Freemasons Inside - Out: Who are they? How they operate? How to join them?

Freemasons Inside - Out: Who are they? How they operate? How to join them?

Status
Not open for further replies.
I had a readings also about Satanism but usually not as extensivelly as you did, i dont know if one is curious and brave enough, should try to draw those circles and symbols and call for the jinis to give them money
 
i don see any evil about them at least from the article, can some one point out what so evil about them, do they kill pipo o smthn? to be honest most pipo talk about them that they are evil though no one pointed out in what way? what is their mission?
 
WE NEED MORE FREEMASONS in Tanzania maana tutaendelea mbele,na nyie mnao link satan,devil or whatever seems hamna idea na hamsaidiki ila kuwasaidia tuu FREEMASONS HAWANA DINI na membership ni kwa yeyote ingawaje kuna namna ya kuingia
 
Principles of Freemasonry

Benjamin Franklin, himself a mason, described the principles and tenets of Freemasonry as follows:
“Freemasonry has tenets peculiar to itself. They serve as testimonials of character and qualifications, which are only conferred after due course of instruction and examination. These are of no small value; they speak a universal language, and act as a passport to the attentions and support of the initiated in all parts of the world. They cannot be lost as long as memory retains its power. Let the possessor of them be expatriated, shipwrecked or imprisoned, let him be stripped of everything he has got in the world, still those credentials remain, and are available for use as circumstances require. The good effects they have produced are established by the most incontestable facts of history. They have stayed the uplifted hand of the destroyer; they have softened the asperities of the tyrant; they have mitigated the horrors of captivity; they have subdued the rancor of malevolence; and broken down the barriers of political animosity and sectarian alienation. On the field of battle, in the solitudes of the uncultivated forest, or in the busy haunts of the crowded city, they have made men of the most hostile feelings, the most distant regions, and diversified conditions, rush to the aid of each other, and feel a special joy and satisfaction that they have been able to afford relief to a Brother Mason.”
Today as in past times, each lodge generally formally states its own basic principles. While the wording and the priorities may vary, however, most Masons agree on a few basic principles that are crucial to Freemasonry:
Charity

Most lodges emphasize philanthropic activities that are designed to improve the welfare and happiness of humankind. Some lodges organize special charity events, give money to specific individuals or organizations or set up scholarships.
Benevolence

All lodges practice treating others well.
Community

While each lodge is created from individual members and while individuality is treasured, lodges are designed to be sociable and to encourage mutual works. Brotherhood is a key tenet in lodges and that is one reason why Freemasonry is designed to allow men to meet together.
Morality

Good works and good actions are seen as essential in a Mason and personal character and righteousness are emphasized.
Education

Masons encourage education through well-stocked libraries, scholarships and other means. Many of the rites require study of the Sacred Law and various books.
Belief

While Freemasonry is not secular or theological, all ceremonies and rituals are based on the belief in a benevolent Supreme Being. Members must believe in such a Deity in order to join, although they can worship this deity as they wish and call him or her what they wish.
Truth and justice

Freemasons believe in the pursuit of justice as well as in helping and forgiving others. Some of the charitable work many lodges do may be designed to help bring justice to situations. Masons are encouraged to be truthful and honest with God, their Country, fellow men, their family and themselves. When becoming part of a lodge, most Masons have to swear not to take part in any act which threatens the peace and good order of society. Masons also sometimes must pledge to follow the law. Masons who are convicted of crimes may be ousted.
Beliefs of Freemasons

There is no one set of written Freemason beliefs and no central authority over Freemasons. Each region has its own Grand Lodge and smaller localities have their own local lodges. Although lodges are part of a larger organization, the members of each lodge ultimately decide what to believe in and what to emphasize. As a result, some lodges prioritize education and may be closely linked with a local university. Other lodges may put more focus on charitable works and may linked to a local organization or children’s hospital, where members devote a lot of energy.
Although there are differences in terms of what each lodge believes, all Masons are taught to believe in three main tenets:
Brotherhood

Known as the Golden Rule in Christianity, this basic tenet is the foundation of many world religions. At its simplest, it states “treat others well” or “treat others as you would like to be treated.” This principle is seen in Buddhism, Christianity, Confucianism, Hinduism, Islam, Judaism, Taoism, and other religions. Although Freemasonry is not a religion, it outlines the same tenet for its members to follow. Masons show their brotherhood by meeting together and by helping one another as needed.
Charity or Relief

While many religions teach that charity on earth brings rewards in the afterworld, Freemasonry teaches that charity improves the lives of people now. Masons are encouraged to help those who need it through good works and monetary contributions. Statistics suggest that Masons worldwide give $3 million every day to charity. US Masons alone provide $2 million daily. Freemasons support a range of charities – those providing relief for natural disasters, help for schools and relief to needy families. They also create scholarships for students. In addition, Masons provide help for members of their lodges. This help include building retirement homes for Masons, paying for some member funerals and building schools and homes for Masons’ children.
Truth

Truth is emphasized in every lodge, but it is a somewhat term that can mean many things. Many Masonic rituals and ceremonies involve the symbol of light, which in Masonic tradition represents spiritual truth and knowledge. Every Mason is expected to seek and find that light or knowledge individually. Each Mason is encouraged to seek knowledge and to educate themselves as well, since no Mason should be “in the dark” or ignorant. Therefore, truth can be understood to mean a quest for education. In addition, every Mason is expected to be honest with themselves, their country, their family, fellow Masons, and with mankind. Dishonesty or underhanded or illegal acts are not tolerated. Perhaps the easiest way to understand truth is to understand that Freemasonry believes in building a Mason’s character and the cornerstone of good character is honesty and truth in all its forms
 
Hapa(Belief) sasa ndio kuna confusion kwa wengi na anybody ambaye hajui anaweza kuita devil worship,satanic or anything lakini deinism haina tofauti sana na dini nyingine kama christianity,Budha etc kwani si dini zote zina worship something invisible figures like GOD,good deeds and life after death na ukiangalia vizuri America founders walioandika constitution yao walikuwa deity na hata laws nyingi tunazotumia waliandika wao,definition hapa [ame]http://en.wikipedia.org/wiki/Deity[/ame]

Belief
While Freemasonry is not secular or theological, all ceremonies and rituals are based on the belief in a benevolent Supreme Being. Members must believe in such a Deity in order to join, although they can worship this deity as they wish and call him or her what they wish
 
Kila mtu ana haki na uhuru wa kuabudu.
Tatizo lililopo kwa mtanzania ni kuamini kuwa anachoabudu yeye ndo halali na ndo yuko Mungu wa kweli.

sasa kuna watu wameponda sana habari za freemason, ile hali wao ama ndugu zao huwa wanafanya matambiko ya kifamilia au ya mtu mmoja mmoja huko ktk mizizi ya makabila yao pasipo kugundua kufanya vile ni sawa na kuabudu Miungu mingine.

Toa kwanza boriti lililopo jichoni mwako...
 
ULIMWENGU WA FRIMASONRI

Kwa karne kadhaa sasa kumekuwa na hofu, gumzo na minong'ono juu ya mitandao inayoendesha siasa za Ulimwengu kwa siri. Mitandao hiyo ni Freemansory na Mafya ambayo yote iko chini ya nguvu za uzayuni wa kimataifa. Maelezo haya yamejaribu kuielezea mitandao hiyo zaidi ikiwa kimejikita katika ule mashuhuri wenye jina la "Freemasonry" au kwa utohozi usiyo rasmi "Frimansori". Mtandao huu umejengwa na watu walioamua kujitoa muhanga wenye kuzingatia miiko na tahadhari zote ili kufanikisha lile walilolikusudia. "Frimansonri" ni tafsiri inayogeuza kidogo matamshi, inatanguliza n kabla ya s na kisha n. Freemansonry-Frimansori. Katika thread hii tutatumia tafsiri hii pamoja na neno Mafya.
 
Chimbuko la Frimasonri

Ufahamu walionao wanahistoria wengi ni kuwa chimbuko la shirika la “Frimansori” ni vita vya msalaba-Crusades, ukweli ni kuwa ingawa shirika hili lilianzishwa na kutambulika rasmi nchini Uingereza mwanzoni mwa karne ya kumi na nane, mizizi yake inaanzia nyuma katika karne ya kumi na mbili. Hata kama baadhi ya watu watang’ang’ania kiyasi gani kuwa vita vya msalaba vilikuwa ni misafara tu ya kijeshi iliyofanywa kwa jina la Ukristo, kimsingi, ilikuwa ni misafara iliyofanywa kwa minajili ya kupata maslahi ya kimali. Katika kipindi ambacho Ulaya ilikuwa ikikabiliwa na umaskini mkubwa na ufukara, mafanikiyo na utajiri wa mashariki ya kati uliwavutia sana wazungu wa Ulaya. Hii ndiyo ilikuwa sababu ya mabadiliko ya ghafla ya Wakristo wa Ulaya kutoka zile sera zao za utulivu na kuingia katika vita vya kijeshi. Mwanzilishi wa vita hivi vya msalaba alikuwa Papa Urban wa pili(Pope Urban II). Papa huyu aliitisha baraza lake, “Council of Clermont” mnamo mwaka 1095 ambapo ile itikadi ya awali ya utulivu waliyokuwa nayo Wakristo ikawekwa kando. Vikatangazwa vita vitakatifu kwa hila ya kuzipora nchi takatifu kutoka mikononi mwa Waislamu. Kufuwatia azimio la baraza hilo, Jeshi kubwa la wapiganaji wa vita hivyo likaundwa, likishirikisha askari wenye mafunzo ya kitaalamu na maelfu ya wapiganaji wa kujitolea. Wanahistoria wanaamini kuwa hila ya Papa Urban II ilitokana na tamaa yake ya kupata nafasi ya ugombea katika kinyang’anyiro cha Upapa. Tukumbuke kuwa mfumo wa uongozi wa kikatoliki chini ya Papa unatokana na tabaka la Umwinyi uliowakandamiza watu kwa kisingizio cha Dini.

Wafalme wa Ulaya na Warithi wao waliuafiki wito wa Papa kwa shangwe kumbe malengo yao yalikuwa ya kiduniya kama alivyosema Donald Queller wa Chuo Kikuu cha Illinos, wakuu wa Ufaransa walitaka tu kujiongezeya nchi. Nao wafanyabiashara wa kitaliano walitumai kupanua biyashara katika bandari za mashariki ya kati. Idadi kubwa ya watu masikini wakajiunga na misafara hiyo ili nao wakajikomboe kiuchumi kutokana na hali zao ngumu za maisha. Umati huu wa watu wenye uchu wa mali uliuwa Waislamu wengi na hata Wayahudi kila mahali ulipopita. Kwa sababu tu ya uchu wao wa kujipatia dhahabu na vito vya thamani, wanamgambo hawa wa Crusade walitumbua matumbo ya wale waliowauwa ili wapate dhahabu na madini ya thamani ambayo walidhani wahanga wameyameza kabla ya kufa. Uchu wao wa mali ulikuwa mkubwa mno kiasi kwamba hawakusita kufanya chochote. Baada ya safari ndefu na ngumu ya uporaji mwingi na mauaji makubwa dhidi ya Waislamu, genge hili lililoitwa la Wanamsalaba likafika Jerusalem mnamo mwaka 1099. Baada ya Jiji kuzingirwa kwa karibu majuma matano, Makruseda wakaingia ndani. Walifanya ushenzi makubwa sana. Waislamu na Wayahudi wa Jiji hilo walikatwakatwa mapanga. Mwanahistoria anasema, Waliwaua Waarabu, Waturuki wote waliowakuta humo, Wanaume kwa Wanawake mmoja wa Makruseda hao Raymond akajitapa kwa mauaji haya kwa kusema:

“Baadhi ya watu wetu walikatakata vichwa vya maadui zao, wengine wakawachoma mishale, wengine wakawatesa kwa kuwatupa kwenye moto. Malundo ya vichwa, mikono na miguu, yalionekana katika mitaa ya Jiji. Mtu alilazimika kukanyaga miili ya watu na farasi ili kupita njia. Lakini yote hayo ni madogo kulinganisha na ale yaliyotokea kwenye hekalu la Suleiman, mahali ambapo shughuli za kidini hufanyika. Katika hekalu hilo, watu walipita kwenye madimbwi ya damu, miguu ilizama hadi magotini.”
 
