Flora Mbasha kufunga ndoa wiki ijayo

Flora Mbasha kufunga ndoa wiki ijayo

Ngoja aolewe iliyule muuza sura wake wa awali apate uchungu wa Kutafuta pesa maana alikuwa anasafiria nyota ,mtoto wa kiume anajiremba kama flora bwana

Hahahaaaa jamani nyie?! [emoji14][emoji14][emoji14] nimecheka Kwa sauti mpaka basi! Watoto wa mjini wanakwambia mapenzi pesa, ufundi peleka VETA ! Na hapendwi Mtu isipokuwa pesa! Imeandikwa fedha ni jawabu la mambo yote! Hata uwe mwanaume hata awe mtanashati kiasi gani bila kuwa Na uwezo wa kupata kipato cha kuweza familia kujikimu ni kazi bure! Halafu ikiwa Kwa miaka miwili mitatu Sawa lakini iwe Siku zote jamani? Mwanamke uhudumie mahitaji ya familia Na mahitaji yako binafsi mwaka wa kwanza, wa pili, wa tatu, Na kuendelea? Acheni nyie ufanye kusikia tu halafu mwisho wa yote asie mwaminifu kwenye ndoa!
 
Biblia inasisitiza sana kusameheana na inasema asiye samehe wengine bila kujali aina ya kosa, basi hata yeye Mungu hatamsamehe mtu huyo.

Kuhusu kisa cha hawa wawili, Flora ndiye aliye mwacha Emma, wakati ule Emma alimbembeleza sana Flora wasahau tofauti zao warudi waishi kwenye ndoa yao lakini Flora alikataaa kata kata hata kumtia aibu mumewe. Wakati huo Flora alikuwa anahatia mbele za Mungu kwa kuvunja ndoa na kukataa msamaha wa mumewe.
maana biblia inasema mtu akikosa hata saba
mara sabini kwa siku akija na kuomba msamaha, msamehe.

Baada ya kesi kwisha, Flora alimtaka mume wake amsamehe warudiane, kakini Emma alikataa katakata. Hivyo hatia ikageuka kwa Emma.

Kwa sababu hiyo Flora amehesabiwa haki kwa sababu aliomba msamaha kabla Emma hajaoa lakini Emma alikataa, kibiblia hata Mungu hajamsamehe Emma dhambi zake kwa kukataa kumsamehe Flora. hivyo Emma anahesabiwa kama mdhambi tu aliye amua kumwacha mkewe.

Hivyo Flora aliye tubu anapata uhalali wa kuolewa kwa neno linalosema:- yeye asiye amini akitaka kuondoka na aondoke, ndipo huyo ndugu mume au mke yu huru.

Kwa sasa Flora yuko huru
kuolewa kwa sababu Emma kamwacha kwa kukataa kumsamehe pale Flora alipoomba Emma amsamehe warudiane.

Emma atabaki na hatia.

Biblia inasema heri kuoa au kuolewa kuliko kuwaka tamaa. Flora bado kijana sana. Hana hatia kabisa mwacheni aolewe amtumikie Mungu vizuri.

HAPPY WEDDING FLORA.
Maelezo yako naamini yamejitosheleza
 
Baadhi ya ndoa za Kikisto ni za kinafiki sana, wanandoa wakiwa kwenye Watu wanajidai kuwa pamoja wengine hata kushikana mikono , Kumbe wanapo rudi nyumbani kila Mtu analala chumba chake mwenyewe! Sasa yote ya nini hayo? Wengine vipigo hata kutishiana maisha halafu eti wengine wanataka kusema nini vile! Yataka moyo kuishi na Mume asiye afanya kazi (lofa) yani ni mtihani mkubwa, halafu kuna Yule ambae unajua leo hana kazi Ila matarajio yapo kwamba anavyo vyeti vya kueleweka kuweza kuajiriwa baada ya muda flani hata Kwa miaka miwili mitatu, lakini unakuta Tumaini la hivyo halipo halafu mwisho wa Siku shukrani za Punda ziwe mateke?! Utuhumiwe uzinifu ?! Mmn mbombongafu
Ongelea udhaifu wa mtu na si Ukristo.dini zote zina watu dhaifu na marijali pia,hapa ni swala la mtu mwenyewe
 
Hawa waimba gosple nao tukiacha kununua kazi zao eti nao wata andamana, why wanatuhamasisha wasiyoyatenda au nao ni wasanii wa uigizaji yaani wanaimba tu kufurahisha watu? Hawana aibu kabisa na huyo atakae bariki huo uzinzi eti nae atakuwa mchungaji kweli jamani?
 
Mwimbaji wa muziki wa Injili nchini, Madame Flora (Flora Mbasha zamani), Jumapili ya wiki ijayo anatarajia kufunga ndoa na mume wake mtarajiwa Daudi Kusekwa katika bustani za hoteli ya Rock Beach jijini Mwanza.

Madame Flora ameliambia Swaggaz kuwa ndoa hiyo itaambatana na uzinduzi wa albamu yake mpya inayoitwa Wakati Wake pamoja na kitabu alichokipachika jina la Siri za Flora Mbasha.

“Ndoa itafungwa asubuhi na jioni kutakuwa na sherehe ya harusi, utambulisho wa albamu yangu mpya pamoja na kitabu, watu wote wanakaribishwa kadi zimebaki chache tu kutokana na idadi ya ambayo imepangwa na kamati,” alisema Flora.

Chanzo. Mtanzania
Huyo dada hakuwa amefunga ndoa na Mbasha? Lini ndoa ya Kikristo ikawa zaidi ya mume mmoja?
 
Naomba kujua je dhambi hii(kuoa/kuolewa na aliyeachwa<uzinzi>) je ukitubu huwezi kusamehewa na ndoa yenu ikawa sahihi kikanisa ?
 
Si ajabu leo hii umezini ndipo ukakomenti hapa. Nani aliyekamilika katika dunia hii kama si mungu pekee.
Kwahiyo kama mimi nimezini. Turuhusu watu wavunje sheria kwa kuwa na Mimi navunja.
HAPANA.
 
Hapa nazungumzia Maswala ya Kiroho. Ndio nikahoji uhalali wa Mchungaji ataaefunga hiyo ndoa.
Kila mtu na imani yake ndugu, tuacheni kujivika utakatifu wa kujikalilisha. Hao wachungaji, mapadri na mashekhe wengi tu nishawahi kuwaona wakiwa na nyumba ndogo na ufuska kibao. Ulitaka Flora aishii maisha ya ki lesbians? Nashangaa sana watu mmeshupalia jambo la kawaida tu. Tena nikujulishe tu kuwa huyo kijana ni jirani yangu na wako na mahusiano kitambo hivyo hawajakurupuka. Hivi ni lini mara ya mwisho wewe umefanya sex na kwa nini? Pia ulitaka madam Flora aishi kama Watawa na wakati si Mtawa?
 
Kila mtu na imani yake ndugu, tuacheni kujivika utakatifu wa kujikalilisha. Hao wachungaji, mapadri na mashekhe wengi tu nishawahi kuwaona wakiwa na nyumba ndogo na ufuska kibao. Ulitaka Flora aishii maisha ya ki lesbians? Nashangaa sana watu mmeshupalia jambo la kawaida tu. Tena nikujulishe tu kuwa huyo kijana ni jirani yangu na wako na mahusiano kitambo hivyo hawajakurupuka. Hivi ni lini mara ya mwisho wewe umefanya sex na kwa nini? Pia ulitaka madam Flora aishi kama Watawa na wakati si Mtawa?
Hakuna ndoa za Kikristo za Mara mbili mbili.
 
Back
Top Bottom