Freeman Mbowe: Dar es Salaam kuna kikosi kazi cha utekaji

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
6,067
Reaction score
10,938
“Kama Chama tumechunguza kutoka vyanzo vyetu vya ndani na vingine vya ndani ya Jeshi la Polisi na Vyombo vingine vya Ulinzi na Usalama, nitaeleza kwa kifupi tulichogundua na tunaowaonyooshea vidole ili Polisi na hao wengine watusute watuambie Mbowe mnasema uongo, uchunguzi wetu unatupeleka wapi? moja kuna kitu kwenye Kanda Maalum ya Dar es saalam kinaitwa Task Force ya Ulinzi na Usalama, Task Force hii iliundwa ikishirikisha Wadau kutoka Jeshi la Polisi, Usalama wa Taifa na hata JWTZ, katika hatua ya baadaye Jeshi la Wananchi liliondoka katika oparesheni hii, na Task Force hii ilipoundwa kwa mara ya kwanza iliundwa kama Kikosi maalum cha kupambana na wizi ambacho kinasimamiwa na ZCO ambaye sasa hivi anayeongoza Ofisi hiyo anaitwa ASP Faustin Mafwele huyu ndio Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Kanda Maalum ya Dar es salaam ambaye anasimamia Kikosi hiki”

“Oparesheni centre ya kikosi hiki ipo nyuma ya Kituo cha Polisi Chang’ombe na mtambue Kikosi hiki hakiingiliwi na mfumo wa kawaida wa utawala wa Polisi kwahiyo hakifanyi kazi ndani ya Vituo vya Polisi, nyuma ya Kituo cha Polisi cha Chang’ombe kuna kambi ya Kikosi hiki na imezungushiwa uzio wa mabanzi pale ndani wanateswa Watu, wanaumizwa Watu, wanafinywa Watu pale ndio mateso ya Watanzania wanapopitia”

“Kwa taarifa tulizonazo kwa mwaka huu na sehemu ya mwaka jana, wapo Watanzania zaidi ya 200 hawajulikani walipo na mambo haya ni mwendelezo wa maelekezo ya Viongozi wa Serikali ambao huko nyuma walipaswa kusema shughulikeni nao”

Soma Pia: Freeman Mbowe: Viongozi wa CHADEMA na Watanzania wasio na Vyama wanaoendelea kutekwa na Vyombo vya Usalama vya Nchi yetu

“Sisi kama Chama tumesema tuyaseme haya kwa sauti ili yasikike zaidi, utekaji huu umeambatana na mauaji, awali waliokuwa wanauawa kienyeji walikuwa wanapelekwa mochwari, wengine kama Sativa walipelekwa pori la Katavi wakaliwe na Fisi kwasababu wanasema Katavi ndio pori lenye Fisi wakali ambao hata mfupa wanautafuna kama biskuti, Mungu hakupenda akamwokoa, Sativa alikamatwa na kikosi hiki na Mafwele anajua na kikosi hiki ndicho kimemkamata Soka, Mlay na Mbise”
 
naona samia ameshamzidi magufuli kwa kuua/kupoteza watu
Wengi wanateteta kuwa sio Samia bali vijakazi wake ila wazungu husema 'Silence means consent', ukimya daima huchukuliwa kuwa ni ridhaa. Samia yupo kimya kuashiria ameridhia haya yote yatokee.

Kwa kila ovu linalofanyika nchini kwa sasa, ni kwa ridhaa ya Samia.
 
“Kama Chama tumechunguza kutoka vyanzo vyetu vya ndani na vingine vya ndani ya Jeshi la Polisi na Vyombo vingine vya Ulinzi na Usalama, nitaeleza kwa kifupi tulichogundua na tunaowaonyooshea vidole ili Polisi na hao wengine watusute watuambie Mbowe mnasema uongo, uchunguzi wetu unatupeleka wapi? moja kuna kitu kwenye Kanda Maalum ya Dar es saalam kinaitwa Task Force ya Ulinzi na Usalama, Task Force hii iliundwa ikishirikisha Wadau kutoka Jeshi la Polisi, Usalama wa Taifa na hata JWTZ, katika hatua ya baadaye Jeshi la Wananchi liliondoka katika oparesheni hii, na Task Force hii ilipoundwa kwa mara ya kwanza iliundwa kama Kikosi maalum cha kupambana na wizi ambacho kinasimamiwa na ZCO ambaye sasa hivi anayeongoza Ofisi hiyo anaitwa ASP Faustin Mafwele huyu ndio Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Kanda Maalum ya Dar es salaam ambaye anasimamia Kikosi hiki”

“Oparesheni centre ya kikosi hiki ipo nyuma ya Kituo cha Polisi Chang’ombe na mtambue Kikosi hiki hakiingiliwi na mfumo wa kawaida wa utawala wa Polisi kwahiyo hakifanyi kazi ndani ya Vituo vya Polisi, nyuma ya Kituo cha Polisi cha Chang’ombe kuna kambi ya Kikosi hiki na imezungushiwa uzio wa mabanzi pale ndani wanateswa Watu, wanaumizwa Watu, wanafinywa Watu pale ndio mateso ya Watanzania wanapopitia”

“Kwa taarifa tulizonazo kwa mwaka huu na sehemu ya mwaka jana, wapo Watanzania zaidi ya 200 hawajulikani walipo na mambo haya ni mwendelezo wa maelekezo ya Viongozi wa Serikali ambao huko nyuma walipaswa kusema shughulikeni nao”

Soma Pia: Freeman Mbowe: Viongozi wa CHADEMA na Watanzania wasio na Vyama wanaoendelea kutekwa na Vyombo vya Usalama vya Nchi yetu

“Sisi kama Chama tumesema tuyaseme haya kwa sauti ili yasikike zaidi, utekaji huu umeambatana na mauaji, awali waliokuwa wanauawa kienyeji walikuwa wanapelekwa mochwari, wengine kama Sativa walipelekwa pori la Katavi wakaliwe na Fisi kwasababu wanasema Katavi ndio pori lenye Fisi wakali ambao hata mfupa wanautafuna kama biskuti, Mungu hakupenda akamwokoa, Sativa alikamatwa na kikosi hiki na Mafwele anajua na kikosi hiki ndicho kimemkamata Soka, Mlay na Mbise”
Ongea mkuu, Mbowe ndio Martin Luther King, wa, sasa hv,
 
Niwapongeze CHADEMA kwa kupenyeza watu katika vyombo vya ulinzi na usalama, kwa hili wameona mbali na wameanza fanikiwa maana mipango na mikakati ovu ya serikali na watesi watakuwa wanafahamu mienendo yao kwa haraka zaidi.

Na hilo la soka huwenda wamepenyezewa na watu loyal waliomo katika mfumo.
 
Back
Top Bottom