Freemasons Inside - Out: Who are they? How they operate? How to join them?

Freemasons Inside - Out: Who are they? How they operate? How to join them?

Status
Not open for further replies.
Miaka sita baada ya kuchapishwa ilani ya humanism, vita vya pili vya Duniya vikaripuka

Katika aya hii ya Qur’an Mwenyezi Mungu anasema, Je! Binadamu anafikiri kuwa ataachwa bure tu (asipewe amri za Mwenyezi Mungu wala makatazo yake)? Je! Hakuwa tone la manii lililotonwa? Kisha akawa kidonge cha damu, kisha akamuumba na akamsawazisha (kuwa mtu kamili)? Kisha akamfanya namna mbili. Mwanaume na mwanamke. Je! Hakuwa hayo ni muweza wa kuhuisha wafu?

Hapa Mwenyezi Mungu anawakumbusha binadamu kuwa wao ni viumbe vyake. Pale mtu anapotanabahi kuwa yeye ni kiumbe wa Mungu basi aelewe kuwa haishi bila ya kuangaliwa bali anawajibika kwa Mwenyezi Mungu.

Dai kuwa binadamu hawakuumbwa ndio msingi wa falsafa ya humanism. Vipengele viwili vya ilani ya kwanza ya Wahumanisti vinatoa ufafanuzi wa itikadi hii.

Zaidi ya hivyo Wahumanisti wanashikilia kuwa sayansi inaunga mkono madai haya. Lakini ni waongo wakubwa.

Tokea ilani yao ya kwanza ilipochapishwa, hoja mbili ambazo wanahumanisti wamezitoa kama hakika za kisayansi, kwamba ulimwengu ni wa milele na wa kievolusheni, zote zimevunjiliwa mbali.

Dhana kwamba ulimwengu ni wa milele ulivunjiliwa mbali na mlolongo wa vumbuzi za angani zilizofanywa wakati ilani ya kwanza ya wanahumanisti ilipokuwa inaandikwa.

Vumbuzi kama vile ulimwengu kutanuka, chanzo cha mionzi ya angani na mahesabu ya uwiano ya Haidrojeni hadi Helium, zimethibitisha kuwa ulimwengu ulikuwa na chanzo chake na kwamba ulitokea kwa mlipuko mkubwa- Big Bang takriban miaka bilioni 15 au 17 iliyopita.

Ingawa wale wanashabikia falsafa ya kihumanisti na ya kilahidi walikataa kuikubali nadharia ya Big Bang lakini hatimaye walishindwa vibaya sana kutokana na ushahidi wa kisayansi ambao umejitokeza.

Jamii ya wanasayansi hatimaye ikaikubali nadharia ya Big Bang kwamba ulimwengu ulikuwa na chanzo chake. Hivyo, Muatheisti Anthony Flew alilazimika kukiri hivi;

….Sasa nitaanza kukiri kuwa Muatheisti lazima atatizike kwa hizi fikra za sasa za maumbile. Kwani inaonekana kuwa wanakosmolojia wanatoa ushahidi kuwa kile alichodai mtakatifu Thomas hakiwezi kuthibitishwa kifalsafa, hii ikiwa na maana kuwa ulimwengu ulikuwa na mwanzo wake.

Nadharia ya evolusheni ambayo ndio hoja kuu iliyomo katika ilani ya kwanza ya humanisti, ikaanza kupoteza nguvu miongo kadhaa baada ya kuandikwa kwake.

Inafahamika hivi leo kuwa ubabaishaji uliofanywa na wanaevolusheni na Waatheisti (na bila shaka Wahumanisti) kama vile A.I. Oparin na J.B.S Haldane katika miaka ya thelasini kuhusiana na chanzo cha uhai hauna msingi wa kisayansi.

Viumbe haviwezi kutokea kwa bahati nasibu kutokana na maada isiyo na uhai kama ilivyodaiwa katika ubabaishaji huo. Kumbu kumbu ya mabaki ya kale inaonesha kuwa viumbe hai hawakuwa hivi walivyo kutokana na hatua za mabadiliko madogo madogo bali walitokea kuwa pamoja wakiwa na sifa zao mbalimbali.

Ukweli huu umekubaliwa na wanaevolusheni wenyewe tangia miaka ya sabini. Sayansi ya viumbe hivi leo imebainisha kuwa viumbe hai hawakutokana na bahati nasibu na kanuni za maumbile bali katika kila kiumbe kuna mfumo madhubuti unaothibitisha kuwa msaniii mwenye hekima ndiye aliyeviumba. Kwa maelezo zaidi rejea kitabu kiitwacho Darwinism refuted. Zaidi ya hivyo, lile dai la uongo kuwa imani ya dini ndiyo sababu inayokwaza watu kuendelea na kuwatumbukiza matatizoni limetupiliwa mbali na ushahidi wa kihistoria. Wahumanisti wamedai kuwa kuondolewa kwa imani ya dini kutawaletea watu faraja na furaha, lakini hali ya mambo imekuwa kinyume chake.

. Vita hii ni kielelezo cha kihistoria cha misiba mikubwa iliyoletwa na itikadi za kifashisti za kisekula. Ikachipuka itikadi ya kikomunisti ya wahumanisti kwanza ilianzia kwa watu wa Urusi, kisha kwa watu wa China, Cambodia, Vietnam, Korea kaskazini, Cuba na katika baadhi ya nchi za Afrika na Latin Amerika. Ulifanyika ushenzi usio na mfano. Jumla ya watu milioni 120 waliuliwa na tawala au Jumuiya za kikomunisti. Ni dhahiri kuwa kundi la Wahumanisti wa magharibi (mabepari) nalo limeshindwa kuleta amani na furaha katika jamii zao na katika maeneo mengine ya Duniya. Kuvunjwa kwa hoja ya Wahumanisti juu ya dini pia kunadhihirika katika fani ya saikolojia. Misingi ya dhana ya Kiatheisti ilibatilishwa na matokeo ya tafiti tokea mwanzoni mwa karne ya ishirini (The Freudian myth). Patric Glynn wa chuo kikuu cha George Washington anaufafanua ukweli huu katika kitabu chake kiitwacho God, The Evidence, The Reconciliation of Faith and reason in a Post Secular World.
 
Lengo la Masoni ni kujenga Duniya ya kufuru

falsafa ya kihumanisti ambayo masoni wanaamini kuwa ndiyo falsafa kuu imejengwa kwa msingi wa kumkanusha Mungu. Lakini hii inazusha swali muhimu je masoni wanaitaka falsafa hii kwa ajili yao tu au wanataka ifuatwe na wengine pia tunapoyaangalia maandiko ya masoni tunaliona bayana jawabu la swali hili. Lengo la jumuiya hii ni kuieneza falsafa hii Duniyani kote ili kuzifutilia mbali dini zinazoamini Mungu muumba. Mathalani katika makala yake iliyochapishwa katika jarida la masoni Mimar Sinan imeelezwa hivi, “masoni hawatafuti chanzo cha fikra za maovu, haki na uadilifu nje ya ulimwengu wa kimaumbile, wao wanaamini kuwa fikra hizi zinaibuka kutoka na mazingira ya jamii ya mtu, mahusiano ya kijamii na vile mtu anavyohangaikia kwa ajili ya maisha yake. masoni wanajitahidi kueneza itikadi hii ulimwenguni kote”. Selami Isindag masoni wa ngazi ya juu wa kituruki ameandika hivi; kwa mujibu wa masoni ili kuwatoa wanadamu katika imani ya nguvu za kiungu inayotokana na maandiko ya dini, ni lazima yajengwe maadili yanayotokana na upendo kwa walimwengu.

