TANZIA Fr. Privatus Karugendo amefariki dunia

TANZIA Fr. Privatus Karugendo amefariki dunia

Sawa Ila alianza shujaa wenu anajifanya hataki barakoa kabetri kakafreeze sijui kalimtandika shoti. Corona ipo ndio uvae barakoa jomba utakufa kama Mungu wenu.
Hebu jitazame hapa ulivyo 🤣🤣🤣

20431DE3-2AC2-45BB-A7F3-7C640FF80C01.jpeg
 
Amefia hospitali gani father, isije ikawa ni yeye aliendika jana hii post ya kutuaga.
 
Apumzike kwa Amani Fr. Peivatus Kalugendo.
Fikra na Msimamo wake kwenye mambo aliyoyaamini vitaishi vizazi na vizazi kwani alitumia vema kalamu kuhifadhi mawazo yake.
Pole kwa ndugu na familia.

Sent from my Nokia 3.1 using JamiiForums mobile app
 
Amefia hospitali gani father, isije ikawa ni yeye aliendika jana hii post ya kutuaga.
75% yaweza kuwa kweli.
 
Kutoka kwa Askofu Kalikawe Lwakalinda Bagonza


BURIANI PACHA WANGU PRIVAT

NOOO. Nashindwa kuamini ninachosikia. Kwamba pacha wangu Privatus Karugendo hatunaye?! No. Hapana siamini hata kama inaaminika.

Juzi nimempoteza mdogo wangu. Haikutosha, nimpoteze pacha wangu?!

Tulifahamiana akiwa Padre kijana nikiwa Shemasi. Wakati huo tulikuwa Ujerumani, nikisoma, alifanya kazi za kitume. Watu wengi walisema tulifanana katika mengi.

Nilipobarikiwa kuwa Mchungaji alikuwepo kijijini kwetu kumzika babake Padre rafiki yake hayati Padre Buhorela.

Tuliyokubaliana yalivutia wengi kuliko tuliyotofautiana. Tulipenda kusoma vitabu, kuandika na kujadiliana. Alikuwa mfuasi wa Baba wa Taifa, Mimi nilikuwa mwanafunzi na sitahitimu.

Sikukubaliana naye aliponipigia. Alikuwa na uwezo wa kuona mazuri ndani ya kitu kibaya. Mimi ni mwepesi wa kuona udhaifu ndani ya kitu kinachoaminiwa na wengi kuwa kizuri.

Wote tuliuanika ujinga wetu kupitia Rai, Raia Mwema, Tanzania Daima, MwanaHalisi, Mwananchi na Mawio. Nilipostaafu hilo yeye aliendelea. Tuliulizana, "hivi ukianika ujinga wako ukaisha kichwani, Nini kinabakia kichwani?"

Pumzika rafiki, Pacha, Mtume wa jamii huria na mpenda watu wote pasipo ubaguzi. Ulijenga madaraja mengi kuliko kuta.
 
Baba Privatus #Karugendo amefariki dunia usiku huu.

#RIPFrKarugendo

Baadhi ya maandishi yake kwenye mitandao ya kijamii.

14/6/2021
“Kutafakari na kuhoji ni dalili Za uhai. Maiti haiwezi kutafakari wala kuhoji! Twaweza kuamua kuishi kama maiti au viumbe hai wenye uwezo wa kuutiisha ulimwengu na kujiletea maendeleo! Maendeleo uletwa na watu hai, si maiti”.

18/3/2021
“Mama Samia, pole sana kwa msiba huu mkubwa. Wengi tulikufahamu na kukupenda wakati wa Bunge la katiba. Simamia katiba mpya, tume huru ya uchaguzi, uzalendo, umoja na mshikamano. Tanzania ni yetu sote”.

19/11/2020
“Hawa wanawake 19 wa Chadema, ninawafahamu vizuri, ninawaheshimu saaaana kwa msimamo wao na uaminifu mkubwa kwa chama chao na taifa lao. Ni kitu gani kimewapata?. Fedha? Hapana! Ubunge? Hapana! Hawa ni wapambanaji, watiifu na wazalendo! Wamejikwaa wapi? Halima! Niambie!”.

19/9/2020
“Mama Samia, ana sifa nyingi, mbali na upole, huruma, umakini na busara hana siasa za chuki na ushabiki, anaiangalia Tanzania, kwa ujumla wake, ni mzalendo wa kweli! Tujifunze kwake! Tanzania ni yetu sote!”.
Mmh huyu sio yule aliyetuaga kwenye ile mada? Ana ID ya kike?
 
Baba Privatus #Karugendo amefariki dunia usiku huu.

#RIPFrKarugendo

Baadhi ya maandishi yake kwenye mitandao ya kijamii.

14/6/2021
“Kutafakari na kuhoji ni dalili Za uhai. Maiti haiwezi kutafakari wala kuhoji! Twaweza kuamua kuishi kama maiti au viumbe hai wenye uwezo wa kuutiisha ulimwengu na kujiletea maendeleo! Maendeleo uletwa na watu hai, si maiti”.

18/3/2021
“Mama Samia, pole sana kwa msiba huu mkubwa. Wengi tulikufahamu na kukupenda wakati wa Bunge la katiba. Simamia katiba mpya, tume huru ya uchaguzi, uzalendo, umoja na mshikamano. Tanzania ni yetu sote”.

19/11/2020
“Hawa wanawake 19 wa Chadema, ninawafahamu vizuri, ninawaheshimu saaaana kwa msimamo wao na uaminifu mkubwa kwa chama chao na taifa lao. Ni kitu gani kimewapata?. Fedha? Hapana! Ubunge? Hapana! Hawa ni wapambanaji, watiifu na wazalendo! Wamejikwaa wapi? Halima! Niambie!”.

19/9/2020
“Mama Samia, ana sifa nyingi, mbali na upole, huruma, umakini na busara hana siasa za chuki na ushabiki, anaiangalia Tanzania, kwa ujumla wake, ni mzalendo wa kweli! Tujifunze kwake! Tanzania ni yetu sote!”.

Apumzike kwa amani Fr. Karugendo.

Tangulia baba nasi tu nyuma yako.
 
Back
Top Bottom