Ni kwa sababu hata huko kusaidia wenye shida wanafanya ili waonekane mbele za watu ili baadaye wajiingize kwenye kisima cha mambo ya hovyo-yaani siasa hizi, na ndio maana, wanaposaidia wanaongozana na makamera ya waandishi wa habari. Lakini neno la Mungu katika Mathayo 6:1-4 linasema:
“Angalieni msifanye wema wenu machoni pa watu, kusudi mtazamwe na wao; kwa maana mkifanya kama hayo, hampati thawabu kwa Baba yenu aliye mbinguni. Basi wewe utoapo sadaka, usipige panda mbele yako, kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ili watukuzwe na watu. Amin, nawaambieni, Wamekwisha kupata thawabu yao. Bali wewe utoapo sadaka, hata mkono wako wa kushoto usijue ufanyalo mkono wako wa kuume; sadaka yako iwe kwa siri; na Baba yako aonaye sirini atakujazi.”