Historia ya Matempla

Kwa kifupi Matempla hawakutoweka kabisa bali falsafa yao. Imani zao na ibada zao bado zinaendelea chini ya mwavuli wa Frimansori. Dhana hii inatiwa nguvu za ushahidi mwingi wa kihistoria na hivi leo inakubaliwa na idadi kubwa ya Wanahistoria wa magaharibi ima awe Mafyoso au la. Katika kitabu chetu, The new Masonic Order, tumeutathmini kwa kina ushahidi huu. Dhana inayoihusisha mazizi ya Mansori na Matempla, mara nyingi inarejewa katika majarida yanachapishwa na Mansori wenyewe kwa ajili ya Wananchama wao. Wanachama wa Frimansori wanaikubali kabisa dhana hii. Mojawapo ya majarida hayo linaitwa Minnar Sinan(ni jarida la Mafyoso wa Uturuki) ambalo linaelezea uhusiano kati ya komandi ya Matempla na Frimansori kwa maneno yafuatayo”

“Mnamo mwaka 1312, pale Mfalme wa Ufaransa kwa shinikizo la kanisa alipolifunga komandi ya Matempla na mali zao kuwapa askari wa mtakatifu John mjini Jerusalem harakati za matempala hazikukoma. Idadi kubwa ya Matempala wakapata hifadhi katika maskani ya Frimansori iliyokuwepo Ulaya wakati huo. Kiongozi wa Matempla, Mabeignac, akiwa na wanachama wengine, wakapata usalama nchini Scotland chini ya mwavuli wa Wall builder na chini ya jina la Mac Benach. Mfalme Scotland Robert the Bruce akawakaribisha na kuwaruhusu kuwa na ushawishi mkubwa katika maskani za Frimansori nchini Scotland. Matokeo yake maskani za Scotland umuhimu mkuibwa kwa mtazamo wao wa kiufundi na fikra zao. Leo hii Mafyoso wanatumia jina la Mac Benach kwa heshima. Mafyoso wa Ufaransa waliorithi vitu vya Matempla wakareje zao Ufaransa miaka mingi baadaye na kuimarisha ngome yao ya kaaida ikijulikana kama kaaida ya Scotland(Scotish Rights).

Aidha, Mimar Sinan inatoa habari nyingi kuhusu uhusiano wa Matempla na Mafrimasonri. Katika makala yake iliyokuwa iliyokuwa na kichwa Templas and Frimanson inasema sala ya sherehe za uzinduzi wa Komandi ya Matempla ni sawa kabisa na sala Mafyoso wa zama hizi. Kwa mujibu wa makala hiyo hiyo, kama ilivyo katika Mansori wanachama wa Komandi ya Matempla wakiitana Brother(ndugu). Mwishoni mwa makala hayo tunasoma maneno haya; “komandi ya Matempla na shirika la Frimansoni yanashajiishana, kwa kiasi kikubwa hata sala za mashirika haya zinashabihiana kwa maana zimaigwa kutoka kwa Matempla. Kwa ajili hii, Mafyoso kwa kiasi kikubwa wamejifananisha na Matempla na yaweza kusemwa kuwa, kile kinachoonwa kuwa ni usiri mkubwa wa Frimansonri kwa kiasi kikubwa kimeigwa kutoka kwa Matempla. Kwa kufupisha hapa ni kuwa, kama tulivyoona twaweza kusema kuwa chanzo cha sanaa za Kifalme na usiri wa Frimansori chatokana na Matempla. Mwisho, tunasema kuwa imetokea huko nyuma kwa Matempla na kwamba Mafyoso wamefuata falsafa ya Komandi ya Matempla. Mafyoso wenyewe wanalikubali hili lakini jambo muhimu kwa tafakuri yetu ni nini asili au chanzo cha falsafa hii. Kwa nini Matempla waliachana na Ukristo na kufuata mafundisho mapya. Kitu gani kilichosababisha wafikiye uamuzi huo? Kwa nini walifanya mageuzi hayo kule Jerusalem na je kupitia tawi hili la Frimansoni kumekuwa na athari gani Duniyani kutokana na Falsafa hii iliyofuatwa na Matempla.
 
Matempla na Kaballa

Kitabu kilichoandikwa na Mafyoso Christopher na Robert Lomas kiitwacho The Hiram Key kinafichuwa mambo fulani ya kweli kuhusu mizizi ya Frimansori. Kwa mujibu wa Waandishi hawa, ni dhahiri kuwa Frimansori ni mwendelezo wa Matempla. Mbali na hivyo, Waandishi hawa piya, wameviangaliya piya vyanzo vya Matempla. Kulingana na dhanna yao, Matempla walipitia hatua kubwa za mabadiliko wakati walipokuwa Jerusalem. Mahala palipokuwa kwa Ukristo wao walianzisha madhehebu nyingine. Katika mzizi wa mabadiliko haya, kuna siri ambayo waliifichua ambayo ni hekalu la Suleiman pale Jerusalem ambalo mabaki yake, walitaka kuyachunguza. Waandishi hawa wanasema kuwa, Matempla walikuwa wakiutumia ule ulioitwa kuwa wajibu wao wa kulinda mahujaji wa Kikristo waliozuru pale Palestina lakini kumbe hiki kilikuwa kisingizio, lengo halisi lilikuwa jingine kabisa. Hakuna ushahidi kuwa wale Waasisi walikuwa wakitoa ulinzi kwa Mahujaji bali tulichokugundua ni kuwa kuna ushahidi mkubwa kuwa walikuwa wakichimbua chini ya mabaki ya hekalu la Herold. Waandishi wa kitabu cha Hiram Key sio wao pekee waliogundua vielelezo vya jambo hili. Gaetani De la Forge, Mwanahitoria wa Ufaransa naye ametoa maelezo kama haya; “jukumu halisi la Wale wanamgambo tisa wa Krusade walikuwa wakifanya utafiti katika eneo hilo ili kupata masalia na kupata kumbu kumbu za maandiko ya awali ambao yanachimbuko ya maelezo ya siri ya dini ya kiyahudi na Misri ya zama za kale.

Mwisho mwa karne ya 14 Charles Wilson wa Royal Engeneers alianza kufanya utafiti wa mabaki ya kale kule Jerusalem. Yeye akafka mahala pa kuona kuwa, Matempla walikuwa wamekwenda Jerusale kutaifiti mabaki ya hekalu. Wilson aligundua chimba chimba na fukua fukua china ya misingi ya hekalu na akahitimisha kuwa kazi hii ilifanywa kwa zana ambazo zilikuwa za Matempla.

Vifaa hivi vingalipo katika hazina ya mabaki ya kale ya Robert Brydon, ambaye anamiliki hifadhi ya kumbu kumbu zinazohusiana na Matempla. Waandishi wa kitabu cha the Hiram Key wanadai kuwa chimba chimba ya Matempla haikuishia matupu, kwamba ile Komandi iligundua kumbukumbu fulani pale Jerusalem ambayo ndiyo iliyobadili mtazamo wao. Mbali na hao watafiti wengine nao wana maoni hayo hayo. Yumkini lazima kulikuwa na jambo lililowapelekea Matempla kubadili mfumo wa imani na falsafa yao tafauti na Ukristo licha ya ukweli kuwa hapo awali walikuwa wakristo waliotoa katika nchi ya Kikristo. Kwa mujibu wa fikra za watafiti wengi jambo hili lilikuwa Kaballa.

Maana ya neno Kaballa, ni fasihi simulizi. Maandiko na makamusi yanalifafanua neno hili kama siri kubwa, tawi la siri siri la dini ya Uyahudi. Kwa mujibu wa ainisho hili neno la Kaballa linachukua maana iliyofichikana katika Taurati na maandiko mengine ya dini Uyahudi. Lakini tunapochunguza kwa undani jambo hili tunaona kuwa ukweli wa mambo ni mwingine kabisa. Hakika ya mambo inatuplekea kufikiri hitimisho jingine kuwa Kaballa ni mfumo wenye mizizi ya ushirikina wa kipagani, kwamba ilikuwepo kabla ya Taurati na ilienea ndani ya dini ya Uyahudi hata baada ya kufunuliwa kwa Taurati. Ukweli huu wa kuvutia kuhusu Kaballa unafafanuliwa kuwa ndio chanzo hasa. Murat Orgen, Frimansori wa kituruki yeye anasisitiza yafuatayo katika kitabu chake Masonluk Nedir Ve Nasirdir?(Frimasonri ni nini, ikoje?).

“Hatujui vizuri wapi ilikotokea Kabbalah au namna ilivyojiendeleza ni jina la jumla la falsafa moja ya siri iliyojengwa kwa iami i ya kiroho hasa hasa inayohusiana na dini ya Uyahudi Huu ni Usufi wa dini ya kiyahudi lakini baadhi ya mambo iliyonayo yanaonesha kuwa likusanywa zamani zaidi kabla ya Taurati. Mwanahistoria wa Ufaransa Gougenot Des Mousseaux yeye anasema kuwa, Kaballa ni ya zamani kabla ya Uyahudi.
 
Historia ya Matempla

Kwa muda wa siku mbili tu jeshi la msalaba liliwaua kinyama Waislamu wapatao 40,000. baada ya hapo Wanamgambo hao katili wakaifanya Jerusalem kuwa mji wao mkuu na kuanzisha utawala wa Kifalme wa Kilatini ambao ulijitanua kutoka mipaka ya Palestina hadi Antiokia. Baadaye Wapiganaji hao wa vita vya msalaba wakaanzisha mapambano ya kuimarisha utawala wao katika eneo la mashariki ya kati. Wakaanzisha kambi za mafunzo ya kijeshi kwenye majumba kama yale ya kitawa. Washiriki katika mafunzo hayo walitoka Ulaya kuja Palestina na wakaishi katika majumba hayo. Mojawapo ya Komandi zao za kijeshi ilitafautiyana kabisa na nyingine yenyewe ilibadilika muundo kukidhi haja ya wakati. Komandi hii mahususi ilikuwa ya wale walioitwa mashujaa watakatifu yaani Templars. Templar hii au kwa jina kamili, askari dhaifu wa Yesu Kristo na hekalu la Suleiman, iliundwa mwaka 1118, miaka ishirini baada ya wanamgambo wa msalaba kuitwaa Jerusalem. Waanzilishi wa Komandi hii walikuwa ni Wafaransa wawili, Hugh de Payens na Godfrey dest Omer. Mwanzoni kulikuwa na askari lakini Komandi ikazidi kuimarika. Sababu ya wao kujipa jina templar ni kuwa mahali walipochagua kuwa kituo chao palikuwa na kilima cha temple ambako ndiko hekalu hili gofu liliko. Japo Wanamgambo hawa walijiita Templer yaani askari wanyonge lakini kwa kipindi kifupi tu wakawa matajiri sana. Mahujaji wa Kikristo kutoka Ulaya kuja Palestina walikuwa chini ya udhibiti wa Komandi hii na kwa pesa zake nao wakawa matajiri. Mbali na hivyo, kwa mara ya kwanza wakaanzisha mfumo wa hundi na mikopo sawa na ule wa Benki. Kwa mujibu wa Waandishi wa Kiingereza Michael Baigent na Richard Leigh, walianzisha aina fulani ya ubepari na wao ndio waliopelekea kuanzishwa kwa shughuli za sasa za mabenki zinazotoza riba kutokana na ule mfumo wao wa uchumi uliojengwa kwa msingi wa riba. Walikuwa ni hawa Matemplar ambao walihusika na mashambulizi na mauaji dhidi ya Waislamu. Kwa sababu hii Kamanda mkuu wa kiislamu Salahuddin aliyelishinda jeshi la Makruseda mnamo 1187 katika vita ya Hattin na baadaye kuikomboa Jerusalem, aliwahukumu kifo Matemplar kwa mauaji waliyokuwa wameyafanya na akawasamehe Wakristo wengi. Ijapokuwa waliipoteza Jerusalem na kupata madhara makubwa, Matemplar wakaendelea kuishi na licha ya kupungua kwa Wakristo Palestina, wakaongeza nguvu zao Ulaya wakianzia na Ufaransa na kisha katika nchi nyingine. Ikawa dola iliyokuwa ndani ya dola. Bila shaka nguvu zao za kisiasa ziliwanyima raha watawala wa Ulaya. Pia kulikuwa na jambo ambalo nalo liliwatia homa Makasisi. Kamandi ilianza kujitoa kidogo kidogo katika imani ya Kikristo.

