Force Account inawamaliza mabosi wa Serikali, Waziri Mkuu anashuhudia madudu ya kutisha

Force Account inawamaliza mabosi wa Serikali, Waziri Mkuu anashuhudia madudu ya kutisha

Jidu La Mabambasi

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2014
Posts
16,419
Reaction score
26,594
Siye wajuvi wa masuala ya ujenzi tulionya na kuonya, tukaambiwa tunatetea ulaji wetu.
Kuna wawakilishi wetu tuliwatuma hadi Bungeni kupinga Force Accout , lakini walibezwa kuwa makandarasi ni mafisadi wa fedhe za umma.

Sasa kazi nyingi zilifanywa kwa spidi kubwa kwa kumtumia fundi Maiko.
Madudu sasa yanaonekana wazi kwa kupata kazi iliyo chini sana katika viwango, na fedha kuliwa vibaya na wasimamizi na mabosi, kuanzia ma DED hadi Madaktari na waalimu.
Kuna waliofungwa, kama yule mwalimu huko Musoma, na wengine kesi zao ziko Mahakamani na zingine kuendelea kuchunguzwa na TAKUKURU.

Tatizo kubwa ni wanasiasa kujifikiria wana akili kubwa kuzidi zile time tested project administration methods na procedures.

Sasa hela za serikali zimeliwa na wajanja kwa vile supervision systems za kifedha na kiujenzi ni very very poor au hakuna kabisa!

Sasa hivi hata Waziri Mkuu kachoka, anatembelea miradi pamoja na TAKUKURU ikiwepo, kila mradi ni madudu ya kutosha.

Mifano michache:
-Waziri Mkuu alitembelea mradi wa hospitali huko Songea. milango ilikuwa haifungi-fundi Maiko huyo na daktari kachukuliwa na TAKUKURU
-Huko Tabora , VETA, jengo la mlinzi milioni 11, msimamizi kachukuliwa na TAKUKURU
-Huko Katavi juzi nyaraka zimechomwa moto kuficha ulaji baada ya kumtumia fundi Maiko, TAKUKURU wamepewa kibarua
-Huko Tanga Mkuu wa Mkoa kawapiga wanted ma DED wawili kwa kufanya kazi na fundi Maiko na jengo likawa ndivyo sivyo, TAKUKURU wameitwa
-Huko Ruangwa, kazi ya fundi Maiko, jengo halina madirisha wala milango, Ths 75 million imaeliwa, TAKUKURU wamepewa kazi
-Huko Ikungi fundi Maiko kajenga jengo la Tsha 500milion ndivyo sivyo, DC kawapeleka TAKUKURU
-Huko Mwanza Mkuu wa Mkoa kawaita TAKUKURU, jengo la abiria, uwanja wa ndege kujengwa chini ya viwango na kusua kusua, hela imeliwa, fundi Maiko anachekelea

Kwa sababu hata hawa wanasiasa wetu haawajui waende wapi wa kukiuka taratibu za ujenzi, inabidi wakumbushwe kuwa TAKUKURU hawana muarobaini wa namna ya kurekebisha taratibu zilizopindwa katika ujenzi

Na kosa kubwa ni hao hao wanasiasa.

Force Account kwa kumtumia fundi Maiko imeleta hasara kubwa sana kwa Taifa.


Tunaiomba serikali, hasa wanasiasa, wadhibitiwe na sheria zinazohusu sekta hii ya ujenzi.
Bodi husika za Wizara ya Ujenzi, CRB. AQRB, ERB, NCC zina kazi kubwa kuwaelimisha wanasiasa wanaoingilia kiutendaji uendeshaji wa sekta ya ujenzi.
 
Makandarasi nao walikua Vimeo tu. Tena mradi Wana demand fedha nyingi angali wanaenda kuwachukua haohao fundi mchundo wa bei rahisi kujenga hiyo miradi. Ishu kubwa ni usimamizi mzuri tu umekosekana
Kukosekana msimamizi ni kosa la mwenye mradi(serikali).
Sasa katika Force Account hakuna mkandarasi, hakuna msimamizi
 
Siku tukiamua kutenganisha Siasa(politics) na taaluma(professionalism) tutakuwa tumepiga hatua hadhimu yenye weledi usio tia shaka sawia katika kuleta mageuzi ya kifikra na utendaji ndani ya azaki za kiraia na taasisi binafsi na za umma.

"Kataa ujinga" "katiba ifuatwe"
 
Hao makandarasi Badala ya kujenga wao huungana na viongozi kisha hupewa pesa na wanagawana na viongozi wakiitelekeza kazi. Waziri WA Maji aliongea baada ya kuwabana makandarasi WA Maji. Bora Force account watu wawajibike.
 
