Fikra za Mama yangu kuhusu Ndoa na Familia

Fikra za Mama yangu kuhusu Ndoa na Familia

Mwizukulu mgikuru

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2021
Posts
5,715
Reaction score
13,739
Jana nilikuwa napiga story na mama yangu mzazi. Katikati ya mazungumzo yetu, aliniambia kwamba laiti kama yeye angekuwa mwanaume, basi asingeoa. Badala yake, angezaa tu na wanawake tofauti ili apate watoto na maisha yaendelee. Bi mkubwa wangu huyu yupo kwenye miaka 65 sasa.

Ninachoamini mimi ni kwamba huwezi kuwa na heshima katika jamii yetu ya Kiafrika mpaka uwe na familia. Hata uongozi wa juu serikalini, kama urais, hauwezi kupewa mpaka wahakikishe kwamba una mke. Pia, sidhani kama unaweza kuishi kwa uchamungu kama unaishi kiholela. Naamini ukiwa na mke ni tiketi kubwa ya kumcha Mungu, kwani kuna asilimia chache sana za kuwa mzinifu ukiwa katika ndoa.

Sasa, bi mkubwa wangu anawaza nini? 😎 Au ndio anataka kunithibitishia kuwa ni kweli motoni wamejaa wanawake?
 
Siku hizi Kuna wimbi kubwa la Wanawake wanaolea watoto bila Baba (Single Moms), Kwa maoni yangu ndiyo maana mmomonyoko wa maadili umekuwa Mkubwa miongoni mwa jamii zetu.

Angekuwa Dokta Ndodi angesema hebu turudi Eden
 
Haya mambo yaache kama yalivyo.

" Lakini mimi nawaambia, amtazamaye mwanamke kwa kumtamani, huyo amekwisha kuzini nae rohoni"

Kumbe unaweza kuogopa kuzini kimwili, lakini kiroho ukawa mzinzi uliyekubuhu, tatizo letu wanadamu tunapenda sana kufurahishana machoni.
 
Vipi yeye aliolewa kabla ya kukuzaa? Ikiwa ndio aliolewa kabla ya kukuzaa ww, so muulize ni kwanini anashauri wengine wazalishwe bila kuolewa? Na kama alizalishwa (kukuzaa ww) bila kuolewa muulize kwanini ilitokea hivyo?

Bimkubwa wako nina imani ana majibu mazuri ya maswali haya niliyokwambia umuulize, pia yatakufanya ufaham vizuri alichomaanisha.

Nahisi lengo lake ni kutaka usiowe ili huduma zote ambazo ungezitoa kwa mke wako ziende kwake. Hapa simaanishi na ile huduma ya kitandani lakini 😀😂
 
Au ndio anataka kunithibitishia kuwa ni kweli motoni wamejaa wanawake..
Mama yako bachelor for life yaan anapigwa Sana mbupu huko nje nna wasi wasi na huyo unaemuita Baba yako km ni kweli Baba yako maana Mama yako kwa mujibu wa maelezo 65 inaonekana kashachezea mbupu nyingi Mno ukiondoa mbupu ya huyo unaemuita Baba kwa Jina
 
Haya mambo yaache kama yalivyo.

" Lakini mimi nawaambia, amtazamaye mwanamke kwa kumtamani, huyo amekwisha kuzini nae rohoni"

Kumbe unaweza kuogopa kuzini kimwili, lakini kiroho ukawa mzinzi uliyekubuhu, tatizo letu wanadamu tunapenda sana kufurahishana machoni.

Mama yako bachelor for life yaan anapigwa Sana mbupu huko nje nna wasi wasi na huyo unaemuita Baba yako km ni kweli Baba yako maana 65 inaonekana kashachezea mbupu nyingi Mno
Nayaheshimu sana mawazo yako
 
Back
Top Bottom