Na wakiwa Jerusalem wakaanza kufuata madhehebu ya kikuhani. Kukawa na uvumi pia kwamba walikuwa wakifanya ibada za ajabu ajabu. Mwishowe mnamo mwaka 1307 Mfalme wa Ufaransa Philip akaamua kuwatia mbaroni Matempla hao. Baadhi yao wakafanikiwa kutoroka lakini wengi walikamatwa. Papa Clement wa Tano(Popedement V) pia nae akafanya hivyo. Baada ya kipindi kirefu cha mahojiano na mashitaka, Matempla wengi walikiri kufuata imani ya kikristo na kumtusi Yesu katika mihadhara yao. Hatimaye viongozi wa Matempla ambao waliitwa mabwana wakubwa akiwemo yule kigogo wao, Jecques de Moky wakamnyonga mwaka 1314 kwa amri ya Kanisa na mfalme. Wengi wao wakafungwa jela na Kamandi ikasambaratika na kutoweka kabisa. Baadhi ya wanahistoria wanakawaida ya kuonesha kuwa shitaka lililowakabili Matempla lililotokana na njama za Mfalme wa Ufaransa kwa kuwataja wapiganaji hao wa vita vya msalaba kuwa si watu wenye hatia. Nesta H. Webster, Mwanahistoria mashuhuri wa kiingereza mwenye elimu kubwa ya Histori ya ukuhani anayachambua masuala haya katika kitabu chake, Secret Society and Subversive Movement.

17.jpg



Kwa mujibu wa Webster, kitendo cha kuwatoa Matempla hatiani kwa yale waliyoyafanya katika kipindi cha mashitaka hakiwezi kukubalia kwanza wakati wa mahojiano, si Matempla wote walioteswa. Isitoshe je yale maneno ya kukiri ya Matempla yametokana na mateso waliyopewa? Kwa kweli ni vigumu kusadiki kuwa maelezo yanayotolewa na watu katika nchi mbali mbali yote yakishabiiana kabisa, eti yote yatokane na uzushi. Kama wahanga wangelishurutisha kwa mateso basi wangetoa maelezo yenye mgongano katika kuelezea aina mgongano katika kuelezea aina zote za sala za ajabu ajabu zilizokuwa zikifanyika. Lakini hasha, kila mmoja anaonekana kuelezea vile vile sala zile zile. Vyovyote iwavyo, shauri la Matempla lilikwisha Sawia na Komandi. Japo Komandi ilikoma rasmi kufanya kazi lakini kwa kweli haikutokomea kabisa. Katika kamatakamata ya mwaka 1307, baadhi ya Matempla walifanikiwa kutoroka. Kwa mujibu wa tasnifu zilizoambatanishwa nyaraka mbali mbali za kihistoria, idadi fulani ya watu miongoni mwao walipata hifadhi katika falme moja ya Ulaya ambayo haikutambua mamlaka ya Kanisa Katoliki katika karne ya kumi na nne, nayo ni Scotland.

Huko walijikusanya upya chini ya ulinzi wa Mfalme wa Uskochi Robert the Bruce. Baada ya muda fulani, wakagundua mbinu muafaka ya kujificha ili waendelee kuishi kisirisiri. Walijipenyeza kwenye makazi muhimu katika visiwa vya Uingereza-the wall builders Lodges. Hatimaye wakapata mamlaka kamili ya kumiliki majumba haya. The wall builders Lodges, ikabadili jina lake, mwanzoni mwa zama hizi na sasa ikajiita the Masonic Lodge. Kwa desturi ya Scotland-The Scotish Rite ndiyo tawi kongwe kabisa la Frimansori, hiyo ikiwa ni mwanzoni mwaka Karne ya kumi na nne, pale Matempla- Mashujaa wa msalaba walipopata hifadhi nchini humo.

Mwanahistoria wa Kiyahudi, Theodore Reinach anasema kuwa kabbalah ni sumu ya ajabu kabisa inayoingia ndani ya vena za Uyahudi na kuziathiri kabisa. Salomoni Reinach anaiainisha kabbalah kama ni moja ya pogo za akili ya mwanadamu. Sababu ya maelezo haya ya Reinach kuwa kabbalah ni moja ya pogo za akili ya binadamu ni kuwa mafundisho yake yananasibiana kwa kiasi kikubwa na uchawi. Kwa maelfu ya miaka, kabbalah imekuwa moja ya misingi ya kila Ibada ya uchawi. Inasadikika kuwa wasomi wa kiyahudi (Rabbis) wanaosomea kabbalah wana nguvu kubwa za kichawi. Aidha watu wengi wasiokuwa wayahudi wameathiriwa na kabbalah na wamejaribu kutumia uchawi kwa kutumia mafundisho yake. Mambo ya siri ambayo yalikita mizizi Ulaya mwishoni mwa zama za kati hasa yale yaliofanywa na wanakemia, kwa kiasi kikubwa mizizi yake ipo katika kabbalah. Jambo la ajabu ni kuwa Uyahudi ni dini ya Mungu mmoja inayokwenda kwa ufunuo wa Taurati ya Musa (a.s) lakini ndani ya dini hii kuna utaratibu unaoitwa kabbalah ambao unafuata yale mafundisho ya msingi ya uchawi yaliyoharamishwa na dini hii. Hii inathibitisha ukweli tuliouelezea hapo juu na inabainisha kuwa kabbalah kwa uhalisi wake ni jambo ambalo limeingia katika Uyahudi kutoka nje ya dini hii. Lakini nini chanzo cha jambo hili?

Mwanahistoria wa Kiyahudi Fabre d’Olivet anasema kuwa kabbalah ilitokea katika Misri ya kale. Kwa mujibu wa mwandishi huyu, mizizi ya kabbalah imetambaa kutoka Misri ya kale. Kabbalah ni hadithi iliyosikiwa na baadhi ya viongozi wa Waisrael katika Misri ya kale na ikawasilishwa kwa njia ya fasihi simulizi kutoka kizazi hadi kizazi. Kwa sababu hiyo, lazima tuiangalie Misri ya kale ili tuone vyanzo hasa vya kabbalah- matempla na Frimansori.
 
Wachawi wa Misri ya zamani

Misri ya kale ya Mafirauni(Mafarao) ilikuwa moja ya nchi zilizokuwa na tamaduni kuu za enzi hizo ulimwenguni. Ilikuwa moja ya nchi za kidhalimu kabisa. Minara mikubwa ambayo bado ipo tangia enzi hizo za Misri ya kale kama mapiramidi yalijengwa na mamia kwa maelfu ya watumwa waliofanya kazi,kwa vitisho vya bakora na kunyimwa chakula hata kufikia mahala pa kufa. Mafirauni, watawala wakuu wa Misri walijitapa kuwa wao ni miungu na kwamba waabudiwe na watu. Moja ya vyanzo vya habari kuhusu Misri ya Kale ni maelezo yao wenyewe.Maelezo haya yaligunduliwa katika karne ya 19 na baada ya kazi ngumu, herufi za Kimisri zikasomeka na hivyo taarifa nyingi kuhusu nchi hiyo zikapatikana. Lakini kwa vile maelezo haya yaliandikwa na Wanahistoria waliokuwa serikalini, yamejaa maelezo ya upendeleo ambayo yalikusudiwa kuitukuza dola.

29.jpg


Bila shaka, kwetu sisi, chanzo cha habari juu ya jambo hili ni Qur’an. Katika Qur’an, katika kisa cha Musa, tunapewa habari muhimu kuhusu utawala wa Misri. Aya za Qur’an zinabainisha kuwa kulikuwa na mamlaka kuu mbili za utawala nchini Misri; Firauni na baraza lake la ndani. Kazi ya baraza hili ilikuwa ni kumtukuza Firauni; mara zote firauni alikuwa akikutana nalo na katika nyakati fulani fulani alikuwa akifuata maoni ya baraza lake . Aya zinazonukuliwa hapa chini zinaonyesha kazi ya baraza hilo; “Na alisema Musa; Ewe Firauni! Mimi ni Mtume nitokae kwa Mola wa walimwengu. Yanipasa nisiseme juu ya Mwenyezi Mungu lolote ila haki tu. Kwa yakini nimekufikieni kwa dalili waziwazi zitokazo kwa Mola wenu. Basi wapeleke wana wa Israel pamoja nami katika (nchi waitakayo, usiwazuilie hapa Misri ukawa unawatesa). Firauni akasema kama umekuja na hoja basi ilete ukiwa ni miongoni wa wasemao kweli. Hapo Musa akaitupa fimbo yake (chini). Na mara ikawa nyoka dhahiri. Na akatoa mkono wake. Mara ukawa mweupe kwa watazamao. Wakasema wakuu wa kaumu ya Firauni (pamoja na yeye Firauni); hakika huyo ni mchawi ajuae (uchawi vema). Anataka kukutoeni katika ardhi yenu. Basi mnatoa shauri gani? Wakasema (kumwambia firauni). Muache kidogo yeye na ndugu yake (huyu Haruni anayejipa Utume pamoja naye, usiwaue). Na watume (wakusanyao mijini wakukusanyie wachawi wakubwa wakubwa wote). Wakuletee kila mchawi ajuae Qur’an sura (7:104-112). Izingatiwe kuwa hapa limetajwa baraza la Firauni ambalo linamshauri, na ambalo linamuhamasisha kupambana na Musa na linapendekeza mbinu fulani. Tukiziangalia kumbukumbu za Historia ya Misri, tunaona kuwa kada kuu mbili za baraza hili zilikuwa ni jeshi na Taasisi ya Ukasisi. Hakuna haja ya kufafanua umuhimu wa jeshi; Jeshi hili ndilo lililojenga nguvu za tawala za Mafirauni. Ila tulitazame kwa mazingatio zaidi jukumu la Makasisi hawa. Makasisi wa Misri ya kale walikuwa ni tababaka la watu ambao katika Qur’an wametajwa kama wachawi. Hawa waliwakilisha dhehebu ambalo liliunga mkono utawala. Iliaminika kuwa nao walikuwa na madaraka maalum na walikuwa na elimu ya sihiri. Kwa madaraka haya, waliwavuta watu wa Misri na kuimarisha nafasi yao katika utawala wa Mafirauni. Tabaka hili kwa mujibu wa kumbukumbu za Misri, lilijulikana kama Makasisi wa Amoni. Hawa walikuwa na kazi ya kufanya uchawi na kuendesha dhehebu lao la kipagani; mbali na hivyo pia walisomea sayansi mbalimbali kama vile unajimu, hesabati na Jiometri. Tabaka hili la makasisi ilikuwa ni Taasisi iliyokuwa na elimu maalum. Katika jarida lililoitwa Mason Dergisi, Jarida lililosambazwa kwa mafyoso wa Uturuki, Mizizi ya Frimansori inatajwa kuanzia katika Taasisi hii ya siri, na wanatajwa rasmi makasisi wa Misri ya kale. Tafakuri inavyozidi kukuwa kwa wanadamu, Sayansi nayo inazidi kupiga hatua na kadri Sayansi inavyopiga hatua siri nyingi zinazidi kuongezeka katika mfumo wa siri. Katika hatua hii ya maendeleo shughuli ya siri ambayo kwanza ilianzia Mashariki, China na Tibet na kisha kuenea India, Mesopotamia na Misri ikajenga msingi wa elimu ya ukasisi ambayo imefanyiwa kazi kwa maelfu ya miaka na kujenga msingi wa madaraka ya makasisi nchini Misri. Kuna uhusiano gani kati ya falsafa ya siri ya Makasisi wa Misri ya zamani na Mafrimansori wa hivi leo? Misri ya zamani ni mfano hai wa mfumo wa siasa usio na Mungu uliotajwa katika Qur’an,ambao ulitokomea maelfu ya miaka iliyopita. Je waweza kuwa na athari hadi leo? Kupata jibu la maswali haya lazima tuziangalie Imani za Makasisi wa Misri ya kale kuhusiana na chanzo cha Ulimwengu na maisha. Kwa kifupi Matempla hawakutoweka kabisa bali falsafa yao. Imani zao na ibada zao bado zinaendelea chini ya mwavuli wa Frimansori. Dhana hii inatiwa nguvu za ushahidi mwingi wa kihistri na hiv leo inakubwaliwa na idadi kubwa ya Wanahistoria wa magaharibi ima awe Mafyoso au la. Katika kitabu chetu, The new Masonic Order, tumeutathmini kwa kina ushahidi huu. Dhana inayoihusisha mazizi ya Mansori na Matempla, mara nyingi inarejewa katika majarida yanachapishwa na Mansori wenyewe kwa ajili ya Wananchama wao. Wanachama wa Frimansori wanaikubali kabisa dhana hii.