Takukuru hawana meno nao wamepewa ulaji mbona ni wapokea rushwa wazuri Sana.
Ni shida kama mwanakijiji wa kule..... Ni mwenyekiti wa kamati ya ujenzi ambaye hakuwahi kujenga nyumba ya vyumba viwili mbavu za mbwa ndiye msimamizi wa kituo Cha afya kinachojengwa kwa shilingi bilioni 2,alafu upate3Es
 
Ukwrli mchungu ni kwamba forced account no matokeo ya nyie wakandarasi kuiba,kuzidisha gharama,kutoa rushwa kwa viongozi kupata kazi,kuchelewesha kazi kitaalamu,nk....kama mngekuwa mnafanya kwa weledi sidhanu kama tunguska kwenye issue za force account
 
Bora tu kuingia ubia na Mchina tujengee nchi nzima Veta, zahanati au miradi fulani then chukua ziwa , mlima au mgodi kwa miaka 50 kuliko kumpa mswahili. Mswahili unafadhili timu ya mpira singida united na namumgo fc huku mshahara wako unajulikana, hizo pesa zingine kama sio kodi zetu unatoa wapi? Wadogo uwaiga wakubwa.
 
Siku tukiamua kutenganisha Siasa(politics) na taaluma(professionalism) tutakuwa tumepiga hatua hadhimu yenye weledi usio tia shaka sawia katika kuleta mageuzi ya kifikra na utendaji ndani ya azaki za kiraia na taasisi binafsi na za umma.

"Kataa ujinga" "katiba ifuatwe"
Tuna wanasiasa ambao wanajiona wanajua kila kitu, kumbe kichwani patupu kabisa.
Hawachuliwi hatua maana Dola liko chini yake.

Kama ingekewa nchi zinazoiheshimu serikali na kanuni zake, wengi wangekuwa lupango kujibu mashtaka ya uharibifu na ukiukwaji mkubwa wa taratibu za ujenzi.
 
Umeongea kisiasa na kishabiki zaidi kuliko kitaalamu!!!

Muundo wa FORCE AACOUNT unataka Ujenzi ufanyike kwa kusimamiwa na Kamati za Ujenzi wa mradi; yaani
1. Kamati ya Ujenzi/Kamati ya usimamizi
2. Kamati ya Manunuzi
3. Kamati ya UKAGUZI na mapokezi.

Aidha best practices ni PROCURING ENTITIES kufanya screening za mafundi Wazuri na kuwaajiri kwenye kazi ya Ujenzi chini ya usimamizi wa Mhandisi wa PROCURING ENTITY....

Fundi anatakiwa kuwa na ujuzi na uzoefu wa kutosha na mwenye UWEZO WA KUSOMA RAMANI NA MICHORO na kuitafsiri kwa USAHIHI.

Wakati wa Utekelezaji wa Mradi Mhandisi wa PROCURING ENTITY anatakiwa kuwepo kwenye hatua zote muhimu kama
1. Wakati wa kuseti msingi
2. Kumwaga jamvi
3. Kuseti ukuta
4. Kwenye concrete zote
5. Kuseti paa n.k

Ukiangalia kwa Uhalisia Utaratibu wa Force account ni mzuri SHIDA NI WASIMAMIZI KUTANGULIZA MASLAHI BINAFSI KULIKO MASLAHI YA UMMAH.

Kununuliwa milango mibovu FUNDI ANAHUSIKA VIPI? Hapa maana yake Wasimamizi wametaka kitu cha bei RAHISI ili wapige HELA!!!!

Kwani MAJUMBA yetu hatujengi kwa kuwatumia hawa MAFUNDI????

UNATAKA KUNIAMBIA KILA NYUMBA NZURI ILIYOJENGWA MTAANI AMETUMIKA MHANDISI ALIYESAJILIWA EQRB, ARB, ERB, NCC n.k?
Mbona Miradi yetu Binafsi hatuweki milango ya hivyo? Au kwenye miradi ya Ujenzi ya UMMA HUWA WATAALAM WETU WANAGEUKA WATU TOFAUTI????

Ninachokiona ni KUENDELEA KUMOMONYOKA KWA UZALENDO MIONGONI WA WATUMISHI WA UMMA NA KUTANGULIZA ZAIDI MASLAHI BINAFSI.

NI KWELI FORCE ACCOUNT inakosesha WAKANDARASI FURSA ZA KUFANYA KAZI LAKINI HATUPASWI KUWA NA USHABIKI HASA KWENYE JAMBO LA UJENZI WA MIUNDOMBINU YA TAIFA LETU..

