Forex: Biashara Yenye Utajiri Mkubwa Zaidi Duniani Ambayo Hakuna Benki Itataka Uijue!

Forex: Biashara Yenye Utajiri Mkubwa Zaidi Duniani Ambayo Hakuna Benki Itataka Uijue!

Status
Not open for further replies.
Hongera na usife moyo ONTARIO kwa wabongo wanajaribu kukukwaza/ au kukukatisha tamaa. Wakujifunza tupo tayari na kama ulivyosema tutakuwa mashahidi wa kuthibitisha ukweli wako. Kwa mara ingine tena naomba niwe mmoja wa hao 150 wa kwanza. Mungu akuongoze ufanikishe juhudi zako hizi. Ngoja tuendelee na hivyo vitabu tukisubiria.
 
Napendekeza kwa wale tuliopo apa dsm tunaopenda kwenda kwenye hayo mafunzo na wengine wanafaham kwa kiasi flani kuhusu hii trade basi tupange kukutana au tujiundie ka,group wasap lengo kujulishana zaidi na kupata mwongozo uku tukiendelea kuchambua vile vitabu na jinsi ya kuhuzuria Venue yake
 
Mtoa uzi nimekuwa nafwatilia sana nyuzi zako zinavutia sana. Kwa hii ya sasa nimeona kikubwa ni changamoto unazokumbana nazo na vikwazo. Naamini kwenyee hili jukwaa kuna kila aina ya watu. Inawezekana unapata ugumu wa kishelia wana shelia wapo. Usalama wana usalama wapo. IT watu wa IT wapo. Kama umeamua kuwasadia hama kutusadia pia tupo tayali kukusadia pia. Kama ulifika ofisi flani ukapata vikwazo nashauli uwe unarudi hapa jukwaani na kupost so wapo watu kwenye hiyo ofisi usika watakusadia.Tupo pamoja sana sana" You will never walk alone in this thin path "
 
Kamanda ONTARIO ,usivunjike moyo,mambo mazuri duniani yanakuwa na vikwazo,hata Mwl Nyerere alipokuwa anaitangaza TANU kuwa itawaondoa Waingereza watu walimbeza,walimpiga vijembe,walimtukana ,walimkashifu,walimkandia,walimg'ong'a na kumfanyia kila aina ya vitimbwi,mwisho Mwl J K Nyerere akaja kuwa Kiongozi wa Tanzania na kutimiza ndoto yake, na Mimi naamini utatimiza ndoto yako ,wengi tuko nyuma yako bali bado hatufahamiana.Ukitaka kuthibitisha maneno yangu kuwa watu tunasapoti mawazo yako ,hata leo hii toa namba ya simu au bank account ya kuchangia kiasi chochote ili kufanikisha azma hii ,utaona mwitikio,Mimi Niko tayari kuchangia bila kujali kuwa nitahudhuria mafunzo au sitahudhuria,naamini hata kama sitahudhuria mafunzo itakuwa ni faida kwa Watanzania wengine na pia faida kwangu INDIRECT.MWISHO NIWAKUMBUSHE WADAU - TUSOMENI POST ZOTE ILI TUPUNGUZE MASWALI YALIYOTOLEWA MAJIBU,INASHANGAZA KUWA JIBU LIMETOLEWA KWENYE POST NAMBA 1739 ,HALAFU MWINGINE ANAULIZA SWALI LILELILE NA KUPOST - POST NAMBA 1740 !!!! INASHANGAZA NA INAKATISHA TAMAA,Hivi post chache hivi baadhi yetu tunakuwa wavivu kusoma ,can we master FX trainings and be expert of it ? Halafu Trainings za mwanzo zitakuwa facilitated na Gurus from SOUTH AFRICA !!!!!!Ahaaaa!!!! Nilikuwa napita tu,- WATANZANIA TUKO SERIOUS KWELI ??????
 
Mkuu ONTARIO naomba katika hizo session 3 ungeweka moja ya watu ambao wapo tayari kulipia hii elimu ili tufaidike wengi, mana tunaohitaji ni wengi but nafasi ni chache so please tupe nafasi na ambao tupo tayari kulipia ili tuanze pamoja hiya June 15
 
Mkuu ONTARIO Mimi ombi langu ni katika sessions hizo tatu (za free na hata zitakapoanza za kulipia)iwepo ya jioni sana,let us say kuanzia SAA 12 jioni.ili sie ambao bado hatujawa financially independent tuweze kuhudhuria baada ya vibarua kumalizika.
 
mkuu na mimi naomba niwepo kwenye session yeyote katika hao watu 150 mkuu.
 
Mkuu ONTARIO.. Mimi wa mkoani na nimejipanga kusafiri kabisa saa yoyote mambo yatakapokuwa tayari...
 