30.jpg


Mojawapo ya majarida hayo linaitwa Minnar Sinan(ni jarida la Mafyoso wa Uturuki) ambalo linaezea uhusiano kati ya komandi ya Matempla na Frimansori kwa maneno yafuatayo”. “Mnamo mwaka 1312, pale Mfalme wa Ufaransa kwa shinikizo la kanisa alipolifunga komandi ya Matempla na mali zao kuwapa askari wa mtakatifu John mjini Jerusalem harakati za matempala hazikukoma. Idadi kubwa ya Matempala wakapata hifadhi katika maskani ya Frimansori iliyokuwepo ulaya wakati huo. Kiongozi wa Matempla, Mabeignac, akiwa na wanachama wengine, wakapata usalama nchini Scotland chini ya mwavuli wa Wall builder na chini ya jina la Mac Benach. Mfalme Scotland Robert the Bruce akawakaribisha na kuwaruhusu kuwa na ushawishi mkubwa katika maskani za Frimansori nchini Scotland. Matokeo yake maskani za Scotland umuhimu mkuibwa kwa mtazamo wao wa kiufundi na fikra zao. Leo hii Mafyoso wanatumia jina la Mac Benach kwa heshima. Mafyoso wa Ufaransa waliorithi vitu vya Matempla wakareje zao Ufaransa miaka mingi baadaye na kuimarisha ngome yao ya kaaida ikijulikana kama kaaida ya Scotland(Scotish Rights). Aidha, Mimar Sinan inatoa habari nyingi kuhusu uhusiano wa Matempla na Mafrimasonri. Katiika makala yenye kichwa Templas and Frimanson inasema sala ya sherehe za uzinduzi wa Komandi ya Matempla ni sawa kabisa na sala Mafyso wa zama hizi. Kwa mujibu wa makala hiyo hiyo, kama ilivyo katika Mansori wanachama wa Komandi ya Matempla wakiitana Brother(ndugu). Mwishoni mwa makala hayo tunasoma maneno haya; “komandi ya Matempla na shirika la Frimansoni yanashajiishana, kwa kiasi kikubwa hata sala za mashirika haya zinashabihiana kwa maana zimaigwa kutoka kwa Matempla. Kwa ajili hiyo, Mafyoso kwa kiasi kikubwa wamejifananisha na Matempla na yaweza kusemwa kuwa, kile kinachoonwa kuwa ni usiri mkubwa wa Frimansonri kwa akisai kikubwa kimeigwa kutoka kwa Matempla. Kwa kufupisha hapa ni kuwa, kama tulivyosema katika anuani ya makala haya, twaweza kusema kuwa chanzo cha sanaa Kifalme na usiri wa Frimansori chatokana na Matempla. Mwisho, tunasema kuwa imetokeya huko nyuma kwa Matempla na kwamba Mafyoso wamefuata falsafa ya Komandi ya Matempla. Mafyoso wenyewe wanalikubali hili lakini jambo muhimu kwa tafakuri yetu ni nini asili au chanzo cha falsafa hii. Kwa nini Matempla waliachana na Ukristo na kufuata mafundisho mapya. Kitu gani kilichowapelekea kufikia uamuzi huo? Kwa nini walifanya mageuzi hayo kule Jerusalem na je kupitia tawi hili la Frimansoni kumekuwa na athari gani Duniyani kutokana na Falsafa hii iliyofuatwa na Matempla.

52.jpg

 
Matempla na Kaballa

Kitabu kilichoandikwa na Mafyoso Christopher na Robert Lomas kiitwacho The Hiram Key kinafichua mambo fulani ya kweli kuhusu mizizi ya Frimansori. Kwa mujibu wa Waandishi hawa, ni dhahiri kuwa Frimansori ni mwendelezo wa Matempla. Mbali na hivyo, Waandishi hawa pia, wameviangalia pia vyanzo vya Matempla. Kulingana na dhanna yao, Matempla walipitia hatua kubwa za mabadiliko wakati walipokuwa Jerusalem. Mahala palipokuwa kwa Ukristo wao walianzisha madhehebu nyingine. Katika mzizi wa mabadiliko haya, kuna siri ambayo waliifichua ambayo ni hekalu la Suleiman pale Jerusalem ambalo mabaki yake, walitaka kuyachunguza. Waandishi hawa wanasema kuwa, Matempla walikuwa wakiitumia ule ulioitwa kuwa wajibu wao wa kulinda mahujaji wa Kikristo waliozuru pale Palestina lakini kumbe hiki kilikuwa kisingizio, lengo halisi lilikuwa jingine kabisa. Hakuna ushahidi kuwa wale Waasisi walikuwa wakitoa ulinzi kwa Mahujaji bali tulichokugundua ni kuwa kuna ushahidi mkubwa kuwa walikuwa wakichimbua chini ya mabaki ya hekalu la Herold. Waandishi wa kitabu cha Hiram Key sio wao pekee waliogundua vielelezo vya jambo hili. Gaetani De la Forge, Mwanahitoria wa Ufaransa naye ametoa maelezo kama haya; "jukumu halisi la Wale wanamgambo tisa wa Krusade walikuwa wakifanya utafiti katika eneo hilo ili kupata masalia na kupata kumbu kumbu za maandiko ya awali ambao yanachimbuko ya maelezo ya siri ya dini ya kiyahudi na Misri ya zama za kale. Mwisho mwa karne ya 14 Charles Wilson wa Royal Engeneers alianza kufanya utafiti wa mabaki ya kale kule Jerusalem. Yeye akafka mahala pa kuona kuwa, Matempla walikuwa wamekwenda Jerusale kutaifiti mabaki ya hekalu. Wilson aligundua chimba chimba na fukua fukua china ya misingi ya hekalu na akahitimisha kuwa kazi hii ilifanywa kwa zana ambazo zilikuwa za Matempla. Vifaa hivi vingalipo katika hazina ya mabaki ya kale ya Robert Brydon, ambaye anamiliki hifadhi ya kumbu kumbu zinazohusiana na Matempla. Waandishi wa kitabu cha the Hiram Key wanadai kuwa chimba chimba ya Matempla haikuishia matupu, kwamba ile Komandi iligundua kumbukumbu fulani pale Jerusalem ambayo ndiyo iliyobadili mtazamo wao.

35.jpg


Mbali na hao watafiti wengine nao wana maoni hayo hayo. Yumkini lazima kulikuwa na jambo lililowapelekea Matempla kubadili mfumo wa imani na falsafa yao tofauti na Ukristo licha ya ukweli kuwa hapo awali walikuwa wakristo waliotoa katika nchi ya Kikristo. Kwa mujibu wa fikra za watafiti wengi jambo hili lilikuwa Kaballa. Maana ya neno Kaballa, ni fasihi simulizi. Misahafu na makamusi yanalifafanua neno hili kama siri kubwa, tawi la siri siri la dini ya Uyahudi. Kwa mujibu wa ainisho hili neno la Kaballa linachukua maana iliyofichikana katika Taurati na maandiko mengine ya dini Uyahudi. Lakini tunapochunguza kwa undani jambo hili tunaona kuwa ukweli wa mambo ni mwingine kabisa. Hakika ya mambo inatuplekea kufikiri hitimisho jingine kuwa Kaballa ni mfumo wenye mizizi ya ushirikina wa kipagani, kwamba ilikuwepo kabla ya Taurati na ilienea ndani ya dini ya Uyahudi hata baada ya kufunuliwa kwa Taurati. Ukweli huu wa kuvutia kuhusu Kaballa unafafanuliwa kuwa ndio chanzo hasa. Murat Orgen Frimansori wa kituruki yeye ansisitiza yafuatayo katika kitabu chake Masonluk Nedir Ve Nasirdir?(Frimasonri ni nini, ikoje?).

"Hatujui vizuri wapi ilikotokea Kabala au namna ilivyojiendeleza ni jina la jumla na kuwa ilikusanywa zamani zaidi kabla ya Taurati. Mwanahistoria wa Ufaransa Gougenot Des Mousseaux yeye anasema kuwa, Kaballa ni ya zamani kabla ya Uyahudi.
 
Imani ya kale ya Misri juu ya dhana ya evolusheni

Katika kitabu chao kiitwacho,The Hiram Key, waandishi wa frimansori wa kiingereza Christopha Knight na mwenzie Robert Lomas wanadai kuwa Misri ya kale inachukua sehemu muhimu kuhusiana na vyanzo vya frimansori. Kwa mujibu wa waandishi hao,fikra muhimu ambayo imezaa frimansori ya sasa kutoka Misri ya kale ni ile ya ulimwengu kujiendesha wenyewe na kutokea kwa bahati nasibu.Wanaifafanua dhana hii kwa maneno haya:

Wamisri waliamini kuwa maada ilikwishakuwepo siku zote; kwao wao lilikuwa ni jambo lisilo kuwa na mantiki kufikiri kuwa Mungu ndiye anayefanya kila kitu kutokana na hamna. Dhana yao ilikuwa kwamba ulimwengu ulianza pale ilipotokea mvurugano,na kwamba tokea hapo kumekuwa na ugomvi baina ya nguvu za asili. Hali hii ya machafuko iliitwa Nun, na kama yalivyo maelezo ya Sumaria kulikuwa na giza tupu sehemu zote, hapakuwa na jua ndipo nguvu kujiumba ilipoamuru maisha yaanze.Nguvu hii isiyoonekana ambayo ilikuwa ndani ya machafuko haikujijua kuwa yenyewe ilikuwepo. Itakumbukwa kuwa imani zilizoelezwa hapa zinafanana kabisa na madai ya walahidi wa zama hizi, imani zinakuzwa na ajenda ya jamii ya wanasayansi wakitumia maneno kama vile nadharia ya evolusheni, nadharia ya mchafuko(chaos theory)na mjumuiko wa maada(essential organization of matter).

37.jpg


Knight na Lomas wanaendelea kusema; Cha kushangaza, maelezo haya juu ya maumbile yanaiolezea kikamilifu dhana inayoshikiliwa na sayansi ya leo hasahasa chaos theory. Knight na Lomas wanadai kuwa kuna uwiano kati ya imani za kale za Misri na sayansi ya leo, lakini wanapozungumza juu ya sayansi ya leo, kama tulivyosema, wanamaanisha dhana za kilahidi,kama vile nadharia ya evolusheni na nadharia ya machafuko. Licha ya ukweli kwamba nadharia hizi hazina msingi wa kisayansi,zimewekwa kinguvunguvu katika fani ya sayansi kwa takriban karne mbili zilizopita, na zinawasilishwa kama nadharia zilizohalalishwa kisayansi.(Katika vifungu vifuatavyo tutawatazama wale walioweka nadharia hizi katika ulimwengu wa sayansi.)