Katika kanuni zao za maadili masoni wamezingatia umbile la mwanadamu, mahitaji yake na maridhio yao, kanuni za maisha ya jamii na taasisi zao , hiyari, uhuru wa kufikiri na kusema mambo yote yanayojumuishwa katika maisha ya kimaumbile. Kwa sababu hii, lengo lake ni kujenga na kuboresha maadili ya utu katika jamii zote. Hapa bwana Isindag ana maana ya kuwatoa wanadamu katika maadili yanayojengwa na vitabu vya dini. Hii ni kuwatenganisha watu wote mbali na dini. Katika kitabu hicho hicho Isindag anafafanua lengo hili pamoja na misingi yake ya kujenga utamaduni ulioendelea;

Misingi madhubuti ya masoni ni ya lazima na inajitosheleza kujenga utamaduni ulioendelea.

Nayo ni kukubali kuwa muasisi mkuu wa Ulimwengu ni evulusheni pekee, kunanusha imani ya ufunuo, usufi na imani nyingine, kuikweza dhana ya utu na kazi. Kipengele cha kwanza hapo juu kinataka watu wakanushe kuwepo kwa Mungu. [masoni hawaamini Mungu bali wanaamini evolusheni] kipengelea cha pili kinakanusha ufunuo kutoka kwa Mungu. Na kipengele cha tatu kinatukuza dhana ya utu na dhana ya kazi [kama ilivyokuwa katika ukomunisti].Tukitafakari jinsi mawazo haya yalivyojikita katika ulimwengu wa leo, basi twaweza kujionea ushawishi wa masoni ulimwenguni. Jambo jingine la kukumbuka hapa ni je masoni wameziendeshaje harakati zao dhidi ya dini? Tunapoyangalia maandiko ya masoni tunaona kuwa wanakusudia kuingamiza dini hasahasa katika ngazi ya jamii kwa njia ya propaganda. Selami Isindag anatoa mwangaza juu ya jambo hili katika ibara hii ya kitabu chake; Hata tawala za kikatili mno hazikufanikiwa katika jitihada zao za kuingamiza taasisi ya dini. Kwa kweli kutumia kwao mbinu nyingi za kisiasa katika jitihada za kuielimisha jamii ili kuwatoa watu katika imani na masonge ya dini walisababisha upinzani mkali. Nyumba za ibada walizotaka kuzifunga, leo hii zimejaa tele kuliko zilivyokuwa huko nyuma na imani ambayo walitaka kuififiliza imepata wafuasi wengi zaidi. Kwa usemi mwingine tunabainisha kuwa katika masuala yanayogusa nyoyo na hisia, marufuku na mabavu hayafai kitu. Njia pekee ya kuwatoa watu gizani na kuwaleta kwenye mwanga ni sayansi halisia na kanuni za hoja na hekima. Iwapo watu wataelimishwa kwa njia hii wataheshimu upande wa wahumanisti na kujinusuru wenyewe na imani za kibubusa.

Ili kuelewa kinachosudiwa hatunabudi kuichambua ibara hiyo kwa makini. Isindag anasema kuwa ukatili dhidi ya dini utawafanya watu wa dini wawe na ari zaidi na utaiimarisha dini yenyewe. Hivyo basi ili kuifanya dini isiwe na nguvu Isindag anaona kuwa masoni wanapaswa kuiuwa dini katika ngazi ya elimu anachokikusudia katika sayansi halisia na kanuni za hoja na hekima kwa kweli sio sayansi, sio hoja wala hekima. Anachokikusudia yeye ni falsafa ya kihumanisti na kilahidi ambayo hutumia misamiati ya ujanja kama mbinu kama vile inavyoonekana katika nadharia ya itikadi ya Darwin. Isindagi anadai kuwa pale dhana hizi zinaposambazwa katika jamii basi wahumanisti watapata heshima yaani kitakachobaki katika dini ni yale mambo tu yanayokubaliwa na falsafa ya kihumanisti. Wao wanataka kukanusha ukweli wa msingi uliomo katika msingi wa dini ya Mungu mmoja. Kwa kifupi masoni wanataka kufutilia mbali chembechembe za imani zinazojenga msingi wa dini. Wanataka kuitweza kazi ya dini iwe kama kipengele tu cha utamaduni ambacho kinazungumzia tu fikra zake juu ya masuala ya kimaadili. Njia ya kutimiza hili, kwa mujibu wa masoni ni kusimika dhana ya kukanusha Mungu katika jamii kwa kisingizio cha sayansi na hoja.

Na hatimaye kufikia lengo lao na kuiondoa dini katika nafasi yake hiyo ya kipengelea cha utamaduni na hivyo kujenga ulimwengu kamili wa kufuru. Katika makala ya Isindag iiyochapishwa na jarida la masoni liitwalo “ Positive Science- The obstacles of mind and Mansonry” anasema matokeo ya haya yote nataka kusema kuwa wajibu muhimu wa masoni sio kuipa mgongo sayansi na hoja kukiri kuwa hii ndio njia bora kwa mujibu wa evolusheni, kueneza imani yetu miongoni mwa watu na kuwaelimisha watu sayansi halisia. Maneno ya Ernest Renan yanabeba uzito zaidi; “iwapo watu wataelimishwa na kuamshwa kwa hoja na sayansi halisia, imani za kibubusa za dini zitaporomoka zenyewe”. Lessing naye anaunga mkono wazo hili; “iwapo wanadamu wataelimishwa na kuamshwa kwa sayansi halisia ipo siku moja hawatakuwa na haja na dini”hili ndilo lengo kuu la Masoni. Wanataka kuifuta kabisa dini na kujenga Ulimwengu unaoegemeya dhana ya utu yaani wanataka kujenga mfumo mpya wa ujahili ambapo watu wamkanushe Mungu aliyewaumba na wajione wao wenyewe ni Miungu. Haya ndio makusudiyo ya kuwepo kwa jumuiya ya Frimasonri.
 
Ulemavu wa hoja za wahumanisti juu ya Dini

Ulemavu wa hoja ya Wahumanisti juu ya Dini pia umedhihirika katika fani ya kisaikolojia. Ile hekaya ya Freud, msingi wa dhana ya ukafiri imefutiliwa mbali kuwa ni uwongo mtupu tokea mwanzoni mwa karne ya ishirini, hekaya hiyo imebatilishwa na data za uchunguzi. Patrick Glynn wa chuo kikuu cha George washington analifafanua jambo hili katika kitabu chake kiitwacho God: The Evidence, The Raconciliation of Faith and Reason in Post secular World.

Ngwe ya mwisho ya karne ya ishirini haikuuendekeza mtazamo wenye mushikeli kiakili. Muhimu zaidi ni kuanikwa hadharani kwa fikra za Freud juu ya Dini (ukiacha mambo mengi mengine) kwamba ni potofu kabisa. Utafiti wa kisayansi katika saikolojia, katika kipindi cha miaka 25 iliyopita umeonesha kuwa, badala ya kuwa bumbuwazi kama Freud na wafuasi wake walivyodai, imani ya dini ni moja ya mambo yanayowiana mno na afya ya akili na maisha ya furaha. Utafiti mmoja baada ya mwingine umeonesha uhusiano madhubuti baina ya imani na mwenendo wa kidini kwa upande mmoja, na maadili kwa upande mwingine, hasa kushughulikia matatizo kama vile vifo vya kujiua, ulevi, madawa ya kulevya, mfadhaiko, mipaka ya starehe ya ngono ndani ya ndoa. Kwa kifupi, ile iliyodhaniwa kuwa hoja ya kisayansi nyuma ya dhana ya Uhumanisti imethibitika kuwa haina ukweli, na ahadi zake zimeishia patupu.

