For serious & single ladies: Nipo kwenye harakati za kutafuta mke mwema


Hili nalo neno Maty
 

kweli kabisa, tena akimpata asiyejua maana ya ndoa atateswa huyu jamaa na watoto wake.
Atafute mke akiwaangalia watoto wake. Tena Bora atafute ambae kashazaa anajua malezi yanaendaje.
Ulimwengu wa sasa mabinti hawataki kulea watoto wa wenzao. Mtoto ni kiunganishi kikubwa cha wazazi, hakuna anayetaka stress za mke mwenzie aliyetangulia.
 


Huyo mama ungempa muda anaweza badilika na kuwa mke bora zaidi hapo mbele, nakubaliana kuna mtu ameoa mwanamke wamezaa watoto wawili lakini huyo mwanamke hafai hata kidogo anagawa kama pipi kama mkeo alikua hivyo hapo waweza muacha mazima lakini kama tabia zingine zinabadilika tu
 

....is more than that!
 
Mke mweeemaa, anatoka kwa BWANA................................ all the best!
 
 
....is more than that!

Pole sana, ila hapo juu umesema unataka mwanamke asiwe vuvuzela, mwenye hasira na mbishi nadhani ndivyo mama chacha wako alikuwa. Na kuhusu hili nakuhakikishia asilimia kubwa ya wanawake hasa ambao hawajawahi ishi na wanaume wako hivyo kwani wengi wakiingia kwenye ndoa huwa wanadhani ni raha tu kwa kwenda mbele kama ambavyo ilikua kipindi cha uchumba (kila mtu nadhani anajua uchumba unavyotia raha) na hata biblia inasema mwanamke mpumbavu ndio ambae huvunja ndoa kwa mikono yake, so utaona hata mungu alipanga wanawake ndio wawe wavumilivu na hili huwa linawashinda wanawake wengi sana kwenye ndoa zao za awali inategemea amepata mume mvumilivu kiasi gani, kama mume ni mvumilivu kwa jinsi miaka inavyoenda mmama anajikuta kumbe nilikua siko sahihi na anajirekebisha, lakini mume asipokua mvumilivu ndio anaamua kumuacha mkewe, anatafuta mwingine ambae hajawahi kukaa na mume anakuta ni yale yale, anatafuta mwingine anakuta ni yale yale. Utajikuta unazaa watoto kibao kila mtu na mama yake
 

Maty,

While asilimia kubwa ya uliyosema ni true, kwangu mimi issue ni tofauti hasa hapo kwenye fact ya nani alianza kutaka kuachana.....!
  • That mama...alianza kudemand kuchana kutokana na tofauti za kiimani...so sio mimi nilianza hii kitu
  • That mama alikuwa na kiburi sijawahi ona.....hii na mamaake mzazi aliconfess
  • Kiburi ni sehemu ya familia yao ....(mtoto wa kwanza hadi mwisho)
  • kwao kuachika ni sifa yao ....yeye watatu kuchana na mume....!
  • that mama alikuwa mchafu sijapata kuona ....ana kazi (she gets money), nina hali nzuri kiuchumi....bado alishindwa kutumia resources hizo vizuri kujipiga sopu sopu....! mama gani hadi leo hazijui ALWAYS....anasundaga matambaa...anayarundika kwenye vipochi na kabatini....arrrrg ...ngoja niishie hapa!
So ukiangalia huo mtiririko hapo, unaweza jua kwanza si mimi nilianza kudemand tuachane.....! Pili, naamini kwenye ndoa kuna issue nyingi sana, lakini naamini pia issue hizo zinatofautiana sana, zipo zingine zinavumilika sana!
 
EEEEEhhh,
Huku Taluma kumbe unatafuta mchumba?
haya bana, si umesikia kule wanasema kutongozwa ni dharau?
sasa huyo mchumba sijui atakuwa ametongozwa juu kwa juu au vipi?
 
FP,

Asante kwa maneno mazuri .....ndicho ninacho kiamini despite all the factors I'm in!

Kama ndio hivyo subiri mungu akupatie, hivyo vigezo utakavyo vibandike kwenye maombi ili mungu akupe wa hivyo, ila uwe mvumilivu na makini sana for the sake of ur lovely children. Maisha mazuri pekee sio wakitakacho watoto, lazima wazazi muwe na furaha mkichanganya na maisha mazuri basi watoto wanakua vizuri.
 

Kwanza nimecheka jamani, ila kuhusu vitambaa kuna wengine always zinawazuru so hawana budi kutumia vitambaa ila kikubwa ni usafi tu kama sio msafi ndio habari inaanzia hapo. Na kiburi chake huyo mama ni kwa sababu na yeye ana pesa, hawa ndio huwa wanaharibia watu wanakataa kuoa mwanamke mwenye cash.


Naomba nikuulize hili swali samahani kama nitakukwaza kwani simaanishi kukukwaza. Je uliwahi mpenda huyo mama? na bado rohoni kwako yumo angalao kidogo
 
:-* kwani katika kusoma kwako kote mpaka chuo kikuu , na kazi zako ulizofanya ni kweli hujaona mwenye ivo vigezo? :-*

.....nipo kwenye mchakato Babygood! ...ofisini, church, hapa kwenye forums all these ni venue ambazo nazitumia effectively kwa sasa....! shuleni wengine tulikuwa ''MABUNDI'' sana so tukakosa kunetwork as result waliobora wa umri wetu washabebwa...ndo tunawatafuta hapa walio salia....!
 

Umeuliza swali zuri sana Maty na wala hujanikwaza.....to be very honesty, sikuwahi hata point mmoja kumlove yule mama.....watu wengine wanangekewa za ajabu.....it was the first kick....mimba hiyo....! nilijaribu kujipa nafasi ya kumpenda ilishindikana kabisa...pia nilijaribu kukaa naye, nikamwambia mambo ambayo nilikuwa siyapendi kwake, tukakubaliana tujipe muda ajirekebishe na mimi nikamwahidi kumsupport lakini wapi.....kichwa ngumu ile, ikashindikana!

Huwezi amini the second baby aliibuka immediately baada ya kudundana .....can't explain this aisee lol!
 
 
 
EEEEEhhh,
Huku Taluma kumbe unatafuta mchumba?
haya bana, si umesikia kule wanasema kutongozwa ni dharau?
sasa huyo mchumba sijui atakuwa ametongozwa juu kwa juu au vipi?

Bacha,

Usiogope, ni mitazamo tu ya watu na mazingira ndo yanayoweza kumfanya mtongozwaji ajione kadharauliwa.....! kwa mila za kiafrika, mwanamke kutongozwa ni heshima sio dharau!
 
taluma vipi?...

yee ukiipwe au pe wii yeva yeva?

ndii hoouuchu uneeeneee!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…