Sasa tumefikia nukta muhimu. Tuelezee kwa kifupi kile tulichokigundua hadi hapa tulipofika;

1. Tulianza mjadala wa kujadili oda ya matempla ambayo ndiyo inayodhaniwa kuwa chanzo cha frimansori.Tumeona kuwa, ingawaje matempla kimsingi walionekana kama wakristo lakini waliathiriwa na mafundisho ya siri waliyoyagundua yerusalemu, wakachana kabisa na ukristo na wakawa na Taasisi inayopinga kabisa dini hii wakitekeleza ibada mpya.

2. Pale tulipouliza ni itikadi gani hiyo iliyowakumba matempla,tukaona kuwa kimsingi ilikuwa kabbalah.

3. pale tulipoichunguza kabbalah ,tukapata ushahidi kuwa ilikuwa ni itikadi ya kipagani ambayo ilikuwa ya zamani mno kuliko uyahudi japo inafanana na usufi wa kiyahudi, kwamba ni baadaye kabbalah iliingia katika dini hiyo, na kwamba mizizi yake halisi inaonekana katika Misri ya kale.

4. Misri ya kale ilitawaliwa kwa utaratibu wa kipagani wa Mafirauni na huko tukaikuta dhana inayojenga msingi wa falsafa ya kikafiri ya hivi leo;kwamba ulimwengu unajiendesha wenyewe na kwamba umetokea kwa bahati nasibu.Hii kwa hakika inatoa picha maridadi.Je ni bahati tu kwamba falsafa ya makasisi wa Misri ya kale bado ipo,na kwamba bado kuna alama za mlolongo wa (kabbalah –matempla –frimansori) .?

Je hawa mafyoso ambao wameweka kumbukumbu katika historia ya ulimwengu tokea karne ya 18 wakifanya mapinduzi wakiendeleza falsafa na mifumo ya siasa ni warithi wa wachawi wa Misri ya kale?

Ili kujibu maswali haya vizuri hebu tuyachunguze kwa undani zaidi matukio ya kihistoria ambayo tumeyagusia kwa kifupi tu.
 
Habari ya ndani juu ya kabbalah

"Kutoka" ni jina la kitabu cha pili cha Taurati. Kitabu hiki kinaelezeya jinsi wana wa Israel chini ya uongozi wa Mussa, walivyoondoka Misri kuepuka udhalimu wa Firauni. Firauni aliwashurutisha wana wa Israel kuishi kama watumwa na hakukubali kuwaachia huru. Lakini pale alipokumbana na miujiza aliyoonesha Mwenyezi Mungu kupitia kwa Mussa na maangamizi aliyowapelekea watu wake Firauni alitulia. Kwa hiyo usiku mmoja wana wa Israel wakakusanyika na kuanza safari yao kuhama Misri. Baadaye Firauni akawashambulia waisrael lakini Mwenyezi Mungu akawanusuru kwa muujiza mwingine zaidi aliouonesha kupitia kwa Mussa. Lakini katika Qur'an tunakuta maelezo sahihi zaidi ya kuhama kwao kutoka Misri, kwa sababu Taurati imehujumiwa baada ya kufunuliwa kwa Musa. Ushahidi muhimu wa hili ni kuwa katika vitabu vitano vya Taurati- Kitabu cha mwanzo, kutoka, walawi, hesabu na kumbukumbu la Taurati- kuna migongano mingi. Ukweli kuwa kitabu cha kumbukumbu la Taurati kimeishia na maelezo ya kufa na kuzikwa kwa Mussa ni ushahidi usiopingika kwamba sehemu iliyobaki itakuwa imeongezwa baada ya kifo cha Musa. Katika Qur'an, katika maelezo ya kuhama kwa wana wa Israel kutoka Misri kama ilivyo katika habari zote zinazohusiana na jambo hili, hakuna mgongano hata kidogo. Habari hii inaelezwa kwa usahihi kabisa. Isitoshe kama zilivyo habari nyingine, Mwenyezi Mungu anafunua hikma na siri nyingi katika jambo linalozungumziwa. Kwa sababu hii pale tunapoziendea habari hizi kwa undani, tunaweza kupata mafundisho mengi ndani yake.


Ndama wa Dhahabu

Moja kati ya mambo muhimu kuhusiana na kuhama kwa wana wa Israel kutoka Misri, kama ilivyoelezwa katika Qur'an, ni kuwa waliasi dhidi ya dini iliyofunuliwa kwao na Mungu licha ya ukweli kwamba Mwenyezi Mungu aliwanusuru na udhalimu wa Firauni kupitia kwa Musa. Wana wa Israel hawakuweza kufahamu ile Tawhiid ambayo Musa aliwafikishia bali wao walizidi kuielekea Ibada ya Sanamu. Qur'an inaulezea hivi muelekeo huu wa ajabu-

"Na tukawavusha wana wa Israel baharini (wakasalimika na balaa la Firauni) na wakawafikia watu waliokuwa wakiabudu masanamu yao. Wakasema Ewe Musa! Tufanyie waungu na sisi (yaani masanamu) kama wao walivyo na miungu. Musa akasema hakika nyinyi ni watu mfanyao ujinga. Hawa yaataangamia haya waliyonayo na ni bure waliyokuwa wakiyafanya.

(Q 7:138-139).

Licha ya maonyo ya Musa, wana wa israel waliendelea na upotevu huo, na Musa alipowaacha na kwenda mlima wa Sinai, upotevu wao ukadhihirika zaidi. Wakitumia fursa ya kutokuwepo kwa Musa, mtu mmoja aliyeitwa Sammir akawajia. Akawashawishi watengeneze sanamu la ndama na kisha waliabudie.

Musa akarudi kwa watu wake kwa ghadhabu na masikitiko. Akasema Enyi watu wangu je Mola wenu hakukuahidini ahadi nzuri, je umekuwa mrefu kwenu muda wa ahadi hiyo (mnaona haitimizwi) au mumetaka ikushukieni ghadhabu kutoka kwa Mola wenu; na kwa hivyo mmevunja ahadi yangu? Wakasema sisi hatukuvunja ahadi yako kwa khiyari yetu walakini tulibebeshwa mizigo ya watu; (vyombo vya dhahabu tulivyoviazima kwa wanawake wa kimisri). Na namna hivi alitia Samir (sehemu yake). Na akawatolea (akawaundia katika myayusho huo) ndama, kiwiliwili kamili kinacholia. Na wakasema; huyu ndio Mungu wenu na Mungu wa Musa lakini Musa amesahau (amekwenda kumtafuata majabalini).
(Q 20:86-8.
 
Ibada ya masanamu ya Waisrael

Kwanini kulikuwa na ung’ang’anizi miongoni mwa wana wa Israel katika kukita na kuabudia masanamu? Nini hasa kilikuwa chanzo cha mwelekeo huu? Ni wazi jamii ambayo hapo kabla haikuwahi kuamini masanamu isingeweza kwa ghafla kufuata mwenendo huo wa kipumbavu kwa kutengeneza sanamu na kuanza kuliabudia. Ni wale tu ambao ibada ya sanamu ilikuwa ya kawaida kwao ndio ambao wangeweza kuamini upuuzi huo.

Hata hivyo, wana Israel walikuwa watu ambao hapo kabla waliamini Mungu mmoja tokea zama za mzee wao Ibrahimu. Jina hili “Waisrael” au “wana wa Israel” kwanza kabisa ilitolewa kwa watoto wa Yaqub, mjukuu wa Ibrahimu. Baadaye jina hili likatumika kwa Mayahudi wote waliotokana naye.

Waisrael walikuwa wameichunga Imani ya Mungu mmoja ambayo waliirithi kutoka kwa wazee wao; Ibrahimu, Is-haqa na Yaqub (a.s). Wakiwa pamoja na Yusufu (a.s), walikwenda Misri na wakaichunga Imani yao ya Mungu mmoja kwa kipindi kirefu, licha ya ukweli kwamba waliishi pamoja na washirikina wa Kimisri.

Inabainika wazi katika maelezo yaliyotolewa katika Qur’an kuwa pale Mussa alipowajia, Waisrael walikuwa watu walioamini Mungu mmoja. Isipokuwa tu ni kwamba pamoja na kuamini kwao Mungu mmoja, Waisrael waliathiriwa na Wapagani waliokuwa wakiishi nao pamoja na wakaanza kuwaiga wakibadili dini waliochaguliwa na Mwenyezi Mungu na kufuata Ibada ya Sanamu ya jamii nyingine.

Tunapolichunguza swala hili kwa undani kwa kuzingatia kumbu kumbu za historia, tunaona kuwa dhehebu la kipagani lililowaathiri Waisrael lilikuwa lile la Misri ya kale. Ushahidi muhimu wa kushadidia hitimisho hili ni kuwa yule ngamia wa dhahabu waliyemuabudia Waisrael wakati Mussa alipowenda mlima Sinai, alikuwa mfano wa masanamu ya Misri, Hatha na Aphis. Katika kitabu chake Too Long in the Sun, muandishi wa Kikristo Richard Rives ameandika hivi;

Hatha na Aphis Ng’ombe jike na fahari miungu ya Misri ilikuwa ikiwakilisha Ibada ya Jua. Ibada yao ilikuwa ni muendelezo wa historia ya utukuzo wa Jua. Yule ndama wa dhahabu wa mlima Sinai alikuwa ushahidi tosha wa kuthibitisha kuwa karamu iliyotangazwa ilihusiana na ibada ya Jua. Athari ya dini ya kipagani ya Misri ilionekana katika sura nyingi tofauti. Mra baada ya kuwashinda wapagani imani yao ya kishirikina ikadhihirika kama aya inavyosema;

Ewe Mussa! Tufanyie waungu na sisi (yaani masanamu) kama wao walivyo na miungu.

(Q 7:13.

Na kumbukeni habari hii pia (mliposema, Ewe Mussa hatukuamini mpaka tumuone Mwenyezi Mungu waziwazi. (2:55). Maneno yao haya yanadhihirisha kuwa wao walitaka kuabudia Mungu wa kimaada ambayo wangemuona kwa macho kama dini yao ya kipagani ilivyo wapatia wamisri mungu kama huyo.

Muelekeo huu wa Waisrael kufuata upagani wa Misri ya kale ambao tumeuelezea, ni muhimu ueleweke kwani ndio unaotupa ufahamu wa jinsi kilivyohujumiwa kitabu cha Torati na unatufahamisha chanzo cha Kabbalah. Tukiyatafakari mafundisho haya kwa mazingatio, tutaona kuwa ni katika vyanzo hivi unapokutikana upagani wa Misri ya kale na falsafa ya kilahidi.