Lakini kwa upande wa Wakandarasi nao ni vilevile Kwani tunashuhudia
1. Miundombinu inajengwa na baadhi ya WAKANDARASI ikiwa haina viwango...
2. Gharama kubwa mno za Ujenzi wa miundombinu

Ifike wakati tutatoa TATIZO NA SII KUKWEPA ILI TUENDELEE KULINDA MASLAHI YETU BINAFSI.
 
Tuna wanasiasa ambao wanajiona wanajua kila kitu, kumbe kichwani patupu kabisa.
Hawachuliwi hatua maana Dola liko chini yake.

Kama ingekewa nchi zinazoiheshimu serikali na kanuni zake, wengi wangekuwa lupango kujibu mashtaka ya uharibifu na ukiukwaji mkubwa wa taratibu za ujenzi.
"Kuna karne itafika kwa wajinga kuwa viongozi na werevu kuwa wafuasi nadhani Karne yenyewe ndo hii" Shaaban Robert

Taifa letu limejaa wajinga ambao ndio hao walio kwenye power kwao siasa ni muhimu kuliko taaluma ndio maana kila uchwao kila sekta ni matatizo matupu sababu ya siasa za maji taka chini ya ccm.

Sababu ya wananchi kuwa mazuzu na mazwazwa imepelekea kuwa amini Wana siasa na sio wataalam alafu mwisho tuna mtafuta mchawi ni nani huu si ujinga.Mabilioni ya pesa yanapotea hasa kwenye ujenzi wa kutumia mafundi Maiko

"Tusisahau deni la taifa ni 91T"

NB: Odious debt
 
Umeongea kisiasa na kishabiki zaidi kuliko kitaalamu!!!

Muundo wa FORCE AACOUNT unataka Ujenzi ufanyike kwa kusimamiwa na Kamati za Ujenzi wa mradi; yaani
1. Kamati ya Ujenzi/Kamati ya usimamizi
2. Kamati ya Manunuzi
3. Kamati ya UKAGUZI na mapokezi.

Aidha best practices ni PROCURING ENTITIES kufanya screening za mafundi Wazuri na kuwaajiri kwenye kazi ya Ujenzi chini ya usimamizi wa Mhandisi wa PROCURING ENTITY....

Fundi anatakiwa kuwa na ujuzi na uzoefu wa kutosha na mwenye UWEZO WA KUSOMA RAMANI NA MICHORO na kuitafsiri kwa USAHIHI.

Wakati wa Utekelezaji wa Mradi Mhandisi wa PROCURING ENTITY anatakiwa kuwepo kwenye hatua zote muhimu kama
1. Wakati wa kuseti msingi
2. Kumwaga jamvi
3. Kuseti ukuta
4. Kwenye concrete zote
5. Kuseti paa n.k

Ukiangalia kwa Uhalisia Utaratibu wa Force account ni mzuri SHIDA NI WASIMAMIZI KUTANGULIZA MASLAHI BINAFSI KULIKO MASLAHI YA UMMAH.

Kununuliwa milango mibovu FUNDI ANAHUSIKA VIPI? Hapa maana yake Wasimamizi wametaka kitu cha bei RAHISI ili wapige HELA!!!!

Kwani MAJUMBA yetu hatujengi kwa kuwatumia hawa MAFUNDI????

UNATAKA KUNIAMBIA KILA NYUMBA NZURI ILIYOJENGWA MTAANI AMETUMIKA MHANDISI ALIYESAJILIWA EQRB, ARB, ERB, NCC n.k?
Mbona Miradi yetu Binafsi hatuweki milango ya hivyo? Au kwenye miradi ya Ujenzi ya UMMA HUWA WATAALAM WETU WANAGEUKA WATU TOFAUTI????

Ninachokiona ni KUENDELEA KUMOMONYOKA KWA UZALENDO MIONGONI WA WATUMISHI WA UMMA NA KUTANGULIZA ZAIDI MASLAHI BINAFSI.

NI KWELI FORCE ACCOUNT inakosesha WAKANDARASI FURSA ZA KUFANYA KAZI LAKINI HATUPASWI KUWA NA USHABIKI HASA KWENYE JAMBO LA UJENZI WA MIUNDOMBINU YA TAIFA LETU..

Lakini kwa upande wa Wakandarasi nao ni vilevile Kwani tunashuhudia
1. Miundombinu inajengwa na baadhi ya WAKANDARASI ikiwa haina viwango...
2. Gharama kubwa mno za Ujenzi wa miundombinu

Ifike wakati tutatoa TATIZO NA SII KUKWEPA ILI TUENDELEE KULINDA MASLAHI YETU BINAFSI.
Sorry mdau ukijibiwa hili naomba unitagi please.
Asante
 
Back
Top Bottom