Hata hivyo wadau wa dhana hii hawajaachana na falsafa yao, badala yake wameendelea na jitihada za kuieneza Duniyani kote kwa njia za propaganda. Hasahasa katika nyanja za sayansi, falsafa, muziki, fasihi, sanaa na sinema. Ujumbe wenye mvuto lakini wa uongo ulitungwa na wanaitikadi wa kihumanisti umekuwa ukipandikizwa kwa watu. Wimbo uitwao “Imagine” ulitungwa na Johnn Lennon, mpiga gitaa wa kundi mashuhuri la muziki liitwalo “The Beatles” ni mfano wa propaganda hizo.

Wimbo unasema; “Itakidi hakuna pepo.

Ni rahisi tu hebu jaribu.
Hakuna Jahannamu.
Juu yetu kuna anga tu.
Itikadi watu wote wanaishi hapa tu.
Hakuna cha kuuliyana wala cha kufiya.
Na wala hakuna Dini.
Huwenda mtasema labda naota ndoto lakini siko peke yangu.
Natumai siku moja mtaungana nasi na Duniya itakuwa moja”.

Wimbo huu ulichaguliwa kama “wimbo wa Karne”katika kura kadhaa za maonizilizopigwa mwaka 1999. Baada ya kukosa msingi wa kisayansi na wa hoja, uhumanisti unapandikizwa kwa njia za namna hii. Dhana ya humanisti haina uwezo wa kujenga hoja za kupinga Dini na ukweli, inajaribu tu kutumia mbinu za kupumbaza kama hizi. Pale ahadi za ilani ya mwaka 1933 ya wahumanisti ziliposhindikana, ikapita miaka arobaini ambapo baada ya miaka hiyo wahumanisti wakawasilisha rasimu ya pili.

Mwanzoni mwa kitabu, lilifanyika jaribio la kuelezea kwa nini ahadi za kwanza zilishindikana. Licha ya ukweli kwamba ufafanuzi ulikuwa hafifu lakini bado Wahumanisti wakakumbatia falasafa yao. Kipengele kikuu cha manifesto hii kilikuwa kile cha kulinda msingio wa kukana Dini kwa ilani ya 1933. Kama ilivyokuwa mwaka 1933, wahumanisti bado wanaamini kuwa imani ya jadi ya Mungu mmoja, hasahasa imani ya Mungu anayesikia maombi (sala), anayedhaniwa kuwa yu hai na anawaangalia watu, akisikia na kuelewa sala zao na kuweza kuwafanyia jambo fulani, ni imani isiyo na ushahidi na imepitwa na wakati. Sisi tunaamini kuwa Dini za jadi za kibubusa au za nguvunguvu ambazo zinaweka ufunuo, Mungu, ibada au itikadi juu ya mahitaji na maisha ya binaadamu haziwasaidii kitu binaadamu. Sisi kama wapinzani wa imani hiyo, tunaanza na binaadamu sio Mungu. Kwa kweli haya ni maelezo ya juujuu sana. Ili kuielewa Dini, kwanza mtu anahitaji akili na mafuhumu kuweza kuelewa mambo ya ndani mno. Kitu cha kwanza ni ukweli wa moyo na kuepuka chuki. Jitihada za wahumanisti kuielezea imani juu ya Mungu na ‘Dini za Mungu Mmoja’ kuwa haina msingi na imepitwa na wakati si jitihada mpya, ni mwendelezo wa dai lilelile, ambalo limetolewa kwa maelfu ya miaka na wale wanaomkana Mwenyezi Mungu.

Katika Qur’an, Mwenyezi Mungu analielezea dai hili kongwe lilitolewa na wale wasioamini. Mungu wenu ni Mungu mmoja. Lakini wale wasioamini akhera nyoyo zao zinakataa, nao wanatakabari. Bila shaka Mwenyezi Mungu anayajua wanayoyaficha na wanayoyadhihirisha. Kwa hakika yeye hawapendi wanaotakabari. Na wanapoambiwa (makafiri) “Mola wenu ameteremsha nini? Wanasema’hadithi za uwongo za watu wa zamani” Qur’an (16-22-24). Aya inabainisha kuwa sababu halisi ya wasioamini kuikataa Dini sahihi ni kiburi kilichomo nyoyoni mwao. Falsafa inayoitwa ‘humanism’ ni taathira ya nje ya kiburi hicho cha kumkana Mungu. Kwa maneno mengine ‘humanism’ sio utaratibu mpya wa fikra kama wanavyodai wale wanaounga mkono dhana hii. Ni fikra kongwe ambayo wamekuwa nayo wale wote wanaomkadhibisha Mungu kwa jeuri.
 
Mizizi ya dhana ya Ukomunisti katika Kaballa

Tumeona kuwa Kaballa ni itikadi ya zamani ya Misri na ikaingia na kuchanganyika na dini iliyofunuliwa na Mungu kwa WanaIsraili. Aidha tumeona kuwa msingi wa Kaballa ni welewa potofu kuwa binadaamu hawakuumbwa. Dhana ya Ukomunisti iliingia Ulaya kwa msingi wa itikadi hii ya Kaballa. Imani ya Kikristo ilijengwa kwa msingi wa imani ya kuwepo kwa Mungu, na imani kuwa Wanadamu ni waja wake walioumbwa naye. Lakini kwa kule kuenea kwa utamaduni wa Matempla sehemu zote za Ulaya, Kaballa ikaanza kuwavutia Wanafalsafa wengi. Kwa hali hiyo, katika karne ya 15 ikaibuka hii dhanna ya sasa ya "humanism" na imeacha taathira zisizofuta katika uimwengu wa fikra wa Ulaya. Uhusiano huu wa humanism na Kaballa umeelezwa zaidi katika vitabu kadha wa kadha. Mojawapo ya vitabu hivi ni kitabu cha Mwandishi mashururi Malachi Martin, kiitwacho The keys of this Blood. Martin ni Profesa wa Historia katika chuo cha mafunzo ya uaskofu na Biblia cha Vatican- Vatican's Pontifical Bible Institute: Yeye anasema kuwa athari za Kaballa zadhirihirika wazi kwa Wakomunisti. Katika mazingira ya kuatatanisha na kwa changamoto iliyoweka historia y awali ya Italia, ukaibuka mtandao wa jumuiya za kihumanisti. Jumuiya hizi, mwanzoni zilikuwa za siri. Mbali na usiri jumuiya hizi zilizkuwa na sifa kuu mbili.

Sifa ya kwanza ni kwamba zilipinga tafsiri iliyozoeleka ya Biblia kama ilivyodumishwa na mamlaka za kikasisi na za kijamii na pili zilizpinga misingi ya kifalsafa na kitheolojia iliyotolewa na Kanisa kwa ajili ya maisha ya kijamii na kisiasa. Kwa kifupi jumuiya za kihumanisti zilizoundwa katika kipindi hicho zilizotaka kuingiza utamaduni mpya wenye mizizi ya Kaballa ndani ya utamaduni wa kikatoliki barani Ulaya. Zilikusudiya kuleta mabadiliko ya kijamii na kisiasa. Mbali na Kaballa katika msingi wa utamaduni huu mpya pia kulikuwa na itikadi za misri ya kale. Prof. Martin ameandika. Waasisi wa zile jumuiya za Kihumanisti walikuwa Waumini wa nguvu kuu- Mwasisi mkuu wa Ulimwengu-ambaye walimwakilisha kwa sura ya Tetragramatton-neno la herufi nne YHWH..(Wahumanisti) wakaazima alama nyingine –Piramid na jicho moja linaloona mambo yote..kutoka kwenye vitabu vya Misri. Wahumanisti Wanatumia dhana ya mkuu wa ulimwengu-Great Architect of the universe; Msamiyati unaotumiwa na Masoni hadi leo. Hii inaonesha kuwa lazima yawepo mahusiano kati ya Wahumanisti na Masoni.
 