Kutoka Misri ya kale hadi Kabbalah

Wakati Mussa angali hai, waisrael walianza kutengeneza masanamu kama yale yale waliyoyaona Misri na kuyaabudia. Baada ya Mussa kutawafu (kufariki Duniya), hakukuwa na kizuizi cha kuzuia Imani potofu. Bila shaka haiwezi kusemwa kwamba ni Mayahudi wote waliokengeuka lakini baadhi yao walifuata upagani wa Misri. Kwa kweli walishikilia mafundisho ya ukasisi wa Misri (wachawi wa Firauni) ambayo yalijengwa kwa msingi wa imani za jamii hiyo, na wakaihujumu Imani yao kwa kutumbukiza mafundisho haya ndani yake. Itikadi mabayo ilitumbukizwa katika Uyahudi kutoka Misri ya kale ilikuwa ni Kabbalah. Kama ulivyokuwa mfumo wa makasisi wa Misri, Kabbalah nao ulikuwa mfumo wa siri, na msingi wake ulikuwa utamaduni wa uchawi. Kabbalah inatoa maelezo ya maumbile tofauti kabisa na yale yaliyokutwa katika Torati. Ni maelezo ya kilahidi yaliyoegamia dhana ya Misri ya kale juu ya uhai wa milele wa maada. Murat Ozgen mwana frimansori wa Kituruki ana haya ya kusema juu ya swala hili;
46.jpg

Ni dhahiri kuwa Kabbalah iliundwa miaka mingi kabala ya Taurati haijaja. Sehemu zaidi ya Kabbalah ni nadharia juu ya muundo wa ulimwengu. Nadharia hii iko tofauti kabisa na maelezo juu ya maumbile yaliyopokewa na dini zinazoamini Mungu. Kwa mujibu wa Kabbalah, mwanzoni kabisa mwa hatua ya kuumbwa kwa ulimwengu, vitu vinavyoitwa Sefiroth maana yake ni duara au mihimili ikiwa na sifa za kiroho na kimaada iliibuka. Idadi ya jumla ya vitu hivi ilikuwa 32.

Ile kumi ya mwanzo ndiyo iliyoshikilia Solar System na mingine iliyobaki imeshikilia makundi ya nyota angani. Imani hii ya kipekee ya Kabbalah inabainisha kuwa inahusiana kwa karibu na mifumo ya Imani ya unajimu. Kwahiyo Kabbalah inatenganishwa mbali kabisa na dini ya uyahudi na inanasibishwa kwa karibu zaidi na dini za kale za siri za mashariki. Kwa kufuata mafundisho ya siri na ya ulahidi ya Misri ya kale ambayo yalijengwa kwa msingi wa uchawi, Mayahudi wakapuuza mambo yaliyoharamishwa katika Taurati. Wakashikilia Ibada za kichawi za wapagani na hivyo Kabballah ikawa itikadi ndani ya uyahudi lakini ikienda kinyume na Taurati. Katika kitabu chake kiitwacho Secrety Societies and Subversive Movements, mwaandishi wa Kingereza Nesta H Webster anasema;

Uchawi kama tuujuavyo ulikuwa ukifanywa na Wakanan kabla ya kuvamiwa kwa Parestina na waisrael. Misri, India na ugiriki nazo zilikuwa na wachawi wao na Miungu yao. Licha ya makemeo dhidi ya uchawi yaliyomo katika sheria ya Musa, Mayahudi wakipuuzilia mbali makemeo haya walijiingiza na kuuchanganya utamaduni mtukufu waliorithi na mawazo ya kichawi yaliyotokea katika jamii nyingine.

Wakati huo huo kwa upande wa Kabbalah ya Uyahudi iliyochukuliwa kutoka katika Falsafa ya Persian Magi na ya Neo Platonists, na ya Neo Pythagoreans hapo ndipo penye maelezo kuwa tunachokijua sisi hivi leo kuhusu Kabbalah hakitokani kabisa na uyahudi. Kuna aya katika qur’an inayozungumzia jambo hili. Mwenyezi Mungu anasema kuwa Waisrael walijifunza tamaduni za kichawi za kishetwani kutoka nje ya dini yao; Wakafuata yale waliofuata Mashetwan, (wakadai kuwa yalikuwa) katika Ufalme wa Suleiman; na Suleiman hakukufuru, bali Mashetwani ndio waliokufuru, wakiwafundisha watu uchawi (waliokuwa wakiujua wenyewe tangu zamani), na (uchawi) ulioteremshwa kwa malaika wawili, Haruta na Maruta katika (mji wa) Babil. Wala (Malaika hao) hawakumfundisha yeyote mpaka wamwambie; hakika sisi ni mtihani (wa kutazamwa kutii kwenu); basi usikufuru.

Na wakafuata yale waliyo zua mashet'ani kuuzulia ufalme wa Su leiman. Na wala Suleiman hakukufuru, bali mashet'ani ndio walio kufuru, wakiwafundisha watu uchawi, na yaliyo teremshwa kwa Malaika wawili, Haaruta na Maaruta katika Baabil. Wala hao hawakumfundisha yeyote mpaka wamwambie: Hakika sisi ni mtihani; basi usikufuru. Wakajifunza kwa hao wawili yale ya kumfarikisha mtu na mkewe. Wala hawawezi kumdhuru mtu ila kwa kutaka Mwenyezi Mungu. Na wanajifunza yatayo wadhuru wala hayawanufaishi. Na hakika wanajua kwamba aliye khiari haya hatakuwa na fungu lolote katika Akhera. Na hakika ni kiovu mno walicho jiuzia nafsi zao laiti wangelijua
(Q 2:102).

Aya hii inabainisha kuwa japo Wayahudi fulani walijuwa kuwa watapata khasara katika maisha ya Akhera lakini bado walijifunza na kufuata tamamduni za uchawi. Hivyo walikengeuka na kutoka katika sheria ambayo Mungu aliwashushia, wakiwa wameuza nafsi zao wenyewe na kutumbukia katika upagani (itikadi za kichawi). Ni kibaya walichojiuzia nafsi zao kwa maneno mengine maana yake waliacha imani yao. Mambo yaliyozungumziwa katika aya hii yanaonesha vipengele vikuu vya mfarakano katika historia ya Uyahudi. Mapambano yalikuwa kati ya mitume ambao Mwenyezi Mungu aliwashusha kwa mayahudi pamoja na mayahudi walioamini na kuwatii kwa upande mmoja dhidi ya wale mayahudi waliopotoka na kuasi amri za Mungu na kuiga tamaduni za kipagani wa watu walioishi nao ambao walifuata ada za utamaduni wao badala ya sheria ya Mungu.
 
Waliokuwa Matempla ndio hao wakaja kuwa Mafrimansori

Wakati tulipowazungumzia Matempla huko nyuma, tulisema kuwa kundi hili maksusi la makuruseda liliathiriwa na “siri” waliyoikuta Jerusalem, kutokana na siri hiyo wakaachana na Ukirsto na wakaanza kufuata mafundisho ya kichawi. Tukasema kuwa watafiti wengi waliishia kutoa maoni yao kuwa siri hii ilihusiana na kabbala. Kwa mfano katika kitabu chake, Histoire de la Magie (Historia ya uchawi ) mwandishi wa kifaransa, Eliphas Le’vi, anatoa ushahidi wa kina kuwa Matempla walijingiza katika itikadi ya siri ya kabbala, kwamba walifundishwa itikadi hiyo kwa siri. Ndio kusema itikadi hii pamoja na mizizi yake ya misri ya kale ilipandikizwa kwa Matempla kupitia kabbala. Katika kitabu chake Foucault’s Pendulum, mwanafasihi mashuhuri wa Italia, Umberto Eco, naye anausimulia ukweli huu. Katika riwaya yake nzima anasimulia kupitia vinywa vya wahusika wakuu wa riwaya yake kuwa Matempla waliathiriwa na kabbala na kwamba wale makabbala walikuwa na siri ambayo chanzo chake chaweza kuwa Mafirauni wa misri ya kale. Kwa mujibu wa Eco, baadhi ya mayahudi mashuhuri walijifunza siri fulani zilizo toka kwa wamisri wa zamani na baadaye wakazipenyeza katika vitabu vitano vya kwanza vya Agano la kale. Lakini siri hii ambayo ilisambazwa kwa siri ilikuwa ikifahamika kwa wana kabbala peke yao. (zohari, iliyoandikwa Hispania na kuunda kitabu cha msingi cha kabbala inazungumzia siri za vitabu hivi vitano. Baada ya kueleza kuwa Wanakabbala waliisoma siri hii ya Misri ya kale katika vipi hekalu la Suleiman , Eco pia anaandika kuwa Matempla nao wakaisoma siri hii kutoka kwa walimu wa kabbala mjini Jerusalem. Siri hii ilikuwa ikijulikana na kikundi kidogo sana cha walimu wa kiyahudi waliobakia Palestina matempla wakaisoma kutoka kwa walimu hao. Pale matempla walipofuata itikadi mchanganyiko ya wamisri na wakabbala ndipo walipofarakana na dhehebu la kikiristo lililokuwa likitawala Ulaya. Ulikuwa ni mfarakano ambapo wao walishirikiana na nguvu nyingine kubwa ya mayahudi. Baada ya matempla kutiwa mbaroni kwa amri ya pamoja ya Mfalme wa Ufaransa na Papa mnamo mwaka 1307 , kundi hili likatokomea chini chini lakini athari zake zikabakia, Tena zikawa hatari zaidi na zenye uelekeo madhubuti.
Kama tulivyosema awali idadi ndogo ya Mtempla ilinusurika katika kamata kamata na kukimbilia kwa Mfalme wa Scotland, utawala pekee wa kifalme wa Ulaya ambao haukuyakubali Mamlaka ya Papa. Kule Scotland wakajipenyeza katika jumuiya ya Wall-builders na wakaitwaa. Jumuiya zikafuata utamaduni wa Matempla na hivyo mbegu ya frimansori ikapandwa Scotland. Hadi leo hii kanuni kuu ya Frimansori ni ule utaratibu wa kale wa maombi wa Scotland. Kama ilvyofafanuliwa kwa kina katika kitabu kiitwacho The New Masonic Order, kuanzia karne ya kumi na nne ndipo yanapoonekana masalia ya Matempla na Mayahudi kadhaa walioshirikiana nao katika vipindi mbalimbali vya Historia ya Ulaya. Bila kutoa maelezo ya kina zifuatazo ni nukta muhimu za utafiti:


-Katika Mji wa Province nchini Ufaransa kulikuwa na kambi ya Matempla waliokimbilia nchini humo. Wakati wa ile kamatakamata Matempla wengi sana walijificha huko. Kielezeo kingine cha eneo hilo ni kuwa hilo ndilo lililokuwa kituo mashuhuri cha Ukabbala barani Ulaya. Province ndipo mahala ambapo fasihi simulizi ya Kabbala ilandikwa katika kitabu.
- Kwa mujibu wa wanahistoria,uasi wa Wakulima nchini Uingereza mwaka 1381 ulichochewa na Jumuiya fulani ya siri. Watafiti wanaoitafiti Historia ya Frimansori wanakubaliana kuwa Jumuiya hii ya siri ilikuwa ya Matempla. Ule uasi haukuwa tu wa kiraia bali pia ulikusudiwa kulishambulia Kanisa Katoliki.-Nusu karne baada ya uasi huu, kasisi mmoja wa Bohemia, John Huss akaanzisha vurugu kulipinga Kanisa Katoliki. Kama kawaida nyuma ya vurugu hizi walikuwepo Matempla. Isitoshe Huss mwenyewe alikuwa akiipenda sana Kabbala. Yeye alikuwa akimpenda sana Avigdor Ben Isaac Kara. Mtu huyu alikuwa Mwalimu mashuhuri wa Kiyahudi katika jamii ya kiyahudi katika mji wa Prague na pia alikuwa Mwanakabbala.


Vielelezo kama hivi vinaonesha kuwa ushirikiano kati ya Matempla na Wanakabbala ulilenga kubadilisha mfumo wa jamii ya Ulaya. Mabadiliko haya yalijumuisha misingi ya utamaduni wa Kikristo ambao ndiyo utamaduni-mama wa Ulaya na badala ya utamaduni huu uwekwe utamaduni uliojengwa kwa msingi wa mafundisho ya kipagani, kama vile Kabbala na baada ya mabadiliko haya, yafuate mabadiliko ya kisiasa. Mifano ni mapinduzi ya Ufaransa na Italia.