Watu naona wanadhani kwamba inahitajika uwe na knowledge ya FOREX ama finance katika kuingia katika huu mtanange maana wengi wananiuliza haya mambo katika PM. My friends, Mimi mwenyewe binafsi sina background yoyote na issue za uchumi, Niliachanaga na mambo hayo ya uchumi na biashara miaka kadhaa iliyopita toka Ben Mkapa akiwa raisi. But kitu chochote kile duniani kinaenda na mafanikio yake yanakuja kwa dhamira na nia ya dhati kufanya hicho kitu.

Na siri moja katika hili, Msituone tunajibujibu viconcept hapa mkadhani sisi tunaelewa haraka sana. la hasha, Mimi binafsi narudiaridia page hata mara tano kabla sijaendelea page inayofuata. Na hata nikimaliza chapter nikafika mbele, Bado nikijiona nimesahau sioni shida kurudia. Hiki kitu hakiepukiki katika hili jambo. Na usijione kuwa wewe huwezi elewa, jaribu kurudiarudia tena na tena. with time nina uhakika utamaster tuu concept. Ukishindwa kuelewa mwenyewe, post hapa jukwaani, wadau watakusaidia kukujibu na kukuelewesha

Na hili nddo maana huwa kuna mazoezi katika kila jambo. si mpira, si uvumbuzi wa kisayansi nk. hivi vitu hatujavivumbua sisi, so no way tutavimaster in single glance.

tuendelee na kazi.
 
Anahitajika!! Binti kwa ajili ya maulizo (receptionist).

Vigezo:
1. Awe mrembo - sitanii, awe mzuri mwenye muonekano wa kueleweka.

2. Awe multilingual - yani awe na uwezo wa kuongea lugha kadhaa, hasa kingereza. Yani awe vizuri kabisa kwenye hii lugha (kusoma, kuandika na kusikikiza).

3. Awe ana uelewa wa computer, awe anafahamu basics kama word, excel, PP na Internet.

4. Awe motivated.

5. Awe problem solver, awe ana ubunifu, sihitaji sana experience wala elimu. Nahitaji quality ya kazi.

Shughuli:
●Kukaribisha wageni kwa kuzungumza nao
●Kupokea simu za office na kujibu maulizo
●Kutoa maelekezo na utaratibu kwa wageni
●Kupanga appointments kati ya wageni na mentors
●Kupokea na kujibu emails za office.


Mshahara nitaanza na 675,000 kwa mwezi, kama tutaridhishwa na jitihada na ubunifu wake basi baada ya miezi mi3 tutaweka long term contract ambayo itakuja na ongezeko na mshahara na incentives zingine

Kama una vigezo niPM, nitajibu week ijayo tarehe 6.
Mkuu kweli umeamua kusaidia mungu akusimamie na nina uhakika utafika mbali nakupa miezi sita tu dunia itakutambua.
 
Wakati tunasubiri update ya mwisho, naomba tuendelee kusoma kitabu cha Forex for dummies. Baada ya kumaliza hicho kitabu tuanze kitabu kingine kiitwacho Naked Forex - High-Probability Techniques for Trading Without Indicators >>Kimeandikwa na Alex Nekritin. Please soma kuelewa, si kusoma kumaliza pages ama kumfurahisha Ontario. Your knowledge is the best weapon to beat the market.

Ontario.[/QUOTE]

Ontario tafadhali Kama unaweza kutupia hivyo vitabu viwili humu ndani itakuwa vyema, iwapo tu unavyo kimtandao Na Nafasi yako inaruhusu. Asante.
 
Watu naona wanadhani kwamba inahitajika uwe na knowledge ya FOREX ama finance katika kuingia katika huu mtanange maana wengi wananiuliza haya mambo katika PM. My friends, Mimi mwenyewe binafsi sina background yoyote na issue za uchumi, Niliachanaga na mambo hayo ya uchumi na biashara miaka kadhaa iliyopita toka Ben Mkapa akiwa raisi. But kitu chochote kile duniani kinaenda na mafanikio yake yanakuja kwa dhamira na nia ya dhati kufanya hicho kitu.

Na siri moja katika hili, Msituone tunajibujibu viconcept hapa mkadhani sisi tunaelewa haraka sana. la hasha, Mimi binafsi narudiaridia page hata mara tano kabla sijaendelea page inayofuata. Na hata nikimaliza chapter nikafika mbele, Bado nikijiona nimesahau sioni shida kurudia. Hiki kitu hakiepukiki katika hili jambo. Na usijione kuwa wewe huwezi elewa, jaribu kurudiarudia tena na tena. with time nina uhakika utamaster tuu concept. Ukishindwa kuelewa mwenyewe, post hapa jukwaani, wadau watakusaidia kukujibu na kukuelewesha

Na hili nddo maana huwa kuna mazoezi katika kila jambo. si mpira, si uvumbuzi wa kisayansi nk. hivi vitu hatujavivumbua sisi, so no way tutavimaster in single glance.

tuendelee na kazi.
Ni kweli kabisa mkuu. Muhimu hapa ni kusoma na kuvielewa vitabu... Hasa dummies imenitoa tongotongo kias kikubwa
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom