ya kung'atuka madarakani alipopinga Mwinyi huyo huyo kuongezewa miaka mingine mitano baada ya kumaliza muda wake mwaka 1995!

Wapambe maslahi wa Mwinyi walimtaka Mwalimu akae kimya wakidai inakuwaje apinge wakati yeye mwenyewe aling'ang'ania madaraka kwa miaka zaidi ya ishirini bila kumpisha mtu!

Chama kile kile, wapambe wale wale...na sasa tunawashuhudia wapambe wa mwenyekiti wa chama mbadala Chadema wakiwa kazini wakifuata nyayo za wapambe wa CCM, hakuna cha ajabu!

Birds of a feather fly together...ndege wafananao huruka pamoja! Ni Lissu tu ndio mpaka sasa ameaonesha nia na ari ya kulikwamua taifa letu kutoka mikononi mwa walafi, wanafiki na wafuata nyayo!
Mbeba maboksi here I come with my two cents from a distance.

Nianze kwa kuwatakia heri ya Krismasi kwenu waumini wa Kristo.

Kwa wasio waumini, nanyi nawatakieni sikukuu njema na mapumziko mema.

Nimekuwa nikiifuatilia hii mijadala ya uchaguzi wa ndani wa CHADEMA kwa juu juu tu.

Sikuwa kabisa na raghba yoyote ile ya kunifanya niufuatilie kwa kina huo mchakato, hapo awali.

Jana ndo nikapata muda wa kusikiliza kidogo mjadala uliofanyika Clubhouse ambao Tundu Lissu alishiriki.

Nilifurahi zaidi nilipomsikia Bw. Lissu akikubaliana na mtazamo wangu kuhusu yale mazungumzo yao na CCM kuhusu maridhiano.

Kabla ya jana sikuwahi kumsikia Lissu akimkosoa Freeman Mbowe hadharani na kwa uwazi kiasi hicho.

Pamoja na kunifumbua masikio, huo mjadala ulizichochea fikra zangu na kupelekea kuwa na maswali mengi zaidi.

Inavyoelekea huko CHADEMA kuna mpasuko ambao ulikuwa unachemka kwa muda mrefu.

Sidhani kama kwenye miaka ya nyuma tokea Mbowe awe mwenyekiti, aliwahi kupewa changamoto kwenye hizo Chaguzi zao za ndani ya chama. Kama imewahi kutokea, mnaojua mtatujuza na kutukumbusha.

Sasa safari hii sijui ni kitu gani kilichomfanya Lissu naye kugombea hiyo nafasi ya uenyekiti wa chama.

Sijui huo uchaguzi wao utafanyika lini.

Na ukishafanyika na mshindi kujulikana, napata shida kuamini kuwa hali ndani ya chama itakuwa salama.

CHADEMA inaweza kutoka kwenye huo ikiwa ni dhoofu sana.

Atayeshindwa atakubali kuwa kashindwa kihalali na baada ya hapo atabaki kuendelea kukijenga chama?

Wakati mwingine napatwa na fikra za huenda Tundu Lissu katumia mwanya huo wa kumpa changamoto Mbowe ili aje kupata kisingizio cha kujitoa kwenye chama hapo mbeleni…

Kwa sasa tumewasikia hao wawili wakiwa hawako pamoja.

Ningependa sana kuona wanafanya mdahalo ili wapiga kura wao wapate fursa ya kuwaona wawili hao wakijinadi mbele zao.

Ila Mbowe naye…..dah. CHADEMA imesha plateau chini ya uongozi wake.

Kwa nini asijiuzulu tu awaachie na wenzie nao wakiongoze hicho chama?

Mbeba maboksi here I come with my two cents from a distance.

Nianze kwa kuwatakia heri ya Krismasi kwenu waumini wa Kristo.

Kwa wasio waumini, nanyi nawatakieni sikukuu njema na mapumziko mema.

Nimekuwa nikiifuatilia hii mijadala ya uchaguzi wa ndani wa CHADEMA kwa juu juu tu.

Sikuwa kabisa na raghba yoyote ile ya kunifanya niufuatilie kwa kina huo mchakato, hapo awali.

Jana ndo nikapata muda wa kusikiliza kidogo mjadala uliofanyika Clubhouse ambao Tundu Lissu alishiriki.

Nilifurahi zaidi nilipomsikia Bw. Lissu akikubaliana na mtazamo wangu kuhusu yale mazungumzo yao na CCM kuhusu maridhiano.

Kabla ya jana sikuwahi kumsikia Lissu akimkosoa Freeman Mbowe hadharani na kwa uwazi kiasi hicho.

Pamoja na kunifumbua masikio, huo mjadala ulizichochea fikra zangu na kupelekea kuwa na maswali mengi zaidi.

Inavyoelekea huko CHADEMA kuna mpasuko ambao ulikuwa unachemka kwa muda mrefu.

Sidhani kama kwenye miaka ya nyuma tokea Mbowe awe mwenyekiti, aliwahi kupewa changamoto kwenye hizo Chaguzi zao za ndani ya chama. Kama imewahi kutokea, mnaojua mtatujuza na kutukumbusha.

Sasa safari hii sijui ni kitu gani kilichomfanya Lissu naye kugombea hiyo nafasi ya uenyekiti wa chama.

Sijui huo uchaguzi wao utafanyika lini.

Na ukishafanyika na mshindi kujulikana, napata shida kuamini kuwa hali ndani ya chama itakuwa salama.

CHADEMA inaweza kutoka kwenye huo ikiwa ni dhoofu sana.

Atayeshindwa atakubali kuwa kashindwa kihalali na baada ya hapo atabaki kuendelea kukijenga chama?

Wakati mwingine napatwa na fikra za huenda Tundu Lissu katumia mwanya huo wa kumpa changamoto Mbowe ili aje kupata kisingizio cha kujitoa kwenye chama hapo mbeleni…

Kwa sasa tumewasikia hao wawili wakiwa hawako pamoja.

Ningependa sana kuona wanafanya mdahalo ili wapiga kura wao wapate fursa ya kuwaona wawili hao wakijinadi mbele zao.

Ila Mbowe naye…..dah. CHADEMA imesha plateau chini ya uongozi wake.

Kwa nini asijiuzulu tu awaachie na wenzie nao wakiongoze hicho chama?
Yetu macho na masikini, but it’s hard to imagine how CHADEMA will emerge unscathed from this seemingly full-fledged civil war!
 
Back
Top Bottom