41.jpg


Huko mbele tutaona vipindi vya mabadiliko ya Historia ya Ulaya. Katika kila kipindi tutakutana na ukweli kuwa kulikuwa na nguvu iliyotaka kuitenganisha Ulaya na mafundisho ya Kanisa na badala yake iweke itikadi ya Kisekula na hivyo izisambaratishe taasisi zote za dini. Nguvu hii ilijaribu kuichagiza Ulaya kuikubali itkadi iliyorithiwa kutoka Misri ya kale kupitia Kabbala. Tulikwishaeleza huko nyuma kuwa msingi wa itikadi hii ni dhana hizi mbili; Humanism na Materialism (Utumtu na Ulahidi).
 
mkuu maelezo haya mazuri ial rekebisha font size! Inaumiza macho pili haivutii kusoma! Font hii ni ndogo mno!
 
Mafundisho ya kipagani yalivyoongezwa katika Taurat

Ni muhimu kukumbuka kuwa maovu ya Wayahudi wapotevu, yameandikwa katika kitabu kitakatifu cha Mayahudi-Agano la Kale. katika kitabu cha Nehemia ambacho ni kitabu cha historia kilichomo katika Agano la Kale, Wayahudi wanakili dhambi zao na kutubu. Waliokuwa wazawa wa Israel wakajitenga na wageni wote, wakasimama, wakaziungama dhambi zao, na maovu ya Baba zao. Basi wakasimama mahali pao, wakasoma katika kitabu cha Torati ya Bwana, Mungu wao, muda wa robo ya siku; na robo nyingine wakaungama, wakamuabudu Bwana, Mungu wao. Ndipo wakasimama madarajani pa Walawi, Yeshua, na Bani, na Kadimieri, na Shebania, na Bani, na Sherebia, na Bani, na Kenani, wakamlilia Bwana, Mungu wao kwa sauti kuu.

( Wakasema😉 walakini (Baba zetu) hawakutii, wakakuasi, wakaitupa sheria yako nyuma yao, wakawaua Manabii wako walioshuhudia juu yao wapate kuwarejeza kwako; wakatenda machukizo makuu. Kwasababu hiyo ukawatia katika mikono ya adui zao, waliowasumbua; na wakati wa shida yao, walipokulilia, uliwasikia kutoka mbinguni; na kwa wingi wa rehma zako ukawapa waokozi walio waokoa katika mikono ya adui zao. Lakini walipokuwa wamekwisha kustarehe, walitenda mabaya tena mbele zako; kwahiyo ukawaacha katika mikono ya adui zao, nao wakawatawala; hata hivyo waliporejea na kukulia, uliwasikia toka mbinguni, ukawaokoa mara nyingi kwa rehma zako; ukawashuhudia ili uwarudishe tena katika sheria yako; lakini walitakabari, wasisikilize amri zako, bali waka zikhalifu hukumu zako, (ambazo mtu akizitenda ataishi katika hizo) nao wakayaondowa mabega yao, wakafanya shingo zao kuwa ngumu, wasitake kusikiliza. Ila kwa rehema zako nyingi hukuwakomesha kabisa wala kuwaacha; kwa maana wewe u Mungu mwenye neema, Mwenye rehema. Basi sasa, Ee Mungu, Mkuu, mwenye uweza, Mungu wa kuogofya mwenye kushika maagano na rehema, mashaka yote yaliyotupata sisi, wafalme wetu, na wakuu wetu, na makuhani wetu, na manabii wetu, na Baba zetu, na watu wako wote, tangu zamani za wafalme wa Ashuru hata leo, na yasihesabiwe kuwa ni madogo. Lakini wewe u mwenye haki, katika hayo yote yaliyotupata; maana wewe umetenda yaliyo kweli lakini sisi tumetenda yaliyo mabaya; na wafalme wetu, na wakuu wetu, na makuhani wetu, na Baba zetu, hawakushika sheria yako wala hawakusikiliza amri zako na shuhuda zako ulizo washuhudia. Kwa kuwa hawakukutumikia wewe katika ufalme wao, na katika wema wako mkuu uliowapa, na katika nchi ile kubwa yenye neema uliowapa mbele yao, wala hawakughaili na kuacha mabaya yao. (Nehemia 9, 2-4, 26-29-31-35).

Kifungu hiki kinaelezea tamaa ya kurejea katika Imani ya Mungu mmoja ambayo Wayahudi wengi walikuwa nayo, isipokuwa katika kipindi cha historia ya Wayahudi kundi moja lilimeguka na kupata nguvu kidogo kidogo, na likaja kuwatawala wayahudi na baadaye likaegeuza kabisa dini yenyewe. Kwasababu hii katika Torati na katika vitabu vingine vya agano la kale kuna masalia yanayotoka katika mafundisho ya Kipagani, na pia kama yaliyotajwa hapo juu yanawasukuma kurejea katika dini sahihi. Mathalani;

- Katika kitabu cha mwanzo cha Taurati, inasemwa kuwa Mungu aliumba ulimwengu mzima kwa siku sita kutokana na hamna. Hii ni sahihi na inatokana na ufunuo sahihi. Lakini, hapo hapo inasema kuwa Mungu alipumzika siku ya saba, huu ni uzushi kabisa. Ni dhana potofu iliyotoka katika upagani ambao unampachika Mungu sifa za kibinadamu. Katika aya hii ya Qur'an, Mwenyezi Mungu anasema;

Na Tumeziumba Mbingu na Ardhi na vilivyomo kati yao katika nyakati sita, wala hayakutugusa machovu

Q 50:3.

Katika sura nyingine za Taurati kuna staili ya uandishi ambayo ni ya utovu wa heshima kwa Mungu, hasa hasa katika zile sehemu ambazo sifa za kibinadamu anapewa Mungu. Imani hizi potofu za kulinganisha udhaifu wa kibinadamu ndizo imani ambazo wapagani walikuwa nazo kwa miungu yao bandia. Maneno mengine ya kufuru ni yale yanayodai kuwa Yakobo, Baba wa Waisrael alipigana myeleka na Mungu, na akashinda. Ni wazi kabisa hiki ni kisa cha kutungwa ili kuwatukuza Waisrael, ni mwigo kutoka katika jamii za wapagani. Katika Agano la kale kuna mtindo wa kumuelezea Mungu kama Mungu wa utaifa – yaani Mungu wa Waisrael peke yao. Lakini Mungu ni Mola wa Ulimwengu na viumbe vyote. Dhana hii ya dini ya utaifa, katika Agano la kale inafanana na dhana za kipagani ambapo kila kabila linaabudia Mungu wake.

-Katika baadhi ya vitabu vya agano la kale (mfano, Yeshua) amri zinatolewa kufanya maovu dhidi ya watu wasiokuwa wayahudi. Mauaji ya halaiki yanaamrishwa bila kujali wanawake, watoto wala wazee. Mwenendo huu wa kinyama uko kinyume kabisa na sheria ya haki ya Mungu, bali badala yake unarandana na ushenzi wa tamaduni za kipagani za kuabudia Mungu bandia wa vita.

Mawazo haya ya kipagani ambayo yametumbukizwa katika Taurati yumkini yana chanzo chake. Lazima kuna mayahudi ambao walifuata mila isiyokuwemo katika Taurati. Wakaishika na kuitukaza mila hiyo. Baadaye wakatumbukiza katika Taurati mawazo yaliyotoka katika mila hii ambayo wao waliyaunga mkono. Chimbuko la mila hii linaanzia nyuma kabisa kwa makuhani wa Misri (Wachawi katika utawala wa Firauni ).

Kwa kweli ni Kabbala iliyorithiwa na wayahudi wengi. Kabbala ilikuwa na sura ambayo iliziwezesha itikadi za Wamisri na Wapagani kujipenyeza katika dini ya uyahudi na kustawi ndani yake. Wahusika wa Kabbala hapana shaka wanadai kuwa Kabbala inafafanua tu kwa kina siri zilizofichikana kabisa katika Taurati, lakini , kwa kweli kama asemavyo mwanahistoria wa kiyahudi aliyezungumzia Kabbala kuwa Kabbala ni sumu isiyotambulika ambayo imeingiya katika dini ya uyahudi na kuiathiri kabisa. Hapo sasa inawezekana kukuta ndani ya Kabbala masalia ya itakdi ya Ulahidi ya Wamisri wa zama za kale.

Kabbala – Itikadi inayopingana na dhana ya kuumbwa kwa ulimwengu.

Katika Qur'an , Mwenyezi Mungu anabainisha kuwa Taurati ni kitabu cha Mungu ambacho kilishushwa kama muongozo kwa Wanadamu,

Hakika tuliteremsha Taurati yenye uongozi na nuru; ambayo kwayo Manabii waliojisalimisha (kwa Mwenyezi Mungu waliwahukumu Mayahudi, na Watawa na Maulamaa pia (walihukumu kwa hiyo Taurati), kwasababu walitakiwa kuhifadhi kitabu (hicho) cha Mwenyezi Mungu; nao walikuwa mashahidi juu yake.

(Q 5:44).

Kwahiyo, Taurati, kama ilivyo Qur'an, ni kitabu chenye elimu na amri zinazohusiana na Tawhiid yanayoelezya kuwepo kwa Mwenyezi Mungu na upweke wake, sifa zake, kuumbwa kwa wanadamu na viumbe wengine, lengo la kuumbwa kwa binadamu, na sheria za maadili za Mwenyezi Mungu kwa wanadamu. Hata hivyo ile Taurati ya asili haipo tena hivi leo. Tuliyonayo hivi leo ni Taurati iliyoandikwa upya na kuhujumiwa na mikono ya binadamu. Kuna nukta muhimu kuwa ile Taurati ya asili na Qur'an zinashabihiana, Mwenyezi Mungu anatambuliwa kama muumba. Anatambuliwa kama aliyetakasika na aliyeepukana na mapungufu yote na amekuwepo bila mwanzo. Chochote minghairi yake ni kiumbe chake. Yeye ndiye aliyeumba ulimwengu wote, maumbile ya angani, maada isiyo na uhai, binadamu na viumbe vyote hai. Mungu ni mmoja tu. Wakati huu ukiwa ndio ukweli halisi, kuna maelezo tofauti kabisa yanayokutikana katika Kabbala, ambayo ni sumu iliyopenya katika mishipa ya uiyahudi na kuuathiri kabisa. Mafundisho yake juu ya Mungu yanapingana kabisa na ule ukweli halisi juu ya maumbile unaokutikana katika ile Taurati ya asili na katika Qur'an.

Katika moja ya maandiko yake juu ya Kabbala, mtafiti mmoja wa Amerika, Lance S. Owens anatoa fikra yake juu ya vyanzo vya itikadi hii ambapo imani ya Kabbala imesababisha dhana kadhaa kuhusu Mungu, nyingi miongoni mwa hizo zimetoka kabisa katika mtazamo wa dini. Msingi mkuu wa imani ya Waisrael ulikuwa ni kalima kuwa Mungu wetu ni mmoja. Lakini Kabbala ikadai kuwa wakati Mungu akiishi katika umbile la peke yake ambalo katika Kabbala linaitwa Ein Sof asiye na udhaifu – upweke huu usiojulikana lazima utakuwa umeanzia katika maumbile mengi ya kiungu. Yaani kundi la Miungu. Miungu hii ambayo mwana Kabbala aliita Sefiroth yaani sura au nyuso za Miungu. Njia ambayo Mungu alitokea katika umoja usioeleweka na kuingia katika wingi ilikuwa ni siri ambayo wana Kabbala walihangaika kuitafuta. Ni dhahiri hii sura ya Miungu mingi inakubaliana na madai ya washirikina. Siyo tu Mungu alikuwa katika wingi katika itikadi ya Kikabbala bali hata kule kutokea kwake mwanzoni katika upweke usiojulikana kulichukuwa sura mbili ya kiume na ya kike, Baba na Mama, Hokhmah na Binah hizi ndizo sura za mwanzo za Mungu. Wafuasi wa Kabbala walikuwa wakitumia tamathali za kijinsia kuelezea jinsi maingiliano ya kijinsia ya Hokhmah na Binah yalivyozaa maumbile mengine.
 
