Freeman Mbowe kuzungumza na Taifa Ijumaa, Januari 10, 2025

Freeman Mbowe kuzungumza na Taifa Ijumaa, Januari 10, 2025

HUYU Jamaa ana uwezo wote wa kuwa mwenyekiti kwa Sifa za uongozi alizo nazo
 
TAL hawezi kusimamia chama kwa miaka mitano,.
Chadema itakuwa yatima soon
ishu ni kwamba hata akiendelea kuwa mwenyekiti chadema haitakuwa kama ilivyo hivi sasa, itabakiwa na wenye maslahi binafsi tu. Lile vibe halitakuwepo tena, chadema ita collapse totally chini ya mbowe again. Amechokwa hana jipya
 
Mjumbe napenda kujua sera za Mbowe ni zipi mpaka sasa. Naomba samari
Nadhani tusikilize atakayoongea kesho labda anazo sera zake zingine nje ya Katiba ya Chadema, lakini kumbuka kwamba sera zote za Chadema ziko ndani ya Katiba yake na miongozo yake, miongozo hii haikutungwa na mtu mmoja.

Ukitaka kuleta jambo jipya ni lazima uombe kwa Kamati kuu kubadili Katiba na useme kwanini
 
Freeman Mbowe Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema kesho Ijumaa tarehe 10/01/25 anatarajiwa kuzungumza na Taifa kupitia Clouds Media kuanzia saa 12 asubuhi katika kipindi cha Power Breakfast.

Freeman Mbowe mwanasiasa mwenye mvuto zaidi kwa sasa hapa nchini anatetea nafasi yake ya uenyekiti katika kipindi kingine cha miaka mitano.

Freeman Mbowe amejitofautisha na wapinzani wake kisiasa kwa jinsi alivyo mnyenyekevu, anayechagua maneno ya kuzungumza, anayeheshimu viongozi wenzake, asiyetoa shutuma bila mpangilio, anayetambua mchango wa wenzake, asiyetoa siri za chama na asiyeropoka hovyo.

Kwa mujibu wa tafiti kupitia wajumbe kadhaa wa Mkutano mkuu kote nchini Freeman Mbowe anatarajiwa kuchaguliwa tena kwa ushindi wa kati ya asilimia 60% mpaka 70% ya kura zote za wajumbe.

Molemo Media Itakuwa live kuwaletea mazungumzo ya Freeman Mbowe na Taifa.
Hizi ni virigu tiunna pressure to ccm
Hamuna kitu uapo
 
Heshima na busara kwa baba angu mbowe nakuomba ujiuzuru TU siasa zimebadilika usiharibu heshima ulivyo jijengea muachie lisu tupambane na maccm kiulalo ulalo siasa za maridhiano kwa sasa hazitakiwa ni chuma kwa chuma TU tunahitaji mtu jasili wa kutuongoza pindi pale TU tunapo ona chama tawala kinazurimu mambo ya msingi
 
Nadhani tusikilize atakayoongea kesho labda anazo sera zake zingine nje ya Katiba ya Chadema, lakini kumbuka kwamba sera zote za Chadema ziko ndani ya Katiba yake na miongozo yake, miongozo hii haikutungwa na mtu mmoja.

Ukitaka kuleta jambo jipya ni lazima uombe kwa Kamati kuu kubadili Katiba na useme kwanini
Mkuu umezunguka sana. Maana yake mpaka sasa Mbowe hana sera yeyote
 
Mjumbe napenda kujua sera za Mbowe ni zipi mpaka sasa. Naomba samari
Mkuu niliiweka huku jana, sema nini Team FAM ni Low battery na wapo tayari kudharirika ili mradi wasifie tu. 🤣🤣🤣

Maisha na dunia ya leo mtu unakuwa muoga na mnafiki ili kumpendeza mtu. Hiyo kwangu ni ngumu sana

20250108_164024.jpg

Muangalie Lema hapo
 
Mkuu umezunguka sana. Maana yake mpaka sasa Mbowe hana sera yeyote
Sasa huu ni muda wenu wa kunadi sera za mnaowaunga mkono na kumwangusha, ni nafasi nzuri ya kushawishi wapiga kura kwamba Jamanii eeee!! Mbowe hana sera mchagueni huyu mtu wetu sera zake hizi hapa.

Msipoteze muda siku zinaisha
 
Mnahubiri demokrasia lakin m/kiti wenu kakalia kiti miaka ishirini na hataki kuachia iko wapi demokrasia mnaoihubir
 
Sasa hapo Clouds PB asubuhi watangazaji ni kina nani? Masoud Kipanya awepo na amuulize maswali, masoud amechora michoro kuhusu chadema, kuna ngumi badala ya ile alama yao ya vidole viwili, kuna makaburi mawili, itapendeza zaidi kama atamhoji mbowe kuhusu hii chadema kuelekea uchaguzi wao. Halafu mbowe mbona anaenda kufanya mahojiano kwenye media ndogo kama hiyo, si bora angeenda TBC?
 
Anajiuzulu lini uenyekiti ili apige kampeni?
Lissu hashikiki kwa sasa.
 
Back
Top Bottom