Alama za Misri ya kale katika maskani za Masoni

Moja kati ya mambo muhimu yanayothibitisha uhusiyano kati ya Misri ya kale na Masoni ni zile alama zao. kwa Masoni alama ni kitu muhimu sana. Masoni wenyewe hubainisha maana ya falsafa yao kwa wanachama wao kwa njia ya alama. Masoni anayepanda ngazi kati ya ngazi 33 za mamlaka ya kimasoni hujifunza maana mbalimbali za kila alama katika kila hatua. sote twajua kuwa Masonri huelezea dhana zake na maadili yake kwa njia ya alama na hadithi yaani tamthilia. Tamthilia hizi hurejea historia ya zama za nyuma. Twaweza hata kusema kuwa zinagusia hekaya za nyuma kabisa ya historia. Kwa utaratibu masonri imeonesha mambo ya kale ya mafundisho yake. Dhana za Wamisri wa zamani ndizo zinazowakilishwa na alama hizi . Kila mahala katika maskani za masoni na mara kwa mara katika machapisho ya masoni michoro ya mapiramidi na masanamu huonekana. Iwapo tutaichagua Misri ya kale kuwa ni jamii kongwe zaidi, sidhani kama tutakuwa tumekosea. Isitoshe ule ukweli kuwa ibada, na falsafa inayokutikana katika Misri ya kale ndiyo hiyo hiyo iliyomo katika masonri, unavuta hisia zetu. Katika zama za kale za Misri ibada za awali katika hekalu la Memphis zilizodumu kwa muda mrefu, zilifanywa kwa mazingatio makubwa na shauku kubwa na zimeonesha mlingano na ibada za kimasoni. Hebu tuiangalie mifano michache ya uhusiano kati ya Misri ya kale na masoni.

Piramidi chini ya jicho; Alama mashuhuri kabisa ya masoni inaonekana katika nembo (ngao) ya Taifa la Marekani. Katika nembo hii kuna nusu Piramidi ambapo juu yake kuna jicho ndani pembe tatu. Jicho hili ndani ya pembe tatu ndiyo alama ya kudumu inayokutwa katika maskani za masoni na katika machapisho yao yote. Idadi kubwa ya maandiko yanayozungumzia masoni husisitiza ukweli huu. Lile Piramid chini ya jicho ndani ya pembe tatu lenyewe lina mvuto mdogo sana. Hata hivyo piramidi hili lina maana kubwa mno ya kufahamia falsafa ya masoni. Mwandishi ya kimarekani Robert Hieronimus amendika tasnifu ya kiitikadi juu ya nembo ya Marekani ambapo ametowa maelezo muhimu sana. Anuwani ya tasnifu ya Hieronimus ni “An Historic Analysis of the Reverse of the America great seal and its relationship to the Ideology of Humanist Psychology” (utafiti wa kihistoria wa siri ya nembo kuu ya Marekani na uhusiano wake na itikadi ya saikolojia ya kihumanisti). Tasnifu yake inaonesha kuwa waasisi wa America ambao kimsingi walitumia nembo hiyo walikuwa ni Masoni na hivyo waliiunga mkono falsafa ya kihumanisti. Uhusiano kati ya falsafa hii na Misri ya kale unabainishwa na alama ya Piramidi iliyowekwa katikati ya nembo hiyo. Piramid hili linawakilisha Piramidi la Cheops moja ya minara mikubwa kabisa ya Firauni.

Maana ya nyota ya pembe sita ya Masoni;Alama nyingine mashuhuri ya masoni ni nyota yenye pembe sita iliyoundwa kutokana na pembe tatu kuwa juu ya pembe tatu nyingine. Hii pia ni alama ya utamaduni wa Wayahudi na leo hii inaonekana kwenye bendera ya Israel. Inafahamika kuwa kwa mara ya kwanza Nabii Suleiman aliitumia kama nembo. Hivyo basi nyota ya pembe sita ni nembo ya Nabii na alama ya kiungu lakini Masoni wana dhana tafauti. Wao hawaikubali nyota ya pembe sita kama alama ya Nabii Suleiman, bali wanasema ni alama ya itikadi ya kipagani ya Misri ya kale. Makala yenye kichwa ‘Allegory and symbols in our Rituals’ [Isitiari na alama katika ibada zetu] iliyochapishwa katika jarida la Mimar Sinan, inaelezea mambo mengi kuhusu jambo hilo kama ifuatavyo; mchoro wa alama mbili za pembe tatu moja juu ya nyingine unaonesha kuwa zina thamani sawa. Alama hii inayotumiwa na Masoni inajulikana kama nyota ya Daud, ni mchoro unaotokana na alama moja ya pembe tatu kuwa juu ya alama nyingine ya pembe tatu, leo hii inajulikana kama alama ya Uyahudi na inaonekana katika bendera ya Israel lakini ukweli ni kuwa asili ya alama hii ni Misri ya kale. Nembo hii kwanza kabisa ilitengenezwa na Matempla, ambao waliitumia kama urembo katika nakshi za kuta za Makanisa yao. Hii ni kwa sababu wao ndio walikuwa watu wa kwanza kugundua mambo muhimu kuhusu Ukristo mjini Jerusalem. Baada ya Matempla kusambaratishwa alama hii ikaanza kutumika katika Masinagogi. Lakini kwa Masonri bila shaka tunaitumia alama hii kwa maana ya jumla ya Ulimwengu mzima kwamba ilitokea katika Misri ya kale. Kwa maana hii tumeunganisha nguvu mbili pamoja. Kwa kweli hatuna budi kuzitafsiri alama zote za masoni kwa mnasaba wa hekalu la Selemani. Kama ilivyobainishwa na Qur’an Selemani alikuwa Nabii ambaye baadhi ya watu walitaka kumpaka matope na kuonesha kwamba hakuwa Muumini wa Mungu mmoja. Katika aya hii ya Qur’an Mwenyezi Mungu anasema; “Wakafuata yale waliyoyafuata mashetani, wakadai yalikuwa katika Ufalme wa Nabii Suleiman, na Suleiman hakukufuru” [2:202]. Masoni wamejenga dhana hii kimakosa kwa kumsingizia Nabii Seleman kuwa ni muwakilishi wa itikadi za kipagani za Misri ya kale kwa sababu hiyo wanampa nafasi muhimu katika itikadi zao. Katika kitabu chake “The occult Conspiracy” mwanahistoria wa kimarekani Michael Hoarld anasema kuwa tangia zama za kati, Suleiman (astaghfirullah!) amekuwa akisadikiwa kama “mchawi” na kwamba yeye ndiye aliyetumbukiza mawazo ya kipagani ndani ya dini ya Uyahudi!