Dhana ya ‘humanism'

Yasadikiwa na wengi kuwa Humanism ndio itikadi madhubuti. Inampandikiza mtu hisia za upendo, utulivu na Udugu. Lakini kifalsafa dhana hii ina maana kubwa zaidi. Humanism ni utaratibu wa fikra ambao unaichukulia dhana ya ubinadamu kama ndio msingi na lengo lake kuu. Kwa maneno mengine inawataka watu wajitenge mbali na Mungu, Muumba wao na washughulike na maisha yao na utu wao. Kamusi ya Kiingereza iitwayo Common dictionary inaliainisha neno humanism kama ni mfumo wa itikadi uliojengwa juu ya msingi wa maadili, sifa na tabia ambazo zinaaminika kuwa bora zaidi kwa vigezo vya binadamu wenyewe bila kutegemea muongozo wowote wa Kiungu.

54.jpg


Ainisho la wazi zaidi la humanism limetolewa na wale wanaounga mkono itikadi hii. Mmoja kati ya wapiga debe wakuu wa dhana ya humanism ni bwana Corliss Lamont. Katika kitabu chake kiitwacho The philosophy of Humanism, mwandishi huyu ameandika hivi: Kwa ujumla Humanism inaamini kuwa maumbile yanatokana na mkusanyiko wa vitu halisi ambavyo msingi wake ni nguvu ya maada. Maada ndio msingi wa Ulimwengu na kwamba nguvu za Kiungu hazipo. Dhana ya nguvu za Kiungu, kwa upeo wa binadamu, haina uthibisho. Kwamba watu hawana roho za kudumu milele yaani zisizo kufa na ulimwengu kwa ujumla hauna Mungu aliyeuumba wala Mungu wa milele.

Kama tunavyojionea wenyewe katika nukuu hizo, itikadi ya humanism karibu inafanana kabisa na Itikadi ya atheism, na ukweli huu unakubaliwa bila ubishi na wanahumanisti. Kulikuwa na ilani mbili muhimu zilizochapishwa na wanahumanisti katika karne iliyopita. Ilani ya kwanza ilichapishwa mwaka 1933, na ikapitishwa na watu muhimu wa wakati huo. Miaka arobaini baadaye, mnamo mwaka 1973, ilani ya pili ya wanahumanisti ilichapishwa. Ilani hii iliithibitisha ile ya kwanza lakini ikatiwa nyongeza kufuatia hatua fulani za maendeleo ambazo zilipigwa wakati huo. Maelfu ya wanafikra, Wanasayansi, Waandishi na Wanahabari walisaini ilani ya pili ambayo inaungwa mkono na chama cha harakati za wana humanisti wa Amerika.

Tunapoziangalia ilani hizi, tunakuta kuwa katika kila ilani kuna huu msingi mmoja mkuu, ambao ni Dhana ya atheism ambayo inasema ulimwengu na wanadamu hawakuumbwa bali wanaishi kwa kujiendesha wenyewe, kwamba binadamu hawawajibiki kwa mamlaka yoyote isipokuwa kwao wenyewe, na kwamba Imani juu ya Mungu imedumaza maendeleo ya watu na jamii. Kwa mfano vipengele sita vya kwanza vya ilani ya kwanza vya wanahumanist ni hivi vifuatavyo:

Mosi:
Wanahumanist wanaitakidi kuwa ulimwengu unajiendeshea wenyewe maisha yake na haukuumbwa.

Pili: Dhana ya humanism ina itakidi kuwa Mtu ni sehemu ya maumbile na kwamba ameibuka kutokana na mfumo unaojiendesha wenyewe.

Tatu: wakishikilia mtazamo wa maisha wakioganiki, Wanahumanisti wanaona kuwa dhana ya pande mbili za nafsi na mwili lazima ipingwe kabisa.

Nne:Itikadi ya humanism inatambua kuwa utamaduni wa kidini wa mtu na ustaarabu wake kama ulivyoelezwa na historia ni zao la hatua za polepole za maendeleo zitokanazo na mahusiano baina yake na mazingira yake na urathi wa jamii yake. Mtu anayezaliwa katika utamaduni fulani kwa kiasi kikubwa anajengeka kwa utamaduni huo.

Tano: Dhana ya humanism inatangaza kuwa maumbile ya ulimwengu yalioelezwa na sayansi ya leo yanatupilia mbali nguvu yoyote ya mbinguni kuhusiana na maadili ya binadamu.

58.jpg


Sita: Tunaamini kuwa dhana za theism, deism, modernism na aina kadhaa za itikadi mpya zimepitwa na wakati.

Katika vipengele hivyo tunaiona wazi nafasi ya falsafa ya common ambayo inajidhihirisha yenyewe kwa majina ya materialism, Darwinism, atheism na agnosticism. Katika kipengele cha kwanza dhana ya ulahidi ya uhai wa milele wa ulimwengu imewekwa wazi.

Kipengele cha pili kinasema kuwa binadamu hawakuumbwa, hivi ndivyo inavyosema nadharia ya evolusheni. Kipengele cha tatu kinakanusha kuwepo kwa roho kikidai kuwa viumbe wanatokana na maada. Kipengele cha nne kinapendekeza mageuzi ya kiutamaduni na kinakanusha kuwepo kwa silika aliyopewa bindamu (Silika maalum ya binadamu katika maumbile).

Kipengele cha tano kinakanusha mamlaka ya Mungu juu ya ulimwengu na walimwengu na kipengele cha sita kinakataa Imani juu ya Mungu. Itakumbukwa kuwa madai haya ndiyo yale yale ya zile duru zenye chuki na dini sahihi. Sababu ni kuwa dhana ya humanism ndio msingi mkuu wa hisia zote zinazopinga dini. Hii ni kwa sababu dhana hii inasema kuwa mtu ataachwa hivyo hivyo bila kuhesabiwa. katika historia yote. Huu ndio umekuwa msingi wa madai ya kumkanusha Mungu. Katika aya moja ya Qur'an Mwenyezi Mungu anasema:

Je! Anafikiri binadamu kuwa ataachwa bure, (asipewe amri za Mwenyezi Mungu wala makatazo yake)? Je! Hakuwa tone la manii lililotonwa? Kisha akawa kidonge cha damu, kisha akamuumba na akamsawazisha (kuwa mwanadamu kamili)? Kisha akamfanya namna mbili, Mwanaume na Mwanamke. Je ! Hakuwa huyo ni muweza wa kuhuisha wafu?

Mwenyezi Mungu anasema watu hawakuachwa tu hivi hivi na anawakumbusha kuwa wao ni viumbe vyake. Hii ni kwa sababu pale mtu anapotanabahi kuwa yeye ni kiumbe wa Mungu, basi aelewe kuwa haishi bila ya kuangaliwa bali anawajibika kwa Mwenyezi Mungu.

Kwa sababu hii, dai kuwa binadamu hawakuumbwa ndio limekuwa msingi wa falsafa ya humanism Vipengele viwili vya ilani ya kwanza ya wanahumanisti vinatoa maelezo ya itikadi hii. Isitoshe wana humanisti wanashikilia kuwa Sayansi inaunga mkono madai haya. Lakini ni waongo. Tokeya ilani ya kwanza ya wanahumanisti ilipochapishwa Premesia mbili ambazo wanahumanisti wameziainisha kama hakika za kisayansi, kwamba ile dhana kuwa ulimwengu ni wa milele pamoja na nadharia ya evolusheni zote zimesambaratika.

1. Dhana kuwa Ulimwengu ni wa milele ilivunjiliwa mbali na mlolongo wa vumbuzi za angani zilizofanywa pale ilani ya kwanza ya wanahumanisti ilipokuwa inaandikwa.. Vumbuzi kama vile ulimwengu kutanuka, chanzo cha mionzi ya angani na mahesabu ya uwiano ya Haidrogen hadi helium, zimeonyesha kuwa ulimwengu ulikuwa na chanzo chake na kwamba uliibuka kutokana na hamna takribani miaka bilioni 15-17 iliyopita kwa mlipuko mkubwa ulioitwa Big Bang.

Ingawaje wale wanaounga mkono falsafa ya kihumanisti na kilahidi walikataa kukubali nadharia ya Big Bang lakini hatimaye walishindwa kabisa. Kutokana na ushahidi wa kisayansi ambao umejitokeza, jamii ya wanasayansi hatimaye imeikubali nadharia ya Big Bang kwamba ulimwengu ulikuwa na mwanzo wake na hivyo wanahumanisti hawana hoja. Hivyo mwanaatheist Antony Flew alilazimika kukiri hivi:

.Sasa nitaanza kukiri kuwa mwanaatheisti lazima atatizike kwa hizi fikra za sasa za maumbile. Kwani inaonekana kuwa Wanakosmolojia wanatoa ushahidi kuwa kile alichodai Mtakatifu Tomas hakiwezi kuthibitishwa kifalsafa hii ikiwa na maana kuwa ulimwengu ulikuwa na mwanzo wake.

2. Nadharia ya evolusheni ambayo ndiyo hoja kuu iliyomo katika ilani ya kwanza ya humanism ikaanza kupoteza nguvu miongo kadhaa baada ya kuandikwa kwake. Inafahamika hivi leo ubabaishaji uliofanywa na wana evolusheni na wakiatheisti (na bila shaka wakihumanisti), kama vile A.I. Oparin na J.B.S. Haldane katika miaka ya thelathini kuhusiana na chanzo cha uhai hauna msingi wa kisayansi.

3. Viumbe haviwezi kutokea kwa bahati nasibu kutokana na maada isiyo na uhai kama ilivyodaiwa katika ubabaishaji huu. Kumbukumbu ya mabaki ya kale inaonyesha kuwa viumbe hai hawakuwa hivi walivyo kutokana na hatua za mabadiliko madogo madogo bali walitokea kwa pamoja wakiwa na sifa zao mbali mbali.

4. Ukweli huu umekubaliwa na wana evolusheni wenyewe tangia miaka ya Sabini. Sayansi ya viumbe hivi leo imebainisha kuwa viumbe hai hawakutokana na bahati nasibu na kanuni za maumbile bali katika kila kiumbe kuna mfumo madhubuti unaothibitisha kuwa Msanii mwenye hekima ndiye aliyeviumba. Ukitaka maelezo zaidi rejea kitabu kiitwacho, Darwinism Refuted.

Zaidi ya hivyo dai la uongo kuwa imani ya dini ndio sababu inayowakwaza watu kuendelea na kuwatumbukiza katika mifarakano limetupiliwa mbali na ushahidi wa kihistoria. Wanahumanisti wamedai kuwa kuondolewa kwa imani ya dini kutawaletea watu furaha na faraja. Hata hivyo hali imekuwa kinyume cha mambo.

Miaka sita baada ya kuchapishwa kwa ilani ya humanism, vita vya pili vya Duniya vikalipuka, hii ni kumbukumbu ya misiba mikubwa iliyoletwa na itikadi za kifashisti za kisekula. Itikadi ya Humanism ya Ukomunisti ikachipuka, kwanza ilianzia kwa watu wa Urusi kisha kwa watu wa China, Cambodia, Vietnam, Korea kaskazini, Cuba na katika baadhi ya nchi za afrika na Latin Amerika, kulikuwa ni ushenzi usio na mfano.

Jumla ya watu Milioni 120 waliuawa na tawala za Kikomunisti au jumuiya za kikomonisti. Ni dhahiri kuwa kundi la wanahumanisti wa Magharibi (mifumo ya kibepari) nalo limeshindwa kuleta amani na furaha katika jamii zao na katika maeneo mengine ya Duniya.

Kuvunjwa kwa hoja ya humanism juu ya dini pia kumedhirishwa katika fani ya saikolojia. The Freudian myth, msingi wa dhana ya kiatheist tokea mwanzoni mwa karneya ishirini imebatilishwa na matokeo ya uchunguzi. Patric Glynn wa Chuo Kikuu cha George Washington anaufafanua ukweli huu katika kitabu chake kinachoitwa God: The Evidence, The Reconciliation of Faith and Reason in a PostSecular World.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom