KERO Foleni Kubwa Barabara ya Mwai Kibaki: Kila Siku ni Kizungumkuti Asubuhi na Jioni

KERO Foleni Kubwa Barabara ya Mwai Kibaki: Kila Siku ni Kizungumkuti Asubuhi na Jioni

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Kumekucha Wadau.

Leo asubuhi wakati nawahi kwenye Mitikasi yangu nimejikuta nimenasa katikati ya foleni ambayo hata kusogeza tu mguu ilikiwa shida na ni mchezo wa kila siku hasa kwenye barabara hii ya Mwai Kibaki.
IMG_0045.jpeg
Katika mji wa Dar es Salaam, foleni barabara ya Mwai Kibaki imekuwa ni kero kubwa kwa wakazi. Kila siku, madereva wanapotoka Kawe kuelekea Morocco, au Kutoka Morocco - Kawe hali inakuwa mbaya zaidi. Wakati wa safari zao, madereva wengi huamua kufungua barabara na kuingia kwenye upande wa pili, wakijaribu kupita kwa haraka, bila kujali sheria za usalama barabarani.
Hali hii inasababisha msongamano wa magari pande zote mbili, huku wengine wakijaribu kupita hadi kwenye sehemu ya watembea kwa miguu. Wakati mwingine, magari yanakosa kabisa kuelekea eneo husika, na hivyo kufanya foleni kuwa ndefu zaidi. Watu wanashuhudia vichochoro vya magari.
IMG_0047.jpeg
Ni wazi kuwa, iwapo hatua stahiki hazitachukuliwa, kwa mchezo huu adha hii ya foleni itakuwa mbaya zaidi.

Pia, Soma:
Barabara ya Mbezi Mwisho, Kimara kuelekea Town kila siku asubuhi kuna foleni kubwa, hivi tatizo ni nini?
LATRA imeshindwa kutuletea usafiri wa daladala njia ya Tegeta/Bunju-Kawe Ukwamani kupitia barabara ya Mwai Kibaki?
 

Attachments

  • IMG_0052.jpeg
    IMG_0052.jpeg
    712.5 KB · Views: 7
Watu wa Dar buana. Kila kitu sheedah. Kuanzia maji, foleni, mgao wa umeme, takataka kila kona, joto kali, mbu wasumbufu n.k. Hamieni huku kwetu hakuna hizo sheeedah. Unaamka saa 1 na nusu na unawahi maeneo yako.
 
Ishu sio kuhama mji, hapa kuna changamoto ya madereva kuvunja sheria na wasimamizi wala hawachukui hatua madhubuti
Watu wa Dar buana. Kila kitu sheedah. Kuanzia maji, foleni, mgao wa umeme, takataka kila kona, joto kali, mbu wasumbufu n.k. Hamieni huku kwetu hakuna hizo sheeedah. Unaamka saa 1 na nusu na unawahi maeneo yako.
 
Kumekucha Wadau.

Leo asubuhi wakati nawahi kwenye Mitkasi yangu nimejikuta nimenasa katikati ya foleni ambayo hata kusogeza tu mguu ilikiwa shida na ni mchezo wa kila siku hasa kwenye barabara hii ya Mwai Kibaki.
Katika mji wa Dar es Salaam, foleni barabara ya Mwai Kibaki imekuwa ni kero kubwa kwa wakazi. Kila siku, madereva wanapotoka Kawe kuelekea Morocco, au Kutoka Morocco - Kawe hali inakuwa mbaya zaidi. Wakati wa safari zao, madereva wengi huamua kufungua barabara na kuingia kwenye upande wa pili, wakijaribu kupita kwa haraka, bila kujali sheria za usalama barabarani.
Hali hii inasababisha msongamano wa magari pande zote mbili, huku wengine wakijaribu kupita hadi kwenye sehemu ya watembea kwa miguu. Wakati mwingine, magari yanakosa kabisa kuelekea eneo husika, na hivyo kufanya foleni kuwa ndefu zaidi. Watu wanashuhudia vichochoro vya magari.
Ni wazi kuwa, iwapo hatua stahiki hazitachukuliwa, kwa mchezo huu adha hii ya foleni itakuwa mbaya zaidi.

Pia, Soma:
Barabara ya Mbezi Mwisho, Kimara kuelekea Town kila siku asubuhi kuna foleni kubwa, hivi tatizo ni nini?
LATRA imeshindwa kutuletea usafiri wa daladala njia ya Tegeta/Bunju-Kawe Ukwamani kupitia barabara ya Mwai Kibaki?
Mambo ya foleni ni ya kulalamikia kweli, si yanajulikana, yashawashinda
 
Mambo ya foleni ni ya kulalamikia kweli, si yanajulikana, yashawashinda
Hakuna anayelalamika, mfano kila dereva akifuata utaratibu bila kuvunja sheria za barabarani unadhani leo hii tungeona kuna watu hawwajibiki ipasavyo? Foleni ipo tu ila mchezo huu wa hii barabara ni wa kukusudia kuvunja taratibu
 
Hakuna anayelalamika, mfano kila dereva akifuata utaratibu bila kuvunja sheria za barabarani unadhani leo hii tungeona kuna watu hawwajibiki ipasavyo? Foleni ipo tu ila mchezo huu wa hii barabara ni wa kukusudia kuvunja taratibu
Siyo kuvunja taratibu, inaelekea asilimia kubwa ya drivers wana usongo wa mawazo. Siamini hizo fujo za kutanua line 4 kuelekea upande mmoja kwenye barabara ya line 2,watu wenye akili timamu wanaweza kufanya.
 
Back
Top Bottom