Hoarld anaendelea kueleza kuwa masoni wanaliitakidi hekalu la Seleman kuwa ni hekalu la kipagani, na kwa sababu hiyo ni muhimu kwao. Picha hii potofu anayopachikwa Nabii Seleman, ambaye alikuwa mja mnyenyekevu na mtiifu kwa Allah (s.w) inabainisha misingi ya Masonry.

Alama ya nguzo mbili; Alama nyingine muhimu katika maskani ya Masoni ni ile ya nguzo mbili katika lango la kuingilia. Maneno “Jachin” na “Boaz” yamechongwa juu ya nguzo kwa kuiga nguzo mbili kwenye lango la hekalu la Selemani. Lakini kwa kweli Masoni hawana maana kuwa nguzo hizi ni alama ya kumbukumbu ya Seleman bali ni ishara ya mambo ya kumuhujumu Seleman. Chanzo cha nguzo hizi ni Misri ya kale. Makala yenye kichwa ‘Allegory and symbols in our Rituals’ inaeleza hivi; kwa mfano nchini Misri Horus na Set walikuwa waanzilishi pacha na washikiliaji wa mbingu. Nguzo mbili katika maskani zetu asili yake ni Misri ya kale. Moja kati ya nguzo hizi ilikuwa kusini mwa Misri katika jiji la Thebes, na nguzo nyingine ilikuwa kaskazini katika mji wa Heliopolis. Katika lango la kuingilia hekalu la Amenta lililotengwa kwa ajili ya Ptah Mungu mkuu wa Misri kulikuwa na nguzo mbili kama zile zilizopo kwenye hekalu la Selemani.Katika riwaya za kale zinazohusu Jua nguzo hizo zinatajwa zikipewa majina ya akili na kipawa.
 
Istilahi za Kimisri zitumiwazo na Masoni

Katika kitabu chao, The Hiram Key, Masoni wa Kiingereza Christopher Knight na Robert Lomas, wanaonesha mizizi ya Masoni katka jamii ya wamisri wa zama zilizopita. Jambo muhimu wanalofichufua ni kuwa maneno yatumikayo katika hafla ya kumpandisha masoni ngazi iitwayo Master Mason ni; ma’at-neb-men-aa,ma’at-baa’ na. Knight na Lomas wanaeleza kuwa maneno haya, mara nyingi hutumiwa bila kuzingatia maana yake, lakini ni maneno ya Wamisri wa zama za nyuma, ambayo yana maana hii; “Great is the established master of freemasonry, great is the spirit of Freemasonry” “Aliyepandishwa ngazi ya masta Masoni juu, juu zaidi, mori wa masoni juu, juu zaidi”

Waandishi hawa wanasema kuwa neno Ma’at maana yake ni ufundi wa majengo[maboma] na tafsiri ya karibu zaidi ya neno hilo ni masonry yaani uwashi. Hii ina maana kuwa Masoni wa hivi leo bado wanaienzi lugha iliyotumika maelfu ya miaka iliyopita katika Misri ya zama hizo.
 
Filimbi ya wachawi ya Mozart

Mojawapo ya vitu vilivotengenezwa na Masoni ni filimbi ya wachawi magic flute, huu ni wimbo wa mtunzi mashuhuri wa nyimbo aliyeitwa Mozart. Mozart alikuwa Masoni. Ni jambo linalofahamika kuwa sehemu kubwa ya wimbo huo ina ujumbe wa Masoni. Na ujumbe huu unanasibiana kwa karibu na upagani wa Misri. Jarida la Mimar Sinan linafafanua jambo hili kama ifuatavyo;

Yafahamika kuwa, kuna uhusiano wa wazi kati ya ibada za Misri ya zama za nyuma na ibada za Kimasoni. Hata wakijaribu vipi wale wanaojaribu kuitafsiri filimbi ya wachawi kwamba eti ni hadithi tu kuhusu mashariki ya mbali, lakini msingi wake ni ibada za Wamisri. Ni miungu wa kiume na wa kike wa mahekalu ya Misri ambao wameshajiisha utunzi wa maneno ya filimbi ya wachawi.
 
Minara ya pembe nne iliyochongoka juu

Alama nyingine muhimu ya Masoni ni obelisk. Huu ni mnara mrefu wa pembe nne , umechongoka kwa juu, ambao ni sehemu ya ubunifu majengo wa Misri ya kale. Piramidi ndio ncha ya mnara huu. Minara hii ilichongwa na wasanii wa uchongaji wa Misri ya kale. Kwa karne nyingi ilikuwa imezikwa chini hadi pale ilipokuja kuoenekana mnamo karne ya kumi na tisa. Ikahamishiwa kwenye miji mikuu ya nchi za Magharibi kama vile New York, London na Paris.

Mnara mkubwa kabisa kuliko yote ulipelekwa Marekani. Mpango wa kuupeleka huko ulifanywa na Masoni. Hii ni kwa sababu minara hiyo pamoja na michoro yake inadaiwa na Masoni kuwa ni alama zao halisi. Jarida la Masoni linataja mnara wenye urefu wa mita 21 uliopo New York. Mfano hai wa minara hii ni mnara uitwao Cleopatra’s needle, uliotolewa na Gavana wa Misri bw. Ismail kama zawadi kwa Marekani mwaka 1878. Mnara huu hivi sasa upo katika eneo la center park la NewYork. Sehemu yake ya chini imesilibwa kwa nembo za Kimasoni. Huu ni mnara ambao kwanza kabisa uliirikwa mnamo karne ya kumi nasita kabla ya Yesu, kwenye lango la kuingilia ndani ya hekalu la Sun god katika eneo la Heliopolis.
 
Hadithi ya mjane

Dhana muhimu ya utambulisho wa Masoni ni ile ya mjane. Masoni hujiita watoto wa mjane, na picha za wajane mara nyingi huonekana katika machapisho yao. Ni nini chanzo cha dhana hii? Huyu mjane ni nani? Tunapoyapekua maandiko ya Masoni, tunaona kuwa alama ya mjane kimsingi inatokana na hadithi ya paukwa pakawa ya Wamisri wa zamani za kale. Hii ni hadithi ya Osiris na Isis. Osiris alikuwa mungu wa kimila na Isis ndio mkewe. Kwa mujibu wa hekaya hii, Osiris alikuwa muhanga wa kifo cha mahaba “a victim of a crime of passion”ambapo Isis akawa mjane. Kwa hiyo mjane huyo wa Masoni ni Isis.

Makala moja katika jarida la Mimar Sinan inalifafanua jambo hili kama ifuatavyo; Hadithi ya Osiris na Isis inazungumziwa sana katika makala nyingi na katika mihadhara mingi. Ni moja ya hadithi za Misri ya kale zinazohusishwa mno na Masoni. Sifa ya kuwa kasisi wa hekalu la Isis ni ile ya mtu kuwa na uanachama wa masoni. Humo mwangaza wa jua huwa tunu muhimu ili mtu azikwe kwenye giza la mashariki, kila siku jua la asubuhi linapoanza kutua mchana, hufanya kazi ya Osiris , kama vile Horus kwa nuru yake kubwa, alivyochukua nafasi ya baba yake aliyeuawa. Hivyo mjane ambaye watoto wake ni sisi si mwingine zaidi ya Isis mjane wa Osiris. Tunaona kuwa masonri ambayo inajieleza kuwa imejengeka kutokana na akili na sayansi, kwa kweli ni hadithi ya paukwa pakawa iliyojaa imani za ajabu ajabu za uchawi.
 
Bikari na pimamraba

Bikari (compass) na pimamraba (square) ni miongoni mwa alama mashuhuri za masoni. Bikari huwekwa juu ya pimamraba. Masoni wanapoulizwa juu ya alama hii, husema kuwa alama hiyo huwakilisha dhana za sayansi, jiometri na kipawa cha akili. Lakini kwa kweli alama hizo zina maana nyingine kabisa.

Tunaweza kuiona maana hii katika kitabu kilichoandikwa na mmoja wa Masoni mashuhuri, Albert Pike. Katika kitabu chake kiitwacho Marals and Dogmas, ameandika hivi; Pimamraba … ni alama ya kimaumbile inayowiyana na duniya hii. Ni alama ya mke na mume. Ni alama ya asili mbili ambayo hapo kale ilihusishwa na mungu,,… Braham na Maya kwa Waariyan, Osiris na Isis kwa Wamisri. Kwa vile jua ni dume basi mwezi ni jike.

Hii ina maana kuwa pima mraba na bikari , nembo mashuhuri ya masoni, ni alama ya wapagani wakiariyani ambayo historia yake inaanzia Misri ya kale kabla ya Ukristo. Mwezi na Jua katika nukuu hiyo ya Pike ni alama muhimu katika jumuiya ya Masoni na haina maana nyingine zaidi ya kuwa kielelezo cha imani potofu za jamii za kale ambazo ziliabudu mwezi na jua.
 
Falsafa ya kipagani ya masoni

Hadi hapa tulipofika, tumejifunza kuwa misingi ya masoni imeegemeya itikadi ya kipagani inatokeya Misri ya kale na kwamba huko ndiko inakofichama maana halisi ya dhana na alama za masoni. Kwa sababu hiyo, masoni wanapingana na dini zinazoamini mungu mmoja. Masonri ndio itikadi ya wahumanisti, walahidi, na wanaevolusheni. Mwana historia wa Kiamerika, Michael Hoard anaielezea siri hii ambayo hufichuliwa kwa masoni wa ngazi za juu tu. Kwa nini Wakristo wanaikosoa Frimasonri?….. Jibu la swali hili lipo katika siri za Frimasonri. Laiti “siri hizi” zingetolewa hadharani, inatia shaka kama maana ya “siri hizo” ingeliweza kueleweka kwa wale ambao hawakuyajua mafundisho ya jamii za kichawi na dini ya kale. Kwa kweli yatia shaka kama wadau wa kawaida wa masoni wanaelewa “siri hizi” zinawakilisha nini. Katika duru za ndani za masoni, Inner cicle of Masonry, miongoni mwa wale waliopata daraja za juu, wamo wanaoelewa kuwa, wao ni warithi wa utamaduni wa kale uliokuwepoa kabla ya Ukristo ambao ni wa zama za upagani. Tukitazama andiko la masoni wa Kituruki, tunaona kuwa wale masoni wa ngazi za juu ndio tu wenye kujua mambo ambayo wenzao wengine wanafichwa. Masta masoni Necdet Egeran anaelezea jinsi masoni wa ngazi za juu wanavyolitazama jambo hili.

Kwa upande mwingine, Frimasonri ni Shirika jingine la Wayahudi. Uanachama wa Shirika hili umegawanyika katika ngazi mbalimbali zinazoitwa “Degrees.” Ili kuingia katika kila ngazi , kuna sheria na kanuni mahususi zinazoambatana na masharti maalum. Mtu anayehusika na ngazi fulani anaweza tu kusuhubiana na mwanachama wa ngazi hiyo hiyo na uhusiano huu hutazamwa kwa makini sana kiasi kwamba mdau anayehusiana na ngazi fulani hawezi kusikia mipango, shabaha wala malengo ya siri ya wadau wa ngazi nyingine.

Malengo ya ngazi za juu za Frimasonri yanafichwa na kuhifadhiwa kwa siri kubwa kwenye faili nyeti mno kiasi ambacho mtu anaweza kupitisha hata maisha yake yote ndani ya shirika hili bila kuambulia kitu. Mbinu za jumuiya hii na njia za ufanyaji kazi wake ni za siri kubwa kiasi kwamba Encyclopedia Britannica ambayo ina habari nyingi juu ya masuala mengi, imelazimika kukiri kuwa ushahidi ni haba sana kuwezesha undani wa lodges kung’amuliwa. Kumbukumbu za lodge na mambo yanayoihusu “zinafichwa” kwelikweli ambapo wale wasio wanachama hawawezi kusikia hata neno moja kuhusiana zao. Wanachama Frimasonri huwasiliana kwa mfumo maalum wa maandishi (code) na huwatambua wanachama wenzao kwa mfumo wa siri wa alama na maneno. Pia wana utaratibu wa kivyao wa kubishiana (kupigiana) hodi milangoni mwao ambapo wenyewe huweza kutambuana haraka hasa wanapokuwa katika nchi za kigeni.

Mdau Frimasonri anapofanya ziara katika nchi ya kigeni, hahitaji utambulisho rasmi kwa wadau wenzie mahala popote pale. Yeye anachohitaji ni kuwa na anuani tu kisha ule utaratibu maalum wa kupiga hodi humfanya yule aliyemo chumbani kutambua na kwenda mlangoni kumkaribisha. Katika mikusanyiko na mikutano na katika hafla ndani ya nchi mbalimbali wao hutambuana na kusabahiana bila shida yoyote na bila kusemeshana hata neno moja. Hujuana na kusalimiana kwa njia ya alama, maneno ya siri, ishara na uchezeshajichezeshaji wa mikono na viwiliwili vyao. Kwa mfano alama yao kuu ni pembe tatu ambayo wenyewe huuita EYE.

Iwapo Masoni yupo katika mazingira ya ugenini na anataka kujua kama kuna wenzie wangapi katika hafla ya kijamii na kadhalika au kama yeye ndiye anayetaka kujitambulisha kwa masoni waliopo kwenye umati wa watu, kitu pekee anachotakiwa kufanya ni kuweka vidole vyake vya mkono katikati ya vifungo[vishikizo] vya koti lake au kizibao chake na kufanya alama ya pembe tatu kwa vidole vyake kwa upande mmoja na pindo la koti kwa upande mwingine. Wanachama wenzie wote waliopo hapo mara moja watamuitikia kwa ishara na pia kila mmoja atawajua wengine bila kusemeshana neno. Masoni hupendelea kuwaingiza katika jumuiya yao Viongozi wakuu wa nchi, Viongozi wa kiraia au viongozi wa kijeshi au Vigogo wa makampuni ya biashara ya wenyeji na wageni. Hakuna kipingamizi cha tabaka,rangi , dini wala utaifa katika kujiunga na jumuiya hiyo.

Bali viongozi wa nchi hushawishiwa zaidi na wakitiwa mkononi, huendeshwa kwa mujibu mpango uliowekwa. Wanatumiwa kwa namna ambayo wenyewe hawawezi kuyatambuwa malengo yaliyofichikana ambayo yanatimizwa kupitia kwao. Pengine kuna watu wawili watatu tu au pengine hakuna hata mmoja mwenye asili ya utaifa wa kiyahudi ambaye ni mwanachama wa umoja huu wa siri katika nchi. Lakini jumuiya daima hutimiza malengo ya Uzayuni [mtandao wa kimataifa wa wayahudi]. Jumuiya hii kwanza ilianzishwa Uingereza mnamo mwaka 1717. muungano wa lodges zipatazo nne ukaunda Lodge kuu grand lodge mjini London pamoja mfumo mpya wa alama za siri. Kuhusiana na kazi na majukumu ya Masoni, pitio la itifaki litafichua ukweli. Haya ni maelezo yanayobainisha kila kitu, na serikali inayotaka kuinusuru nchi yake na hatari ya malengo ya chombo hiki chenye nguvu na ushawishi, basi haina njia nyingine ila kuking’olea mbali. Hapana shaka hiyo haitakuwa kazi rahisi kwani mizizi ya shirika hilo imeota ndani kabisa ya mfumo wa serikali ya nchi. Kwa kweli mikono ya masoni ni mirefu mno.
 
Freemason,kimsingi ni ant christ,ambao kwa wale wasomaji na wanaoamini bibilia watakuja,na ndio wanaoratibu swala zima la kuwa na SERIKALI MOJA YA DUNIA,Ili watakaporuhusiwa iwe rahisi kwao kuendelea na mipango yao.Kuna ushahidi wa kutisha kabisa jinsi wanavyoratibu shughuli zao,kisayansi,
 
Freemason,kimsingi ni ant christ,ambao kwa wale wasomaji na wanaoamini bibilia watakuja,na ndio wanaoratibu swala zima la kuwa na SERIKALI MOJA YA DUNIA,Ili watakaporuhusiwa iwe rahisi kwao kuendelea na mipango yao.Kuna ushahidi wa kutisha kabisa jinsi wanavyoratibu shughuli zao,kisayansi,


Na wanaoTAMBIKA na kuamini mizimu je?
 
Masoni maana yake ni kuachana na dini

Tunapoyatupiya macho maandiko ya Masoni, tunaona kuwa Masoni wa ngazi za juu wanaelewa mambo ambayo wenzao wa ngazi za chini wanafichwa wasiyajuwe. Masoni wa ngazi ya juu aitwaye Necdet Egeran anafafanuwa kuwa;

Baadhi ya Masoni huelewa kuwa Mansori ni aina ya nusu-dini na nusu -Taasisi ya hisani ambapo wanaweza kujenga uhusiyano na kuyaendesha kwa utaratibu huwo. Wengine wanadhani kuwa Lengo la Masonri ni kuwafanya watu wawe tu wema zaidi. Aidha wengine wanaona kuwa Mansori ni Taasisi ya kujenga maadili. Kwa kifupi wale wasiojuwa kusoma wala kuandika lugha ya Masoni wanaelewa alama na hekaya za masoni kwa maana hii au kwa maana iliyosawa na hii. Lakini kuna masoni wachache sana wanaoweza kujuwa undani wa mambo.

Mansori iko tafauti kabisa na malengo hayo. Mansori maana yake ni Elimu ya ufunuwo, kujibuwa na kuanza upya. Maana yake ni kuachana na utaratibu wa zamani wa maisha na kuingiya katika maisha mapya na matakatifu zaidi. Katika siri ya chimbuko la Masonri na katika msingi wa dhana ya alama, kuna msururu wa siri zinazotusaidiya kuingiya katika maisha ya ndani zaidi na kujuwa siri ya maisha yetu. Hivyo, ni katika maisha haya ya ndani zaidi na kwa kuingiya katika maisha hayo ndipo inapowezekana kupata elimu ya Masonri. Hapo tu ndipo inapowezekana kuujuwa undani na nyendo za maendeleo na mageuzi.

Nukuu hiyo inabainisha kuwa japo Masoni wachache wa ngazi ya chini huwona kuwa masonri ni Taasisi ya hisani na ya kijamii, lakini kwa kweli inahusiyana na siri za maisha ya Mwanadamu yaani haiba ya nje ya mansori kama shirika la hisani na la kijamii, kwa kweli ni mwavuli tu wa kufunika falsafa ya jumuiya hiyo. Kwa uhalisi wake Mansori ni shirika lenye shabaha ya kushajiisha falsafa fulani kwa wadau wake na kwa watu wengine kwa kutumiya mfumo maalumu. Kama tulivyosema mwanzoni, kipengele cha msingi cha falsafa hii ambacho kimepandikizwa kwa masoni kutoka tamaduni za kipagani hasa hasa upagani wa Misri ya kale ni Ukafiri.
 
Ukafiri katika vitabu vya Mansori

(1) Imani juu ya maada inayojitegemeya

Mansoni wa hivi leo , kama walivyokuwa mafirauni, makuhani na matabaka mengine ya jamii ya Misri ya zamani, huamini umilele wa maada na dhana ya maada kutoumbwa na Mungu Muumba, na kwamba kutokana na maada hii isiyo na uhai, viumbe hai vikazuka kwa bahati nasibu. Katika maandiko ya Masoni, tunapata maelezo ya kina ya vipengele vya msingi vya falsafa ya ukafiri. Katika kitabu chake, Mason luktan Esin meleler (Funuwo za Frimasonri, Masta Mason Selami Isindag ameandika kuhusu falsafa hii ya ulahidi:

“Anga lote, angahewa, Nyota, Silika, vitu vyote vilivyo hai na visivyo hai vinajengwa na Atomu. Wanadamu si chochote bali ni mkusanyiko tu wa Atomu uliojizukiya wenyewe kibahati bahati. Ule Urari katika mtiririko wa umeme kwenye Atomu ndio unaouhakikishiya uhai viumbe hai. Pale urari huu unapovurugika, ndipo tunapokufa, tunarejeya udongoni na kusambazika katika chembechembe za Atomu.

Yaani sisi viyumbe tumetokana na Atomu na nishati, na tutarudi tena katika maada na nishati. Mimeya hutumiya Atomu zetu na viumbe vyote hai tukiwemo sisi hutumiya mimeya. Kila kitu hutengenezeka kwa vitu hivyo. Lakini kwa vile ubongo wetu umekuwa zaidi ya wanyama wote, akili ikazuka. Tukiyangaliya matokeyo ya uchunguzi wa kisaikolojiya, tunaona kuwa maisha ya utu wetu wenye sehemu tatu za hisiya, akili na hiyari ni matokeo ya utendaji kazi madhubuti wa seli katika tabaka la nje la ubongo na homoni.

....Sayansi yakinifu inakubali kuwa hakuna kilichopata uhai kutokana na hamna kile na hakuna kitakachotoweka kabisa kabisa. Kwa hiyo yaweza kuhitimishwa kuwa hakuna muweza yeyote ambaye watu wanahitaji kumshukuru na kuwajibika kwake.

Ulimwengu huu ni mkusanyiko tu wa nishati isiyo na mwanzo wala mwisho. Kila kitu kinazalishwa kutokana na mkusanyiko huu wa nishati, huibuka na kufa lakini hakitoweki moja kwa moja. Vitu hubadilika na kubadilika hali na muundo. Hakuna mambo kama vile kifo au kutoweka; Yapo tu mabadiliko yanayoendeleya daimadumu, mabadiliko ya hali moja kwenda nyingine na mabadiliko ya muundo wa kitu. Lakini ni vigumu kulifafanuwa jambo hili kubwa na ni vigumu kufafanuwa siri za ulimwengu kwa kutumiya kanuni za kisayansi. Lakini fafanuzi nyingine zaidi ya zile za kisayansi ni yale maelezo yatokanayo na njozi tu, imani tu ya kibubusa na tena ni Imani ya kipumbavu. Kwa mujibu wa sayansi yakinifu na hoja ya kiyakili, hakuna roho inayotengana na mwili.

Hapa msomaji ataona fikra zinazofanana kabisa na zile za vitabu vya wanafikra wanaokanusha Muumba kama vile: K. Marx , F,. Engels, B. I. Lenin, G.Politzer, C.Sagan na J. Monod. Wote hawa wanaamini dhana ya msingi ya ulahidi kuwa ulimwengu umekuwepo wakati wote. Maada ndiyo muhimili pekee wa maisha. Wanadamu wanajengeka kwa maada na hawana roho. Maada ndiyo iliyomjenga mtu ndani na nje na uhai ukatokeya kwa bahati nasibu. Ni sahihi kutumiya neno dhana kwani kinyume na dai la Isindag kuwa maelezo haya yanatokana na sayansi yakinifu na hoja ya kiakili, fikra zote hizi zimebatilishwa (zimefutiliwa mbali) na vumbuzi za kisayansi katika nngwe ya pili ya karne ya Ishirini.

Kwa mfano nadhariya ya mlipuko mkuu inayokubalika katika duru za kisayansi kuwa ni sahihi, inabainisha kisayansi kwamba ulimwengu uliumbwa kutokana na hamna mamiliyoni ya miyaka iliyopita. Kanuni za ‘Thermodynamics’ zaonesha kuwa maada haina uwezo wa kujipangiliya yenyewe na kwamba Urari na mpangiliyo uliyopo ulimwenguni ni matokeyo ya kazi ya uumbaji iliyofanywa kwa nguvu yenye utambuzi. Kwa kule kubainisha kwake usanii wa kuajabisha katika viumbe hai, Baiolojiya inathibitisha kuwepo kwa Muumba aliyeumba vyote1. Katika makala yake moja, Isindag anazidi kufafanuwa kwamba, kwakweli Masoni ni Wakanusha Mungu na kwa hivyo ni wapinzani wa Dini zinazoamini Mungu na kwamba wanatumiya dhana ya Great Architect Of the Universe kwa maana ya Evolusheni ya Maada:
Kwa kifupi sana, nataka kugusiya kanuni na dhanna fulani zinazofuwatwa na Masoni: Kwa mujibu wa Masonri, uhai huwanza na seli moja, inayojibadilsha na kugeuka kutoka hali moja kwenda nyingine na kuendeleya hivyo hivyo hadi kuwa mtu. Chanzo, au sababu, au lengo au mazingira ya mwanzo huu hayawezi kufahamika.
Maisha hutokana na mchanganyiko wa maada na nishati na kisha hurejeya tena katika vitu hivyo. Anasema endapo tutakubali kuwa Great Architect of the Universe ndiyo msingi mkuu na ndiyo upewo usiyo ukomo wa wema na uzuri, na kuwa ndiyo kilele cha evolusheni, na kuwa ndiyo hatuwa yake kuu kabisa na ndiyo lengo ambalo wanadamu wahangaike kuliendeya, na kama hatulipi sifa ya umbile, basi twaweza kuepukana kabisa na itikadi za kibubusa. Kama tuonavyo, moja ya misingi mikuu ya falsafa ya Masoni ni kwamba vitu hutokana na maada na hurejeya tena katika maada. Muhimu katika mtazamo huu ni kuwa, Masoni hawaioni falsafa hii kama ipo kwa ajili yao tu; bali wanataka kusambaza mawaza haya katika jamii zote. Isindag anaendeleya;

Masoni aliyepata mafunzo kwa misingi ya itikadi hizi huikubali dhima ya kuelimisha watu... Na kuwaadilisha kwa kuwafundisha misingi ya hoja na sayansi yakinifu. Kwa utaratibu huwo, Masonri huenezwa kwa watu, hufanyakazi kwa niyaba ya watu licha ya watu wenyewe kuwepo. Maneno haya yanabainisha vipengele viwili vya jukumu la Masoni katika jamii:

Mosi, chini ya mwavuli wa Sayansi yakinifu na hoja, Masoni hujaribu kupandikiza katika jamii falsafa ya kilahidi ambayo ni dhana ya Misri ya kale. Pili, wanakusudiya kufanya hivi bila kujali watu. Yaani hata kama jamii inaamini Mungu na haina utashi wa kuikubali falsafa ya kilahidi, Masoni watakazana tu kufanya jitihada za kuubadili mtazamo wa watu juu ya ulimwengu bila ridhaa yao. Kuna jambo muhimu ambalo hatuna budi kulitiliya maanani hapa. Lugha ambayo Masoni huitumiya ni ya ghiliba. Katika maandiko yao hasa hasa yale yanayolengwa kwa watu wa jamii nyingine, huwa wanatumiya lugha inayokusudiya kuonesha kuwa falsafa yao haina ubaya, ni ya busara na stahamala.

fano wa hili waweza kuonekana katika nukuu ya hapo juu. Katika dhana ya kuwabadilisha watu kwa kuwafundisha misingi ya hoja na sayansi yakinifu. Kwa kweli falsafa ya Masoni haihusiyani kabisa na sayansi wala hoja. Yenyewe inahusiyana na dhana ya kale ambayo inavuma kwa sura ya sayansi. Si lengo la Masoni kuwaadilisha watu bali kusudiyo lao ni kupandikiza watu falsafa yao. Kwa kukamiya kwao kuwa watafanya hivyo hata bila ya ridhaa ya watu, tunaona kuwa wao si watu wenye stahamilivu. Ikiwa ni sehemu ya itikadi zao za kilahidi, Masoni wanakanusha kuwepo kwa roho na maisha baada ya kifo. Masoni hawaamini kuwepo kwa roho ya binadamu na wanapinga kabisa imani ya kuwepo kwa maisha mengine baada ya kifo.

121.jpg
 
Mkuu , unachosema ni kweli kabisa hawa jamaa wamepania kuivuruga dunia , maana wameingia katika dini nyingi tu na wanafanya mambo tofauti kabisa ili kuvuruga watu , mfano mambo ya ushoga na usagaji makanisani na mpaka wachungaji kukubalika inastaajabisha sana , makanisani mapadre,wachungaji na viongozi mbalimbali wanatamka wazi kabisa kama hujalipa michango yako HUPATI huduma huu ni upinga kristo kabisa Yesu Mwenyewe alishasema ukisaidia maskini umenisaidia mimi sasa hawa watu waliopewa dhamana ya kusimamia dini wanajifanyia miradi ya Fedha tu , shida kweli . Biblia nyingi zinatofautiaona sana siku hizi hata kama ni za dhehebu moja la kikristo watu wachunguze maneno yanapunguzwa ukali ,ni Kumuomba mungu atusaidie maana watu wengi kama wametiwa upofu wanatazama lakini hawaoni au hawajali kuhusu imani ya kweli kwa mungu , watu wanajenga mahekalu mazuri yaliyonakshiwa kwa vitu na vito vya gharama na kuvaa vizuri tu kudhuria hapo mahali kusali, yaani tunajaribu kupatakatifusha mahali tunaposalia , lakini andiko linasema mahekalu yenu na sala zenu ni kama kelele mbele za Mungu maana Mioyo yetu imejaa uovu tuu !
 
i havent found anything wrong with these guys
 
i don see any evil about them at least from the article, can some one point out what so evil about them, do they kill pipo o smthn? to be honest most pipo talk about them that they are evil though no one pointed out in what way? what is their mission?

I fully support this comment because it is to the point. I find that all the other comments are way off. Where did they get the information that free masonry is demonic. Wacheni uswahili, stick to facts.
 
i don see any evil about them at least from the article, can some one point out what so evil about them, do they kill pipo o smthn? to be honest most pipo talk about them that they are evil though no one pointed out in what way? what is their mission?

I fully support this comment because it is to the point. Other comments are filled with assumptions and uneducated guesses
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom